Archive Page

JINSI YA KUTUMIA

Mwongozo wa Mwezeshaji

Mwongozo huu utatumika pamoja na slaidi za uwasilishaji na kijitabu kilichotolewa na Focus on the Family. Mwongozo umeandaliwa kama ifuatavyo:

Kitengo

Kuna vitengo vinne katika mtaala wa Hakuna Majuto .

Moduli

Kila kitengo kina moduli nne hadi tano. Kwa mfano, 2.1 inaonyesha Moduli ya 1 chini ya Kitengo cha 2.Kila moduli itaeleza malengo, usuli na mantiki yake.

Aikoni Muhimu

Activities Icons

Mazoezi ni sehemu za warsha zinazohusisha kushiriki. Kila shughuli inasema nyenzo/ vifaa inavyohitajika, pamoja na maelekezo ya jinsi ya kulitekeleza zoezi.

Video Clips Icons

Klipu za video zinapendekezwa ili kuwashirikisha washiriki na kuonyesha hoja maalum. Ama filamu inayofaa au kiungo cha mtandaoni kitapendekezwa.

Aikoni za Ziada

Slides Icons

Aikoni hii inaonyesha kuwa maudhui yanaweza kupatikana katika slaidi zinazotolewa na Focus on the Family.

Handbooks Icons

Aikoni inaonyesha kwamba washiriki wanapaswa kurejelea vitabu vyao vya mazoezi, kwa kawaida ama kukamilisha zoezi, au kusoma kwa habari zaidi. Hapa, nambari inaonyesha kwamba unapaswa kurejelea ukurasa wa 7.

Small Group Icons

Aikoni inaonyesha mada au maswali ya majadiliano ya kikundi kidogo (washiriki 4 hadi 6) ikiwa muda unaruhusu.

Instructions For The Facilitator Icons

Aikoni inaonyesha maelekezo maalum kwa ajili ya mwezeshaji kuzingatia wakati wa ku kuelezea yaliyomo.

Share A Real Life Story Icons

Aikoni inaonyesha mahali panapofaa kwa mwezeshaji kushiriki hadithi ya maisha halisi. Inaweza kuwa hadithi ya kibinafsi au akaunti ya mtu mwingine ya uzoefu wake. Kwa kawaida hadithi ya mfano hutolewa

Extra Content Icons

Aikoni hii inaonyesha maudhui ya ziada ambayo mwezeshaji anaweza kutumia wakati wa warsha ikiwa ni yanafaa kiutamaduni.

Take Home Activity Icons

Aikoni hii inaonyesha shughuli za ziada ambazo zinaweza kutumika kama zoezi la kupeleka nyumbani kwa washiriki au mahali ambapo zaidi ya saa nane zitatumika kwa warsha. Kwa kawaida, shughuli hizi zitahitaji muda zaidi.

Going Deeper Icons

Aikoni hii inaonyesha kuingia ndani zaidi katika mada. Wahimize washiriki kutumia muda zaidi wa kutafakari.

Going Home Icons

Aikoni hii inaonyesha Kwenda Nyumbani. Wahimize washiriki kujadili na wazazi wao kile walichojifunza. 7

Lengo

Ili kuchangamsha washiriki jenga mazingira ya utulivu na ya furaha.

Mahitaji

Usajili

  • Fomu za uchunguzi wa awali (sio lazima)
  • Kadi za maswali/ maoni
  • Kijitabu cha mwanafunzi cha mazoezi
  • Kalamu ya mate/Kalamu ya wino
  • Sanduku la maoni (sanduku lililokuja na viatu vipya linalosha)

Maagizo

Kitini:

Wapatie fomu za kabla ya uchunguzi washiriki na uzikusanye wakisha zikamilisha. Wahimize washiriki kutoa majibu yao halisi kwa ajili ya swali hili, ““Ni wakati gani unaofaa kwa mtu kushiriki ngono, na kwa nini?” wahakikishie ya kwamba haitajulikana ni nani ametoa jibu gani. Sio lazima washiriki kuweka majina yao kwenye fomu. Uwaonyeshe kwamba maoni yao ya uaminifu yatakuwa msaada katika kufanya utafiti. Majibu yao yatakuwa kielelezo juu ya maoni ya washiriki.

Kijitabu cha mwanafunzi: Moja kwa kila mshiriki.

Kadi za maswali/maoni: Himiza washiriki kuandika maswali waliyo nayo kuhusu maisha, mapenzi ama ngono, kisha wayaweke maswali hayo kwenye kisandulu kilichowekwa kwa sababu ya warsha. Iwapo hawaoni uhuru maswali yao kujibiwa wakati wa warsha, waruhusu wakuachie anwani/namba za mawasiliano kwenye kadi ili uwasiliane nao kando.

Activities Icons

Zoezi 1: Unganika!
Chaguo la 1: Lengo la Cupid (Malaika wa mapenzi)

Blank Icons

Lengo

Wachangamshe washiriki na uwatambulishe mada zitakazojadiliwa—Maisha, Mapenzi na Ngono.

Slides Icons

Mahitaji

  • 8 A-Roketi/milipuko ya vidoleni (finger blasters)
  • Ubao utakaolengwa shabaha au slaidi ya “Maisha, Mapenzi, Ngono”.
  • Watu 8 wa kujitolea (wavulana 4 na wasichana 4) 
Blank Icons

Maagizo

  1. Bila kutoa mafunzo yoyote, Chagua watu 8 wa kujitolea (wavulana 4 na wasichana 4) wasimame mbali na kujaribu kulenga shabaha sehemu yoyote ya ubao/slaidi.
  2. Baada ya washiriki kujaribu (na kuhangaika kutumia blaster ya kidole au kulenga shabaha), mwakirishi awaonyeshe washiriki jinsi ya kutumia blaster ya kidole na kulenga kwa usahihi.
  3. Wape washiriki nafasi kulenga shabaha mara ya pili, wakilenga neno mojawapo (Maisha, Mapenzi au Ngono), wanalofikiria kuwa ni mada ya kuvutia zaidi ya mengine.
  4. Eleza kwamba kama vile ambavyo kila wakati tunapolenga shabaha hatuipigi , hivyo ndivyo tunaweza tukajikuta tunalenga na kukosa tunapokuja kwenye suala la kuelewa maisha, mapenzi na ngono. Bofya neno Ukweli na utambulishe mada zitakazojadiliwa katika karakana-siyo tu kuhusu ngono, lakini lengo ni kugundua UKWELI kuhusu ngono, mapenzi na mahusiano, ambayo itatutambulisha maisha ni nini hasa.
Activities Icons

Chaguo la 2:
Kulia-Kushoto-Kulia

Instructions For The Facilitator Icons

Kama programu hii si ya kiingereza katika jamii yako, maneno kushoto na kulia yanaweza yasitafsiriwe vyema katika zoezi hili.

Blank Icons

Maagizo

  1. Waulize washiriki wasimame ikiwa wamefumba macho (ili wasiwafuate marafiki zao) unaposoma hadithi (zinapatikana chini) kwa sauti. Kila mara maneno KUSHOTO ama KULIA yanaposomwa, waliojitolea wanapaswa kugeuka digrii 90 upande huo.
  2. Ili kufanya zoezi liwe la kuvutia zaidi, soma hadithi haraka, tulia kati kati ya sentensi na usisitize KUSHOTO/KULIA. Washiriki waanze kwa kutazama mbele.
  3. Mwisho wa hadithi wanapashwa kuwa wameelekea kulia.
  4. Malizia kwa kuwaambia kwamba kukua kunaweza kutatanisha kama zoezi hili lilivyokuwa, hivyo inatubidi kuuchunguza ukweli kuhusu maisha, mapenzi na ngono.

Hadithi ya Kulia-Kushoto-Kulia

Carol hakujua ni jozi gani ya viatu vilivyolifaa kuvaliwa kwenye hafla hiyo. Viatu vyake vyeusi vya michezo ama vile visivyo na visigino? Alikuwa akienda kwa tamasha lamichezo na kundi la marafiki, na Nathan beki wa KULIA wa timu ya soka ambaye alimpenda sana, alikuwa awepo pia. Alitaka kuhakikisha kuwa atamvutia leo.

“Bor boooooooor!” Carol alipumua, akachukua viatu vya michezo na kukimbia nje ya nyumba kukutana na rafiki yake.

Kikundi chake kilipitia vituo mbalimbali vya michezo kilikuta bango lililosema, “Mechi ya Soka ya Mchanganyiko. Saa kumi jioni. Wachezaji sita kila timu. Jisajili KUSHOTO.” Kilikuwa na idadi iliyotosha hivyo kilijisajili. KULIA

Kikundi hicho kilikimbilia uwanjani na kuchukua nafasi zao. Katika kipindi cha kwanza walifungwa mabao matano kwa bila; timu hiyo nyingine ilikuwa inacheza mpira mchafu hasa jamaa mkubwa aliyekuwa KULIA. Katika kipindi cha pili kikundi hicho kiliwafikia wapinzani wake. Dakika mbili kabla ya mechi kuisha mabao yalikuwa 5 kwa 4.

Kikundi hicho kilikuwa na mpira wakati jamaa mnene alipomkimbiza Nathan ghafla kutoka KULIA. Nathan aligeresha KUSHOTO naye jamaa huyo mnene alimpita na kumkimbilia Carol. Alimwangukia na kumvunja mguu wake wa KULIA. Carol aliteguka kisigino chake cha KUSHOTO. Refa alipuliza filimbi kusimamisha mpira. Jamaa huyo mnene aliinuka akasonya na kutoweka uwanjani.

Nathan alikimbia alipokuwa Carol akamshika mkono wake wa KULIA na kumsaidia kuinuka. Polepole walichechemea pembeni ambako Nathan alimkalisha Carol chini. Baada ya kuhakikisha kuwa Carol yuko sawa alirejea uwanjani; hata kama hawangeweza kushinda hawakutaka kukata tamaa.

Huku zikisalia sekunde 90 mechi ilianza tena. Hiyo timu nyingine ilikuwa inacheza mpira mchafu zaidi ikiiumiza ile timu nyingine KUSHOTO na KULIA na hivyo walipoteza milki ya mpira. Baada ya bidii kubwa timu hiyo iliupata tena mpira. Nathan ndiye aliyekuwa na mpira na zikiwa zimesalia sekundi 12 na hakukuwa na mchezaji mwenzake aliyekuwa bila upinzani, aliendelea mbele, akielekea KULIA kwa uwanja.

Ghafla akakata KUSHOTO, akaifanya ya KULIA, akaifanya ya KUSHOTO, akageuka KULIA, kisha KULIA tena, akakata KUSHOTO, na hatimaye akaupiga mpira a akidhania umeingia wavuni.

Lakini uligonga mlingoti. Refa alipuliza filimbi mchezo ukaisha. Walikuwa wameshindwa.

Kwa vile Carol alikuwa ameumia kila mtu aliamua kwenda nyumbani. Wote waliingia kwenye gari lililokuwa KUSHOTO kwa lango la kuingilia, na kuendesha hadi machweo ya jua..

Activities Icons

Chaguo la 3:
Iliyochanganyikiwa

Blank Icons

Mahitaji

Instructions For The Facilitator Icons

Maagizo

1. Kabla ya warsha, kata kamba moja (kwa kila mshiriki), yenye urefu wa sentimita 150 kutoka kwenye mpira wa kamba.

2. Funga kitanzi kinachoweza kubadilishwa kila mwisho wa kila kamba .

3. Angalia maagizo ya video ya jinsi ya kutenganisha-suluhisho la shughuli hii kama matayarisho.

4. Wakati wa warsha, toa kamba kwa kila mshiriki.

5. Waombe washiriki kutafuta mwenzao wa jinsia moja.

6. Waombe washiriki kuweka kitanzi kwenye ncha zote mbili za uzi na kuziweka kama pingu kwenye mikono yao.

7. Baada ya hayo, pamoja na mwenzao, mmoja wao atachukua kamba kutoka kwenye mkono mmoja, ipitishe kwenye kamba ya mwenzao na kuiweka tena kwenye mkono wake (angalia maagizo ya video).

8. Wajulishe washiriki kuna sheria 2 tu za zoezi hili:

  • Usiondoe kamba mikononi mwa mwenzako,
  • na usiivunje au kuikata kamba.

9. Kwa sheria hizi 2, lengo lao ni kujikomboa kutoka kwa mwenzao . Wendelee kujikomboa hadi muziki utakaponyamaza. Anza!

10. Fafanua kwa kuuliza:

  • Tunaweza kujifunza nini kutokana na zoezi hili?
  • Unapokuwa na tatizo, unaweza kufanya nini ili kulitatua?
Slides Icons

Somo muhimu tunaloweza kujifunza ni kuwa:

  • Unapokuwa na shida, pata msaada kutoka kwa watu sahihi.
  • Wakumbushe washiriki umuhimu wa jumuiya na kuwa na washauri wa kuwaongoza katika safari yao ya kujifunza ukweli kuhusu maisha, mapenzi na ngono.
Activities Icons

Zoezi 3:
Wanachosema kuhusu Mapenzi na Ngono

Blank Icons

Lengo

Wajulishe washiriki wazo sahihi la mapenzi na ngono.

Blank Icons

Mahitaji

  • 8 puto (balloons)
  • (Ukubwa wa karatasi A3/A4) Kadi za “Hadithi au Ukweli?”
  • pini/sindano
  • vibandiko vya rangi
  • Chapisha/mkanda
Blank Icons

Maagizo

1. Kabla ya semina, jaza hewa puto na uzibandike kote kote chumbani kwenye ubao mweupe au ukutani. Bandika kadi za “Hadithi au Ukweli?” kando ya kila puto.

Slides Icons

2. Wakati wa warsha, weka slaidi ya “Wanachosema kuhusu mapenzi na ngono” na uelezee kikundi kwamba hizi ni baadhi ya kauli tunazozisikia kuhusu vijana, mapenzi na ngono.

Instructions For The Facilitator Icons

Mwezeshaji achague sentensi zisizozidi nane zinazoakisi hadithi potofu zilizoenea katika jamii yako kutoka kwa taarifa iliyo hapa chini

Handbook 4 Icons
  • 1. Uamuzi wa kufanya ngono ni kati ya watu hao wawili pekee na hauathiri mtu mwingine yeyote. (Hadithi)
  • 2. Ninachofanya na mwili wangu hakina athari kwangu kama mtu. (Hadithi)
  • 3. Kungoja tu kujamiiana baada ya ndoa ni jambo lisilowezekana. (Hadithi)
  • 4. Ngono ni sawa na mapenzi. (Hadithi)
  • 5. Kuangalia ponografia ni kawaida na haina madhara; haitaathiri jinsi ninavyoona mapenzi na ngono. (Hadithi)
  • 6. Ngono sio tu tendo la kimwili. (Ukweli)
  • 7. Vijana wengi wanataka kuwa na mahusiano ya kudumu na yenye upendo. (Ukweli)
  • 8. Vijana siku hizi watashiriki ngono bila kujali umewaambia nini. (Hadithi)
  • 9. Maadamu kondomu inatumiwa wakati wa kujamiiana, mtu hatapata magonjwa ya zinaa au kupata mimba. (Hadithi)
  • 10. Ngono itakuwa bora ikiwa nitapata uzoefu zaidi kabla ya ndoa. (Hadithi)
  • 11. Wavulana wanataka ngono zaidi kuliko wasichana. (Hadithi)
Blank Icons

3. Wape washiriki dakika 5 kuzunguka chumbani ili kusoma kadi. Iwapo wanafikiri kuwa kauli hiyo ni hadithi, wanapaswa kuweka kanda/kibandiko kwenye puto, ili “kupiga kura” ni puto gani ipasuliwe.

4. Muombe mtu ajijitolee kusimama karibu na kila puto na ampe kila mmoja sindano/pini.

5. Pitia kila oni lililoshikiliwa na watu wengi. Waulize waliopigia kura puto hiyo kupasuliwa watoe sababu zao. Inapothibitishwa kuwa maoni hayo ni hadithi, mwambie aliyejitolea kuipasua puto. Ambapo maoni ni ukweli, iache puto bila kuipasua.

Instructions For The Facilitator Icons

Wawezeshaji watumie muda huu kueleza kwa ufupi kwa nini maoni hayo ni hadithi au ukweli, na kutaja kwamba itajadiliwa katika warsha ujao. Hakuna haja ya kwenda kwa kina; Lengo la shughuli hii ni kuwasaidia washiriki kuanza kufikiria maoni yaliyoenea kuhusu mapenzi na ngono.

Blank Icons

Mstari mwingine wa kawaida unaosikika kutoka kwa vijana ambao wamefanya ngono:

Slides Icons

Ilitokea tu...

Lakini “Haitokei tu.” Ni wakati mipaka haikuwekwa kwa uwazi na vijana hawafikirii juu ya matokeo ya vitendo vyao ndipo wanajikuta wamenaswa katika hali zinazoathiri na jambo moja husababisha lingine.

Blank Icons

Haitatokea kwangu

Mtazamo mwingine wa kawaida ni mawazo ya “ mimi si wa kawaida”. Vijana wengi hufikiri kwamba hawahitaji kulichukulia kwa uzito suala la kushiriki ngono kabla ya ndoa bila kujua kwamba iwapo hawataamua mapema maadili na mipaka yao, watakumbwa.

Kitengo hiki kinasisitiza upekee na thamani ya kila mtu binafsi, umuhimu wa tabia njema zinazojenga mahusiano yenye afya na kukabili maisha ya baadaye kwa makusudi imara.

Dk. Juli Slattery katika kitabu chake, Ngono na Msichana Mseja (Sex and the Single Girl), alisema kwamba tumeumbwa wanaume na wanawake “tukiwa na maumbile ya kimwili na sifa za kibayokemikali za kijinsia.” Hii ina maana kwamba tunayo hamu ya urafiki wa karibu, uhusiano na furaha ya kimwili. Hivyo ndivyo tulivyo na tulivyoumbwa na si wakati tu tunaposhiriki ngono au tunapoolewa/kuoa. Matendo haya katika hali hizi huthibitisha jinsi tulivyoumbwa.

Ngono, ujinsia na urafiki wa karibu mara nyingi maneno haya yanatumiwa bila kutofautishwa katika utamaduni wetu. Hii inaleta matata katika kujadili mambo haya. Ujinsia wako ni zaidi ya tendo la kushiriki ngono. Hamu yako ya kuwa na urafiki wa karibu ni zaidi ya tamaa ya ngono. Kumbuka ufafanuzi huu ufuatao:

Ujinsia: Dhana pana inayojumuisha nyanja zote za jinsia ya mtu, hamu ya ngono, imani juu ya ngono na uzoefu wa ngono.

Urafiki wa karibu: Uhusiano wa karibu na wenye upendo kwa mtu unayemfahamu sana. Ukaribu unahusisha kujisikia uko salama na huyo mtu, kufahamiwa kwa kina naye na kujua siri za ndani baina yenu.

Ngono: Zoezi la kimwili ambalo mara nyingi ni pamoja na kujamiiana.

Tunaweza kuzingatia sana tendo la ngono (ambalo huonekana mara kwa mara kwenye vyombo vya habari) na kukosa picha kubwa ya ngono, ambayo inajumuisha mtu mzima na hamu yetu ya uhusiano wa kweli. Au tunaweza tu kuishi kwa baadhi ya miongozo na tukaepuka sababu ya kina ya ujinsia wetu, ambayo ni kujisikia tuko na usalama, kufahamiana kwa kina na kujuliana siri za ndani. Hebu tuanze safari hii ya kujitambua kwa kuelewa sisi ni nani na jinsi tulivyoumbwa ili tuwe na mahusiano ya kweli na yenye afya.

KITENGO 1.1 WEWE NI WA KIPEKEE

KITENGO 1.2 NDOTO ZA MAISHA NA MALENGO

KITENGO 1.3 TABIA

KITENGO 1.4 MARAFIKI

KITENGO 1.5 NINA THAMANI GANI?

Lengo

Kuwafahamisha washiriki kuwa wao ni watu wa kipekee, tofauti, wana mseto wa mambo yanayowajenga na thamani ya ndani, na kwamba wanafaa kuchukuliwa kwa uangalifu na heshima.

Usuli

Kila kijana ni wa tofauti, wa kipekee na thamani ya ndani, anayepaswa kuchukuliwa kwa uangalifu na heshima. Kipindi hiki cha kubaleghe ama kuvunja ungo ni wakati ambapo maoni ya vijana wenzao huwa muhimu, vijana wanahitaji kusikia ujumbe huu “ wewe ni wa thamani” bila kujali ufanisi wa masomo, sura na hata mambo mengine.

Haijalishi ni jinsi gani vijana wanavyojiona, hawajakomaa, sio watu wazima na kwamba wangali wanakua katika sehemu zote, kiakili, kijamii, kihisia, kimwili, kiadili na kiroho. Mwanadamu ni mseto wa mambo mengi na kila mara anafaa kuzingatiwa hivyo – kwa ujumla na sio kwa sehemu. Uamuzi mkubwa wanaoufanya unaweza kuwaathiri katika kila sekta ama sehemu.

Hili linahusu hasa kwenye eneo la ngono, ambalo sio tu tendo la kimwili ama hisia tu. Uamuzi wa kushiriki ngono kabla ya ndoa unaweza kwenda kinyume cha malengo ya mtu ya elimu, viwango vya kibinafsi/maadili, maadili ya familia na uhusiano na marafiki. Mtu anaweza kuwa amekomaa kimwili lakini mchanga kwa maswali ya kijamii.

Activities Icons

Zoezi 1:
Wewe ni wa Kipekee!

Blank Icons

Lengo

Washiriki wafahamu thamani ya upekee wa kila mtu.

Blank Icons

Maagizo

  • Chagua mshiriki mmoja kujibu swali. Unaweza kuielezea kama sehemu ya mchezo maarufu.
Instructions For The Facilitator Icons

Mapendekezo: iwapo washiriki hawajitolei, unaweza kuuliza mshiriki aliyepata maksi nyingi kuliko wote kwenye somo la hesabu au aliyezaliwa wa kwanza katika kundi.

Slides Icons

1. Uliza, “Kisia uwezekano wa wewe kuzaliwa (kama wewe?

  • (a) 1 katika millioni 2
  • (b) 1 katika millioni 200
  • (c) 1 katika millioni 20
  • (d) 1 katika billioni 2
  • ((Jawabu ni b.))
  • Sababu: Shahawa inayomwagika mara moja wakati wa ngono ina karibu mbegu milioni 200. Ni mbegu chache tu zinazofika kwenye yai, na kati ya hizo ni mbegu moja tu inayochaguliwa kukamilisha safari ya kurutubisha yai. Kwa upande wa mapacha wa kindugu, mbegu mbili za kiume hutungisha mayai mawili. Mapacha wanaofanana (kwa mwonekano) hutoka kwenye yai moja lililorutubishwa ambalo hugawanyika katika viini viwili tofauti.
Slides Icons

2. Uliza:

  • Idadi ya watu ulimwenguni ni wangapi?
  • Idadi ya watu [kwenye taifa lako] ni wangapi?
  • Idadi ya watu ulimwenguni inakisiwa kuwa takriban bilioni 8 (kufikia Disemba 2021) Idadi ya watu kwenye taifa lako inafaa kupatikana kwenye mtandao. K.m, Idadi ya watu nchini Misri inakisiwa kuwa milioni 117 (kufikia Septemba 2024).
Handbook 7 Icons

3. Je, wajua?

  • Kuna zaidi ya watu bilioni 8 duniani,ila hakuna mtu aliye na alama za vidole zinazofanana na zako!
  • Hakuna mtu anayeweza kuwa na sauti kama yako! Koromeo na nasali za kila mtu zinatofautiana kwa kiasi kwa umbo na urefu. [1] Mbali na hayo, midomo, meno, ulimi, kaakaa na misuli ya taya husaidia mtu kuzungumza kwa njia tofauti ukilinganisha na mwenzako. [2] Tofauti hizi zote huchangia kuleta ama kufanya sauti ziwe tofauti. Ijapokuwa tofauti si zakusikika, mashine zinaweza kubainisha tofauti hizi ndogo. Huu ni mfumo wa kipekee wenye utambulisho wa sauti.
  • Mboni la jicho lakio ni la kipekee! Sehemu iliyo na rangi ya jicho lako inaamuliwa na vinasaba tukiwa tumboni na huundwa kikamilifu wakati tunapotimiza umri wa miaka miwili. Sio tu kwamba mboni za macho yetu ni tofauti (hata kwa mapacha wanaofanana), ruwaza ya jicho lako la kushoto na kulia ni tofauti.
  • If you write your DNA code on paper, it would form a book 23 stories high! You are unique (with a unique DNA) at fertilization. When a sperm reaches the egg, a chemical reaction causes the egg to seal up, so no other sperm can join with the egg. At the same time, the sperm releases its DNA information, and it pairs with the DNA from the egg to form a complete human DNA strand. This is the first cell from which an entire person will grow. The DNA in this cell can only be formed by this specific egg and specific sperm. If any other sperm had fertilized the egg or if fertilization had occurred during a different menstrual cycle, a different person would have been created.
Blank Icons

4. Sisitiza hoja hii kuwa uko wa kipekee – na hilo ni la muhimu. Hakuna mtu anayefanana na wewe. Waombe washiriki kumwambia mtu aliye karibu nao ‘wewe ni wa kipekee!’

Activities Icons

Zoezi 3:
Mwanadamu

Blank Icons

Lengo

Mwanadamu – mtu ni mseto wa mambo mengi.

Blank Icons

Mahitaji

  • Shuka la kitanda jeupe lisiyo na madoa ama (karatasi yenye kimo kiasi cha mwanadamu)
  • Vikolezi vinavyofutika.
  • Watu wawili wa kujitolea ikiwezekana wa jinsia moja hasa wanaume
Blank Icons

Maagizo

1. Pata mtu mmoja wa kujitolea alale chini kwenye shuka kubwa la kitanda ama karatasi kubwa akiwa ameangalia juu na mtu mwingine achore nje ya mwili wake kwenye shuka hilo kwa kutumia kalamu ya rangi.

2. Akisha kamilisha, omba watu wawili wa kujitolea watakaloliinua shuka hilo ili kila mmoja alione.

Handbook 8 Icons

3. Chora sehemu tano za mwanadamu kisha ufafanue kila moja.

  • Akili Chora ubongo.Eleza kuwa mwanadamu/mtu hufikiria kuhusu masuala, mawazo na kufanya maamuzi kuhusu maisha yake. Wanadamu wana akili na utashi – uwezo wa kuchagua.
  • Jamii Chora Mdomo.Eleza kuwa kila mtu ni sehemu ya jumuiya. Anajifunza kushirikiana na wenzake, kukuza urafiki na kufanya kazi na wenzake kwa manufaa yake mwenyewe na wao.
  • Hisia Chora moyo.Eleza kwamba hisia hupenya utu wetu wote. Mtu aliyekomaa ni yule ambaye anathibiti hisia zake.
  • Mwili Chora misuli.Eleza kuwa mwili ni muundo unaotuhifadhi. Unakua na kukomaa haraka zaidi kuliko vipengele vingine vya utu wetu.
  • Maadili Chora umbo la pembe tatu kwenye utumbo.Hadithi za zamani za wenyeji wa Marekani zinalinganisha dhamiri na umbo la pembe tatu katika eneo la utumbo. Kitendo kibaya kinapofanyika, umbo hilo la pembe tatu linazunguka, na kumchoma mtu (hivyo msemo “dhamiri inachoma”). Elezea kuwa watu wote hukabiliwa na maswali ya wema na ubaya, sahihi na makosa. Lazima waishi maisha yao kulingana na kanuni za maadili.
  • Mwanadamu – mtu anafaa kuzingatiwa kwa ujumla wala sio kwa sehemu.
Blank Icons

4. Elezea washiriki kuwa kuna sehemu ya kiroho ambayo hatuwezi kuiona lakini imo ndani ya kila mmoja wetu. Ni hamu iliyopo ya ndani la kila mmoja wetu kuwa kuna mtu ama kitu kilicho juu zaidi yetu kuliko sisi wenyewe.

5. Waombe washiriki warudie vipengele vitano vya sehemu za mwanadamu bila kuangalia slaidi

Activities Icons

SHUGHULI MUHIMU
Zoezi 3: Mnyororo wa Mwanadamu

Blank Icons

Lengo

Kila linalofanywa na sehemu moja ya mwili wako huathiri sehemu nyingine.

Blank Icons

Mahitaji

  • Tayarisha vitambulisho 5 kwa kila sehemu moja ya mtu (akili, jamii, hisia mwili, maadili).
  • Watu 5 wa kujitolea wa jinsia moja.
Blank Icons

Maagizo

1. Hawa watu 5 wa kujitolea, wachague kibandiko watakachovalia kwenye shingo zao. Waombe wapige foleni wakiangalia kundi huku mikono yao imeunganishwa kwa mkazo. Eleza kuwa hiyo inamwakilisha binadamu.

2. Waambie watu 5 waliojitolea kuwa lazima waendelee kuunganishwa kwani wanachukuliwa kama mtu mmoja. Mnyororo hauwezi kukatika hata itokee nini.

3. Wapatie kundi mfano wa tukio na uwaulize ni sehemu gani ya binadamu ambayo inaathirika zaidi katika hali hii.

Matukio :

  • Ukikaripiwa na wazazi wako
  • Ukiachwa na mpenzi
  • Ukipata ajali ya barabarani
  • Kuvuta sigara/dawa za kulevya
  • Kushiriki ngono kabla ya ndoa
Instructions For The Facilitator Icons

Badilisha matukio ili kuonyesha yale ambayo hutokea ama yameenea sana katika jumuiya yako.

4. Kwa kila tukio, omba mmoja wa watu 5 waliojitolea kupiga hatua 2 mbele ikiwa wanahisi kuwa kipengele chao ndicho kinachobainisha jibu. (Waombe waliojitolea kurejea kwenye nafasi yao ya awali kabla ya kuendelea na tukio lifuatalo). Kikundi kitagundua kuwa mnyonyoro wote wa binadamu unasonga kila mtu mmoja anaposonga mbele.

Slides Icons

Binadumu lazima daima afikiriwe kwa ujumla –– wala sio kwa sehemu.

Kwa kuwa kipengele kimoja kinaonekana kuathirika zaidi ama kuhisi athari mara moja, haimaniishi kuwa sehemu zingine haziathiriwi.

Blank Icons

Fikiria!

Slides Icons

Kwa sababu bongo zetu, “zingali zinakua” tukiwa vijana, ni muhimu tutafakari kabla ya kufanya maamuzi badala ya kutegemea tu hisia au tamaa zetu za kimwili..

  • Waambie washiriki kunyosha vidole vyao viwili (shahada na kile cha kati, na wajiguse au wamguse (yule aliye karibu nao) kwenye kipaji cha uso na kusema “Fikiria!”
  • Kwa mujibu wa utafiti nchini Marekani, asilimia 60% ya vijana kati ya umri wa miaka 12-19 ambao wameshiriki ngono wanatamani kuwa wangesubiri. [6] Ili tusifanye maamuzi ambayo tutajutia baadaye, tunahitaji kufikiria!.
Extra Content Icons

Maelezo Ziada

Blank Icons

Ukuaji wa sehemu Tano za Binadamu –Mtu

Ukuaji wa polepole: Kiakili, Ubongo

Kinyume cha imani za muda mrefu kuwa ubongo hukamilika kukua mwisho wa umri wa utoto, utafiti unaonyesha kuwa vijana huingia awamu ya pili ya ubongo kukua wakati wa kuvunja ungo ama kubalahe [3]. Awamu hii ya ukuaji huongeza kiwango cha kufanya uamuzi wa ukomavu, udhibiti wa msukumo, huku ubongo ukihama hatua kwa hatua kutoka kituo cha mihemko (amygdala) hadi kwenye gamba la mbele la ubongo (kituo cha sababu na mantiki)[4]. Hii ina maana kuwa ubongo wa kijana haswa sehemu inayothibiti uamuzi inaendelea kukua. Kwa vijana wengi awamu hii ya ukuaji huishia katika miaka 20 na zaidi.[5]

Ukuaji wa haraka: Kimwili

Kila mtu hupitia awamu ama kipindi cha kukua kinachoitwa kubalehe ama kuvunja ungo kwa wasichana. Kwa wasichana, kipindi hiki hutokea kati ya umri wa miaka 10 hadi 12, lakini kwa wengine huanza mapema miaka 9; kwa wavulana, mchakato huo huanza baadaye, kati ya umri wa miaka 12 hadi 14. Katika kipindi hiki, mwili wa mtoto hupitia mabadiliko mbali mbali ili uwe mwili wa “mtu mzima”; wasichana hukua matiti na kuanza kupata hedhi, huku wavulana huanza kuwa na ndevu, nywele kwenye uso na mwili, sauti nzito, na sehemu zao za siri kuongezeka. Kwa vijana wengi mchakato huo hukamilika wakiwa na umri wa miaka 16; kwa wakati huo wanaweza kufanya kazi za watu wazima.

Going Deeper Icons

Kwenda Ndani Zaidi

Blank Icons

Unawezaje kujipa changamoto ya kukua katika kila moja ya maeneo haya? Taja baadhi ya mifano.

Handbook 9 Icons
  • Kiakili
  • Kihisia
  • Kijamii
  • Kimaadili
Blank Icons

[Mifano inaweza kujumuisha: kusoma kitabu kisichoeleweka kwa urahisi na kuangalia
ndani zaidi, au kujadili mada na mtu fulani. Kuwa na mlo na watu walio nje ya “kikundi”
cha mtu, kudhibiti hasira ya mtu kwa kuhesabu hadi 10 wakati kawaida yake ni kulipuka, kutimiza ahadi ikiwa kuna tabia ya kuzivunja.]

Take Home Activity Icons

Zoezi la Nyumbani:
Mimi ni wa Kipekee!

Blank Icons

Upekee wako ni zaidi ya kile chembechembe zako za msimbojeni-DNA zinavyokuelezea. Kwa kila sehemu andika jambo linalokuhusu na uone jinsi ulivyo wa kipekee.

Handbook 10 Icons
  • Familia (k.m mwana wa pekee, paka 2 )
  • Marafiki:
  • Mambo uyapendayo:
  • Malengo ya Taaluma
  • Elimu:
  • Maadili:
  • Hulka:
  • Mtindo wako

Lengo

Kuwapa washiriki moyo wa kuota ndoto, kuweka malengo ya baadaye na kutambua kile wanachohitaji kufanikisha malengo hayo.

Usuli

Miaka ya ujana ni wakati wa kutafuta umuhimu wa maisha na kile maisha yatakachokupatia. Ni muhimu kwa vijana kufahamu malengo na ndoto zao na kile kitakachowagharimu kuzifanikisha. Sisi sote tuna ndoto, lakini kama hatuchukui hatua zozote zitasalia kuwa ndoto tu.

Kujifahamu kuwa wewe ni nani, jinsi unavyojifunza, nguvu zako, na vipaji vyako kutakusaidia kufika mbali katika kufanikisha malengo yako.

Jambo kuu ni kuyaandika malengo na ndoto zako kwenye daftari kisha kuchunguza jinsi unavyoweza kuzifanikisha kihalisi – hata kama ina maana kuchukua hatua moja kwa wakati mmoja kuelekea lengo lako. Kumshirikisha lengo hilo mtu mwengine na huyo mtu akakutia moyo wakatindoto yako inavyoendelea kuanza kutimilika mbele yako, utasikia furaha waisikiayo watu wenye mafanikio.

Vijana walio na mipango ya kuafikia ndoto zao – na wana watu wanaowaunga mkono kufanya hivyo - wana uwezekano mkubwa wa kuafikia ndoto zao badala ya kuhatarisha ndoto hizo kwa kujihusisha na kukidhi tamaa ya mwili ya muda mfupi.

Activities Icons

SHUGHULI MUHIMU
Zoezi 1: Lenga na Upige Risasi

Blank Icons

Lengo

Kuonyesha umuhimu wa kuweka malengo.

Mahitaji

  • Magazeti
  • Sanduku tupu

Maagizo

1. Andaa mapema bila ya ufahamu wa washiriki, sanduku tupu, lililowekwa kwenye kona moja ya chumba. 

2. Mkabidhi kila mshiriki sehemu ya gazeti. Waambie kila mmoja wao, kurarua gazeti katika sehemu tatu kisha waikunje iwe mipira mitatu.

3. Waombe washiriki kuchukua mpira mmoja wa karatasi “na kuutupa baada ya kuhesabu hadi tatu”. Utatarajia kuona mipira ya karatasi ikitupwa pande tofuati.

4. Waombe washiriki kuchukua mpira wa pili na “kuutupa mbele baada ya kuhesabu hadi nambari tatu”.

5. Hatimaye, weka sanduku tupu mbele ya washiriki na uwaombe kuchukua mpira wa tatu na kuutupa ndani ya sanduku tupu baada ya kuhesabu hadi tatu.

Instructions For The Facilitator Icons

Washirikishi hawapashwi kutoa maagizo zaidi ya yale yanayohitajika kutolewa. Mpira wa karatasi wa kwanza – tupa”, mpira wa pili – “tupa mbele”, mpira wa tatu – “tupa kwenye sanduku tupu”.

Blank Icons

6. Waeleze washiriki kwamba kuwa na malengo ni sawa na kujua ni wapi pa kulenga mpira wa karatasi. Iwapo hawana malengo na hawana mpango wa kuyatimiza, huenda wasifanikiwe kupata kitu chochote mwishoni (kama mpira wa kwanza). Hata hivyo iwapo watachukua muda kuweka malengo yaliyo wazi wana uwezekano wa kuyafikia ama kuwa karibu na kuyafikia (mpira wa tatu).

Slides Icons
  • “Iwapo hutalenga chochote, hutapata chochote kila wakati.” –hajulikani
Activities Icons

Zoezi 3:
Ota Ndoto kubwa. Fikiria kwa Busara

Blank Icons

Lengo

Kuwasaidia washiriki kuanza kufikiria kuhusu siku zao za baadaye na kuanza kutekeleza mambo yatakayowafikisha wanapotaka.

Mahitaji

  • Kijitabu cha mwanafunzi cha mazoezi
  • Kalamu ya mate/Kalamu ya wino
  • Muziki wa kuliwaza na unaotuliza

Maagizo

1. Uliza:

  • Ndoto ni nini kwako?
  • Nini baadhi ya vikwazo ambavyo vinaweza kuzuia kufikia ndoto zetu?
Slides Icons

2. Uliza washiriki ina maana gani kuwa na NDOTO KUBWA

  • Huanza na shauku
  • Ni halisi
  • Itahitaji kuifanya kwa bidii
Blank Icons

3. Uliza washiriki maswali haya ili waweze kufikiria:

  • Ni kitu gani ambacho hujawahi kufanya lakini umekuwa ukitaka kukifanya?
  • Unataka kuwa wapi miaka kumi ijayo?
  • Iwapo pesa sio swala kwako ungependa kufanya nini maishani?
Handbook 12 Icons

4. Uliza washirki kurejea kwenye vitabu vyao na kuandika kile ambacho wangependa kutimiza kwa wakati ujao. Vijana wengine huenda wakaogopa kuelezea ndoto zao kwa kuhofia kufanyiwa dhihaka ama mzaha.

5. Kuandika husadia kuhuisha ndoto zao mawazoni na pia kwenye mioyo yao. Himiza washiriki kuwa mahususi iwezekanavyo kuhusu malengo yao. Wape washiriki dakika 7 – 10 kuandika majibu yao wakianza na malengo ya kipindi cha muda mfupi (mwaka mmoja) na kuendelea hadi malengo ya muda mrefu (miaka 10) ukitoa mifano inayuhusu maisha yako ili kuwapa moyo. Cheza muziki wa mandharinyuma kwa sauti ya chini unaowatuliza washiriki.

Uliza maswali haya ili kuwasaidia washiriki kuzingatia athari za nje kwenye ndoto na malengo yao:

  • Iwapo niko kwenye mahusiano na mtu wa jinsia tofauti sasa, huyu mtu anaunga vipi mkono ama kutounga mkono malengo na ndoto zangu?
  • Je, marafiki zangu wanajenga mazingira mazuri kwa ndoto na malengo yangu, kama sivyo, je ninahitaji kufanya mabadiliko gani?
  • Je, ninajihusisha na tabia yoyote ya hatari ambayo inaweza kunizuia kufikia ndoto na malengo yangu?

Kwa mfano msichana ambaye angependa kuwa tabibu wa mifugo ama mwalimu, akipata mimba shuleni itamrudisha nyuma ama kukatiza masomo yake na huenda asifanikishe ndoto yake.

6. Kwa mfano msichana ambaye angependa kuwa tabibu wa mifugo ama mwalimu, akipata mimba shuleni itamrudisha nyuma ama kukatiza masomo yake na huenda asifanikishe ndoto yake.

Slides Icons
  • Baada ya washiriki kuandika chini malengo yao, waulize wayatathmini -malengo yao ya mwaka mmoja kulingana na utaratibu wa S.M.A.R.T, na kufanya marekebisho yanayohitajika kwenye vitabu vyao:
  • Specific/mahususi - je unajua kile unachotaka kuafikia? Je, umeelezea kikamilifu? Kwa mfano, lengo la kimsingi – Nataka kuwa na afya nzuri vs lengo maalum - nataka kula lishe bora na kuhakikisha chakula changu kina protini, mboga za majani na matunda.
  • Measurable/Linaloweza kupimwa – Je, unaweza kutathmani maendeleo yako? Attainable/Linayoweza kutimizwa – je lengo hili linaweza kutimizwa kwa sasa?
  • Relevant/ Ni la maana– Je, lengo lako linakwenda sambamba na na kile unachotaka maishani?
  • Time-sensitive/Muda– Je, umeweka tarehe ya kukamilisha?

Zoezi hili linaweza likafanywa kwa makundi madogo au watu wawili huku kila mshiriki akitathmini malengo ya rafiki yake..

Blank Icons
  • “Hatari kubwa kwa wengi wetu sio eti tunalenga juu sana na tunakosa, bali tunalenga chini sana na tunapafikia,” – Michelangelo, Karne ya 16 msanii, Mtaliano
Going Deeper Icons

Kwenda Ndani Zaidi

Handbook 13 Icons

Wakati mwingine ni vigumu kufikiria malengo na ndoto kwa sababu vijana bado wako kwenye safari hii ya kujitambua. Orodha ya Maslahi ya Uholanzi itawasaidia kupima yale wanayoyapenda, kuchunguza kazi gani wanaipendelea na waifuatie, na kuzingatia mipango yao ya baadaye. Kujua maeneo yao wanayoyapenda kutawasaidia kufanya mpango sahihi. Wahimize kutumia zana hii. Inatoa ripoti ya kina ya maana ya alama zao, kile kitakachowasaidia kwenye kufanya maamuzi sahihi kuhusu kazi watakayoifanya.

Orodha ya Maslahi

Jua alama yako ya Maslahi ya NA na kiungo hiki cha tathmini.

Activities Icons

Zoezi 3:
Vizuizi vya Malengo

Handbook 14 Icons

Lengo

Inaweza isiwe rahisi kufikia malengo yetu lakini inawezekana. Waombe washiriki waorodheshe vikwazo mahususi vya malengo yao kwenye vitabu vyao. Baada ya hapo, washiriki wanapaswa kuafikiana na vikwazo chini ya mojawapo ya kategoria tatu zinazopatikana katika kitabu chao cha mazoezi: Tabia Hatarishi, Kasoro za Tabia au Mazingira. Mifano ya vikwazo kwa malengo yao inaweza kuwa:

Tabia Hatarishi

Kunywa pombe na kuendesha gari, ngono nje ya ndoa, kutumia dawa za kulevya, kuzagaa nje sana (bila kufanya kazi), kuingia kwenye mapigano, kuvuta sigara au kuvuta bangi.

Slides Icons

Kukosa Tabia Nzuri

Kukosa heshima, kukosa uaminifu, kutowajibika, ubinafsi, kutokuwa na fadhili, mvivu.

Mazingira

Matatizo ya afya ya muda mrefu, wazazi hawawezi kumudu “vitu vya ziada”—ni mahitaji ya kimsingi tu, mzazi akipoteza kazi, kuonewa shuleni, wazazi wakiachana.

Zoezi hili linafaa kufichua kuwa hali nyingi hazichangii vizuizi vingi. Ijapokuwa hali huwa hazizuiliki, tunaweza kuamua jinsi ya kukabiliana na hali hizo kwa mienendo yetu. Watu ambao wanaweza kuangalia kihalisi jinsi vikwazo vinavyoweza kuzuia ndoto zao, hujiandaa vizuri kubuni mipango mbadala na kuendelea kusonga mbele katika maisha yao.

Blank Icons
  • “Huwezi kumzuia ndege kuruka juu ya kichwa chako, lakini unaweza kuhakikisha kuwa hajengi kiota kwenye nywele zako.” – Dk. Martin Luther King
Take Home Activity Icons

Zoezi la Nyumbani:
Mpango wa kutekeleza

Blank Icons

Taja vitendo ambavyo unaweza ukachukua kusaidia kufanikisha malengo yako ya siku za baadaye. Mifano ni pamoja na kuepuka mahusiano ambayo yatakutatiza kufikia malengo yako, kufanya bidii kwenye masomo, kujitolea kufanya kazi kwenye jamii na kudumisha afya.

Kutafuta watu kadhaa wakusaidie (wazazi,marafiki, mtu mzima anayeamika, mchungaji wa vijana) ambao watakuhimiza kufikia ndoto na malengo yako. Andika majina ya watu hawa kwenye kitabu chako.

Lengo

Washiriki watahakiki sifa ambazo zinajenga tabia nzuri na kuchunguza tabia zao wenyewe kwa kufanya mtihani.

Usuli

Tabia sio kitu unachozaliwa nacho. Ni kitu unachokijenga. Mahusiano mema yanajengwa kwa misingi ya tabia njema kama vile heshima, uwajibikaji, uaminifu, fadhili na kujithibiti. Tabia njema inahitaji tu uamuzi kuwa nayo na sio vigumu. Tabia njema inasaidia kushinda changamoto na hata hali ambazo zinaweza kutuzuia kufanikisha ndoto na malengo yetu. Kimsingi tabia ndio kichocheo cha ufanisi wa mtu.

Activities Icons

SHUGHULI MUHIMU
Zoezi: Mtihani wa Tabia

Blank Icons

Lengo

Kuwawezesha kuzitambua tabia zao wenyewe.

Mahitaji

  • Ubao mweupe/ chaki
  • Kitabu cha mwanafunzi cha mazoezi
  • Kalamu ya mate/Kalamu ya wino
  • Chaki
  • Muziki wa mandharinyuma unaotuliza

Maagizo

1. Waombe washiriki kuorodhesha tabia nyingi nzuri kuanzia herufi A, hadi herufi Z.

Instructions For The Facilitator Icons

IKama hii program haiwasilishwi kwa lugha ya kiingereza basi washiriki na waorodheshe sifa 10 za tabia nzuri].

Slides Icons

Mifano ya sifa za tabia nzuri:

  • Kuthibitisha, Kujitolea, Bidii, Ukamilifu, Heshima Kuwajibika Subira Wema, Huduma Huruma Uaminifu Uadilif.
Handbook 15 Icons

2. Ili kusaidia washiriki kuanza kufikiri kuhusu tabia zao, uliza: Kwenye mizani ya sifa za tabia hizo uko wapi?

3. Wape washiriki dakika 10 kukamilisha mtihani wa tabia kwenye vitabu vyao Weka muziki mandharinyuma kujenga mazingira matulivu.

4. Cheza muziki wa kutuliza chinichini ili kuunda hali ya utulivu.

5. Wakikamilisha, washiriki waorodheshe viwango vya alama walizopata ili kukadiria tabia zao.

6. Waulize washiriki zipi zilikuwa sifa zao tatu kuu kisha uwaafiki.

7. Wasaidie washiriki kutathmini tabia zao tatu bora, uliza “Marafiki zako wanaweza kusema kuwa una hizo tabia?”

8. Waombe washiriki kuzingatia ni tabia gani ambayo wangependa kuboresha na kufanya tena huo mtihani baada ya miezi kadhaa ili waone kama wameimarika..

Jaribio la Hulka

Kamilisha “Mtihani wa Urafiki” mtandaoni kwa kiungo hiki kiungo hiki cha tathmini.

Kuwa na Tabia Nzuri kuna maana gani?

Handbook 18 Icons

KICHWA - KUFAHAMU mazuri

MOYO - KUHISI kilicho kizuri

MIKONO - Kutenda yaliyo mema

Fa Unit 1 Good Character
Slides Icons

Tunajengaje tabia nzuri?

Fanya tunavyosema

Pana haja kuwa na uwiano kwa kile tunachojua ni kizuri, hamu yetu ya kufanya mema (kujisikia vizuri) na kutenda mema.

K.m, tumefundishwa kuwa ni vyema kuwapa watu wakongwe ama wanawake wajawazito wakae kwenye viti ndani ya magari ya abiria ya umma. Huenda tukahisi vibaya kuwa mtu mkongwe ama mjamzito anasimama kwenye safari kwenye basi ama treni. Lakini kile kitakachothibitisha iwapo tuna tabia nzuri ni iwapo tutampatia kiti chetu.

Fanya yawe mazoea

Mazoea ni uwanja wa vita vya kila siku dhidi ya tabia. Fanya mazoea ya kutenda yale yanayoonyesha tabia njema kama vile, subira, heshima na fadhili, haitapita muda utafahamika kuwa mtu mwenye sifa hizo.

Blank Icons
  • “Tabia huenda ikaonekana wakati wa matukio makuu, lakini hujengwa katika mambo madogo” – Phillips Brooks
Share A Real Life Story Icons

Shiriki maisha halisi ya watu ambao:

Walioshinda hali mbaya (mazingira) kupitia nguvu za tabia zao, kwa mfano,

  • Nic Vujicic alizaliwa Desemba 4, 1982, akiwa na ugonjwa wa nadra wa tetra-amelia. Mikono yote miwili haikuwepo kuanzia kwenye mabega na hakuwa na miguu miwili japo alikuwa na makanyagio mawili. Kando ya ulemavu huu wa kimwili, alikuwa na afya njema.
  • Shuleni, Nic alidhulumiwa na akaanza kufikiria kujitia kitanzi. Hata hivyo, mambo yalibadilika alipogundua kuwa hakuwa peke yake aliyezongwa na ulemavu mbaya na kwamba mafanikio yake yalikuwa msukumo kwa wengi. Hatimaye alianzisha shirika lisilo la kibiashara, Life Without Limbs (Maisha Bila Viungo)
  • Baada ya kufuzu kutoka chuo kikuu na shahada mbili za Uhasibu na Mipango ya Fedha, Nic alianza kusafiri akitoa mihadhara na kuzungumzia masuala yanayowakabili vijana. Yeye huzungumza kwenye mikutano ya mashirika makubwa.
Instructions For The Facilitator Icons

Washirikishi wajumuishe hadithi zao binafsi au za washindi wa jumuiya.

Tabia nzuri zinazoonyeshwa ukikabiliwa na changamoto za kila siku kama vile kudhulumiwa na shinikizo za marafiki, kwa mfano:

  • Katika warsha yangu ya mwisho, tunapowa patia zawadi ya peremende washiriki, tuligundua kuwa wanafunzi walitupa karatasi za peremende sakafuni baada ya kuzila. Lakini kulikuwa na huyu mwanafunzi mmoja ambaye alibaki nyuma na kuokota karatasi hizo na kuzitupa kwenye pipa la takataka. Hakuna aliyemwomba kufanya hivyo; hakuna aliyekuwa akimwangalia; hakuna mtu mwingine aliyefanya hivyo. Alifanya kilichokuwa sawa na haki, bila kujali.
Take Home Activity Icons

Zoezi la Nyumbani:
Tulia. Cheza Tena. Cheza haraka

Blank Icons

Sifa za tabia yako huonekana kwenye matendo yako. Fikiria jinsi ambavyo umeonyesha baadhi ya tabia hizo.

Tulia

Tambua ama elezea sifa tatu kuu za tabia yako baada ya majaribu.

Cheza tena

Jaribu kukumbuka matukio matatu yaliyopita ambapo ulionyesha ama kudhihirisha sifa hizo.

Cheza haraka

Piga picha ya watu waliokusanyika kwenye ibada ya mazishi yako. Ungependa watu hawa waseme nini kukuhusu wewe?

Lengo

Kuwasaidia washiriki kuelewa umuhimu wa marafiki na jinsi wanavyoathiri uamuzi na matendo, halikadhalika kutambua sifa za urafiki wa kweli ili waweze kuchagua marafiki kwa hekima.

Usuli

Kubalehe ama kuvunja ungo ni wakati muhimu ambapo shinikizo kutoka kwa marafiki huwa na athari kubwa kwa vijana.

Sote tunahitaji marafiki. Marafiki hushiriki wakati mzuri, hutusaidia kihisia kupitia wakati mbaya, hutusaidia kujua maeneo ya upungufu wetu na hutuhimiza kuimarika. Urafiki ni kiungo muhimu cha ustawi. Hutoa nafasi kwa vijana kujitambua, kujisikia kukubalika na kukuza hali ya kuhusika. Hata hivyo urafiki unaweza kukuletea uchungu mwingi.

Ni muhimu kutambua kuwa kuna shinikizo hasi ama mbaya na vilevile kuna zile nzuri. Vijana wanastahili kujifunza kutofautisha kati ya hizo mbili ili wafanye uamuzi bora katika maisha.

Activities Icons

Zoezi1: Rafiki Mwema ni Yupi?

Blank Icons

Lengo

Kutafakari juu ya sifa za tabia zilizo kwenye ushawishi chanya.

Mahitaji

  • Kitabu cha mazoezi cha mwanafunzi
  • Kalamu ya mate/Kalamu ya wino
  • Muziki wa mandharinyuma unaotuliza
Handbook 20 Icons

Maagizo

1. Waulize washiriki kutazama orodha ya maelezo ya marafiki zao kwenye kitabu na 😠 kuchora iwapo wanadhani 🤩 kama rafiki mzuri.

2. Maelezo yanaelezea rafiki MBAYA, na J iwapo yanaelezea rafiki MZURI. Mwisho wa zoezi , soma vielelezi 12 kutoka kwenye orodha kamili na waombe washiriki majibu yao kwa kunyoosha mikono inapoeleze rafiki mzuri. Vinginevyo, unaweza kuwaomba washiriki kusimama, wakati inaelezea rafiki mzuri na kukaa wakati inaelezea rafiki mbaya.

Orodha ya vielelezi:

  1. Hunikosoa kila wakat 😠
  2. Hunifariji nikivunjika moyo 🤩
  3. Tunashiriki riba sawa 🤩
  4. Hujisifia kila wakati 😠
  5. Hujali usalama wangu 🤩
  6. Hunidhihaki ninapokataa kufanya anayotaka nifanye 😠
  7. Hunisengenya 😠
  8. Huwa tunaandamana kuburudika 🤩
  9. Hutangaza uvumi kunihusu 😠
  10. Ana hamu ya kujua kinacheondelea maishani mwangu 🤩
  11. Hunishirikisha siri zake 🤩
  12. Haweki ahadi zake 😠
  13. Hutenga muda wetu wa pamoja 🤩
  14. Hunisaidia nikiwa na shida 🤩
  15. Hutukana familia na marafiki zangu 😠
  16. Huchukua vitu vyangu bila ya ruhusa 😠
  17. Ni mtu ninayeweza kucheka naye 🤩
  18. Hunidhalilisha mbele za watu 😠
  19. Hulalamikia katika kila jambo 😠
  20. Ni mtu ninayeweza kumshirikisha siri zangu 🤩
  21. Ni mtu asiye mwaminifu 😠
  22. Huchelewa saa moja kila tukipanga kukutana 😠
  23. Hunipongeza kwa ufanisi wangu 🤩
  24. Atanambia nikikosea 🤩
  25. Anakubali akifanya makosa 🤩
  26. Huenda kinyume yangu nikiwa sipo 😠
  27. Huniita wakati anapohitaji kitu kutoka kwangu 😠
  28. Anaweza kusema kile ninachofikiria kabla sijamwambia 🤩
  29. Hutongoza msichana/mvulana ninayempenda mbele yangu 😠
  30. Hunihimiza kufanya vyema 🤩
Blank Icons

3. Uliza washiriki:

  • Kutoka kwenye orodha iliyosomwa, kipi ambacho unakichukia zaidi?
  • Je, umewahi kuwatendea hivyo marafiki zako?
  • Je, ungependa marafi zako wakutendeeje?
  • Je, wewe unawatendea hivyo marafiki zako?
Share A Real Life Story Icons

4. Shiriki kuhusu rafiki yako mwema na sababu gani unamchukulia hivyo.

Going Deeper Icons

Kwenda Ndani Zaidi

Je, una marafiki wa kweli? Wataje.Ni nini huwafanya wawe marafiki wa kweli kwako?
Ninawezaje kujenga urafiki utakaodumu?

Nini Hufanya Rafiki?

Kamilisha “Mtihani wa Urafiki” mtandaoni kwa kiungo hiki kiungo hiki cha tathmini.

Slides Icons

Aina ya Marafiki

Handbook 22 Icons

Wa kijuu juu, Unaofahamu: Watu unaowajua kwa sura, lakini huwezi kushiriki nao nje ya shule

Kikundi Chako: Watu unaoshinda nao unahisi kuhusishwa nao.

Marafiki wa dhati: Watu unaowaita marafiki bora na wa milele (BFF)/ndugu wanajua kila kitu “kinachokuhusu”

Urafiki haujengeki tu kwa usiku mmoja. Kwa “viungo” sahihi, uhusiano unaweza kuhama kutoka kuwa wa kijuu juu hadi ukawa ule wa karibu-wa dhati.

Nini kinajenga Urafiki wa Kweli?

  • “Rafiki mwema hukudunga mbele,” – Oscar Wilde
  • “Rafiki mwema anaweza kukufahamisha tatizo lako mara moja. Huenda asionekane mwema baada ya kukufahamisha,” – Arthur Brisbane

Rafiki wa kweli ni yule ambaye hakufichi chochote na ni mkweli kwako na wewe ni mkweli kwake. Lakini kuwa na rafiki mwema kunaanza sisi tunapokuwa wema, hapo ndio urafiki mzuri unajengwa.

Going Deeper Icons

Kwenda Ndani Zaidi

Handbook 22 Icons

Jinsi ya Kujenga Urafiki

Tabia

Sifa bora za urafiki ni uaminifu na ukweli. Unafaa kuwa na athari nzuri kwa marafiki zako.

Uamuzi mwema

Unahitaji uamuzi mwema kutambua kati ya rafiki mzuri na yule mbaya na kujua namna ya kuhusiana nao ipasavyo.

Subira

Mahusiano mema huchukua muda na juhudi kujengeka. Urafiki unaopitia misukosuko ya maisha unakuwa na uthabiti.

Ujasiri

Unahitaji ujasiri kujenga marafiki na kukabiliana na kukataliwa na wengine. Wakati mwingine unahitaji ujasiri kuzungumzia mambo mabaya yanayohitaji kurekebishwa.

Handbook 24 Icons

Urafiki 101 – Kufanya urafiki wako uwe thabiti

Kumbuka.Kumbuka mambo muhimu kuhusu rafiki zako kama vile, kile wanachopenda, wasichopenda, siku yao ya kuzaliwa n.k.

Usijifanye/Uwe mkweli.Kuna marafiki wa kijuu juu na kuna marafiki. Marafiki wana uhusiano mzito. Kuwa muwazi na rafiki yako-Usijifanye kuwa mzuri mbele yao, na huku nyuma unawasengenya.

Uwe mwelewaji.Msikilize rafiki yako hata kama mnagombana, kabla ya kuanza kujitetea. Jaribu kuangalia mambo kwa mtazamo wake. Siku zote kuna kutoa na kupokea katika urafiki.

Kuwa nyeti.Usijifkirie wewe tu wakati wote hata ukashindwa kutambua rafiki yako anapokuwa hajisikii vizuri au ni mgonjwa. Pia uwe mwangalifu sana mnapokuwa na maongezi yanayogusia hisia kama vile wapenzi wenu na hali za familia..

Usiwe kupe.Usimkwamilie rafiki yako masaa 24/ siku 7 kama kupe, mpatie rafiki muda wa kuwa peke yake na wewe upate kuwafahamu marafiki wengine.

Uwepo.Usiwe kupe, lakini pia usipotee kabisa. Mara kwa mara ili uonyeshe kwamba unawajali marafiki zako, waandikie ujumbe mfupi, shiriki nao kwa muda, hata wapatie zawadi. Tumia ujumbe wa simu ama barua pepe kama njia ya mwisho –kukutana uso kwa uso ni bora wakati wote. Tenga muda wa kuwa na rafiki yako wakati wa mema na wakati wa mabaya, hata kama ni wewe tu uliyebakia naye, kwa maana wakati huo ndipo anapokuhitaji zaidi.

Take Home Activity Icons

Zoezi la Nyumbani:
Mtihani wa Urafiki

Handbook 23 Icons

Tambua wewe ni rafiki wa aina gani kwa kujibu maswali machache kuhusu urafiki. Nakili matokeo. Alama 40 inaonyesha kuwa wewe ni rafiki wa kweli katika hali zote. Alama kati ya 25 – 39 inaonyesha kuwa wewe ni rafiki mwema lakini kuna nafasi ya kuboresha zaidi. Alama kati ya 15 – 24 inapendekeza kuwa una kibarua cha kujifunza kuweka marafiki mbele kabla ya maslahi yako. Alama chini ya 15 inaonyesha kuwa una kibarua kikubwa zaidi cha kuboresha mbinu zako za urafiki.

Kwenda Dijitali

Kamilisha “Mtihani wa Urafiki” mtandaoni kwa kiungo hiki kiungo hiki cha tathmini.

Blank Icons

Ushawishi wa Marafiki

Slides Icons

Shinikizo za Marafiki

Kila mtu anataka kuhisi kuwa yumo kundini — yumo ndani. Unataka kuhisi unakubaliwa na watu wanaopenda mambo ambayo na wewe unayapenda. Kabla ya kufanya kitu, mara nyingi huwa tunajiuliza, “Marafiki zangu watafikiriaje?”

Handbook 28 Icons

Je, Shinikizo za Marafiki kila mara huwa ni mbaya?

Shinikizo Chanya la Warika Lako:

  • Kuhimizwa kufanya jambo ambalo hukuwa na ujasiri wa kulifanya.
  • Kushawishiwa USIFANYE jambo ambalo huenda likawa baya kwako.
  • Kutiwa moyo kufanya jambo zuri pamoja.

Shinikizo Hasi la Warika Lako:

  • Kusukumwa kufanya jambo ambalo hutaki.
  • Kushawishiwa kufanya jambo ambalo ni kinyume cha maadili yako na imani yako Kushinikizwa kufanya jambo ambalo unafahamu ni baya ili.
  • Kuonyesha ujasiri wako.
  • Fahamu: Shinikizo la rika linaweza kujitokeza kwa njia ya kukataliwa, kudhihakiwa ama hoja. Kwa hivyo ni muhimu kufikiria iwapo uko kwenye shinikizo chanya au hasi. Marafiki ambao unashinda nao wataamua iwapo unaweza kuyashikilia au kuyaeleza maadili yako.
Share A Real Life Story Icons

Shiriki hadithi za kweli ambazo vijana wanaathiriwa na marafiki kwa mfano:

  • Mwanafunzi mwenzangu alikuwa akiongoza darasani, lakini matokeo yake yalianza kudorora kwa kuwa alikuwa anashinda na makundi mabaya na kuhusika kwenye tabia hatarishi. Ilifikia wakati ambao alipaswa kubadilisha darasa kwa kuwa matokeo yake yalishuka kupita kiwango cha chini.
Activities Icons

Zoezi 2: Kusalia thabiti

Blank Icons

Lengo

Kuonyesha umuhimu wa kukumbatia maadili imara ya kibinafsi.

Mahitaji

  • Kiti
  • Watu 2 wa kujitolea wa jinsia moja, haswa wa kiume

Maagizo

1. Mmoja wa waliojitolea asimame juu ya kiti na mwengine kando yake kwenye sakafu.

2. Waelezee kuwa yule aliye juu ya kiti anawakilisha mtu mwenye viwango vya juu kimaadili kama vile, mwaminifu, anayejali, mnyenyekevu, mwerevu, anayewajibika na yuko tayari kuwasaidia wenzake wakati wote. Upande mwingine yule aliye kando yake anawakilisha mtu mwenye viwango vya chini kimaadili, ambaye huwahimiza wenzake kushiriki vitendo vibaya wala hawaheshimu watu wengine.

3. Waambie waliojitolea kuwa ukihesabu hadi tatu, waanze kuvutana, yule aliye juu ya kiti aanze kumvuta mwenzake na yule aliye chini aanze kumvuta aliye kwenye kiti. Itakuwa rahisi kwa mshauri aliye chini kumvuta mwenzake aliye juu ya kiti.

4. Hii inaonyesha kuwa ni rahisi kuathiriwa na kundi baya, lakini inachukua juhudi kubwa kuwaathiri watu kufikia viwango vya juu.

Ni muhimu kuwa na malengo wazi na kuzungukwa na watu wataokusaidia kushika hivi viwango vya juu kimaadili. Mtu aliye weka viwango si rahisi kushawishiwa na shinikizo za marafiki.

Activities Icons

SHUGHULI MUHIMU
Zoezi 3: Nani ataleta Utofauti?

Blank Icons

Lengo

Kuhimiza washiriki kuwa gurudumu la mabadiliko yanayohitajika. (Ushawishi Chanya).

Mahitaji

  • Chupa mbili (takriban millilita 500 kila moja)
  • 20 Rangi nyekundu ya chakula
  • Bleach kioevu isiyo na rangi
  • Kifaa cha kumwagia (Dropper)
  • Mtu mmoja wa kujitolea

Maagizo

1. Iandae mapema: Chupa mbili zilizojazwa nusu; moja ina maji, nyingine ina bleach.

2. Inua ile chupa yenye maji na uwaelezee washiriki kuwa chupa hiyo inawakilisha mtu asiye na viwango.

3. Ongeza tone la rangi nyekundu ya chakula kwenye chupa iliyo na maji nauitikise, ukielezea washiriki kuwa rangi ya chakula inawakilisha athari mbaya zinazomkabili kijana, km, shinikizo ya kushiriki ngono, kuvuta sigara, dawa za kulevya, pombe, kutoroka darasani, kutumia lugha chafu, nk. Iwapo mtu hajaweka viwango kuhusu mambo muhimu maishani, atakuwa kama maji yanayochukua rangi yoyote- ataathirika kwa urahisi.

4. Inua chupa yenye bleach kioevu lakini usifichulie washiriki kuwa imejazwa bleach kioevu badala ya maji. Waeleze washiriki kuwa chupa hii inawakilisha mtu aliyeweka viwango vya juu na malengo maishani. Ongeza tone la rangi nyekundu ya chakula kisha utikise chupa hiyo. Kioevu hicho hakitachukua rangi nyekundu. Hii inawakilisha mtu ambaye ana viwango vyake na kuwa hawezi kuathirika kwa urahisi.

5. Taratibu mwaga maji yaliyo na rangi nyekundu kwenye maji yaliyo kwenye chupa yenye bleach. Waombe washiriki waangalie jinsi maji ya rangi nyekundu hayawezi “kuchafua” “maji” safi. Waelezee kikundi kuwa mtu mwenye viwango anaweza kuhimili shinikizo la watu wa rika lake.

6. Mwishowe mimina chupa iliyo na bleach kwenye chupa yenye rangi nyekundu. Waeleze kwamba sio tu mtu mwenye viwango anaweza kuhimili shinikizo la rika, lakini pia anaweza kuathiri marafiki zake kwa uzuri. Wahimize washiriki wawe wale wanaowashawishi vyema wenzao na sio wale wanaoshawishika.

Slides Icons

Athari ni ya pande zote.

Badala ya kuathiriwa vibaya na wengine, unaweza kuwashawishi na kuwatia moyo wengine kufanya mambo mazuri na sahihi.

Instructions For The Facilitator Icons

Mwezeshaji: Baadhi ya chapa za bleach hufanya kazi vizuri zaidi ya nyingine, hivyo mshirikishi anafaa afanye majaribio ama uchunguzi kabla ya majaribio yenyewe.

Activities Icons

Zoezi 4: Ieleze. Iuze. Isogeze.

Blank Icons

Lengo

Kuonyesha jinsi ya kuhimili shinikizo la rika.

Mahitaji

  • Kadi zenye hali mbalimbali(1 kwa kila kundi la washiriki 3-5)

Maagizo

1. Kwenye vikundi vidogo, waombe washiriki wafikirie na kujadili hali tofauti hapo chini, kwa kutumia mbinu ya Ieleze. Iuze. Isogeze.

Small Group Icons

Kwenye vikundi vidogo, waombe washiriki wafikirie na kujadili hali tofauti hapo chini, kwa kutumia mbinu ya Ieleze. Iuze. Isogeze.

Instructions For The Facilitator Icons

Badilisha hali ama taswira kuwakilisha mambo yanayofanyika kwenye kijiji ama jumuiya yako.

Blank Icons

Matukio :

  • Rafiki yako alisahau kusoma kwa ajili ya mtihani. Anakuomba umsaidie kwa kukaa karibu naye ili aone majibu yako.
  • Mtu anakushawishi kwa kukupatia pombe kwenye sherehe na marafiki zako waliokuzunguka wanaanza kulewa.
  • Rafiki yako wa kiume/kike anapendekeza uende naye nyumbani kwao kwa kuwa hakuna mtu yeyote na unajua anataka mshiriki ngono.
  • Rrafiki yako shuleni anatumia dawa za kulevya na anata ujiunge naye kutumia mhadarati.
  • Baadhi ya marafiki zako wanakutaka mtoroke shuleni mkaibe dukani badala yake.
  • Kikundi cha marafiki kinajumuika kusomea mtihani wa mwisho. Baada ya saa kadhaa msichana mmoja anatoa dawa za kusisimua mwili ili kuongeza nguvu.
  • Marafiki kadhaa mnakusanyika kwenda kuburudika. Baada ya burudani unagundua kuwa aliyeteuliwa kuwa dereva amelewa.
  • Rafiki yako wa kiume/kike anakualika nyumbani kwake baada ya shule. Anakuambia kuwa mama yake yuko nyumbani, lakini ukifika unakuta hakuna mtu.
  • Wewe na rafiki yako mko dukani pamoja. Unamuona rafiki yako akiingiza kitu mfukoni mwake.
  • Rafiki yako anataka kukuonyesha picha za ngono alizozipata kwa bahati mbaya kwenye mtandao akifanya utafiti wa zoezi lake la shuelni

2. Viagize vikundi viigize matukio hayo na majibu wanayoyapendekeza.

Ni muhimu kwetu kufahamu mapema kile tutakachosema kwa mtu anayejaribu kutushinikiza kwenye hali mbaya. Kila kijana ana fursa ya kukubali au kukataa maoni ya umati. Inabidi kuwa jasiri kwenda kinyume na umati, hasa inapokuwa ni wewe pekee yako usiyekubaliana nao. Katika kujifunza mbinu za kukataa kuna hatua tatu za kukumbuka. Katika kila hatua, kuna mapendekezo kadhaa ya watu kuelezea hoja zao.

Ieleze: Sema “hapana” na uwaeleze ni kwa nini.

  • Elezea sababu ya kukataa: “Sidhani.”ama “Hilo si wazo zuri. Je, waweza kufikiria jambo jingine?”ama “Sahau.”ama “Mimi simo, niko nje!”
  • Tumia shinikizo kinyume: “Siamini kuwa wataka nifanye hivyo!”ama “ Je, unanitania? Kwa nini nifanye hivyo?”
  • Sisitiza kwa mifano hai: “Yawezekana kuwa mraibu wa kuvuta sigara. Hapana ahsante. Sitaki kuanza.” Ama “nilisoma hadithi kwenye gazeti ambapo mtoto mmoja aligongwa na gari lililokuwa likiendeshwa na dereva mlevi. Sitaki kufa kwa njia hiyo; nitachukua teksi.”
Handbook 29 Icons

Iuze: Pendekeza njia mbadala..

  • Fanya Mzaha: “Afadhali niende kuona filamu. Mbali na hayo nilisikia kuwa pombe imejaa sukari. Ninakula chokoleti ya kutosha ili niongeze uzito.”
  • Tia Moyo: “Afadhali niende nyumbani kwangu niangalie filamu na marafiki. Zaidi ya hapo hekima uliyonayo wewe ni kubwa sana kutaka kunywa na kuendesha.”
  • Shinikizo kinyume: “Siwezi kuamini kuwa uliniomba nifanye hilo. Hungependa tukutane na marafiki zetu twende kunywa kahawa?”

Isogeze: Tekeleza mpango wako na uache mlango ukiwa wazi kwa yeyote kuingia.

  • Anzisha tena mjadala huo: “Naam, wacha nielewe vyema. Unataka niibe chupa ya pombe, ninywe nawe kisha niendeshe gari bila ya kukamatwa? Huu ni wenda wazimu Naenda kutazama filamu, ninywe kahawa, kisha nielekee nyumbani. Je unakuja?” (Ondoka na usiangalie nyuma.)
  • Sisitiza: “Jamaa nimewaambia kile nitakachofanya – je, mnakuja?” (Ondoka na usiangalie nyuma.)
  • Fanya mzaha: “ninafurahia kuwa mnajifanya kwamba mnao mpango na mawazo ya uenda wazimu, lakini mimi ninaenda kucheza mpira. (Ondoka na usiangalie nyuma.)

Jambo la muhimu ni kushikilia mpango wako na usishawishike. Ondoka na usiangalie nyuma.

Lengo

Kuwajulisha washiriki kuwa thamani yao haiamuliwi na kile wanachosema watu au jamii, bali kwamba wao ni watu binafsi.

Usuli

Kujenga utambulisho wa kijana ni mchakato mrefu. Bila kujua, vijana wengi huacha wengine wawambie wao ni akina nani; wanaruhusu kile wengine wanachosema kuwaathiri taswira yao binafsi. Hivyo wengi huishia kujichukia na hata kujihisi kuwa hawafai kitu. – “sio warembo wa kutosha, hawana nguvu za kutosha, si werevu wa kutosha, sio maalumu, hawastahili”.

Vijana walio na taswira nzuri ya ubinafsi wao hawategemei kuthibitishwa na wenzao. Wanajiamini utambulisho wao na wana uwezo wa kujithibiti wanapokosolewa kuhusu thamani yao. Wana uwezo mkubwa wa kuendelea kushikilia maadili yao licha ya shinikizo za vijana wenzao na athari nyingine.

Activities Icons

Zoezi 1: Noa bongo

Blank Icons

Lengo

Kila kijana hupitia mchakato mgumu wa kujitambua.

Slides Icons

Maagizo

1. Wasilisha “Fumbo la slaidi A” na washiriki wajaribu kulitatua.

Handbook 30 Icons
  • Mvulana anapashwa kuvusha mtoni, mbwa mwitu, kuku na gunia la mahindi.
  • Akitumia mashua, anaweza kuleta kitu kimoja tu kwa wakati mmoja.
  • Mbwa mwitu hawezi kuachwa pekeeyake na kuku, na kuku hawezi kuachwa peke yake na mahindi.

2. Suluhisho:

  • Vusha kuku mtoni na umuache upande huo.
  • Chukua mahindi ng’ambo ya mto na uyaache hapo, kisha umrudishe kuku.
  • Mwache kuku mahali ulipoanzia, na umvushe mbwa mwitu.
  • Mwache mbwa mwitu na mahindi, rudi umchukue kuku.

3. Kupitia maisha ya ujana ni kama kufumbua fumbo. Kutaka kujua sisi ni akina nani na iwapo ni wazuri vya kutosha, mwanzoni inaonekana kama haiwezekani na inaonekaana kuwa ngumu na masuala tata. Hata hivyo kwa subira, uvumilivu na mipango makini ya hatua-kwahatua tunaweza kufaulu kutatua masuala tata tunavyoendelea kukua.

Activities Icons

SHUGHULI MUHIMU
Zoezi 2: Hisia za Mtu Duni

Blank Icons

Lengo

Mashaka juu ya uthamani wetu ni kawaida lakini hayatufafanui.

Slides Icons

Maagizo

1. Weka slaidi ya “Je Unaweza ukatambua?”.

  • Ili kuwasaidia wanafunzi kutambua hisia za hali duni katika maisha yao na kutambua kwamba ni tishio juu ya kujistahi kwao. Waombe washiriki wachunguze mawazo ambayo yamepita akilini mwao katika wiki au mwezi uliopita.
Handbook 31 Icons

2. Mwisho wa zoezi, jumlisha alama zote na ufanye utafiti mdogo kuhusu majibu ya washiriki. Wahakikishie kuwa hawafai kuonyeshana majibu yao bali jumla ya sentensi zilizo wekewa alama.

Instructions For The Facilitator Icons

Badilisha sentensi zifuatazo ili ziangazie mambo yanayofanyika sana katika jumuiya ama eneo lako.

Blank Icons
  • Hakuna mtu anayenipenda.
  • Haijalishi nikienda shuleni leo; hakuna mtu atakayegundua kuwa sipo.
  • Niko peke yangu.
  • Watu wengine ni bora zaidi yangu.
  • Laiti ningelikuwa bora kama yule katika kucheza [weka michezo maarufu].
  • Nimeshindwa kila kitu.
  • Natamani aniangalie mimi badala ya rafiki yangu.
  • Mimi ni mnene.
  • Mimi ni mfupi sana.
  • Hakuna kitu cha kipekee juu yangu.
  • Mimi si mrembo vya kutosha.
  • Natamani ningetoweka ili nisichekwe tena.

3. Waeleze washiriki kuwa kila mtu katika kiwango fulani huhisi hivyo, haswa vijana, kwa sababu miili yao inapitia kipindi kikali cha mabadiliko. Lakini hisia hizi sio sawa na sio kweli.

  • “Hizi ni hisia za kuwa duni, ambazo zinaweza kuelezwa kuwa “kuhisi kushuka kwa umuhimu, thamani, au sifa.” – Merriam Webster
Slides Icons

Bonde la Kukosa Thamani

Blank Icons

Hisia kuwa sisi si bora vya kutosha inafananishwa na bonde lenye kina kirefu ambalo hutuingiza kwenye huzuni kila wakati..

Handbook 32 Icons

Tunaanguka bondeni iwapo:

  • Tutaruhusu maneno ya wengine/maoni kuathiri mtazamo wetu
  • Tunajilinganisha na wengine
  • Tunajaribu kutimiza matarajio ya wengine
  • Tunajikosoa sana tunaposhindwa

Sio makosa kutaka kuwa mtu mzuri ama kuwa na viwango vya juu, lakini tatizo huanza wakati tunapotaka “kuwafurahisha wengine”. Iwapo hatutaweza kukabili hali ya kushindwa, ni rahisi kuanguka ndani ya korongo la kukosa thamani.

Mfano:

Mbona ninahisi hivi?

  • Kimwili, mwili wetu unakua; kiakili tunakomaa na tunajifunza kufikiria wenyewe; hisia tunazohisi ni nzito.
  • Ni wakati ambapo hisia zetu zinakuwa makini kwa yale wengine wanayofikiria, wanayosema, na pia wanayohisi kutuhusu sisi. Kwa hivyo ni wakati ambapo tunaathiriwa kwa urahisi zaidi.
Slides Icons

Njia Mbadala uko Mbele!

Blank Icons

Kwa sababu watu wengi huingia kwenye korongo la kukosa thamani, inaonekana kama kawaida ya kila kijana. Lakini, hii sio njia ya lazima ya kufikia utu uzima. Unaweza kuiepuka iwapo:

Handbook 33 Icons

Utatambua kuwa hauko peke yako

  • Ukichukua muda na kuchunguza vijana wengine, utagundua kuwa ndani ya kicheko na tabasamu zao, wengi wanakabiliana na suala la thamani yao. Kila mtu anapitia mabadiliko hayo; hauko peke yako.

Kabiliana na Matatizo yako

  • Tumia muda kufikiria kinachokufanya ujihisi vibaya, kisha uviorodheshe kulingana na kiwango cha jinsi vinavyokutatiza. Kisha, chagua rafiki ambaye atakusaidia kuwajibika. K.m, iwapo huwa unakasirika mdogo wako akiazima vitabu vyako bila ya kukuomba ruhusa,unaweza ukazungumza na dada yako mkubwa na kumwomba akusaidie utulie ikitokea tena.

Fidia “udhaifu” wako

  • Sio kila mtu atakuwa mrembo ama mtanashati kuliko wote au kuwa na akili kuliko wote shuleni. Lakini kwa sababu wewe sio hivyo, haimanishi kuwa wewe sio mjuzi kwa jambo jingine. Shiriki kwenye mazoezi mbalimbali utambue mahali unapofanya vyema; yaweza ikawa ni kucheza vyombo vya muziki, mchezo ama hata tahajia. Punde utakapotambua, anza kufanya mazoezi ya kina; utagundua kuwa unapata ujasiri wa kujiamini kila wakati unapotekeleza jambo hilo.

Kuwa na marafiki wa dhati

  • Hakuna kitu kinachosaidia kuimarisha ujasiri kama kuwa na marafiki wa kweli ama wa dhati. Marafiki wa kweli hawajishiriki na wewe kwa kuwa u mrembo, mwerevu, ama tajiri; wanajumuika na wewe kwa sababu ya jinsi ulivyo.
  • [Imechukuliwa kutoka kwa Preparing for Adolescence, na Dk. James C. Dobson]
Activities Icons

Zoezi 3: Kujenga Kujithamini

Blank Icons

Lengo

Kuwasaidia vijana kutiana moyo na kuthamini upekee wao.

Mahitaji

  • Vikaratasi vidogo vya kuandikia

Maagizo

1. Waagize wanafunzi kuunda vikundi vya watu 3-4

2. Waombe washiriki waandike kitia moyo kimoja kwa kila kategoria:

Slides Icons
  • Malengo na Ndoto [k.m., ninaamini nitakuwa __ ” bora siku moja]
  • Tabia Njema [k.m., ninasimama na imani yangu kwamba “uaminifu ndio sera bora”]
  • Nguvu [k.m., napenda ukweli kwamba mimi ni mzuri katika sanaa / baiskeli / kuimba / hisabati]
Handbook 34 Icons

3. Waombe washiriki waandike kitia-moyo kimoja kwa kila mtu katika kikundi chao.

  • Kisha waulize:
  • Ulijisikiaje ulipotiwa moyo?
  • Ulijisikiaje ulipompatia mwingine kitia-moyo?

Hata kama hisia zetu za kuwa duni ni za kweli, hazitufafanui. Badala yake, hutufanya kuwa wa kipekee! Hebu tujifunze namna ya kutiana moyo na kuthamini upekee wetu.

Blank Icons

Hitimisho

Slides Icons

Mimi ni nani?

Wewe ni wa KIPEKEE – kama mwanamume au mwanamke -mzima, wa thamani, uliyeumbwa kwa ajili ya mahusiano yenye afya na matumaini ya siku zijazo!

Going Deeper Icons

Kwenda Ndani Zaidi

Handbook 35 Icons

Ni Sawa Kutokuwa Sawa.

Safiri kutoka kwenye kushikilia kwa shida na ufikie kwenye kushikilia kwa nguvu.

Mahitaji ya maisha ya ujana yanaweza kuwafanya wahisi wasiwasi, mkazo au hata huzuni. Kila mtu anapambana na ustawi wa kihisia na ni sawa kutokuwa sawa, wakati wote. Ni sawa kuhisi kila aina ya hisia na ni muhimu kukubali na kukubalina na hisia zetu.

Hisia chanya mara nyingi hupuuzwa katika safari yetu ya afya ya akili. Kiwango Chanya cha Ukadiriaji wa Hisia (PERS) ni dodoso jipya la kujiripoti kwa kupima hisia chanya katika watu wanaopambana na hisia zao.

Taarifa katika hati hii haikukusudiwa kuchukua nafasi ya ushauri wa kitaalamu wa matibabu, utambuzi au matibabu. Unapohisi kuelemewa, tafadhali wasiliana na mshauri au mtu mzima anayewajibika ili kukusaidia kushughulikia hisia zako.

Instructions For The Facilitator Icons

Afya ya Akili na Masuala Mengine Mazito
Wawezeshaji wanahitaji kufahamu upungufu wao wenyewe na wanashauriwa sana kuwaelekeza washiriki kwa vyombo au mashirika husika kwa ajili ya kuingilia kati zaidi na usaidizi katika masuala ya afya ya akili, unyanyasaji wa kijinsia, kutelekezwa, vurugu au masuala mengine makubwa ya familia.

Kiwango chako cha Ukadiriaji wa Hisia Chanya

Kamilisha “Mtihani wa Urafiki” mtandaoni kwa kiungo hiki kiungo hiki cha tathmini.

Going Home Icons

Kwenda Nyumbani

Maswali ya Majadiliano ya Mzazi/Kijana kwa Sehemu ya 1

Mzazi mpendwa,

Hakuna Majuto ® Sura ya 1, inasisitiza upekee na thamani ya mtu binafsi; umuhimu wa tabia njema kwa mahusiano yenye afya na kukabili siku zijazo kwa makusudi.

Maswali:

  1. Ni hali gani au matukio gani ambayo wewe (Kijana) unaona yatatokea katika miaka michache ijayo ambapo ni muhimu kuweka viwango?
    (Mzazi) Unaweza kusaidiaje kufafanua viwango hivyo na kutoa utegemezo?
    Hali tatanifu zinaweza kuwa kama vile shinikizo la kushiriki ngono kabla ya ndoa, shawishi la kunywa pombe, au kuendesha gari pamoja na mtu ambaye amekunywa pombe kwenye karamu, au kukubaliana na namna fulani ya kufikiri inayopingana na maadili ya familia yenu.
  2. Mzazi na Kijana—Shiriki ndoto au lengo moja ulilonalo kwa mwaka ujao na moja kwa miaka mitatu ijayo. Mnawezaje kusaidiana ili kufikia ndoto au malengo haya?
  3. Mzazi na Kijana—Ni lini mara ya mwisho ulipofurahishwa? Ni nini kilikufanya ufurahi sana? Je, huwa unafanya nini ikiwa una wasiwasi au msongo wa mawazo?

Mada hii inawasaidia vijana kuelewa kwamba mtazamo na fikira zetu kuhusu upendo, ngono na mahusiano kwa kiasi kikubwa zinaundwa na vyombo vya habari—kwa ubora au ubaya—inabidi kutumia utambuzi wa hekima [uwezo wa kuhukumu vyema, kuwa na hekima ya kutofautisha kati ya mema na mabaya, sahihi na isiyo sahihi], na kutumia vyombo vya habari kwa usalama, uwajibikaji na kimaadili.

MODULE 2.1 Utambuzi

MODULE 2.2 Ulimwengu Pepe

MODULE 2.3 Ponografia (PICHA ZA NGONO)

Lengo

Kuwawezesha wahusika kuelewa ya kwamba jumbe wanazopokea kutoka kwa vyombo vya habari zinaathiri mtazamo wao kuhusu upendo, ngono, na mahusiano hivyo basi kuwasaidia kuona umuhimu wa kutathmini na kutumia vyema vyombo vya habari na kuwa na utambuzi mwema.

Usuli

Slides Icons
  • Tunaishi katika mazingira yanayotawaliwa sana na vyombo vya habari kiasi kwamba uhalisia, ukweli, tabia nzuri na maadili hayazingatiwi tena. Mitandao, vipindi vya miziki, mitandao ya kijamii, huduma za utiririshaji, tasnia ya filamu vinachangia ushawishi duniani kote unaoletwa na vyombo vya habari. Upekuzi wowote wa ghafla wa Instagramu za vijana au video za Tik Tok utaibua jumbe zisizofaa katika simulizi na maudhui yake.
Handbook 32 Icons
  • Ingawa watu mashuhuri wengine hutumia umaarufu wao kwa njia iliyo bora na inayokuza maadili na taswira chanya, baadhi yao hawazingatii maadili na wanafanya mambo yasiyofaa ikiwemo kudhulumu wenzao mradi tu wajinufaishe kibinafsi. Pia vyombo vya habari vinatangaza na kuonyesha watu walio uchi au wakishiriki ngono katika maisha yao ya kila siku ili wengine waangalie matendo hayo.
  • Hivyo basi, ni jambo la busara kwa vijana kuwa na “chujio” la kuwawezesha kutathmini au kuchunga ujumbe wanaoupata kutoka kwa vyombo vya habari ili waweze kuelimika kuhusu vyombo vya habari.”

Kuelimika katika masuala ya vyombo vya habari ni nini?

Vijana wengi hutoa majibu ya aina mbalimbali wanapoulizwa kuelimika kwenye masuala ya vyombo vya habari ni nini. Wanapodadisiwa iwapo vyombo vya habari vina jumbe nyingi sana zenye fujo/vurugu na ngono, wanaitikia ndiyo, japo wanalichukulia kama jambo linalowaathiri watu wengine - lakini sio tatizo lao. Kuelimika katika maswala ya vyombo vya habari ni kuwa na ujuzi na uwezo wa kuchuja jumbe mbali mbali na kuelewa athari za ujumbe huo kwa jumuiya au utamaduni kama ni huduma za utiririshaji au mitandao.

Ni hali ya kusisitiza umuhimu wa mtu kuchunguza kwa makini na kuchuja ujumbe wowote wa vyombo vya habari unaomfikia akielewa ushawishi wa aina mbali mbali ya vyombo vya habari, kwa mfano redio, magezeti, televisheni, muziki na mtandao na huduma za utiririshaji kama vile Netflix, Disney+, Amazon Prime Video na video za YouTube, IG reel au TikTok.

“Kuanzia redio ya saa inayotuamsha asubuhi mpaka kabla ya kulala usiku tunapotazama kipindi cha mazungumzo ya usiku, tunaonyeshwa picha nyingi sana kadiri ya mamia—hata maelfu na kupewa mawazo mengi kutoka vyombo mbalimbali ikiwamo televisheni, vichwa vya habari vya magazeti, picha zilizo juu ya magazeti, filamu, tovuti, michezo ya video na mabango. Vyombo vya habari havibadilishi tu utamaduni wetu. vimekuwa ndio utamaduni wetu.”

- Kituo cha Elimu ya Vyombo vya Habari Tunawezaje kuwasaidia vijana kuelimika kuhusu vyombo vya habari? Hebu tuwasaidie wawe na uwezo, wawe na fikra makini na walioelimika katika aina zote za vyombo vya habari, ili waweze kutafsiri na kudhibiti kile wanachokiona, wanachosikia na kuingiliana nacho badala ya kuruhusu ujumbe wa vyombo vya habari kuwadhibiti.

Kuwa na ujuzi wa vyombo vya habari ni kujifunza kuuliza maswali sahihi kuhusu kile tunachotazama, tunachosoma na tunachosikiliza.

Mwandishi wa Kufundisha Vyombo vya Habari, Len Masterman, anauita huu uhuru muhimu au uwezo wa kufikiria mwenyewe, ukiwa na utambuzi.

Going Deeper Icons

Kwenda Ndani Zaidi

Blank Icons

Pata maelezo ya ziada kuhusu kuwasaidia vijana kukuza uhuru muhimu—akili ya utambuzi, katika Kituo cha Elimu ya Vyombo vya Habari, Elimu inayotegemea mfumo wa utafiti.

Dhana Tano za Msingi

Ujumbe wote wa vyombo vya habari umeundwa.

1. Swali kuu la kujiuliza: Ni nani aliyeunda ujumbe huu?

  • Ujumbe wa vyombo vya habari hujengwa kwa kutumia lugha bunifu yenye kanuni zake.

2. Swali muhimu la kujiuliza: Je, ni mbinu gani za ubunifu zinazotumiwa ili kuvutia usikivu wangu?

  • Ujumbe mmoja uliotolewa na vyombo vya habari unapokelewa kwa njia tofauti na watu mbalimbali.

3. Swali kuu la kujiuliza: Je, watu mbalimbali wanaweza kuelewa ujumbe huu kwa njia zipi tofauti?

  • Vyombo vya habari vina maadili na maoni yaliyopachikwa katika kila ujumbe.

4. Swali muhimu la kuuliza: Ni maadili gani, mitindo ya maisha na mitazamo gani inayowakilishwa katika, au kuachwa kutoka, ujumbe huu?

  • Ujumbe mwingi wa media hupangwa ili kupata faida na/au nguvu.

5. Swali kuu la kujiuliza: Kwa nini ujumbe huu umetumwa?

Activities Icons

SHUGHULI MUHIMU
Zoezi 1: Spoti

Blank Icons

Lengo

Kuonyesha jinsi vyombo vya habari vinavyotuathiri.

Mahitaji

  • Ubao mweupe. Maka za rangi tofauti

Maagizo

1. Eleza mhusika huyohuyo kurejelea neno” spot” mara kumi.

2. Mwombe arudie neno spot tena ila wakati huu, kwa mwendo wa kasi.

3. Kisha bila kukawia, mwulize,” Wewe hufanya nini unapoona taa zikigeuka rangi ya kijani kibichi unapokuwa waendesha gari?’

  • Mara kwa mara, utakuta mhusika akisema atasimama “stop” ingawaje jawabu kamili linapaswa kuwa “kwenda”.
  • Muhtasari: Eleza kwamba binadamu anapozoea kuona ujumbe fulani kila mara, ataamini sana katika uhalisia wa ujumbe huo na dhana hiyo itaota mizizi katika fikra za mtu huyo. Hali hiyo ya kuonyesha mtu ujumbe mara kwa mara huwa ni kama kupanda mbegu katika akili ya binadamu na mbegu hiyo inapokuwa ndipo mtu huyo anaamini zaidi katika jambo hilo. Aidha, vyombo vya habari vinaweza kutushawishi na kuwa vielelezo vya namna tunavyopasa kufikiria. Hivyo basi, tunapaswa kufanya kila juhudi kuhakikisha kuwa tunachuja na kutathmini jumbe za habari tunazo pata, ili tunakili zile zinazotufaa na kutupilia mbali zile zisizotufaa (kuwa na utambuzi).
Handbook 37 Icons

4. Uliza: Je, unaweza kufafanuaje utambuzi?

  • [majibu yanayowezekana: uwezo wa kuhukumu vyema, kuwa na busara ya kutofautisha kati ya mema na mabaya, sahihi na isiyo sahihi; maarifa; akili]

5. Je, unafanyaje mazoezi ya utambuzi unapokuja kwenye suala la vyombo vya habari?

  • Kuangalia undani wa jumbe za mawasiliano inatuwezesha kuwa wadadisi badala ya kupokea tu. Vyombo vya habari aghalabu hutangaza ujumbe ambao huwarubuni vijana kwa jumbe potofu katika maswala ya upendo, mahusiano, jinsia na ngono. Kuweza kubainisha ujumbe muafaka na ule wenye dosari kutatusaidia kujisikia vyema kuhusu uamuzi wa kuwa na ujinsia wenye afya.
  • Tunao uwezo wa kuchagua na wa kubadilisha stesheni ya televisheni ama redio. Pia kama watumizi wa vyombo hivi tunaweza kudai video na muziki ulio bora zaidi (maneno na maudhui muafaka)
Activities Icons

Zoezi 2: Maneno ya wimbo ni muhimu

Blank Icons

Lengo

Kuwahimiza washiriki kuwa makini wanaposikiliza nyimbo.

Mahitaji

  • Maneno ya wimbo uliochaguliwa—ikiwezekana mmoja wenye maneno chanya na mmoja wenye maneno has.
Instructions For The Facilitator Icons

Tumia maneno ya nyimbo kuakisi taswira iliyoko katika jumuiya yako. Tafadhali hakikisha kuwa uchaguzi unaofanya hauharibu maadili kwa kuonyesha matusi ama vitendo vyenye kuudhi.

Handbook 38 Icons

Maagizo

1. Swali:: Ni nini hufanya wimbo uwe wa kuvutia?

  • [Majibu yake yanaweza kua mdundo, mahadhi, muimbaji ama maneno yake n.k]

2. Swali:: Kati ya hayo hapo juu ni lipi linalokuvutia zaidi wewe?

  • Elezea kuwa mara nyingi sio maneno yanayoweza kuvutia mtu katika wimbo aghalabu sisi huanza kufuatilia mahadhi hata kama maneno yaliyo kwenye wimbo huo hatujui maana yake.]

3. Onyesha maneno ya wimbo uliyochaguliwa katika slaidi au cheza sehemu ya wimbo.

4. Wakiwa katika vikundi vidogo waombe wanafunzi wajadili maswali yafuatayo:

  • Wimbo unaongelea juu ya nini?
  • Je wimbo unaongelea nini ju ya upendo ama mahusiano?
  • Je maneno au vitendo katika wimbo vinakuza uradhi wa mara moja [fuata tu hisia au tamaa yako ya ngono]?
  • Je ni tabia gani inapaliliwa katika wimbo mfano, unywaji pombe, madawa ya kulevya ama vurugu?
  • Kama kuna maadili yanapendekezwa katika wimbo huu, ungesema ni yapi?
  • Iwapo wewe ni mzazi je ungependa mtoto wako achukue mawaidha kutokana na wimbo huu?
  • Je unakubaliana na mtindo wa maisha ya msanii?

5. Sisitiza kuwa ingawa nyimbo ni kama maneno tu, yanaweza kuwa na athari kubwa sana katika maisha ya watu na matendo yao. Hii ni muhimu sana kuona jinsi sauti ya virusi inavyoweza kuchukua udhibiti wa majukwaa maarufu ya mitandao ya kijamii kama vile TikTok, ambapo kila mtu anaonekana kushiriki katika hisia za virusi au aina fulani ya dansi au matendo.

Hivi majuzi, uchunguzi wa Uingereza uligundua jinsi muziki wa “kuchimba” - aina ya rap inayojulikana kuwa na maneno ya kutisha - inahusishwa na watu wanaotafuta kufanyika mashuhuri kwa kufanya uharibifu. Sio kwamba hilo ni jambo jipya, lakini kuibuka kwa mitandao ya kijamii kumeruhusu kusambaa kwa kurekodi na kushirikisha watu wengi zaidi.

[Hata hivyo], utafiti unaonyesha matokeo yaliyo mchanganyiko sana . . . watu ambao tayari wana mwelekeo wa ujeuri wanaweza kuvutiwa na muziki wenye ujeuri, lakini hiyo haimaanishi kwamba kila mtu anayefurahia muziki huo ni jeuri.

Muziki unatufanya tuhisi hisia za kila namna, baadhi zikiwa hasi . . . na muziki mwingine unaweza “kuwaleta watu pamoja na kuchochea ukaribu wa jamii,” ambayo inaweza kuwa chanya na hasi vile vile.

Muziki una nguvu juu ya hisia zetu. Hakuna viumbe vingine ambavyo vimeibuka kwa njia ya kuhusisha maana na kuunda majibu ya kihemko kwa muziki kama wanadamu. Ni “sehemu ya urithi wetu wa kibiolojia” kwamba muziki hauna upande mzuri tu wa uhusiano wa kijamii lakini pia upande mbaya. “Tunahitaji kutambua hilo ikiwa tunataka kutumia muziki kwa njia nzuri.”

Activities Icons

SHUGHULI MUHIMU
Zoezi 3: Mbinu za Kushawishi Kupitia Rufaa za Kihisia

Blank Icons

Lengo

Kuwahimiza washiriki kuwa na utambuzi na kutumia ujuzi wao wa kutathmini wanapotazama matangazo ya biashara katika vyombo vya habari.

Mahitaji

  • Daftari la mazoezi la mwanafunzi
  • Matangazo mawili au matatu—ikiwezekana moja yenye ujumbe chanya na moja yenye hasi.
Instructions For The Facilitator Icons

[Washirikishi wana uwezo wa kubadilisha tangazo husika na yale yanayopatikana katika mazingira lengwa.Vile vile kuna uhuru wa kuamua kutumia gazeti au jarida katika matangazo husika. Tafadhali hakikisha kuwa uteuzi wako hauna maudhui ya ngono, machafu au vurugu ambayo yanaweza kuudhi au kukasirisha.]

Blank Icons

Maagizo

1. Tazama matangazo na/au chunguza kwa makini matangazo katika magazeti/majarida kwa karibu.

2. Ukitumia orodha iliyoko kwenye madaftari ya wanafunzi, fuatilia kwa makini mvuto wa hisia ambao umetumika katika matangazo mbalimbali. Weka alama katika kijisanduku kila mara unapokutana na mvuto huo mahususi.

Handbook 40 Icons
  • Umaarufu
  • Mahaba
  • Hisia za ngono
  • Ushindani
  • Ucheshi
  • Wivu
  • Huruma
  • Usalama
  • Uoga
  • Utambuzi
  • Kiburi
  • Kujihisi kuwa bora/wa dhamana

3. Uliza: Ni mvuto upi ambao unahisi kuwa ulikuvutia au kukuteka? Ni kwa nini?

4. Elezea kikundi hicho kwamba hisia ina jukumu muhimu katika utangazaji.

  • Watangazaji wanajua kuwa iwapo wataibua hisia (aidha chanya au hasi) watafikia malengo yao kuambatana na bidhaa wanayotangaza. Hivyo basi litakuwa jambo la busara iwapo hatutakubali kuamini au kukubali matangazo yote ya biashara, bali tunapasa kuyapiga msasa na kuchuja yale ambayo si salama na ya manufaa kiafya kwetu. Kufanya utambuzi kwa namna hii ni muhimu kwa kufikiri kwa kina na kufanya maamuzi.
  • Ingawa vijana hawatumii matangazo kwa njia ya kawaida kupitia televisheni na magazeti, wanakabiliwa na matangazo ya mauzo kila siku kupitia mitandao ya kijamii, video za kutiririsha, programu za michezo na mitandao. Ni muhimu kuwa na ufahamu na kufanya maamuzi ya busara ambayo yanafaa mahitaji yetu, badala ya kushawishika kwa mbinu zinazotumiwa na makampuni ya utangazaji.
Blank Icons

Uliza: Ni wapi unapata matangazo ya biashara?

  • Elezea washiriki kwamba matangazo yanapatikana kila mahali, hatuwezi kuepukana nayo kwa mfano katika mabasi, mabango, redioni, kwenye runinga, na kabla na baada ya filamu kwenye kumbi za michezo.
  • Haya ni matangazo ”dhahiri” ambayo tunayaona. Hata hivyo kuna matangazo mengine “ya siri” ambayo hupatikana katika maonyesho na filamu tunazozitazama.

Uonyeshe mfano wa filamu au onyesho la TV lenye matangazo ya bidhaa

Uliza: Ni bidhaa, sura ya bidhaa ipi ambayo huonyeshwa kwenye vipindi husika.

  • Elezea washiriki kwamba kwa sababu tekinolojia ya kisasa inaruhusu watu kutazama vipindi bila matangazo ya biashara ( kwa mfano kutazama picha za video ambazo hupeperushwa kupitia kwa mitandao, kurekodi vipindi bila kurekodi au kuweka ndani matangazo ya biashara) kampuni zimeanza kutumia njia mbadala kutangaza bidhaa zao

Je, unafikiri kampuni hulipa kiasi gani ili bidhaa zao kuwekwa kwenye filamu/onyesho?

  • Hakuna bei moja inayolipwa kutangaza bidhaa kwa kampuni zote, Kwa ujumla, mitandao ya televisheni inao watazamaji wengi kuliko sinema, kwa hiyo television hulipisha bei kali zaidi kwa watangazaji bidhaa.
  • Maonyesho ya mazungumzo ya usiku, kwa mfano, yana lebo ya bei ya juu kwa sababu yana hadhira kubwa. Makampuni yanaweza kutarajia kulipa zaidi ya $1 milioni ili bidhaa kutangazwa. Mara nyingi, bei hii inaweza kuwa kubwa zaidi.
  • https://www.popoptiq.com/how-much-do-companies-pay-for-product- placement-in-movies/

Kwa nini makampuni yako tayari kulipa pesa ili bidhaa zao zionyeshwe kwenye filamu/onyesho?

Activities Icons

Zoezi 4: Tambua Tofauti

Blank Icons

Lengo

Kusaidia washiriki kukuza jicho pevu kwa kile ambacho ni halisi au bandia.

Mahitaji

Maagizo

Wasaidie washiriki kukisia ni nembo gani ni ya asili na ipi ni bandia.

Uliza: Je, itachukua nini kwa mtu kujua ni nembo gani halisi au bandia?

  • [Elekeza swali hili kwa wale waliopata jibu sahihi]

Je, itachukua nini kwa mtu kukuza jicho pevu kwa kile ambacho ni halisi na kilicho bandia kwenye vyombo vya habari?

  • [majibu yanayowezekana: utafiti wa kina, elimu, kuwasiliana na watu wengine au vyanzo vya kuaminika]
Instructions For The Facilitator Icons

Vidokezo kwa wawezeshaji:
Kulingana na commonsensemedia.org, vijana wengi wanapata habari zao kutoka kwenye mtandao. (https://www.commonsensemedia.org/press-releases/new-survey-reveals-teens-get-their-news-from-social-media-and-youtube). Ni muhimu kuwasaidia vijana kusitawisha jicho pevu, kuwa na utambuzi, kuhusu mambo wanayoyasoma mtandaoni.

Blank Icons

Maswali ya kuzingatia wakati wowote vijana wanapokutana na chombo cha habari:

  • Ni nani aliyeitengeneza hii?
  • Ni umati gani unaolengwa na hili?
  • 💭 Nani aliyelipia hii? Au, ukibofya hii, je ni nani anayelipwa?
  • Ni nani anaweza kufaidika au kudhuriwa na ujumbe huu?
  • 💭 Ni nini hakikuwekwa kwenye ujumbe huu ambacho kinaweza kuwa muhimu?
  • Je, hii inaaminika (na ni nini kinakufanya ufikiri hivyo)?
  • Je, tovuti ina URL zisizo za kawaida au majina ya tovuti?
  • 💭 Je, makala yana makosa dhahiri ya kisarufi, madai dhabiti yasiyo na mwanzo na picha za kusisimua?
  • 💭 Ni nani anayetumia tovuti au ni nani anayehusishwa nayo?
    https://www.commonsensemedia.org/articles/how-to-spot-fake-news-and-teach-kids-to-be-media-savvy
Activities Icons

Zoezi 5: Netflix na Ujuzi

Blank Icons

Lengo

Kuwasaidia washiriki kukuza utambuzi na kufanya maamuzi ya busara katika matumizi yao ya televisheni/filamu.

Mahitaji

  • Tumia emoji na uwaombe washiriki wakisie filamu.
  • Bunia Mchezo wa Filamu:

1.
2. 
3. 
4. 
5. 

🥋🙅🐼
🎈🏠
🔝🔫
🚀🧑‍🚀 1️⃣3️⃣
⚰️🏊🏊

Jibu: Kung Fu Panda
Jibu: Juu
Jibu: Top Gun
Jibu: Apollo 13
Jibu: Deadpool

Vipindi vya televisheni na sinema vinaweza kuathiri mitazamo, tamaa na tabia za watazamaji wachanga. Bila shaka, burudani huathiri hisia zetu. Inafuata, basi, kwamba lazima kuwe na mabadiliko fulani katika uchaguzi na matendo yetu. Watu wengi wanaamini kuwa kuna uhusiano baina ya vyombo vya habari na tabia halisi. Uchunguzi unaonyesha kuwa maudhui ya ngono na vurugu yameenea sana katika vyombo vya habari, na vijana wanaoangalia maudhui haya wana uwezekano mkubwa wa kuwa na tabia hatarishi za ngono na tabia za fujo.

Ingawa kuna mabadiliko chanya katika mitazamo ya vijana baada ya kutazama filamu,https://www.ncbi.nlm.nih.gov/pmc/articles/PMC7288198/bado wanahitaji kuamua na kutambua jumbe wanazopokea kutoka kwa jukwaa hili maarufu la vyombo vya habari.

Ukweli ni kwamba vijana wachache wataruhusu ushawishi wa vyombo vya habari kuwageuza kuwa wahalifu au wanyanyasaji wa ngono. Lakini ni vijana wangapi ambao watavutwa wanaposhawishiwa na mtu wa jinsia tofauti kwa kufuata ushauri wa sinema walizoona zenye hisia za kimapenzi au picha chafu?

Ni wangapi watajaribu kuvuta sigara au dawa za kulevya kwa sababu tu programu maarufu ya televisheni ilizifanya zisikike zenye kupendeza? Uwezekano kwamba matendo ya vijana yataathiriwa angalau kwa kiasi fulani na chaguo lao la vyombo vya habari ni kubwa mno, hasa kwa kuzingatia wingi wa burudani zinazotumiwa na vijana

Je, utachaguaje kipindi/filamu yako?

Handbook 41 Icons
USHAWISHI MKUBWAUSHAWISHI KIASILITTLE/NO INFLUENCE
1) Marafiki zako wanasema nini juu yake

2) Muhtasari (onyesho fupi) unaonekanaje

3) Nani ni mwigizaji

4) Nani ni mkurugenzi wa filamu

5) Ni filamu ya aina gani-vichekesho, vitendo, vitisho, mapenzi

6) Imekadiriwaje

7) Maoni ya wakosoaji

Unaweza kupata taarifa muhimu kutoka kwenye orodha hii lakini huwezi kuamini kabisa sifa hizi. Kuchagua filamu kutokana na ni nani mwigizaji, aliyeitengeneza, imekadiriwa nini, au aina yake sio jibu kamili. Waigizaji na wakurugenzi wengi wana filamu nzuri na mbaya kwenye wasifu wao.

Muhtasari (vionyesho vifupi) unaweza kufichua sauti ya filamu lakini hauwezi kukupa habari kamili kwa sababu huitayarisha kwa ajili ya hadhira ya jumla, na kwa kawaida hawaonyeshi picha za walio uchi au wenye majivuno.

Muhtasari wa Filamu ni kipengele muhimu kinachoelezea ukadiriaji wa filamu. Muhtasari wa kawaida unaweza kusema kitu kama “Iliyokadiriwa R kwa vurugu ya picha, matumizi ya dawa za kulevya, hali ya ngono na uchi.” Hayo ni maelezo muhimu kuwa nayo unapojaribu kuamua.

Kutegemea wengine wakufanyie maamuzi kuhusu sinema yako ni kosa. Kupata habari ambayo itakusaidia kufanya maamuzi yako mwenyewe ni wazo nzuri. Tovuti yenye manufaa: www.pluggedinonline.com

Blank Icons

Aina 4 za maonyesho/filamu unayopaswa kujiepusha nayo:

Slides Icons

1. Maonyesho/filamu zinazo kufuru

  • Maonyesho haya yanaidhihaki dini au kuionyesha kwa njia zisizopendeza au zisizo na heshima.
Handbook 41 Icons

2. Maonyesho/filamu za uchawi

  • Kuna tofauti kati ya kufanya mazoezi ya uchawi na kutazama sinema zinazohusu uchawi. Lakini ujumbe wake bado una athari kwetu.

3. Maonyesho/filamu Potofu

  • Hizi ndizo aina zinazosababisha watu kutikisa vichwa vyao na kuuliza, “Ni aina gani ya akili iliyopotoka inafikiria mambo haya?”

4. Maonyesho /filamu za ngono

  • Filamu ambazo ni zaidi au chini ya mkusanyiko wa matukio ya ngono. Watu wengine huzitaja kama “porn-core laini.” Filamu hizi zina kusudi moja: kuzua mawazo ya ngono. (tazama zaidi kuhusu mafundisho juu ya athari za ponografia katika Moduli ya 2.3.)
Blank Icons

Miongozo kwa zile zilizo na ukungu:

Slides Icons

Miongozo kwa zile zilizo na ukungu: Hata baada ya kuondoa kategoria hizo zilizo wazi, bado kuna chaguo nyingi za filamu ambazo zina baadhi ya ngono, vurugu, lugha chafu au mchanganyiko wa hizo tatu.

Handbook 41 Icons

Je, ni muda gani unaokubalika kwa tukio la ngono kupita? Vipi kuhusu idadi kamili ya watu katika filamu wenye jeuri? Je, una mfumo wa uhakika wa kuhesabu maneno ya matusi?

Nambari yoyote itakuwa ya chini sana au ya juu sana. Badala yake zingatia baadhi ya maswali unapotathmini kipindi/sinema:

1. Toni ya kipindi/filamu ni nini?

  • Je, inasamehe au hata kusherehekea mambo ambayo ni machukizo? Je, ngono na jeuri huchezwa kwa vicheko na burudani?

2. Je, kuna maadili katika hadithi?

  • Je, wahusika wazuri wanatuzwa au kuheshimiwa? Je, filamu inaonyesha matokeo ya kufanya maamuzi yasiyo sahihi? Je, angalau inaonyesha kwamba uhalifu hauna faida?

3. Je, unaweza kujifunza chochote kutokana na kipindi/filamu?

  • Je, kuna jambo lolote litakalokufanya uwe mtu mwenye hekima zaidi au mwenye ujuzi zaidi? Kando na kuburudishwa, je, unaweza kupata manufaa mengine yoyote kwa kutazama filamu hiyo?

4. Je, filamu inaweza kuzidisha tatizo ambalo tayari unalo?

  • Ikiwa tayari unakuza tabia ya kuapa, haitasaidia kuona filamu yenye mazungumzo yaliyojaa matusi. Ikiwa umeshuka moyo, hadithi ya giza kali labda haitakuchangamsha. Ikiwa una shida na mawazo ya ngono, “comedy ya ngono ya vijana” sio dawa kwako. Ili kujibu swali hili, itabidi uwe mwaminifu katika kufahamu mapambano yako.

5. 💭 Je, utajuta baadaye ikiwa matukio kutoka filamu hii yatajirudia kichwani mwako?

  • Kama vile maneno ya nyimbo, vivyo hivyo picha za filamu zinaweza kukaa kwenye ubongo wako. Tukio hilo la kutisha linaweza kurudi kukusumbua katikati ya usiku. Tukio hilo la ngono linaweza kutokea tena unapojaribu kupinga kishawishi cha kuwa karibu sana na mpenzi wako.
Slides Icons

Kwa sinema zingine, majibu ya maswali haya yatakuwa dhahiri lakini kwa nyingine, majibu yake ni magumu kuyapata. Huenda ukajihisi kama mpuuzi mwanzoni, ukifanya “utafiti” na kujibu maswali kuhusu kitu ambacho ni burudani tu, lakini itakufaa baada ya muda mrefu na utambuzi unapokuwa mazoea, utakuza fikra makini na uchaguzi bora katika maisha yako.

Lengo

Kuwasaidia washiriki kuelewa namna ya kujishirikisha katika changamano la ulimwengu pepe (wa dijitali) na kukuza ufahamu wa uzuri na ubaya wa michezo ya kitekinolojia, mitandao ya jamii, na kustawi kwa ujuzi katika jumuiya hii ya pepe wakitumia mazungumzo na mahusiano yaliyo mema na ya afya njema.

Usuli

Mtandao na ulimwengu pepe, kama tunavyoujua, unabadilika na kubadilisha jinsi tunavyofanya kazi, kufanya biashara, kucheza na kushirikiana. Ukuzaji wa ulimwengu pepe una maana kuwa tunaweza kufanya kitu chochote na, mahali popote.

Bob Hoose kutoka Plugged In alitoa angalizo hili muhimu:

“Sasa hivi ulimwengu pepe haujafanya kazi kikamilifu”. Lakini, kama mtandao, polepole kutakuwa na mabadiliko kidogo kidogo mpaka utakamilika, nasi tutaukubali. Lakini wakati huu, tunao ujuzi wa kile tunachokitegemea katika mabadiliko ya ulimwengu wa mtandao, na iliyo vyema zaidi ni kwamba tunayo mawazo ya mahali ambapo tungependa mambo haya kwenda. Na huo ni mwanzo mzuri hata kama ni wa kudhania tu.”

Tofauti kati ya ulimwengu halisi na ulimwengu pepe inapoanza kupungua na kukawa kama kuna ukungu, ni rahisi kuelemewa. Kuzuia kabisa ufikiaji wa jukwaa hili la media haiwezekani, kwani shule nazo zimeanza kuitumia katika elimu. Kukosoa mara nyingi maovu ya vyombo vya habari kutapanua pengo la mawasiliano kati ya watu wazima na vijana.

Tunachoweza kufanya ni kuwasaidia vijana kustawi katika nafasi hii ya ulimwengu pepe, na kuwawezesha kuwa na ujuzi (kuitumia huku wakiwajibika na kwa usalama) makini (uwezo wa kutathmini) na elimu (maarifa ya kutafsiri).

Pia ni muhimu kuwasaidia vijana kuweka mipaka mizuri kuhusu lini, wapi na jinsi wanavyopata mitandao. Wahimize kuweka njia za mawasiliano wazi, kiuhalisia na kimwili, na marafiki zao, wazazi na watu wazima wanaoaminika kuhusu mambo yanayowavutia na uzoefu wao mtandaoni. Pia ni muhimu kujifunza kujenga uaminifu na mahusiano ya maana pamoja nao.

Ulimwengu pepe upo hapa sasa, na utawasilisha changamoto mpya kila wakati kadri teknolojia inavyoendelea kukua. Kuwasaidia vijana kujenga mwingiliano wao wa kijamii na kihisia katika ulimwengu pepe na ulimwengu halisi kutawasaidia kustawi katika jumuiya hii..

Activities Icons

Zoezi 1: Mchezo Uliopo

Blank Icons

Lengo

Kuwasaidia washiriki kuelewa wema na ubaya wa michezo ya mitandaoni na jinsi ya kufurahia kuzama kwenye hii michezo kwa usalama na kuwajibika huku wakiweka mipaka inayofaa.

Mahitaji

  • Tumia mifano 3 au 4 ya meme za michezo (Tafuta mtandaoni picha za “meme za michezo”).
Instructions For The Facilitator Icons

Tumia picha kuakisi baadhi ya faida na hasara za michezo ya mitandaoni. Tafadhali hakikisha kuwa uteuzi wako hauna maudhui ya ngono, lugha chafu au vurugu ambayo inaweza kuleta usumbufu.

Blank Icons

Maagizo

Small Group Icons

Waweke washiriki katika vikundi vidogo au wahimize kuinua mikono yao ili kuchangia mjadala wa darasa. Washiriki wachague meme za michezo zinazowavutia zaidi—zile wanazoweza kuzitambua zaidi. Waambie waeleze ni kwa nini.

Handbook 41 Icons

Baada ya mwingiliano huu, endelea kuwauliza washiriki wakueleze faida na hasara za michezo mtandaoni, na uandike majibu yao kwenye ubao mweupe.

ULIZA: Unafikiri vijana wanawezaje kucheza kwa usalama na kwa kuwajibika wakiwa na mipaka na vikomo?

Activities Icons

SHUGHULI MUHIMU
Zoezi 1: Mchezo Uliopo (Mbadala)

Blank Icons

Lengo

Kuwasaidia washiriki kuelewa wema na ubaya wa michezo ya mitandaoni na jinsi ya kufurahia kuzama kwenye hii michezo kwa usalama na kwa kuwajibika huku wakiweka mipaka inayofaa.

Mahitaji

  • Ubao mweupe. Maka za rangi tofauti
Handbook 41 Icons

Maagizo

Wakusanye washiriki katika vikundi vidogo kwa ajili ya majadiliano au wahimize kutoa majibu yao kwa sauti kubwa.

Waombe washiriki kuorodhesha faida na hasara za uchezaji mtandaoni.

Andika ubaoni wakati washiriki wanapotaja majibu yao. Hitimisha shughuli hii kwa maswali haya.

ULIZA: Unafikiri vijana wanawezaje kucheza kwa usalama na kuwajibika wakiwa na mipaka na vikomo vya afya?

Kwa mashirikiano ya kina, wawezeshaji wanaweza kuendeleza majadiliano yao na maswali haya.

  • Je, unafikiri ni kiasi cha muda gani unaofaa kwa michezo ya mitandaoni?
  • Je, unafikiri michezo ya video yenye jeuri/vurugu husababisha watu kuwa na jeuri/vurugu katika ulimwengu wa kweli? Toa sababu kwa nini ni hivyo au sio hivyo?
  • Je, unapaswa kutumia pesa kwa ajili ya michezo ya video? Kwa nini ndio au kwa nini sivyo? Ikiwa ndio, unafikiri unapaswa kutumia pesa kiasi gani?
  • Je, unadhani ni mipaka gani ya michezo ya video inaweza kuwa mizuri kwako? Kwa nini?
  • Je, unafikiri kuna uwiano gani mzuri kati ya shughuli za skrini na shughuli zisizo za skrini? Unawezaje kufikia usawaziko huo?
  • Unapotangamana na wengine mtandaoni, ni tabia zipi unafikiri hazikubaliki? Utafanya nini ukiona wengine wanashiriki kwa njia hiyo?
Activities Icons

Zoezi 2: Mchezo Mzuri

Blank Icons

Lengo

Kuwasaidia washiriki kugundua vipengele vinavyofanya michezo ivutie sana, na mitego yake (matatizo).

Mahitaji

  • Kukagua video maarufu ya mtu wa kwanza akipiga risasi (FPS):

Maagizo

Waweke washiriki katika vikundi vidogo kwa ajili ya majadiliano au wahimize kutoa majibu yao kwa sauti kubwa. Wanafunzi wajadili mambo ya kusisimua ya uchezaji wa video na mitego yake.

Uliza: Kwa nini ni vigumu kuacha kucheza michezo ya mtandaoni? Ni vipengele gani vinavyoifanya kuvutia sana?

  • [majibu yanayowezekana: msisimko wa kufikia kiwango kipya; kutotaka kuachana na wachezaji wenzako, n.k.]

Je, kuna programu maalum za michezo ya mitandaoni au aina ambazo zinaleta “uraibu” zaidi?

  • (k.m., Saga ya Kuponda Pipi, Ninja ya Matunda)

Tunaweza kujifunza nini kutokana na michezo ya mitandaoni?

  • [majibu yanayowezekana: uongozi, kazi ya timu, taaluma inayowezekana ya michezo ya mitandaoni, n.k.]

Je, kuna matatizo gani ya michezo ya mtandaoni siku hizi?

  • [majibu yanayowezekana: lugha chafu, tabia za kijeuri/vurugu, kucheza kwa muda mrefu sana, uraibu]

Tufanye nini basi sisi ili tusiwe na uraibu wa michezo”?

Uzuri wa Michezo ya Mtandaoni

Instructions For The Facilitator Icons

Ulimwengu pepe ni mahali pa kuvutia kwa sababu unaweza:

  • Kuchukua majukumu ambayo kwa kawaida usingeyaweza
  • Kufanya mambo ambayo huna uwezo wa kufanya kama binadamu
  • Kujichagulia nafsi, maumbile ya mwili na vipaji
  • Kuwa na udhibiti
  • Kuyatoroka mafadhaiko ya siku. Shule, kazi za nyumbani, familia, mnyanyasaji, nk.
  • Kuwa sehemu ya hadithi kubwa zaidi. Unazama mchezoni kama sehemu ya simulizi mahiri, changamano na shirikishi ambalo hukuleta katika uhalisia mpya.
  • Kushirikiana na wengine. Unapata marafiki wapya unapoalikwa mchezoni, kutumia jumbe fupi kufanya kazi pamoja mnaunda mikakati ya timu.
  • Kufanya michezo ya mitandaoni kuwa taaluma na maendeleo ya haraka ya esports.
  • Kuboresha ujuzi wa utambuzi, kutatua matatizo, kufanya maamuzi, kufikiri kimkakati, kiwango cha usikivu, ustadi wa mikono, ujuzi wa kompyuta na inaweza kuwasaidia watoto katika kusoma, hesabu na sayansi (kupitia michezo ya wastani.
  • https://www.researchgate.net/publication/349489852_Using_Video_Games_to_Improve_Capabilities_in_Decision_Making_and_Cognitive_Skill_A_Literature_Review

Ubaya wa Michezo ya Mitandaoni

Instructions For The Facilitator Icons

Tatizo la Michezo ya Mitandaoni

Tabia - kufichuliwa mara kwa mara kwa vurugu katika michezo ya mitandaoni huathiri tabia. Tabia ya mtu kwenye hiyo michezo huwafanya watu fulani kuathiriwa zaidi na jeuri baada ya kumuona. Bila kujali kama mtu anakuwa na jeuri kwa sababu ya michezo ya mtandaoni, mtu yeyote anaweza kutohisi vurugu na kutopenda vurugu katika maisha halisi. Mtu anapoona matukio ya jeuri/vurugu mara nyingi, inasababisha kukosa huruma kwa wahasiriwa halisi wa vurugu.

Dhidi ya jamii - Ingawa michezo mingi inaweza kuwa na jumbe chanya au kuwapatia nafasi vijana wenye haya kuungana na wenzao, kuna hatari pia ya ujumbe dhidi ya jamii au kuwahimiza wachezaji kuona vikwazo kama ni vitu vinavyopaswa kuharibiwa.

Tabia hizi huwa zinaathiri ujuzi wa kujua namna ya kuwa na mahusiano ya kweli na jamii.

Michezo ya video imeundwa ili kuangaza vituo vya zawadi kwenye ubongo wetu kwa kutoa changamoto zinazoendelea, na kutoa dopamini kila tunapokuwa na mafanikio. Tusipokuwa waangalifu, hii inaweza kusababisha msukumo, kutokuwa na subira na kuonyesha hasira mchezo unapokatizwa.

Limits - Katika nyumba yoyote, pengine kuna skrini nyingi kuliko wakazi. Fursa za michezo ya mitandaoni ziko kila mahali—kompyuta za kibinafsi, koni za michezo, kompyuta kibao, simu mahiri, n.k. Zaidi ya hayo, mtandao hutoa michezo mingi isiyolipisha hela na bila vizuizi au kanuni za umri unaofaa, muda unaotumika na maudhui. Wakati mwingine, maudhui katika michezo hii yanaweza kuwa kinyume kabisa na maadili yetu, na huna udhibiti wa picha unazoziona (asili ya ngono au vurugu). Matumizi ya kupita kiasi yanaweza pia kusababisha hali ya kuwa na msisimko mkubwa wakati wote.

“Msisimko unajitokeza kwa njia tofauti kati ya mtu na mtu, unaweza kujidhihirisha kwa ugumu wa kuzingatia, kudhibiti hisia, kudhibiti msukumo, kufuata maagizo na kuvumilia fadhaa.” -Fiona Swanson, mfanyakazi wa kijamii wa kliniki katika Saikolojia huko Mankato, Minnesota.

Mfiduo - Kuua ni njia tu ya kuondoa adui bila madhara kwako. Kulingana na Chuo cha Marekani cha Madaktari wa Watoto, 85% ya michezo ya video, hata ile iliyopewa alama ya “E kwa kila mtu,” ina baadhi ya vipengele ambapo mchezaji hudhuru mwingine kimakusudi.

Uraibu - Watafiti wamegundua kwamba kuna mabadiliko ya kiutendaji na ya kimuundo katika neva za waraibu wa michezo ya mtandaoni, kwani wanapowawekea ishara za michezo ya mitandaoni inayoleta tamaa, mfumo wa neva unakuwa na mabadiliko ya aina fulani. Mabadiliko haya ya neva kimsingi ni sawa na yale yanayoonekana katika waraibu wa matatizo mengine.

Tabia Bora za Kucheza Michezo ya Mtandaoni

Instructions For The Facilitator Icons

Dkt. Mitch Prinstein, mwanasaikolojia wa kimatibabu na afisa mkuu wa sayansi wa Shirika la Kisaikolojia la Marekani, alionyesha wasiwasi wake kwamba wakati wa michezo ya mtandaoni, kijana anaweza kujifanya na kucheza kama mtu mwingine ambaye sio ubinafsi wake. Hii ni hatari kwa vijana ambayo inaweza kuathiri kujitambua uhalisi wao wenyewe wakiwa hawako mtandaoni. Vyombo hivi vipya, na uwezekano huu mpya, unaweza kutumika kwa wema au kwa uovu”

Blank Icons

Unaweza kucheza kwa usalama na kwa kuwajibika, ukiwa na mipaka na vikomo vinavyofaa, ukitumia miongozo hii michache.

Jipanue - Chunguza mambo yanayokuvutia katika uchezaji wa mtandaoni kwa kutembelea maeneo mbalimbali, watu na mada zinazohusiana na mchezo unaoufurahia. Iwapo unapenda michezo yenye muktadha wa kitamaduni, nenda kwenye jumba la makumbusho linaloonyesha vipengele vya kihistoria. Ikiwa unajihusisha na michezo ya spoti, jaribu michezo yenyewe halisi. Itakushangaza jinsi ambavyo utaboreshwa na mambo hayo.

Uwezekano - Panua uchezaji wako uwe ni zaidi ya kucheza tu mtandaoni. Chunguza jinsi michezo hii inavyotengenezwa hasa vipengele vya ubunifu na ufundi. Pia uangalie utungaji wa hadithi, muziki unaoambatana nazo, wanavyoziuza na hata talanta ya sauti zinazotumika kuongea. Fanya uchunguzi juu ya uwezekano wa kuunda mchezo wako mwenyewe na kila kinachohitajika kuufanikisha. Uwezekano wa kugeuza kupenda kucheza michezo kukawa taaluma yako unasisimua.

Tumia Mzani - Haijalishi jinsi ambavyo unazama na hata kuona uhalisi wa ulimwengu pepe, kamwe hautachukua nafasi ya mawasiliano na watu ana kwa ana. Weka mipaka ya michezo ya mitandaoni na uthamini mahusiano halisi na watu. Onyesha ukomavu na heshima kugawanya muda wako kati ya kucheza na wazazi wako. Utashangazwa na jinsi wazazi wako watakavyokufurahia unapoonyesha kuwajibika.

Usalama - Tabia nzuri za kucheza michezo mtandaoni ni kujua jinsi ya kukaa kwa usalama mtandaoni. Usiwahi kufichua taarifa za kibinafsi na maelezo yako na ya familia yako kwa mtu yeyote—hata marafiki unaowajua. Usipange kamwe kukutana na mtu ana kwa ana ambaye umekutana naye mtandaoni peke yako bila mtu mzima unayemwamini.

Orodha - Amua orodha ya vile utavyovifanya au vile ambavyo hutavifanya. Kwa mfano: Nitaweka kikomo cha muda wa kuwa kwenye michezo yangu mtandaoni; nitakuwa na heshima ninaposhiriki na wengine mtandaoni; nitamweleza mtu mzima ninayemwamini kama jambo baya likinitokea wakati ninacheza; Sitashiriki katika michezo iliyokadiriwa kuwa ya watu wazima (jifunze kuhusu kufaa kwa michezo kupitia kategoria za ukadiriaji wa mchezo wa ESRB: https://www.esrb.org) ; Sitaanza mchezo wangu ikiwa sijatimiza wajibu wangu mwingine kama vile kazi za shule, kazi za nyumbani na miradi.

Kwa ufahamu wa kina zaidi juu ya ulimwengu wa michezo ya mitandaoni:

Instructions For The Facilitator Icons

Vidokezo kwa wawezeshaji:
Vidokezo kwa wawezeshaji:Wawezeshaji hawana haja ya kucheza kila mchezo ambao vijana wanacheza, lakini itasaidia kujua sheria na masharti machache ya michezo ya mitandaoni. Hapa kuna baadhi ya misingi:

Blank Icons
  • Battle Royale : (Vita ya Kifalme): Mchezo wa video wa wachezaji wengi mtandaoni unaohusisha mamia ya wachezaji wengine kwenye vita ili kuwa mchezaji wa mwisho aliyesimama.
  • Kampeni: Msururu wa matukio au changamoto zilizoundwa ili kusimulia hadithi; pia inajulikana kama Njia ya Hadithi.
  • FPS: Mshambuliaji wa Kwanza—Mchezo wa mpiga risasi ambao unaangazia mtazamo wa mchezaji. Unaweza kuona tu kile mhusika anachoona.
  • MMO: Wachezaji Wengi Mtandaoni, michezo yenye maelfu ya wachezaji katika ulimwengu wazi, wanaokutana na wote kucheza pamoja.
  • NPC: Mhusika Asiye Mchezaji—Wahusika wote katika mchezo huu wameundwa ndani ya mchezo, binadamu mchezaji au mpinzani wake hawadhibiti hawa wahusika. Tabia ya wahusika inadhibitiwa na akili ya bandia (AI).
  • PvP: Mchezaji dhidi ya Mchezaji—Mchezo au hali iliyoundwa kushindana na inayolenga kuwashinda wachezaji wengine walio wanadamu.
  • RPG: Michezo ya Kuigiza—michezo ambapo unaunda na kuchukua tabia ya mhusika katika ulimwengu mzuri kupindukia. Lengo ni kuwa mhusika huyo.
  • Troll: Mtu anayefanya vitu vibaya ili kujifurahisha yeye mwenyewe; hii inaweza ikawa ucheshi kwa kutumia lugha chafu hata kutuma maudhui ya lugha chafu au ya kutatanisha lakini anavipeleka kwa kutumia viunga vinavyoonekana kuwa bila hatia.
Going Deeper Icons

Kwenda Ndani Zaidi

Blank Icons

Mnamo mwaka wa 2018, Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) liliainisha uraibu wa michezo ya mitandaoni (ugonjwa wa michezo ya mitandaoni) kama hali ya afya ya akili.

  • “Uchunguzi unaonyesha kwamba matatizo ya michezo ya mitandaoni huathiri sehemu ndogo tu ya watu wanaojihusisha na shughuli za michezo ya kidijitali au video. Hata hivyo, watu wanaoshiriki katika michezo ya mitandaoni wanapaswa kuwa waangalifu kuhusu muda wanaoutumia kwenye shughuli za michezo ya mitandaoni, hasa ikiwa ni kutofanya shughuli nyingine za kila siku, pamoja na mabadiliko yoyote katika afya zao za mwili au kisaikolojia na mahusiano yao na jamii ambayo yanaweza kutokana na mtindo wao wa tabia ya michezo ya mitandaoni.” -WHO

Sio tu kwamba mchezo wa video unaweza kuwa wa matatizo na unahusishwa na athari chanya na mahusiano ya kijamii, lakini pia unaambatana na dalili za kisaikolojia, mikakati ya kukabiliana na hali mbaya, hisia hasi, kutojithamini, kupendelea upweke, na utendaji duni shuleni.

Handbook 44 Icons

Maswali yafuatayo yanatoa zana rahisi ya uchunguzi ili kuwasaidia vijana kuchakata ikiwa tabia zao za uchezaji zimeanza kuwa kitu kinachoweza kuwadhuru.

NDIYOHAPANAWAKATI MWINGINE
1) Kazi ya shule haimaliziki

2) Unaacha masomo na shughuli nyingine ili kucheza mtandaoni.

3) Unashikwa na hasira na kutokuwa na raha unapojaribu kupunguza au kuacha shughuli za mtandaoni.

4) Unawadanganya familia/marafiki kuhusu matumizi, tabia ya mtandaoni.

5) Unahitaji kutumia muda au pesa zaidi kwenye shughuli za mtandaoni ili kuendelea kusisimka kama ulivyozoea.

6) Unakuwa mtandaoni ili kuepuka matatizo, hisia mbaya au mafadhaiko.

7) Unafikiria shughuli za mtandaoni mara nyingi

8) Unaiba hela ili kufanya shughuli za mtandaoni.

9) Unakopa hela ili uzitumie kwa shughuli za mtandaoni.

10) Unajaribu kucheza mara chache au kupunguza muda wa kucheza lakini unashindwa.
  • Imetolewa kutoka kwa Mwongozo wa Uchunguzi na Takwimu wa Matatizo ya Akili, (DSM IV), (Mataifa, Sim, Khoo & Choo, 2007)

Kwenda Dijitali

Kamilisha mtandaoni kwa kiungo hiki cha tathmini.

KIPIMO:

Waombe washiriki kuzingatia maswali haya ndani ya muda wa mwaka uliopita (mwaka 1). NDIYO (1) , HAPANA (0), WAKATI MWINGINE (0.5). Jumla ya alama zako.

Zaidi ya pointi 5: Tafuta usaidizi wa kitaalamu ili kujua ukubwa wa tatizo lako.

Pointi 2 hadi 4.5: Kuwa mwangalifu, kwani shida yako inaweza kuongezeka.

Chini ya pointi 2: Matumizi yako yana usawa kwa kiasi fulani.

Instructions For The Facilitator Icons

Kumbuka kwamba maelezo katika waraka huu hayakukusudiwa kuchukua nafasi ya ushauri wa kitaalamu wa matibabu, utambuzi au tiba. Tafadhali wasiliana na mshauri au mtaalamu kwa usaidizi zaidi.

Activities Icons

SHUGHULI MUHIMU
Zoezi 3: Mitandao ya Kijamii na Wewe

Blank Icons

Lengo

Kusaidia washiriki kudhibiti teknolojia yao ili wanufaike na kustawi ulimwenguni wanamoishi kulikojaa mitandao ya kijamii.

Usuli

Dunia inaonekana kuwa ndogo zaidi siku hizi za mitandao ya kijamii. Imekuwa jukwaa bora la kuonyesha wewe ni nani (au unataka kuwa nani), kuendelea kuwasiliana na marafiki wa sasa, kuungana tena na marafiki wa zamani, na kuwasiliana na kile kinachotokea katika maisha ya marafiki zako. Majukwaa ya mitandao ya kijamii yamekuwa nafasi ya kuandaa mikusanyiko, vikundi vya maslahi, na vya misaada mbalimbali. Lakini haya mahusiano ya mitandaoni je yanaweza kuimarika? Je, mahusiano ya ulimwengu pepe ni sawa na mahusiano ya ana kwa ana? Kutegemea mahusiano ya mitandao ya kijamii kunaweza kutoa hisia potofu za urafiki na sio mbadala wa jambo halisi.

Je, itakushangaza kwamba wataalamu wa teknolojia wa wakati wetu huona muda wa kutumia mtandao kama kitu kibaya na huweka mipaka mikali kwa muda wa skrini wa watoto wao wenyewe?

Shida kuu ya mitandao ya kijamii ni hali yake ya uraibu na inahusishwa na watu kutokuwa na furaha, wasiwasi, unyogovu na usingizi duni.

Mahitaji

  • Ubao mweupe. Maka za rangi tofauti
Blank Icons

Maagizo

Small Group Icons

Wakusanye washiriki katika vikundi vidogo kwa ajili ya majadiliano au wahimize kutoa majibu yao kwa sauti kubwa.

Waombe washiriki kuorodhesha wanachopenda na wasichokipenda kuhusu mitandao ya kijamii.

Handbook 42 Icons

Andika majibu ya wanayoyatoa washirika ubaoni. Hitimisha shughuli hii kwa maswali yafuatayo.

ULIZA: Unafikiri vijana wanawezaje kuwa washawishi chanya (badala ya kushawishiwa) na kuleta mabadiliko katika nafasi hii?

Kwa mashirikiano ya kina, wawezeshaji wanaweza kuendeleza majadiliano yao na maswali haya.

  • Je, watu wametumiaje mitandao ya kijamii kwa manufaa?
  • Je, watu wametumiaje mitandao ya kijamii kwa ubaya?
  • Je, umewahi kuhisi kama unapaswa kuangalia mitandao yako ya kijamii mara kwa mara? Nini kinatokea usipofanya hivyo?
  • Je, unadhani unatumia muda mwingi kwenye mitandao ya kijamii? Eleza.
  • Je, ulishawahi kutumia simu yako kuepuka mazungumzo au hali zisizokufurahisha? Nini kinaweza kuwa mbadala na si kutumia simu yako?
  • Unawezaje kupumzika vizuri? Je, mitandao ya kijamii inaingiaje katika malengo yako ya kupumzika vizuri?
  • Je, unatambua kuwa mitandao ya kijamii imeundwa ili kukufanya uangalie mtandao kwa bidii kwa muda mrefu iwezekanavyo? Je, umeshafanya hivi au kuona dalili ukiwa kwenye majukwaa unayoyapenda?
Activities Icons

Zoezi 4: Maungamo ya Mitandao ya Kijamii

Blank Icons

Lengo

Cheza mchezo wa bingo na uone upande wa kejeli wa mitandao ya kijamii.

Mahitaji

Kadi ya Bingo ya Maungamo ya Mitandao ya Kijamii.

Je, Unatumia Teknolojia au Inakutumia Wewe?

Nimeanguka kwenye shimo refu.
[kunaswa katika hali ya kushangaza, ya kutatanisha au isiyo na mantiki, na mara nyingi ni ngumu kutoka]
Nimeangalia mtandao badala ya kulala, kusoma au kuhusiana na watu ana kwa ana .Nilitumia muda mrefu kujipiga picha nzuri au niliiweka kwa gramu [Instagram].
Nimepata maoni kwenye chapisho langu kutoka kwa mtu nisiyemfahamu kabisa [nani huyo].Nihudhurie Hakuna Majuto® ili kujifunza jinsi ya kudhibiti [kwa hakika, ninyi nyote].Nililiona tangazo likitokea kwenye mipasho yangu nilipokuwa nikilifikiria [inatisha]
Naliwafuatia watu ambao walinifanya nijisikie vibaya au hata siwapendi [kwa nini].Nilivunja urafiki kwa sababu ya mtazamo na maoni yake ya kipuuzi [hiyo ni kweli].Nilichapisha makala bila kusoma ujumbe wote [Vichwa vya habari ni bora zaidi]
  • Imetolewa kutoka Maabara ya Matatizo ya Kijamii na Mfiduo

Maagizo

Wagawe washiriki katika vikundi au waambie watafute mshirika wa karibu nao.

Piga picha ya kadi ya bingo na simu yako na utumie lebo ya simu yako au programu ya kuhariri ili utumie simu kucheza bingo. (Kwa warsha wa mtandaoni, unaweza kupiga picha ya skrini na kutumia kalamu.)

Weka mviringo kwenye maungamo yako, na uonyeshe kadi yako kwa kikundi au mshirika wako na uchague kigae kimoja ili kushiriki uzoefu wa kibinafsi.

Katika vikundi au wawili wawili, jadili jinsi unavyoweza kuchukua hatua kupunguza athari mbaya za teknolojia hizi kwenye maisha yako.

Activities Icons

Zoezi 5: Mtanziko wa Mitandao ya Kijamii

Blank Icons

Lengo

Kuwa na majadiliano ya uwazi na washiriki kuhusu swali hili: Je, teknolojia kama vile mitandao ya kijamii inatusaidia au inatuumiza?

Video Clips Icons

Mahitaji

  • KIPENGELE CHA VIDEO: Matatizo ya Kijamii - Ushawishi wa mitandao ya kijamii kwenye unyogovu na tabia ya vijana (2:15)

Maagizo

Tazama klipu ya video na uwaombe washiriki kuweka maanani nambari na mwenendo.

Wakusanye washiriki katika vikundi vidogo kwa majadiliano au wahimize kutoa majibu yao kwa sauti kubwa baada ya kutazama klipu ya video.

Instructions For The Facilitator Icons

Vidokezo muhimu kutoka kwa klipu:

  • Netflix ilichapisha hali halisi ya “Tatizo la Kijamii” (Septemba 2020) kuhusu athari za mitandao ya kijamii na jinsi inavyotumia saikolojia kudhibiti maisha yetu.
  • Theluthi moja ya watu wazima wa Marekani—na karibu nusu ya wale wenye umri wa miaka 18–29—wanasema wako mtandaoni “karibu wakati wote.” [Kituo cha Utafiti cha Pew, 2019]
  • Vijana wanaotumia saa tatu kwa siku au zaidi kwenye vifaa vya mitandaao wana uwezekano wa 35% zaidi, na wale wanaotumia saa tano au zaidi wana uwezekano wa 71% wa kuwa na hatari ya kujiua kuliko wale wanaotumia chini ya saa moja. [iGen, 2017]
  • Utafiti wa watu 5,000 uligundua kuwa matumizi sana ya mitandao ya kijamii yanahusiana na watu binafsi kuripoti upungufu wa afya ya akili na mwili na kutoridhika kwa maisha. [Jarida la Marekani la Epidemiology, Feb. 2017]
  • Nchini Marekani, matukio ya kujidhuru na kujiua katika miaka 10 iliyopita (tangu 2011-2013) yameongezeka zaidi ya mara mbili (62% kwa kujidhuru, 7% kwa kujiua) kwa wasichana wa umri wa miaka 15-19 na karibu mara tatu (182% kwa kujidhuru, 151% kwa kujiua) kwa wasichana wenye umri wa miaka 10-14.
  • Ongezeko kubwa lilianza na kuanzishwa kwa mitandao ya kijamii. Katika klipu hii, inazungumzia tatizo la afya ya akili.

Uliza: Ni sehemu gani ya klipu hii ya video inasema na wewe? Je, una uzoefu wa kibinafsi wa kushiriki?

Ni aina gani ya maudhui kwenye mitandao ya kijamii huwa yanakufanya ujisikie vibaya? Je, unayaona mara ngapi?

Je, unadhani mitandao ya kijamii inaundaje tabia zako za kila siku?

  • Upende usipende, mitandao ya kijamii ni sehemu ya ulimwengu wetu halisi na pepe. Kuitumia kwa kiasi wakati huo huo tukidumisha urafiki na mahusiano katika ulimwengu wa kweli ni muhimu. Kujua athari za mitandao ya kijamii kwenye afya ya akili zetu kutatusaidia kuwa na nia ya kuweka mipaka na kustawi katika anga hii pepe.
Instructions For The Facilitator Icons

Vidokezo kwa wawezeshaji:
Tuwafundishe vijana kutumia mitandao ya kijamii vizuri na kuwa na ushawishi mzuri. Tunahitaji kukiri mambo mazuri juu yake. Ikiwa tutazungumza tu na vijana kuhusu jinsi mitandao ya kijamii ilivyo mibaya, tutawatenga na kushindwa kuwatayarisha kufanikiwa katika nafasi hii.

TunachoPENDA kuhusu Mitandao ya Kijamii

Instructions For The Facilitator Icons

Inaelimisha. Kuna maudhui yasiyo na mwisho ya kutufundisha kuhusu jambo lolote chini ya jua.

Inaunganisha na hutusaidia Kuwasiliana. Imeruhusu uhusiano mkubwa na wa kina na watu wengine. Imetusaidia kuwasiliana na mtu yeyote duniani kote, wakati wowote. Inatusaidia kukuza ujuzi wa kijamii.

Inatupatia Sauti. Sio kila mtu ana fursa ya kuingia kwenye vyombo vya habari vya kawaida kama televisheni na redio. Imewapa watu wengi sauti na kwa kuongezeka kwa wafuasi, ujumbe wao unasikika kwa njia za nguvu.

Inatupa Kufikia Wengi. Haitoi tu maudhui bali pia kufikia watu kutoka kwa uzoefu mbalimbali na asili tofauti. Tunapata kujifunza kuhusu matukio ya ulimwengu na mambo yaliyopo nje ya mazingira yetu ya karibu. Inapanua mtazamo wetu wa ulimwengu na kutuwezesha kuwa raia wanaoshughulika katika jumuiya.

Inatia Moyo na Inafurahisha. Inatoa maudhui ya kuinua na kuchekesha na inaweza kuwa jumuiya ambayo inatumika kama faraja kwa watu walio wapweke, wanaopambana na maisha, na waliokumbwa na masuala ya afya ya akili. Kicheko kinaweza kuwa dawa nzuri.

Mambo ambayo HATUPENDI kuhusu Mitandao ya Kijamii

Instructions For The Facilitator Icons

Mtu aliyeandika mtandaoni hajulikani ni nani. Kutokujulikana kunawarahisishia watu kuandika maneno ya chuki na ukatili kwa mtu mwingine ambaye hawajawahi kukutana naye au ambaye kamwe hawatakutana naye. Mfano wa kusikitisha wa hili ni hadithi ya Amanda Todd, kijana aliyejiua baada ya kudhulumiwa mtandaoni kwa kuwa alituma ujumbe wa ngono.

Inatufanya tujihisi kuwa duni. Kujilinganisha kila wakati na mwili “mkamilifu” na maisha “makamilifu” huathiri kujithamini kwetu. Tunajisikia vibaya tunapokosa kupendwa vya kutosha mtandaoni na tunahisi kuwa hatufikii picha ya maisha bora tunayoyaona mtandaoni kila wakati.

Inakengeusha. Tunakengeushwa kila wakati arifa ya simu inapotuarifu kuingia kwa ujumbe, na mara nyingi ujumbe ni kuhusu jambo dogo. Ni desturi yetu kukusanyika na marafiki ili kuongea —lakini maongezi yanakatizwa na arifa za simu zetu mara kwa mara.

Inahusu Kutosheka Papo Hapo. Mtandao umetuunganisha kwa hivyo tunatarajia watu wengine watujibu mara moja, wasipofanya hivyo tunakasirika. Pia tunaona kama ni lazima kujibu kila ujumbe tunaoupokea na tunashindwa kuwafurahia watu tulionao, au tunavurugika wakati tukiwa kazini.

Ni kuhusu kuweza kupata kwa wingi maudhui na taarifa . LAKINI, inakuwa vigumu kutambua ni habari gani ni za thamani au za kutegemewa. Kuweza kufikia jumuiya nyingine nyingi ni vizuri lakini pia ni hatari. Unaweza kushawishiwa polepole kuchukua maadili kutoka kwenye jumuiya hizi ambayo ni kinyume cha maadili yako au ya familia yako. Kupata habari kwa wingi pia huleta hofu (Kujihisi Kupungukiwa) kwa sababu sasa tunajua mambo mengi zaidi ya yaliyo uzoefu wetu

Inachukua Muda. Tunaweza tukawa hatufanyi kitu chochote kibaya kwenye mitandao ya kijamii lakini hatufanyi chochote kizuri kwani mtandao unachukua muda na nguvu zetu nyingi na kutuzuia kujenga mahusiano na ujuzi, kwa vile muda mrefu tunautumia kwenye huu ulimwengu pepe.

Kama chombo kilichoundwa kwa sababu nzuri ya uhusiano wa kibinadamu, kina mapungufu yake. Maandishi, picha, meme na emoji haziwezi kujaza kina na wingi wa mwingiliano wa ana kwa ana.

Je Mitandao ya Kijamii Inatuathiri kwa Namna Nyingine Zipi?

Instructions For The Facilitator Icons

Hatari ya Kuibiwa Vitambulisho Vyako

Taarifa yoyote unayoweka kwenye mtandao (anwani ya barua pepe, maelezo ya kadi ya benki, tarehe ya kuzaliwa, wanafamilia, elimu yako, historia ya kazi, n.k.) inaweza kufikiwa na kutumiwa vibaya na mtu mwingine kwa niaba yako. Taarifa hizi zinaweza kutumiwa na “wezi” wanaojifanya kama kwamba wao ni wewe na wakafikia rasilimali au marupurupu yako. Kadiri unavyoweka habari zako mtandaoni, ndivyo unavyojihatarisha zaidi. Sio salama au busara kutembea barabarani na jina na anwani yako vimeandikwa kwenye shati lako, sasa kwa nini uweke habari kama hiyo kukuhusu kwenye mtandao?

Slides Icons

Kila wakati angalia mipangilio yako ya faragha ili kuzuia umma kufikia mambo yako ya kisiri?

Blank Icons

Hatari ya Ukosefu wa Mipaka

Mipaka ya mtandaoni mara nyingi hukosekana—kutoka kwa kushiriki mara nyingi sana au kuunganishwa na watu usiowajua. Inapashwa kututia wasiwasi jinsi ilivyo rahisi mtandao kuwa na maudhui yasiyofaa (maudhui ya ngono, vurugu au ya kutatanisha). Kushiriki picha mtandaoni ukifanya mambo ya kipuuzi na ya kitoto kunaweza kukachekesha ukiwa na umri wa miaka 15, lakini picha hizi zinaweza kukudhuru baadaye maishani, kwa mfano, mwajiri mtarajiwa au mama mkwe anapokutafuta mtandaoni. Hata kama picha uliyoweka wewe imeshaondolewa, mtu mwingine anaweza akawa ameichapisha mahali pengine. Alama yako ya kidijitali inaweza kufuatiliwa. Kama huamini hebu tafuta jina lako mtandaoni, uone.

Mitindo mingine ina uwezo wa ajabu wa kuenea na kuwa na uwezo wa kushawishi watu kufanya maamuzi ya kubadilisha maisha yao. Mitindo mingine ni ya ucheshi na mingine ina nia njema kama vile Shindano la Ndoo ya Barafu - Ice Bucket Challenge.

Walakini, zingine ni za kushangaza na hatari kabisa kama Shindano la Tide Pod.

Vijana nchini Indonesia wamekuwa wakiruka mbele ya malori yaliyo mwendoni barabarani huku wakishiriki katika shindano hatari la TikTok linaloitwa “mzaha wa malaika wa kifo” ambao umesababisha vifo vya watu wawili tayari.

Hatari ya Wanyanyasaji wa Mtandaoni na Waviziaji

Unyanyasaji mtandaoni unazidi kuwa ni jambo linaloenea kwa kasi duniani kote, hasa miongoni mwa vijana. Kwa sababu ya upatikanaji mkubwa wa mtandao, na kwa sababu ya urahisi wa kusambaza habari, inakuwa rahisi kwa watu wenye nia mbaya kueneza uvumi, dhihaka, vitisho au kuwaogopesha wengine. Ingawa si vigumu kutambua chanzo cha vitisho na uvumi, athari ya jumbe hizi inaweza kusababisha uharibifu zaidi kuliko inavyotarajiwa. Katika baadhi ya matukio, inaweza hata kusababisha mtu kujiua.

Hatari ya Urembo Mtandaoni

Kuanzia vyumba vya mazungumzo katika michezo maarufu hadi mifumo ya mitandao ya kijamii, watu wanaonyanyasa kingono huwalenga vijana ambao wanaweza kuwahadaa, kuwadanganya au kuwatishia kwa urahisi. Wanachukua fursa ya kwamba vijana wanapotumia mitandao ya kijamii hujibu maombi yasiyo na hatia na kukubali kuunganishwa. Basi wanawaambia maneno ya kuvutia na kuwatia moyo ili wawe na mawasiliano zaidi. Urafiki unaoonekana mwanzoni kutowa na hatia unapoendelea mwishoni mtu anaomba picha za uchi au mazungumzo ya ngono yasiyofaa. “Unyanyasaji wa ngono” pia ni tishio linaloongezeka. Unaweza kutoka kwa mpenzi wa zamani au mtu aliyepata picha au video za ngono za mwathiriwa. Wakitumia hizo na kutishia kuzifichua kwa familia, marafiki au kwenye majukwaa ya umma, wavamizi “hunyanyasa ngono” wakidai picha nyingine za uchi, video au hata kushiriki ngono nao.

Tazama ripoti hizi za ufichuzi kuhusu mada ya urembo wa kingono mtandaoni. Unaweza kuonyesha klipu hizi za video kwa washiriki ili kuleta ufahamu juu ya suala hili. Video Clip: Dating A Predator: “The Teacher” [https://youtu.be/i4iIBEM-gvoMwandishi wa habari wa siri, aliyejificha kama mtoto wa miaka 15, anakutana na mwindaji wa ngono ya watoto ambaye aliwasiliana naye kwenye WeChat. Haikuchukua muda mrefu akamwomba aende naye kwenye chumba cha hoteli.

Video Clip: Social Media Dangers Exposed by Mom Posing as 11-Year-Old

Mama mwenye umri wa miaka 37 anajifanya kama msichana wa miaka 11 ili kufichua hatari zinazowakabili watoto kwenye majukwaa ya mitandao ya kijamii kama vile Instagram, Snapchat, TikTok, na Kik. Wakiachwa bila kusimamiwa, watoto wadogo wanaweza kukabiliwa na wavamizi wa mtandaoni, na unyanyasaji wa kisaikolojia ndani ya dakika chache.

Tunaangazia maswala haya ili kuleta ufahamu na sio hofu. Tunaamini kujifunza kutumia mitandao ya kijamii vizuri na kwa usalama kunawezekana. Badala ya kufuta akaunti yako ya mitandao ya kijamii au kuikumbatia ovyo, unaweza kuwa na hekima na utambuzi kuwa mshawishi chanya badala ya kuathiriwa vibaya.

Unafikiri vijana wanawezaje kuwa washawishi chanya na kuleta mabadiliko kwenye nafasi hii?

Kanuni Ni Muhimu. Kuna sababu nzuri kwa nini tovuti za mitandao ya kijamii zina ruhusu watu wa umri usiopungua miaka 13. Hii ni kwa sababu za kisheria na usalama/faragha. Shiriki kwenye tovuti zinazofaa umri wako, hii itakusaidia kukaa salama. Japo mipangilio ya faragha sio mikamilifu lakini inasaidia sana. Chukua muda ujifunze mipangilio na udhibiti wa faragha inayokufaa.

Slides Icons

Chapisho Lako Ni Muhimu. Fikiri kabla ya kuchapisha. Kila kitu tunachochapisha kinaweza kuonekana na hadhira kubwa. T.H.I.N.K (FIKIRI) kabla ya kuchapisha:

Handbook 43 Icons
  • T: ni kweli? Chapisha taarifa ambazo una uhakika 100% ni za kweli. Ikiwa una shaka, usiichapishe.
  • H: Je, linasaidia? Je, chapisho langu litasaidia au kuwa la manufaa kwa hadhira yangu? Ikiwa ni “hapana,” fikiria tena ujumbe wako.
  • I: Je, linatia moyo? Sio machapisho yote yanayokusudiwa kuhamasisha au kutia moyo, lakini hatupaswi kutumia mitandao ya kijamii kama jukwaa la kulalamika au kuwakatisha tamaa wengine. Fikiri upya chapisho lako ikiwa ni la kutoa maoni hasi au kulalamika tu.
  • N: Je, ni za lazima? Nani atafaidika na habari hii? Je, unasambaza habari ambazo wengine wanapaswa kujua? Ikiwa ndivyo, basi ichapishe! Lakini ikiwa unashiriki habari za kibinafsi au kusengenya, basi usizichapishe.
  • K: Je, zina fadhili? Kumbuka kuwa kejeli ni ngumu kutafsiri mtandaoni. Kuna mtu anaweza kutafsiri chapisho lako kama la kuumiza? Kinachoonekana wazi kwako kinaweza kisiwe wazi sana kwa wengine.
Blank Icons

Kusuluhisha Migogoro. Usiepuke ugomvi wa ana kwa ana na badala yake ukawasilisha “mawazo” yako kwenye mitandao ya kijamii. Kuwasiliana ana kwa ana na walengwa wako ni njia bora zaidi. Tengeneza nafasi za kuunganishwa na kuongea, sio za kuchanganyikiwa na machafuko.

Omba Ruhusa. Usiweke mtandaoni picha za watu wengine bila idhini kutoka kwa watu wamiliki wa picha hizo.

Tabia. Uwe mtu mwenye adabu wakati wote. Mheshimu kila mtu na usiweke mtandaoni chochote ukiwa na hasira. Fuata Kanuni Bora—Watendee wengine jinsi unavyotaka kutendewa. Watendee na kuzungumza juu yao mtandaoni kama vile ambavyo ungewatendea na kuzungumza nao ana kwa ana. Huwajibikii jinsi watu wanavyoguswa, lakini ni jambo la kuzingatia ikiwa chapisho litamfanya mtu mwingine ajisikie vibaya.

Mambo ya Jumuiya. Endelea kuwasiliana na jumuiya inayoaminika ambayo unajua itakuwa ushawishi mzuri kwako

Activities Icons

SHUGHULI MUHIMU
Zoezi 6: Kuyafikiria Upya Maisha Yangu ya Kidijitali

Blank Icons

Lengo

Kuwawezesha washiriki kubadilisha jinsi wanavyotumia vyombo vya habari .

Mahitaji

  • Daftari
Handbook 43 Icons

Maagizo

Waombe washiriki wakamilishe taarifa iliyo hapa chini ili kuwasilisha jukumu la vyombo vya habari vya kidijitali katika maisha yao:

  • Maisha yangu ya kidijitali ni kama ________________________ , kwa sababu ____________________________.

Mifano:

  • Maisha yangu ya kidijitali ni kama dirisha la dunia, kwa sababu linaniruhusu kuona kila aina ya mambo mapya na kunipatia mafikara mengine mapya.
  • Maisha yangu ya kidijitali ni kama kifaa kiendacho kasi chini na juu (roller coaster), kwa sababu yananisisimua na yananijaza heka heka.
  • Maisha yangu ya kidijitali ni kama tafrija ambapo ninakutana na watu wengi tofauti, kwa sababu inasikika kwa sauti kubwa, bila kudhibitiwa, na bado, inanifurahisha.

Changamoto kwa washiriki

Fanya mpango wa jinsi ambavyo ungependa kubadilisha tabia yako ya mitandao ya kijamii. Fikiria ni wakati gani utafanya kitu tofauti na unavyofanya sasa na kitu gani unachoweza kufanya badala yake. (Kubadilisha tabia si rahisi. Usifikirie tu kile ambacho hutafanya. Orodhesha mambo ambayo utafanya pia!)

Blank Icons

[Majibu yatatofautiana, yafuatayo ni baadhi ya majibu yanayowezekana]

Changamoto zangu za media ni pamoja na:

  • Kuacha kufuata akaunti fulani.
  • Kuweka vikomo vya muda kwa siku au kwa programu.
  • Kutumia programu ya kufuatilia tabia za midia kama vile Moment au ZenScreen.
  • Kuweka muda wa kutotumia kifaa kwa siku, kama vile chakula cha jioni au kazi ya nyumbani.
  • Kuchaji simu yangu nje ya chumba changu wakati wa usiku.
    Imechukuliwa kutoka kwa Midia ya Kawaida

Lengo

Kuwawezesha washiriki kuelewa madhara ya ponografia (filamu za kuzua tamaa).

Usuli

Ingawa vyombo vya habari vinaweza kupotosha mtizamo wetu kuhusu upendo wa kweli, kuna njia nyengine ya mawasiliano iliyo na madhara mengi zaidi- ponografia.

Mtazamo wa mtu kuhusu wanawake au wanaume unaweza kubadilishwa kutokana na kuangalia picha potovu za jinsia mbalimbali za kuzua tamaa.Picha hizi potovu hazibadilishi tu mtazamo wetu wa upendo bali pia zinapotosha kuelewa kwetu kuhusu uhusiano wa kindani.

Badala ya kukuza maadili na heshima, ponografia hudunisha watu na kuwafanya kama vyombo vya anasa. Hata kutazama tu picha za ashiki kijuujuu kunaweza kumfanya mtu awe na mtazamo tofauti kuhusu uhusiano wa kindani.

Athari ya picha za ngono ni mbaya kwa uhusiano na inadumu zaidi kuliko athari inayotokana na vyombo vya habari. Nyenzo zinazoonekana kuwa zisizo na madhara kama vile picha kwenye Instagram, zinaweza kumvutia mtu na kumfanya aangalie mambo machafu zaidi. Aidha, mtu huenda akawa mtawaliwa na mraibu wa picha za ngono. Hatimaye, mambo yaliyo kuwa ya kuchukiza yanageuka na kuwa ya kupendeza na kukubalika. Ili kukabiliana na athari hii, basi tunapaswa kufanya zaidi ya kuchagua jumbe tunazopokea na kujiepusha kabisa na picha za aina yoyote zinazozua tamaa.

Activities Icons

SHUGHULI MUHIMU
Zoezi 1: Ponografia ni nini?

Blank Icons

Lengo

Kuwezesha washiriri kuelezea maana ya ponografia.

Mahitaji

  • Ubao mweupe. Maka za rangi tofauti
Small Group Icons

Maagizo

1. Gawa kundi hilo katika vikundi viwili, moja likiwa la wanawake jingine la wanaume. Kisha wajadiliane na uwaambie waandike jinsi wanavyoelewa neno “ ponografia”.

  • Maneno/misemo inayoweza kutajwa: miili iliyo uchi, wanawake na wanaume wazuri, kushiriki ngono, haramu, vibaya, mtandao, msisimko wa ngono, punyeto.
Handbook 46 Icons

2. Waonyeshe wasichana majibu ya wavulana, na wavulane wayaone majibu ya wasichana pia. Waonyeshe sasa mitazamo tofauti kati ya wavulana na wasichana au uiongelee baadaye wakati warsha inaendelea. Mitazamo tofauti inayowezekana.

WAVULANAWASICHANA
Kuiangalia ni kawaidaWavulana au watu wenye matatizo ndio wanaangalia ponografia
Kwa ujumla inavutiaInachukiza japo unataka kujua ni nini
Unaweza kuijadili na marafiki zakoNi siri ambayo huwezi kumwambia mtu yeyote hata rafiki wa karibu

Ufafanuzi:

  • Ponografia inarejelea nyenzo yoyote inayoonyesha vitendo vya kuchochea tamaa ya ngono (iliyochapishwa, inayoangaliwa, inayosikika).
  • Ponografia ni kitu chochote kilichotengenezwa ili kusababisha msisimko wa ngono kwa watu.
Activities Icons

SHUGHULI MUHIMU
Zoezi 2: Ponografia na Ubongo

Blank Icons

Lengo

Kuwaonyesha washiriki jinsi ponografia hutengeneza na kuimarisha njia ya neva ndani ya ubongo.

Mahitaji

  • Udongo wa mfinyanzi
  • Kisu cha plastiki

Maagizo

1. Kwa kutumia udongo wa mfinyanzi tengeneza umbo la ubongo na uushike mikononi mwako ukiwaelekea washiriki.

2. Waeleze kwamba kila tunapokuwa na tukio, njia ya neva inaundwa kwenye ubongo. [Tumia kisu cha plastiki kutengeneza njia kwenye udongo.]

3. Ikiwa tukio lina manufaa, ni rahisi ubongo kupendelea tukio hilo. [Eleza kwamba kama maji yatamiminwa kwenye ubongo, ni rahisi maji hayo kufuata njia ambayo tayari imeishatengenezwa.]

4. Tunapochagua tukio hilo tena, njia iliyokwisha tengenezwa inapanuliwa zaidi. [Tumia ukingo wa kisu cha plastiki kuipatia njia kina zaidi.]

Slides Icons

Waeleze:

  • Unapotumia ponografia kwa mazoea, unatengeneza njia kwenye ubongo wako zinazokufanya utake kuendelea kutazama ponografia zaidi.
  • Uzoefu wetu huunda njia kwenye ubongo. Matukio yanayorudiwa huongeza njia hizi, na kufanya iwe rahisi kwa mtu kuchagua tabia hiyo hiyo kila wakati.
  • Kadiri mtu anavyotazama ponografia—na kupata kuridhika, ndivyo anavyotaka kuendelea kutumia ponografia.
  • Kwa sababu njia imeisha tengenezwa kwenye ubongo, ni rahisi sana kurudia na kujihusisha (kutazama ponografia), hii hufanya njia iwe na kina kirefu sana hata inakuwa vigumu kuiacha tabia hii.
  • Neuroni ambazo huwaka pamoja huungana pamoja, yaani, ubongo huhusisha shughuli mbili tofauti kuwa moja. Kwa hiyo, baada ya muda, ponografia tu ndiyo inayousisimua ubongo kufanya ngono.
  • Unapotazama ponografia na kupata furaha ya ngono, ubongo wako utaunganisha ponografia na furaha ya ngono.
  • Hii itazuia uwezo wako wa kupata urafiki wa kweli/kweli wa kijinsia na mwenzi wako katika siku zijazo, kwa sababu ubongo wako badala yake utaendelea kuhusisha uhusiano wa kimapenzi na picha za ponografia.
  • Kimsingi, ponografia ni uraibu na inasisimua sana akili zetu. Kwa sababu hii, ponografia inaleta tishio kubwa kwa jinsi akili zetu zinavyofanya kazi kawaida.
  • Ikiwa ponografia ambayo inatazamwa ina vitu vilivyo na vurugu, uchawi, ubakaji, udhalilishaji au aina zingine zozote zisizo na kikomo za ponografia potovu, mambo haya huanza kuwa yale ambayo mtazamaji anadhani kuwa ni ya kuvutia na yanayo hitajika.
    https://fightthenewdrug.org/true-story-how-porn-twisted-my-sexuality/
  • Kuna hadithi za wanaume na wanawake wanaotumia ponografia mara kwa mara, ambao hawawezi kusisimka kingono wanapokuwa na wenzi wao wa ndoa. Kwa kweli wanaona ponografia kuwa yenye kusisimua zaidi kuliko ngono na wenzi wao wa ndoa.

Wakumbushe washiriki kuwa ponografia SIO uhusiano dhabiti wa undani.

Ponografia ni:

Slides Icons

Ina madhara

Kwa sababu lengo lake kuu ni kuzua tamaa ya ngono, inadhuru ndoa na mahusiano dhabiti.

Handbook 46 Icons

Watu katika tasnia ya ponografia mara nyingi ni wale wanaonyonywa. Tasnia ya ponografia inahusishwa na ukahaba na biashara ya kuwauza binadamu ili kuwatumia kingono. Kwa kulipia na/au kutazama ponografia, inahimiza unyonyaji na madhara ya wale walio katika tasnia hiyo.

Blank Icons

Huenea na kukua

Wataalamu wanasema kuwa picha za ashiki ambazo zinaweza kuchukuliwa bila uzito wowote zinapochapishwa kwenye magazeti, zina uwezo wa kumfanya mtu kutawaliwa na kuwa mraibu wa ponografia. Hatimaye mtu huyo anaweza kuwa mfuasi sugu wa mambo ya ponografia ambayo yanapatikana kwa wingi na kwa urahisi kwenye mtandao.

Ina uraibu

Mtu anapokuwa na mazoea ya kutazama picha za kuamsha tamaa, anakuwa na uchu wa kutaka kuzitazama kila mara. Mara nyingi, waraibu hawa hupata msisimko na kilele chake huwa ni aina ya utulivu na amani inayopatikana baada ya aina fulani ya homoni (serotonin) kutolewa. Hali hii ya kupata punyeto au kujichua ndio humfanya mtu kuirejelea kutazama picha hizi za ashiki mara kwa mara.

Baada ya muda fulani, uraibu wa kisaikolojia hubadilika na kuwa uraibu unaoathiri mtu kimwili. Hii ni kwa sababu uraibu wa picha za ngono hufanya kazi kwa njia sawa na uraibu wa dawa za kulevya. Wakati dawa za kulevya husisimua mtu na kumpa furaha ya aina fulani, ponografia huanzisha utoaji wa homoni ambayo inaleta furaha ya aina yake. Iwapo hali hii itarudiwa mara kwa mara, mtu anaweza akawa na uraibu wa kemikali za kusisimua akili yake. Muathiriwa mara kwa mara hutamani kupata msisimuko wa juu kama tu vile mraibu wa dawa za kulevya hufanya, na anataka kurejelea kuona picha za kuzua ashiki. Hii ndio sababu inakuwa vigumu kwa mraibu wa picha za ngono kuacha kuzitazama licha ya kuwa na nia kuu ya kuacha tabia hiyo.

Zaidi ya hapo, kuzoea picha za ngono huleta tabia ambayo huathiri mtu kisaikolojia ambayo inachangia kukosa hisia. Kama tu vile wanasaikolojia wanaweza wakamsaidia mteja wao kuacha tabia ya kuogopa wadudu kwa kumleta mara kwa mara karibu na wadudu kama vile buibui , mtu aliye na uraibu wa picha za ngono ataanza kukosa mnato anapotazama picha hizo na kuzichukulia kuwa dhaifu. Licha ya picha hizo kuwa na uwezo wa kusisimua mtu kiashiki, mraibu wa picha hizo ataanza kuzichukulia kama za kawaida. Ili kupata msisimuko sawa na aliyokuwa akiupata alipoanza tabia hiyo ya kutazama picha za ngono, itambidi atafute fasihi iliyo na picha za mvuto zaidi, kama kifungo na usagaji (BDSM) ponografia, ngono na wanyama, au ngono ya kulazimishwa kwa wanaoshiriki. Wakati mwingine mraibu anaweza kuenenda katika uzoevu wa starehe hizo kama jambo dhahiri maishani mwake.

Ponografia SIO:

Blank Icons

Burudani tu

Ponografia ina mathara kwa mwili na akili kisaikolojia. Aidha ina athari kwa hisia na uhusiano. Ngono ni zawadi ambayo bibi na bwana huhifadhiana ili wazawadiane katika ndoa baina ya mke na mume mmoja. Ponografia na aina nyengine za tamaa huichukulia ngono kama kitu cha kunyakua kutoka kwa mwengine. “Kunyakua” huku badala ya “kutoa” kunaweza kusababisha unyanyasaji, maumivu moyoni, na taabu.

Slides Icons

Heshima

Ponografia inadunisha watu na kueneza dhana kuwa binadamu hana utu bali ni chombo kinachoweza kutumiwa kujipatia anasa. Mara nyingi, wanawake husawiriwa kama vyombo vya kutumiwa na kudhulumiwa kwenye ngono ambavyo hutupwa baada ya shughuli hiyo. Wanaume kwa upande mwingine huchukuliwa kama vyombo vinavyoendeshwa na tamaa.

Mfano:

Handbook 46 Icons
  • Mwishoni mwa 2013, filamu ya kwanza ya Joseph Gordon-Levitt (mwigizaji wa Amerika) ilionyeshwa kwenye sinema. Don Jon iliyotolewa kwa wingi, ilikuwa mada ya majadiliano mengi kwenye vyombo vya habari kwa sababu ya mada ya filamu-ponografia.
  • Katika mahojiano akizungumzia tabia yake kwenye filamu na ujumbe wa filamu hiyo, Gordon- Levitt alisema:
    “Kila kitu katika maisha ya Jon kinaonyesha ubinafsi. Yeye hajiunganishi au kujihusisha na mtu yeyote. Wanawake katika maisha yake ni kama kipengee kwenye orodha; hawasikilizi; yeye ananyakua tu. Mwanzoni mwa filamu, anaona kwamba haridhishwi na matendo yake, kwa sababu kuna mlolongo ambapo anamleta mwanamke kijana nyumbani kutoka kilabuni na anamlinganisha na orodha hii ambayo ameipata kutoka kwa kile anachopenda kukiona kwenye video ya ponografia.
    Nadhani hakuna tofauti kubwa kati ya vyombo vya habari vingi vya kawaida na ponografia. Wao wanawapunguzia utu wanadamu na kuwatendea kama kwamba ni vitu visivyo na uhai. Hii inadhihirika wanapokadiria maonyesho kama X au “yanapoidhinishwa na FCC kwa watazamaji wote jumla,” ujumbe ni ule ule. Katika tamaduni zetu tunachukulia watu kama kwamba ni vitu.
  • Tangu filamu hiyo, Gordon-Levitt amekuwa wazi kuhusu hisia zake kwamba vyombo vya habari na ponografia zinaonyesha vibaya juu ya watu na mahusiano.
Blank Icons

Kuridhisha

Mara nyingi watu wanaohusudu ponografia huwa pweke na kukatishwa tamaa na mahusiano yao. Tendo hili laweza kulinganishwa na kutafuna kitu unachokienzi kwa minajili ya utamu wake tu kisha baadaye ukakitema.

Uraibu wa ponografia hauridhishi kwa sababu binadamu aliumbwa kuwa na uhusianao wa kindani na wetu wengine. Lakini kutazama ponografia kunashirikisha picha za mtu mmoja pekee ambaye hana uhusiano wala hawezi kunyoosha hisia zake kwa yule anayemtazama. Hali ya upweke huwatawala sana wapenzi wa ponografia kwa sababu picha hizi za ashiki huchangamsha kitengo cha akili na miili yao vilivyokusudiwa kuwa na uhusiano na watu wengine. Hatimaye waraibu hao wa ashiki hufungia ndani hisia zote za mapenzi zinazokusudiwa kuonyeshwa kwa watu wengine. Ni kutokana na haya ambapo watu ambao hujichangamsha na ponografia wanapaswa kujiepusha na haya na kujumuika na watu na marafiki halisi wanaowajali- Huu ndio mshikamano wanaoukosa!

Uhusiano thabiti wa undani

Katika ponografia, kunakosekana uhusiano wa kindani wa dhabiti baina ya watu halisi, unaopatikana katika uhusiano dhabiti na uliojengwa kwa misingi ya maadili. Uhusiano wa kindani wa kweli haubagui wapendanao kwa misingi ya kasoro za kimaumbile.

Mfano:

  • Katika kitabu chake Manhood, Terry Crews (mwigizaji wa Marekani, mtangazaji wa hivi majuzi wa televisheni na mchezaji wa zamani wa kandanda wa Marekani) alizungumza waziwazi kuhusu jinsi alivyokuwa mraibu wa ponografia tangu akiwa na umri wa miaka 12 na jinsi ilivyoathiri sana ndoa yake. Katika sehemu ya mahojiano na kipindi cha Tom Joyner Morning Show, Crews na mke wake wa miaka 25, Rebecca, waliongea wazi kuhusu athari walizokuwa nazo kwenye maisha yao pamoja:
  • “Nilikuwa baba mwenye upendo, mume mwema, lakini katika akili yangu nilihitaji kitu kama ponografia ili kujituliza. Ni kama kutokubali kuwa wewe ni mlevi au mraibu. Ukweli ni kwamba huwezi kuishi katika dunia mbili, nilikuwa naendelea kujitenga mbali na Rebecca.
  • Ponografia inaua uhusiano wa dhati na wa undani. Ilianza kujenga ukuta kati yetu. Watu wengi hupeana talaka bila kujua mwanzo wa kutengana. Sio kwamba mke wangu alinishika nikiangalia ponografia. Bali aliniambia, ‘Unalo tatizo’ na hatimaye ilinibidi nikiri kwamba kweli lilikuwa ni tatizo . . . Niligundua kwamba nilikuwa siwezi kuacha ponografia.”

Ponografia na Punyeto:

Instructions For The Facilitator Icons

Kwa ufafanuzi wa kamusi, kupiga punyeto kunahusisha kujisisimua kimakusudi kwa madhumuni ya kupata furaha ya ngono kwa ajili yako mwenyewe na ukiwa peke yako.

Kupiga punyeto ni shughuli ya ngono, ingawa si kujamiiana yenyewe, lakini inaweza hatimaye kusababisha kujamiiana.

Zaidi ya 95% ya wanaume na karibu 50% ya wanawake wamepiga punyeto. Kwa sababu kitu kimefanyika na wengi/kinajulikana haimaanishi kuwa ni cha manufaa/kizuri kwetu kila wakati. Kwa mfano, hata kama watu wengi wanatupa takataka au kuvuta sigara, hilo bado halitafanya kutupa takataka au kuvuta sigara kuwa kitu chenye manufaa kwetu au kwa jamii.

Kwa sababu ya kutokea kwa wingi miongoni mwa wanaume, punyeto huwa ni tatizo la wanaume zaidi kuliko wanawake.

Mambo kadhaa yanayohusu kitendo cha kupiga punyeto:

Masafa: Akili zisizo na kazi husababisha mikono isiyofanya kazi, na wengi ambao walianza tabia ya kupiga punyeto walifanya hivyo wakati hawakuwa na chochote (bora) cha kufanya (yaani, bila kazi). Ingawa hakuna kitu kibaya kuhusu kitendo chenyewe, kinaweza kuwa tabia inayosababisha uraibu wa ngono.

Motisha/Kusudi: Ni kwa ajili ya kujiridhisha tu. Kupiga punyeto kunaweza kuwa tatizo ikiwa mtu anajishughulisha mara kwa mara au kwa madhumuni ya ubinafsi. Hii inathiri vibaya uwezo wa mtu wa kuhusiana kwa karibu na mtu mwingine; inachukua nafasi ya uhusiano wa undani na wa kweli.

Kuoanisha: Kupiga punyeto mara nyingi huambatana na ponografia. Watu wanaopiga punyeto kwa kawaida huangalia ponografia, ndoto za ngono au majaribio ya ngono (ambayo yanaweza kukengeuka kadiri uraibu unavyoongezeka). Kupiga punyeto ni mteremko unaoteleza ambao huongeza tu tatizo la uraibu wa ponografia. Kiasi cha ponografia kinachopatikana kwa urahisi kwa vijana leo kinastaajabisha akili na kinaweza kumwangamiza mtu kupitia uraibu. Inaweza kumfuata mtu katika maisha yake yote, kuathiri mahusiano, maamuzi na amani yake.

Kupiga punyeto huathiri jinsi ulivyo kama mtu kwa sababu kile tunachokifanya na miili yetu ni vigumu kukitenganisha na utu wako.

Activities Icons

Zoezi 3: Ponografia na mtazamo

Blank Icons

Lengo

Kuelewa namna ponografia huathiri mahusiano yetu kwa njia isiofaa.

Mahitaji

  • Ndoo ya maji ( iliyojaa hadi pomoni)
  • Mawe/kokoto/mawe makubwa
  • Vitambara/vijipande vya turubai

Maagizo

1. Weka ndoo ya maji kwenye hema ambalo limetandazwa chini au kwenye sakafu ambayo haiwezi kudhuriwa na maji. Waulize washiriki wanachodhani kitatendeka iwapo utatupa mawe kwenye ndoo hiyo.

2. Tupa mawe kadhaa kwenye maji hadi maji yaanze kumwagika.Waambie ya kwamba mawe yanawakilisha picha za ponografia, ndoo inawakilisha mawazo yao, na maji ni mtazamo wao “msafi” juu ya mahusiano ambao haujapotoshwa.

3. Elezea kwamba kama vile mawe yanapozama chini ya ndoo, yanalazimisha maji kumwagika nje. Vile vile tunapotazama picha za ngono, zinazama katika mawazo yetu na kutufanya kupoteza ubikira wetu wa kimawazo kutokana na maswala ya ngono, hali hii aidha inaathiri uhusiano wetu na wenzetu wa jinsia tofauti.

4. Endelea kuongeza mawe zaidi katika ndoo ya maji. Kila jiwe husababisha tone la maji kumwagika, kama vile picha za ngono zinavyotufanya kupoteza usafi wetu katika mtazamo wetu.

5. Acha kuongeza mawe. Uelezee washiriki kwamba hata unapoacha kutazama picha za ngono zile picha ambazo uliona hapo awali zina mnato mkubwa na uwezo wa kusalia kwenye mawazo kwa kipindi kirefu. Huwezi kuzifuta kutoka akilini kwa urahisi. Wala usafi wako wa mawazo kuhusiano na maswala ya ngono hauwezi kurejeshwa tena baada ya kuchafuliwa na picha za ngono, kama vile maji yaliyomwagika ambavyo hayawezi kurudi kwenye ndoo.

Kwa bahati mbaya, picha hizi za ngono hubadilisha mtazamo wetu wa mahusiano na zinakwama akilini mwetu, hivyo basi kuathiri mahusiano yetu ya baadaye. Kile kinachoweza kuchukuliwa kama uamuzi wa mtu binafsi kinaweza kumuumiza mtu mwingine vibaya sana.

Kwa wale ambao wanakabiliwa na athari za uraibu wa maswala ya ponografia, elewa kwamba haupaswi kuficha swala hili. Ni jambo la busara kuchukua hatua bila kuyumbayumba ili kujinasua kutoka kwenye minyororo ya uraibu huu , haijalishi kiwango cha uzito ambacho uraibu huu umekuathiri.

Hatua Tatu Kukabiliana na Uraibu wa Ponografia

Slides Icons

1. Kubali - Uwe jasiri na ukubali ponografia ni tatizo
Kukubali tatizo ni hatua ya kwanza ya mabadiliko. Unaweza kujihatarisha ukakamatwa au ukapoteza sifa yako, lakini uraibu wa aina yoyote—hasa ngono—si jambo la kuchukulia kirahisi.

Handbook 46 Icons

2. Badilika – Kubadilika kwa ujumla
Jitahidi kudhibiti nyanja mbalimbali za maisha yako kama vile mwili, akili, hisia na imani na uhakikishe kwamba viungo hivyo vyote vina mshikamano.

  • Mwili
    Tambua udhaifu wako. Ikiwa una mazoea ya kuangalia filamu za ngono wakati una uchovu, au unapohisi njaa kama njia moja ya kujitosheleza au kujitia nguvu, basi anza kutilia maanani tabia ya kula vizuri na kuwa na mpango mahsusi wa kupumzika. Elekeza nguvu zako katika kitu kitakachokufurahisha na kukunufaisha. Wakati watu wengine wanapofanya mazoezi ya viungo au kujihusisha na shughuli za kuendeleza nidhamu, wengine hucheza michezo ya pamoja kama timu, michezo ya kuogelea, kukwea milima na kadhalika.
  • Mawazo
    Kuwa mwangalifu wa mambo unayoyaruhusu kuingia mawazoni mwako. Je unawafikiria watu wanaokuzunguka kwa njia ambazo ni za fadhili na heshima? Unawaona jinsi walivyo wakamilifu au unafikiri jinsi unavyoweza kujinufaisha, ukiwaangalia mawazo mapotovu yanaijaza akili yako? Badala ya picha chafu za mambo ya ngono yaliyomo kwenye ponografia weka mawazoni mwako picha ambazo ni za afya; jifunze kutambua uthamani wa binadamu. Anza na watu ambao unawajua kwa kuorodhesha tabia zao nzuri unazozipenda, na uwaambie ni kwa nini unawathamini (zaidi ya maumbile yao)
  • Hisia
    Ni kawaida kujihisi duni maishani. Hata hivyo, tunapaswa kukabiliana na mambo ambayo yanatunyima furaha kwa njia ya manufaa. Kuwa na marafiki unaowadhamini ambao unaweza ukawaelezea changamoto za mawazo na hisia zinazokukumba ni bora zaidi. Kushirikiana na marafiki kama hao kunaweza kutufaa sana kuliko kukimbilia kutazama picha za ngono iwapo tumekumbwa na changamoto.
  • Imani / Itikadi
    Imani yako itaathiri msimamo wako kuhusu uhusiano. Iwapo unafikiria kwamba maisha yanakuhusu tu “wewe” peke yako, na ngono ndicho kitu muhimu katika uhusiano, basi mtizamo huu utaathiri mwelekeo wako katika mahusiano. Itaathiri jinsi utakavyoshughulikia hii tabia ya kutazama ponografia.

3. Uwajibikaji - Chukua hatua madhubuti
Iwapo una matatizo kuacha hii tabia licha ya kukusudia kuiacha, pata msaada! Zungumza na mzazi au mshauri wa kitaalamu- kujadili swala hili kutasaidia kuondoa aibu na siri iambatanayo na tabia hii. Kujitenga hakutasaidia kwani kutaongeza hali ya uraibu. Wengi wamepambana na swala hili hakuna haja ya kujificha. Unaweza kujiondoa katika mtego wa tabia hii na athari zake dhidi yako.

Blank Icons

Chukua hatua madhubuti kukatisha na kusimamisha tabia hii isiendelee kukolea na kuzama ndani yako na kukita mizizi kabisa. Hatua ambazo unapaswa kuchukua ni pamoja na:

  • Tumia mfumo wa kuchuja mtandao ili kuondoa vitu ambavyo vinaambatana na picha za ngono.
  • Tumia au weka tarakilishi yako mahali wazi, usiitumie unapo kuwa chumbani mwako pekee yako, ambapo unaweza ukajaribiwa kuitumia ikizingatiwa kuwa hamna mtu anayekuona.
  • Jadili changamoto unazopitia na mtu mzima ambaye unamwamini ambaye ataweza kukuhimiza kujitenga na kila aina ya picha za ngono. Mruhusu mtu huyo kudurusu historia ya kuvinjari mtandaoni. Hali hii itakupunguzia majaribio ya kujihusiha tena katika mambo ya picha za ngono. Hata hivyo, inafaa kufahamika kuwa, ni vigumu kujiwekea mipaka kibinafsi bila kushirikisha watu wengine tukikusudia kuangamiza uraibu huu kabisa kwani mara nyingi, tutapata vijisababu vya kuturejesha katika tabia ya kutazama picha za ngono tena.

Unaweza Kuanza Upya

Instructions For The Facilitator Icons

ANZA UPYA: Unaweza ku-waya upya-/kuondoa waya-wa-sasa kwenye ubongo wako

Bila kujali kama umejihusisha na ponografia, unaweza kuuwasha ubongo wako uanze upya ili kuepuka matokeo mabaya ya ponografia.

Ikiwa umekuwa katika tabia hizi kwa muda, usikate tamaa. Jambo lile lile lililosababisha ubongo wako kuwa na mazoea ya kutazama ponografia linaweza kukusaidia pia kutoka.

Kila wakati unapofanya chaguo la kutotenda kulingana na tabia hizi, unadhoofisha njia katika ubongo wako ambayo ilikufanya uvitake vitu hivi.

Kwa hiyo kadiri unavyochagua kutotazama ponografia mara nyingi zaidi, ndivyo itakavyokuwa rahisi kwako kujiepusha na mazoea haya.

Blank Icons

UDHIBITI: Ni katika udhibiti wako ni kitu gani utakachofanya

  • [Rejelea: mwelekeo wa kiakili ya mwanadamu]

Tambua vichochezi vyako

  • Mara nyingi, tamaa zetu ni nzuri [k.m., ni kawaida kuhisi haja ya urafiki au kuwa wake]. Njia nzuri ya kukidhi hitaji hili itakuwa kuwaita marafiki zako na kubarizi nao, kushiriki katika shughuli ya afya kama vile kufanya michezo au kutazama filamu pamoja.
  • Lakini nyakati fulani tunaweza kushawishiwa kutimiza tamaa hizi kwa njia zisizo na afya. Kwa nini? Baadhi ya watu huhisi hamu ya kutazama ponografia wanapohisi upweke/huzuni/ hasira/msongo wa mawazo.
  • Vichochezi vya kawaida: Njaa, Hasira, Upweke, Uchovu, Mkazo.
  • Unapojikuta na tamaa ya kuangalia ponografia, chunguza kwa kujiuliza: Ni kitu gani kimetokea ambacho kinanifanya nitake kutazama ponografia? Inawezekana ulikuwa na ugomvi na rafiki mzuri na hiyo ikakufanya uhisi huzuni na kutoeleweka. Unataka kupata faraja na kitulizo fulani, na hivyo unageukia ponografia ili ujisikie vizuri.

“Ripoti”: Mwambie mtu unayemwamini

  • Usihisi kwamba unapaswa kukabiliana na ponografia peke yako. Kumbuka kwamba watu wengi wamejihusisha au wameonyeshwa ponografia.
  • Ukigundua kuwa tayari umekuwa mraibu, usaidizi fulani wa nje na wa ziada ni wa manufaa ili kudhibiti tabia hiyo. Unaweza pia kuwasiliana na washauri wako wa shule kwa usaidizi.
  • Zungumza na wanafamilia au marafiki unaowaamini kuhusu nia yako ya kuacha na wakusaidie katika safari hii na kukuhimiza. Utashangazwa jinsi ambavyo uwajibikaji unavyotusukuma kutenda ipasavyo Kushiriki na mtu unayemwamini kunamruhusu kukuhimiza kubadilika.

MBADALA: Tafuta shughuli mbadala zenye afya au unda tabia mpya chanya

Zibadilishe tabia mbaya na uwe na tabia nzuri

Waambie washiriki:

  • Usifikirie dubu mweupe wa polar. Kubeba mwavuli. Kuendesha baiskeli. . . Waulize swali, Unafikiria nini sasa hivi? (dubu mweupe wa polar).
  • Inashangaza, jinsi tunavyozingatia kutofanya kitu, ndivyo tutakavyotaka kukifanya. Njia bora ni kufanya kitu kingine.
  • Ikiwa sitaki kutazama ponografia, badala ya kuelekeza nguvu zangu katika kutofanya hivyo, badala yake ninapaswa kuzingatia kitu chanya ninachoweza kufanya.
  • [Kwa mfano, ninaweza kujishughulisha na kubarizi na marafiki zangu, kucheza michezo au kufanya shughuli nyingine muhimu za kiafya kama vile kujitolea katika jumuiya.]

Jiulize: Je, kuna njia nyingine za kuvunja mzunguko wa vichochezi vyangu?

  • Ikiwa ni upweke ndio unaokusukuma kupata faraja na kitulizo katika ponografia, unaweza kuzungumza na rafiki yako unayemwamini kuhusu hali hiyo.
  • Fanya vitendo. Huenda ikawa unawapa ruhusa ya kuangalia mara kwa mara jinsi unavyofanya katika kuacha tabia hizi.
  • Labda unaweza kufanya mapatano na wazazi wako kwamba utawaambia kila mara unapohisi msukumo wa kutenda kulingana na mazoea hayo, na kwa njia hiyo, wanapojua, wanaweza kuzungumza nawe na kukusaidia kuchagua jambo lingine ambalo ni chanya. Zingatia kile kitu cha afya unachotaka kufanya badala yake.

Jiulize: Je, kuna njia bora na yenye afya zaidi ya kukidhi hitaji hili?

  • Inaweza ikawa kwenda kukimbia ili kupata mawazo safi kichwani. Huenda ikawa ni kumwendea rafiki uliyekosana ili kurekebisha urafiki na kushughulikia mambo yaliyokusumbua.

Kuimarisha ulinzi

Linda tabia zako za kiafya ili kujikinga na nyakati za udhaifu. Uwe na mazoea ya kuacha mlango wako wazi au angalau ukiwa umefunguliwa. Jijengee mazoea ya kutumia vifaa vyako vya rununu na dijitali ukiwa sebuleni au maeneo mengine “ya umma” nyumbani. Sakinisha vichungi kwenye simu mahiri na kompyuta ya mkononi,

FUTA: Futa mazoezi na tabia mbaya kutoka kwenye maisha yako

Jiondoe kutoka katika hali tatanishi zisizofaa

  • GEUKA kwa bidii kutoka kwa kile kinachoweza kukurudisha kwenye mazoea yasiyofaa. Ni jambo la hekima KUTOkaribia majaribu, hasa unapojua uko katika hali hatarishi [k.m., kujifungia mwenyewe ili kujihurumia baada ya kuvunjika kwa uhusiano; kusikiliza muziki wenye maneno yenye kuchochea ngono].

Ondoa vitu vinavyoweza kukunasa

  • Ondoa vichochezi mahali unapoweza [k.m., kutupa nyenzo za ponografia zilizopo hapo; ondoa kitu cha faraja ambacho unakihusisha na ponografia].

Weka matarajio halisi utakayoweza kufikia!

  • Ikiwa umekuwa katika tabia hizi kwa muda, haitakuwa rahisi wala haitakuwa mabadiliko ya mara moja. Kwa hivyo ukianguka tena katika tabia mbaya, usijisikie hatia kupita kiasi. Badala yake, zingatia jinsi unavyoweza kufanya vizuri zaidi wakati ujao.
  • Kumbuka kwamba kila unapofanikiwa kuchagua kutotenda kulingana na matakwa haya, itakuwa rahisi zaidi kutoka kwenye tabia hizi (zizibe njia zilizo kwenye ubongo wako) na kujenga mpya za afya na za manufaa (tengeneza njia mpya kwenye ubongo wako).

Hitimisho

Slides Icons

Ni nani anayesukuma mkokoteni?

Uwe mtumiaji mwenye busara! Usiruhusu vyombo vya habari kuamuru maisha, maadili na uhusiano yako. Linapokuja suala la vyombo vya habari:

Handbook 49 Icons
  • Je ni wewe uliyeko katika mkokoteni au wewe ndiwe unayesukuma mkokoteni?
  • Je, unatumia teknolojia au teknolojia inakutumia?
  • Je, unashawishiwa au unakuwa mshawishi chanya?

Tunapokuwa watu wa kupokea tu jumbe kutoka kwa vyombo vya habari, tunaruhusu ujumbe wa kila aina katika akili zetu pasipokuwa na msimamo au uwezo wa kuzichuja, na namna ya kuzichukulia. Kwa mfano baada ya shughuli za siku nzima, sisi hutaka kurudi nyumbani na kujituliza mbele ya runinga. Kwa msingi sisi huketi chini na kuruhusu runinga ituzungumzie pasipokufikiria kuhusu ujumbe husika na namna unavyoathiri mtazamo na imani yetu.

Kuwa mtazamaji shirika, kunaanza na kuelewa jinsi tunavyoathiriwa na jumbe za vyombo vya habari na kisha kutenganisha (kuchuja) ujumbe mzuri kutoka kwa ule mbaya. Tunaanza kutambua jinsi vile matangazo ya biashara hutuchukulia, au maoni ambayo kipindi kinataka kuleta kwa mtazamaji, na kutathmini jinsi ujumbe huo unavyokubaliana au kutofautiana na misimamo na maadili yetu. Kisha tunaanza kuamua iwapo ujumbe husika ni wa ukweli au ni maoni yaliyopotoshwa na lengo la kumhadaa msikilizaji.

Si kwamba yote ambayo yamo kwenye vyombo vya habari ni mabaya.Jambo kuu ni : Ni nani anayesukuma mkokoteni?Je uko katika mkokoteni ukisukumwa hapa na pale, ukiruhusu vyombo vya habari kukuelekeza kiimla namna unavyofikiria au kukuamrisha kuhusu ni nini unapaswa kufanya? Au je, wewe unasukuma mkokoteni ukielekeza ujumbe huo kulingana na ule ujumbe ambao una uruhusu uje maishani mwako?

Teknolojia na vyombo vya habari ni nguvu ya manufaa tu wakati inaposimikwa na kuungwa mkono na maadili mema na chanya.

Changamoto kwa vijana kubadili simulizi:

  • Vyombo vya Habari Vijana wana uwezo wa kujenga ufahamu,
  • Vyombo vya Habari Vijana wana uwezo wa kuweka ajenda,
  • Vyombo vya Habari Vijana wana uwezo wa kupendekeza na kushawishi, uwezo wa kuwasilisha habari mpya chanya, na uwezo wa kushawishi. Kuwa mfanya mabadiliko!
Going Home Icons

Kwenda Nyumbani

Maswali ya Majadiliano ya Mzazi/Kijana kwa Kitengo cha 2

Mzazi mpendwa,

Katika Hakuna Majuto® Kitengo cha 2, tulijadili athari za vyombo vya habari katika utamaduni wetu.

Vyombo vya habari vichache sana huonyesha vijana ambao hawashiriki tendo la ndoa kwa mtazamo chanya. Ngono inauzwa, na vyombo vyetu vya habari huiuza wakati wote. Vijana wamezingirwa pande zote na jumbe za ngono. Kujaribu kuchuja jumbe hizo ni changamoto kwa vijana wanaokulia kwenye utamaduni huu.

Vijana walijifunza [GA 10] katika Kitengo cha 2 jinsi ya kukuza utambuzi kupitia kutathmini maneno, vipindi vya televisheni na filamu kutofautisha jumbe nzuri na zile zisiofaa. Pia walitathmini matangazo ya biashara na majarida ili kufuatilia jinsi utangazaji ambavyo hutegemea mvuto tofauti wa kihisia.

Maswali:

  1. Je, tunatumia muda kiasi gani kuzungumza kama familia dhidi ya kuwa kwenye vifaa vyetu? Tunawezaje kufanya maendeleo kama familia?
  2. Je, wewe (Mzazi) unakumbana vipi na shinikizo hasi la rika na unastahimili vipi? Je, wewe (Kijana) unapataje shinikizo hasi la rika na unakabiliana nalo vipi?
  3. Tazama filamu au kipindi cha televisheni pamoja na zungumza kuhusu ujumbe unaoonyeshwa na filamu/kipindi. Uliza: Je, ni ujumbe gani mzuri kutoka kwa filamu/onyesho hili? Uliza: Je, ni ujumbe gani hasi kutoka kwa filamu/kipindi hiki?

Kitengo hiki huwasaidia vijana wanaobalehe kuelewa kwamba kuweka mipaka ya kihisia na kimwili huleta uhuru wa kweli na ni muhimu katika kujenga mahusiano bora.

KITENGO 3.1: Kuielewa mipaka

KITENGO 3.2: Mipaka na kuepuka kujihusisha kwenye tabia hatarishi

KITENGO 3.3: Mipaka kwenye mahusiano

KITENGO 3.4: Madhara ya kuvuka mipaka

KITENGO 3.5: Kupunguza hatari ama kuondoa hatari?

Lengo

Kuwawezesha wanaoshiriki kuelewa umuhimu wa kuweka mipaka katika maisha yao – mipaka wanayoweka leo ina umuhimu kwenye maamuzi yao siku za usoni na kuna athari iwapo mipaka iliyopo haitazingatiwa vizuri. Mipaka inapashwa kutegemea maadili yetu na yale mambo ambayo ni muhimu kwetu.

Usuli

Katika kitabu chao kinachohusu mipaka wakati wa uchumba , Daktari Henry Cloud na Dr John Townsend waliandika, ‘”Mipaka ina umuhimu na majukumu mawili. Kwanza, mipaka inatutambulisha kwamba tuko watu wa namna gani kwa yale tunayo kubaliana nayo, tusiyoyakubali, tunayoyapenda na tunayoyachukia.”

Tunawezakosa kujieleza kwa kina mbele ya marafiki, lakini wakati wa mazungumzo baina yetu, mahali ambapo mipaka ipo ama haipo panajieleza wazi na kuwaonyesha sisi ni watu wa hulka ipi. Ninapochagua kujiusisha katika tukio fulani, ninaonyesha kwamba ninakubaliana na matendo, maadili na hisia zinazoambatana na hilo. Kinyume chake, ikiwa ninakataa kabisa kutoshiriki katika mdahalo huo ni dhahiri ya kutofurahia matendo, maadili na hisia zinazoambatana na yale yatakayo afikiwa. Kwa mfano, ninaamua kushiriki katika michezo, kwa sababu ninaamini inasaidia kuishi maisha yenye afya bora na kufurahia uzima; ninakataa kujiunga wakati marafiki zangu wanapowadhihaki wengine, kwa sababu watu wanafaa kuheshimiwa jinsi walivyo na wasidharauliwe kutokana na maumbile yao, ulemavu, ama kasoro zao.

Dr Henry Cloud na Dr John Townsend pia wameandika, “Kazi ya pili ya mipaka ni kwamba inatulinda. Mipaka inahifadhi mambo mazuri na mambo mabaya yanawekwa pembeni. Tunapokosa kuwa na mipaka iliyo dhahiri, tunaweza jiusisha na vikundi vya marafiki wasio na tabia nzuri … Mipaka inawatambulisha wengine kama utalikubali hilo ama laa.”

Kukiwepo mipaka inajidhihirisha wazi kama unatendewa wema ama kuhusishwa na mambo yasiyo mema, na hilo litachangia ni maamuzi yapi utakayochukua katika kujilinda na hilo. Bila mipaka, itakuwa vigumu kwako na kwa wengine kujua ni ni lipi linalofaa na linalokubalika. Mara nyingi, watu ambao hawana mipaka iliyo wazi wanakerwa pasipo wao kufahamu ama linawapata ghafla.

Unapokuwa umeweka mipaka, unaweza kufanya maamuzi yaliyo mema, kwa mfano uhusiano kati ya msichana na mvulana, na umbali ambao mtakaribiana katika uhusiano huo?

Mipaka isipokuwepo mnaweza kuangukia katika vitendo ambavyo mtajutia baadae, ama kujikuta katika majukumu ambayo bado hamko tayari kuyashughulikia. Kinyume na hilo mipaka inakuletea uhuru zaidi wa kibinafsi- kuchagua- badala ya kuruhusu marafiki, homoni, na matokeo kukuchagulia.

Katika kitabu chake Boundaries, Where to Draw the Line, Anne Katherine aandika, “kwa kila tukio, sisi huonyesha kwamba tutalinda kile tunachothamini au kwamba tutajitoa. Mipaka yenye afya huhifadhi uadilifu wetu. Tofauti na ulinzi, unaotutenga na utu wetu wa kweli na wale tunaowapenda, mipaka huchuja madhara.”

Activities Icons

Zoezi 1: Tambua Maadili Yako

Blank Icons

Lengo

Wasaidie washiriki kutambua maadili yao ya binafsi kwa sababu yanaathiri maamuzi yao na uwezo wao wa kuweka mipaka yenye afya maishani.

Mahitaji

  • Waombe washiriki waandae karatasi 16 zenye umbo la miraba midogo 16 (au noti za kunata za Post-It).

Maagizo

Tumia kipande kimoja cha karatasi kuandika na kubainisha yafuatayo:

Values
  • Shughuli TATU Unazozipenda (3)
  • Watu WATANO muhimu katika maisha yako (5)
  • Malengo MATATU ya maisha yako ya baadaye (3)
  • Vitu / mali TATU Uzipendazo (3)
  • Mambo MAWILI ambayo ungependa kumiliki siku moja (2)
Blank Icons

Kila shughuli, mtu, lengo, milki unayopenda na kitu cha kumiliki siku moja, viandikwe kwenye kipande tofauti cha karatasi.

Kabla ya kuanza, waambie washiriki waviweke vipande vyao vyote vya karatasi juu ya meza zao.

Waambie washiriki utakuwa unasoma hadithi fupi. Baada ya kila sehemu ya hadithi, wataombwa kufanya uamuzi na watapewa sekunde 10 kufanya hivyo.

Soma hekaya iliyopo hapa chini kwa sauti, kila baada ya kitengo (sehemu) nyamaza kwa sekunde 10 ili kuwaruhusu washiriki kufanya uamuzi ni kipande kipi cha karatasi watakachochagua kutupa kando. Karatasi iliyotupwa lazima ikunjwe au kuchanwa.

Blank Icons

Soma Hadithi

MARA MOJA . . .

Values 1

1. Ulienda kwenye mbuga za wanyama na kuumwa na aina ya mdudu adimu. Unaanza kujisikia kuwa mgonjwa, na daktari wako anagundua kuwa una ugonjwa mbaya sana. Hana uhakika jinsi ya kukutibu na pia hana uhakika kama ugonjwa huo unaua. Anasema ni lazima uache MOJA ya shughuli zako unazozipenda.

  • [Nyamaza kwa sekunde 10 ili kuruhusu washiriki kufanya uamuzi]
Values 2

2. Umelazwa hospitalini kwa muda mfupi kwa sababu ya ugonjwa wako. Lazima uache MOJA ya malengo yako.

  • [Nyamaza kwa sekunde 10 ili kuruhusu washiriki kufanya uamuzi]
Values 3

3. Kwa sababu ya kutokuwepo kazini kwa muda mrefu, huna pesa na huna budi kuacha MOJA kati ya vitu/mali zako unazozipenda.

  • [Nyamaza kwa sekunde 10 ili kuruhusu washiriki kufanya uamuzi]
Values 4

4. Unahitaji kulazwa hospitalini tena kwa sababu ya ugonjwa mbaya wa kuambukizwa. Malipo ya matibabu ni makubwa sana na inabidi utoe MOJA ya vitu/mali zako nyingine uzipendazo.

  • [Nyamaza kwa sekunde 10 ili kuruhusu washiriki kufanya uamuzi]
Values 5

5. Unajaribu kuendelea na kazi yako lakini umechoka kutokana na ugonjwa wako. Unapoteza MOJA ya malengo yako na lazima uachane na MOJA ya shughuli zako nyingine. Pia, kwa sababu sasa huwezi kudumisha mahusiano, watu WAWILI muhimu wametoka maishani mwako.

  • [Nyamaza kwa sekunde 15 ili kuruhusu washiriki kufanya uamuzi]
Values 6

6. Ugonjwa wako unazidi kuwa mbaya na unapaswa kulazwa hospitalini moja kwa moja. Unaruhusiwa kuwa na mgeni (mtu) MMOJA tu na unaweza kuchukua kitu KIMOJA pekee unachokipenda hospitalini. Tupa watu WAWILI muhimu, kitu/mali MOJA unayoipenda na kitu kimoja ambacho ungependa kumiliki siku moja.

  • [Nyamaza kwa sekunde 15 ili kuruhusu washiriki kufanya uamuzi]
Values 7

7. Daktari wako ameipata hospitali moja nje ya nchi yenye utaalamu wa kutibu walioumwa na wadudu nadra. Unahamia huko maisha yako yote ili kuishi karibu na hiyo hospitali, iwapo utapata dalili za ugonjwa tena. Lazima utoe karatasi zako TATU kati ya zilizobaki. Zitakuwa ni nini?

  • [Nyamaza kwa sekunde 15 ili kuruhusu washiriki kufanya uamuzi]
Values 8

8. Unaanza maisha yako upya na mtu huyu tu, lengo, shughuli, mali au kitu ambacho ungependa kumiliki siku moja. (vipande 2 vya karatasi vimesalia)

  • [Nyamaza kwa sekunde 15 ili kuruhusu washiriki kufanya uamuzi]
Blank Icons

ULIZA: Je, kuna baadhi ya uchaguzi uliokuwa mgumu zaidi kuufanya?

  • Maamuzi yetu yanatokana na maadili tuliyo nayo. Ingawa ni muhimu kuheshimu maadili na sheria za wengine, ni vigumu kuwa mtu halisi na anayejiheshimu kama hutaishi kulingana na maadili na sheria zako mwenyewe. Maamuzi tunayofanya yanaonyesha kile tunachothamini sana maishani. Hivi ndivyo unavyoanza kujiwekea mipaka yenye afya.

Kwa Nini Maadili Ni Muhimu?

Maadili yetu yanapokuwa wazi, yanaweza kutusaidia kujibu maswali haya magumu sana:

  • Ni nini hufanya maisha yangu yawe na maana?
  • Je, ninawashawishi wengine kwa njia zipi?
  • Ni kazi gani yenye thamani kwangu?
  • Ni mtu wa aina gani ambaye ningetaka kama mwenzi wa maisha?

Mifano ya kuwa na maadili fulani:

  • WAJIBU
    John alikubali uzito wa matokeo ya matendo yake wakati mradi wa kikundi chake uliposhindwa kufanikiwa, kwa sababu ya thamani anayoiweka kwenye kuwajibika.
  • HUDUMA
    Kwa sababu Sam anathamini huduma kwa wengine, yeye hutumia wikendi yake kujitolea katika shirika la kutoa misaada.
  • FAMILIA
    Familia ni kipaumbele kwa Sue, kwa hiyo anajitahidi kuwa nyumbani kwa chakula cha jioni kila siku licha ya ratiba yake ya shughuli nyingi.
  • KUJIHESHIMU
    Kwa kuwa Janice anawekea mkazo kujiheshimu, aliachana na mpenzi wake ambaye hakuyaheshimu maoni yake na alikuwa akimdharau kila wakati mbele ya wengine.

Kwenda Dijitali

Toleo la dijitali la shughuli hii linaweza kupatikana hapa.

Blank Icons

ZOEZI MBADALA
Zoezi 2: Tambua Maadili Yako

Blank Icons

Lengo

Wasaidie washiriki kutambua jinsi maadili yao yanavyoathiri maamuzi wanayoyafanya.

Maagizo

Waambie washiriki utasoma mfululizo wa chaguzi mbalimbali nao wanahitaji kuamua ni chaguo lipi katika hayo wanalolipendelea. Wanaweza kuonyesha chaguo lao kwa kusimama kama wanapendelea chaguo katika safu X, na kukaa chini kama wanapendelea chaguo kutoka safu ya Y. (Kwa kipindi cha mtandaoni, wanaweza kutumia majibu ya “dole gumba” kwa safu X na “makofi ” kwa safu Y).

Je ungependa X au Y:

XY
Tumia SpotifyTumia Netflix
Tumia InstagramTumia TikTok
Kuwa jukwaaniKuwa katika hadhira
Poteza funguo za nyumba yakoPoteza simu mahiri
Kuwa mwanamichezoKuwa msanii
Fanya kazi katika kikundiFanya kazi peke yako
Kukwama kisiwani na mtu ambaye hawezi kuacha kuongeaKukwama kisiwani peke yako
Kuwa na marafiki wengi wa wastaniKuwa na rafiki mmoja mzuri sana
Kumuoa mwenzi unayempenda sana (mtu wa ndoto zako)Uwe na kazi unayoitamani sana (ndoto yako)
Kuwa na muda na marafikiKuwa na muda na familia
Uwe na afya njema lakini maskiniUwe mgonjwa karibu ya kufa lakini uko tajiri
Watu wafurahie matendo yako memaWatu wakuheshimu kwa uwezo wako

Wawezeshaji wanapaswa kujumuisha yale yanayofaa na maarufu katika nchi yao.

ULIZA: Je, kuna baadhi ya uchaguzi uliokuwa mgumu zaidi kuufanya?

  • Waombe washiriki watoe mifano ya chaguzi ambazo waliona ni ngumu kuzifanya na waeleze walifikiaje uamuzi wao
  • Tunafanya maamuzi kila siku. Maamuzi mengine ni rahisi na mengine ni magumu yanahitaji kufikiriwa zaidi. Kile tunachothamini huathiri maamuzi na uchaguzi wetu. Kwa sababu hii, ni muhimu kwetu kuzingatia maadili yetu—kile tunachokiona kuwa muhimu. Kujua kile tunakichothamini hutusaidia kuweka mipaka inayofaa na kufanya maamuzi mazuri maishani.

ULIZA: Tunapata wapi maadili yetu?

  • Je, yaliathiriwa na mtu fulani katika mduara wangu wa kijamii au yaliathiriwa na taarifa nilizozipata kutoka kwenye vyombo vya habari?
  • Je, ni uamuzi ulioufanya ukiwa na taarifa kamili na unataka kuupitisha kwa sababu utakunufaisha?
  • Maadili yanaweza kubadilika kutegemea na marafiki tunaojihusisha nao na ujumbe tunaoukubali kutoka kwenye vyombo vya habari, lakini nguvu ya tabia zetu HAIBADILIKI.
  • Kwa hiyo, ni muhimu kuendelea kujenga na kuimarisha tabia zetu ili maadili yetu yasibadilike na kuwa legelege njiani.

Ni lazima kufikiria kwa makini ili kuweka mipaka yenye afya na kufanya maamuzi mazuri.

Activities Icons

SHUGHULI MUHIMU
Zoezi 3: Ana kwa ana

Blank Icons

Lengo

Wasaidie washiriki kuelewa mipaka – kujifunza kwamba mipaka inatambuliwa kibinafsi na maamuzi ya kipekee yanafaaa kuheshimiwa.

Slides Icons

Mahitaji

  • Onyesha slaidi ya “Ana kwa Ana”
  • ULIZA: Tunapata wapi maadili yetu? Je, yaliathiriwa na mtu fulani katika mduara wangu wa kijamii au yaliathiriwa na taarifa nilizozipata kutoka kwenye vyombo vya habari? Wape kila mtu jozi, mvulana na mvulana, na msichana na msichana. (Ikiwezekana kila jozi isijumuishe marafiki wa karibu)
  • Acha kila jozi iamue ni nani atakuwa “A” na nani atakuwa “B” na uwafanye wasimame wakitazamana kama inavyoonyeshwa kwenye mchoro hapa chini.

A

◀︎UREFU WA MIKONO MITATU▶︎

B

A

◀︎UREFU WA MIKONO MITATU▶︎

B

Blank Icons

Maagizo

1. Elekeza “A” Kuchukua hatua moja baada ya nyingine kuelekea “B”na kusimama karibu na “B” karibu iwezekanavyo hadi “B” atakapoinua mkono kuomba asimame. “B” pia anaweza kumuomba “A” kurudi nyuma ikiwa anahisi kuwa “A” amekuwa karibu sana.

2. Umbali wa mwisho kati ya “A” na “B” unaashiria mipaka ya nafasi ya kibinafsi ya “B”. Unaweza kutumia mkanda unaonata kuashiria umbali lakini waambie wabakie kwenye nafasi zao.

3. Uliza kundi “B”: Je, ungejisikiaje ikiwa “A” atachukua hatua nyingine karibu nawe baada ya wewe kuinua mkono wako? Kwa nini?

  • Je, ikiwa si rafiki yako lakini mgeni kabisa kwenye kituo cha basi?
  • [“B” anapaswa kuonyesha usumbufu fulani kama mwenzake atasogea karibu na “kuvuka mstari.” Kama anayejisogeza ni mgeni kabisa, kiwango cha usumbufu kinapaswa kuwa kikubwa zaidi.].

4. Elezea kwamba “umbali salama” huu unatenganisha kile kinachojulikana kama “nafasi ya kibinafsi” ya mtu. Ni mpaka ambao kila mtu amejizungushia.

  • Tunapohusiana na watu nao wakabaki nje ya mipaka hii, tunafurahia uhusiano wetu. Hili linaweza kubadilika kadiri muda unavyoendelea, tukawaamini zaidi,na tunayo mipaka tofauti miongoni mwa watu tofauti mfano, kwa mfano marafiki wa karibu ama familia. Na iwapo mipaka itakiukwa, inasababisha hisia ya kutokuwa na usalama na inaleta wasiwasi na kutufanya tujihami.
  • Vile vile tunapaswa kuzingatia kuwepo kwa mipaka kwenye shughuli tunazo jiusisha nazo. Mipaka aina hiyo haipo « kutuzuia » bali kutulinda.
Slides Icons

Mipaka inatutambulisha...

Handbook 51 Icons
  • Wewe ni nani?
  • Unachofikiria, kuhisi, na kutenda?
  • Mapendeleo yako yale unayokubaliana nayo na usiyoyakubali, na kufanya maamuzi kulingana na yale uliyoamua kuwa muhimu kwako hapo awali.
  • Kile ulicho nacho na ambacho huhusiki nacho ili uendelee katika hatua ya kuthibiti na sio hisia zako, homoni, marafiki au hali.
Blank Icons

5. Waombe washiriki kuangalia na kulinganisha umbali uliopo kati ya kila jozi; kwa kawaida umbali unapaswa kuwa tofauti. Watu wengine wanahitaji nafasi zaidi; wengine nafasi ndogo, lakini kila mtu ana hitaji la nafasi ya kibinafsi na hii inapaswa kuheshimiwa.

  • Vile vile kwenye masuala ya shughuli mbalimbali, watu tofauti wana mipaka tofauti na muda ambao wameutenga kwa hilo. Kwa mfano watu wazima wameweka mipaka hawatabugia mvinyo kabisa jambo ambalo watu wengine wanalichangamkia, mradi wasilewe. Usifikiri kwamba kile kinachokubalika kwako pia kinakubalika kwa wengine; daima ujue na kuheshimu mipaka waliyoichagua wengine.
  • Weka mipaka kuambatana na unalolijua (litakufaidi) na sio jinsi unavyohisi Bila kujali wapi mstari unachorwa, kila mtu anahitaji mipaka ikiwa anataka kujilinda. Uamuzi ni wapi mipaka inahitajika kuambatana na hisia si kigezo bora cha kipimo hicho.
  • Kwa mfano, unafanya mazoezi ya mbio za marathon, lakini unapenda chakula cha haraka pia (kisicho cha afya). Kuweka mipaka yako juu ya ulaji wako wa vyakula vya haraka kulingana na jinsi unavyohisi kuhusu chakula cha haraka itakuwa upumbavu! Uamuzi wako wa kupunguza chakula cha haraka utategemea ukweli kwamba chakula cha haraka kina virutubishi kidogo, mafuta mengi na kuna uwezekano mkubwa kitakuzuia kufikia lengo lako la kuwa mwanariadha.

Hatua hiyo, ina ambatana na mambo mengine, tunaweza amua kuweka mipaka kuambatana na lipi litatufaidi na sio jinsi tunavyo hisi.

Going Deeper Icons

Kwenda Ndani Zaidi

Blank Icons

ULIZA: Je, ni vikwazo gani unakumbana navyo wakati wa kuweka mipaka bora?
Majibu yanayowezekana:

Handbook 51 Icons
  • Hofu ya kukataliwa au kupoteza marafiki
  • Hofu ya makabiliano
  • Hatia au aibu
  • Hatukufundishwa mipaka yenye afya
  • Kuhisi kuwa mahitaji ya wengine ni muhimu zaidi kuliko ya kwako
Blank Icons

Je, ni njia zipi za kushinda vikwazo hivyo?
Majibu yanayowezekana:

  • Tambua ni maeneo gani ya maisha yako ambapo unahitaji kuweka mipaka
  • Wafahamishe mipaka hiyo wengine.
  • Usiruhusu hatia au aibu kukuzuia kuweka mipaka. Hii mipaka ni sehemu muhimu ya kujitunza.
  • Chukua muda ujifunze jinsi ya kuweka mipaka. Ni mchakato.
  • Jizungushe na watu wanaounga mkono na kuheshimu mipaka yako.

Maisha na mahusiano yanaweza kuwa ya kusumbua zaidi bila mipaka. Kuwa na uhakika wa maadili yako na kuweka mipaka yako ili kuyalinda.

Activities Icons

SHUGHULI MUHIMU
Zoezi 4: Kipimo cha maisha

Blank Icons

Lengo

Wasaidie washiriki kuona ya kwamba Mipaka inaweza kuonekana kama inakuzuia mambo mengi bali itakuwezesha kuwa huru zaidi.

Mahitaji

  • Kipimo – funeli (hasa kikubwa na kinachong’aa)

Maagizo

1. Weka ngamba yenye maneno “Unapokataa” jambo hili leo … “unalikubali” jambo jingine siku zijazo.

2. Shikilia kichungi (faneli) juu mbele ya darasa ukielekeza upande wenye ncha pana.

3. Uliza: “Ni wangapi wenu kati yenu wanapenda uhuru? – hamna masharti; unaweza kutenda unalotaka.”

  • Waeleze kwamba tunaweza kuishi katika upeo mpana wa faneli wakati tukiwa wachanga-kujihusisha na mahusiano mengi yaliyo mapotovu na washiriki wa ngono wengi miaka mitano hadi kumi ya ujana wetu. Ama tunaweza kuchagua kuvuta sigara, matumizi ya mihadarati na unywaji wa pombe. Lakini tunapoendelea maishani, tunatambua kwamba baadhi ya matokeo yake yanapunguza uchaguzi wetu. Kwa mfano, ngono ya usiku mmoja inasababisha kupata mimba haramu, na mama mwenye umri mdogo anapaswa kuachana na ndoto zake za kwenda shule. Tunaishia kutumia miaka ya baadaye na sehemu kubwa zaidi ya maisha yetu katika mwisho mwembamba wa faneli—tukiwa na matokeo ya baadhi ya maamuzi mabaya tuliyofanya tukiwa kijana. Ni kama kupokezwa mkopo kutoka benki na kutumia vibaya na baadaye kulipa mkopo huo miaka kumi na hamna lolote ambalo la msingi ulilolifanya kutokana na mkopo huo.

4. Inua faneli tena lakini uelekeze kwenye ncha nyembamba.

  • Eleza kwamba ikiwa tutaweka mipaka katika mahusiano na shughuli zetu kwa “kujiwekea mipaka” sasa, tunaishi katika mwisho mwembamba wa fanelil. Polepole sogeza vidole vyako kwa mwendo wa kuelekea mwisho mpana na ueleze: Lakini kwa kweli tunajipa uhuru zaidi na zaidi—kufuatilia ndoto zetu katika siku zijazo na kufurahia mahusiano yenye afya.
Slides Icons

Mipaka ➡️Uhuru.

Handbook 51 Icons

Badala ya kutuwekea vikwazo, huleta uhuru wa:

  • kufahamiana kama marafiki
  • kufwatilia malengo ya maisha yetu
Blank Icons

Huenda mipaka isivutie kila mara lakini hutulinda.

Lengo

Kufahamisha washiriki kuwa ni rahisi kujikuta kwenye mtelemko mkali unaoteleza na wakajikuta mahali pabaya iwapo hawataeleza kwa uwazi mipaka yao waliyoweka kuhusu tabia hatarishi.

Usuli

Kwa njia moja ama nyingine, tayari tunaweka mipaka katika maisha yetu. Kwa mfano tunaweka mipaka inayozunguka vitu vyetu, twaweza kutambulisha mipaka kama “chumba changu cha kulala na vilivyomo ndani yake ni vyangu- nafurahi mama yangu akichukua nguo zangu ili kuzifua lakini sitaki aanze kupanga upya chumba changu.”

Kuna mipaka mingi ambayo inaweza zingatiwa maishani, na kweli kadiri ya mipaka inayofaa tunayoiweka, ndivyo tunavyojifungulia milango ya maamuzi mengi zaidi siku zijazo.

Activities Icons

Zoezi 1: Je, kweli si jambo la “Kutilia Mkazo”?

Blank Icons

Lengo

Wasaidie washiriki kutafakari juu ya maadhara ya tabia hatarishi na hitaji la kuweka mipaka.

Mahitaji

  • Ubao mweupe
  • Chaki
Small Group Icons

Maagizo

1. Gawa darasa lako katika vikundi vidogo (Kipindi cha mtandaoni: Gawa darasa katika vyumba vya vipindi vifupi)

2. Kipatie kila kikundi tabia hatarishi

3. Waombe washiriki kujibu maswali yaliyo hapa chini, nakili hoja zao kwenye ubao mweupe kulingana na tabia zao hatarishi. (Kipindi cha mtandaoni: Mteue mtu wa kuandika majadiliano)

Unafahamu nini kuhusu ... Pombe

Ni pombe aina ipi unayofahamu?

  • Majibu yanayowezekana: mvinyo, bia, vinywaji vikali, Vileo na kadhalika. Pia wanaweza kutoa majina mengine ya pombe hizo..

Je, nakili jina la pombe inayotambulika kote na wengi>inayo asilimia ngapi ya pombe?

  • Majibu yanayowezekana: bia ya nchini : karibia 5%, mvinyo : karibia 12%, vinywaji vikali (gin, ramu, tequila, vodka, whisky, nk) karibia 40%.

Je pombe inakuwezesha kuhisije?

  • Majibu yanayowezekana: vizuri, vibaya, kufurahi, kuhuzunika, mwenye mkururo wa fikira, huhisi chochote, mwenye usingizi, na kadhalika.

Je umri upi ni halali kununua ama kunywa pombe?

  • Tazama maelezo zaidi kuhusu pombe na umri unaokubalika kisheria.

Baadhi ya madhara ya unywaji wa pombe kupindukia ni nini?

  • Tazama maelezo hayo kuhusu madhara ya pombe na afya na uamuzi unaoambatana na hilo.

Ni kwa nini watu hunywa pombe?

  • Majibu yanayowezekana: Kupumzisha akili mtu kusahau yanayomkabili, kuwa mmoja wapo wa kikundi cha wanywaji, kufurahia ladha ya vinywaji hivyo, kusherekea/kilabuni, uraibu.

Unafahamu nini kuhusu Matumizi Mabaya ya dawa za kulevya

Ni mihadarati ipi unayofahamu?

  • Majibu yanayowezekana: opioid (dawa za kuagizwa na daktari) Heroin, Cocaine, Marijuana (Kumbuka kwamba baadhi ya washiriki wanaweza kutoa “majina ya barabarani” ambayo yanaweza yasiwepo kwenye orodha)

Je madawa ya kulevya yanamfanya mtu kujisikia namna gani?

  • Majibu yanayowezekana: Kumfurahisha mtu, kutulia, mwenye nguvu, mgonjwa, kusikia kichefuchefu, kuchanganyikiwa, kuishiwa nguvu kabisa, nk.

Je ni halali kutumia mihadarati?

  • Majibu yanayowezekana: Ndiyo (Kumbuka: Inawezekana mtu kutumia vibaya dawa zilizohalalishwa na baadhi ya dawa zilizoagizwa na daktari.) na Hapana (Sheria inakataza kumiliki na kusambaza, pamoja na adhabu kali zaidi kwa dawa za Hatari ambazo ni pamoja na heroini, methadone, kokeni, uyoga uliochakatwa wa hallucinogenic na LSD).

Baadhi ya madhara ya dawa za kulevya ni yapi?

  • Tazama maudhui ya ziada kuhusu utumizi mbaya na madhara ya mihadarati.

Ni kwa nini watu hutumia dawa za kulevya??

  • Majibu yanayowezekana: udadisi, shinikizo la rika, kuepuka matatizo, uraibu, kama njia ya kuboresha utendaji katika michezo, masomo na kadhalika.

Unafahamu nini kuhusu Uvutaji sigara

Ni kemikali sampuli ngapi zinapatikana kwenye sigara?

  • Majibu yanayowezekana: zaidi ya 7,000 katika moshi wa tumbaku ; angalau 250 zinajulikana kusababisha madhara.

Ni kemikali ipi inayosababisha uraibu wa uvutaji sigara?

  • Majibu yanayowezekana: aina ya Nicotine.

Unastahili kuwa na umri upi ili ununue sigara?

  • Tazama maelezo zaidi hapo chini: uvutaji sigara na umri unaokubalika.

Ni nini baadhi ya madhara ya kuvuta sigara?

  • Tazama maelezo zaidi: kuhusu uvutaji wa sigara.

Ni kwa nini watu huvuta sigara?

  • Majibu yanayowezekana:Watakavyoonekana kwa watu, kuondoa mkururo wa fikra, shinikizo la rika,kutaka kupunguza uzito, uraibu.

Kiasi gani unajua kuhusu. . . Kamari

Kamari ni nini?

  • Kamari ni wakati mtu yuko tayari kupoteza kitu cha thamani kwa matumaini ya kushinda na kupata kitu cha thamani zaidi

Je, kucheza kamari ni halali?

  • Kamari inaweza kuwa halali chini ya sheria katika baadhi ya nchi duniani lakini kunakuwa na vikwazo muhimu. (Kumbuka: waeleze sheria za mahali penu).

Watu hucheza kamari wakitumia vitu gani?

  • Pesa, nyumba, vitu vya thamani, heshima n.k.

Ni yapi baadhi ya madhara ya kucheza kamari?

  • Tazama Maudhui ya Ziada kuhusu Kamari kwa madhara ya kamari.

Kwa nini watu hucheza kamari?

  • Majibu yanayowezekana: Haja ya pesa, msisimko wa kucheza, kutumaini kupata utajiri kwa haraka, ukosaji kazi (haswa kwa wazee waliostaafu), kutafuta hasara, uraibu

4. Sahihisha kwa makusudi (na kwa upole) mitazamo isiyo sahihi, na utie mkazo taarifa sahihi.

5. Sisitiza kwamba orodha ya maswali inaisha na swali la kwa nini. Kwa nini watu wanajihusisha na tabia hatarishi :

Kwa nini watu wanajihusisha na tabia hatarishi?

  • Raha - unafuu wa papo hapo au starehe wanayoipata
  • Shinikizo - ushawishi wa marika au tabia zinazotarajiwa katika mazingira fulani
    [Unaweza kuleta wepesi katika haya mazungumzo mazito ikiwa washiriki watakisia motisha hizi mbili kwa kucheza mchezo wa “Kujitia kitanzi” (“Hangman.”)]
  • Motisha zote mbili hazizingatii matokeo ya muda mrefu yaletwayo na hivi vitendo. Wakumbushe washiriki kuhusu Funeli ya Maisha.

6. Elezea kwamba kuweka mipaka mizuri sio tu kuhusu kile wanachokihisi wao kwamba ni sawa; ni kufanya uamuzi makini wa jambo lililo sahihi kwao wenyewe na kwa wengine, bila kujali jinsi wananavyojihisi, na kuzingatia uamuzi huo.

Extra Content Icons

Maelezo Ziada

Blank Icons

Kuhusu Pombe

Pombe husababisha hisia tofauti kutoka katika tamaduni mbalimbali. Katika mataifa mengine kama vile Brunei ama Saudi Arabia pombe imepigwa marufuku kabisa, wakati nchi nyingine pombe ni sehemu ya urithi wa utamaduni wao kwa mfano nchini Ujerumani (bia) na Ufaransa (mvinyo).

Hata hivyo’ mataifa mengi yameweka kiwango cha unywaji wa pombe miongoni mwa vijana kupitia sheria ya kuwadhibiti. Kwa mfano taifa la Norway halina sheria inayolenga umri unaoruhusiwa unywaji pombe japo, lazima anayetumia awe na miaka kumi na minane ama ishirini ikitegemea na aina ya pombe. Kwa upande mwingine nchini Kanada, umri wa kunywa na kununua pombe ni miaka 18 au 19 (kulingana na sheria za mkoa), ingawa unywaji wa pombe chini ya uangalizi wa wazazi wao unaruhusiwa.

Sheria hizo zipo, vijana wanashiriki mvinyo kupitia njia zisizo tambulika kisheria ama kwa kukwepa macho ya wenye maduka au kupata usaidizi kutoka kwa wenzao wakubwa ambao wanaweza kununua pombe.

Madhara ya pombe kwa Afya

Sumu iletwayo na pombe

Sumu iletwayo na pombe hutokea wakati kiasi kikubwa cha pombe kimebugiwa katika muda mfupi. Hilo hutendeka wakati mtu anapokunywa pombe kupita kiasi katika kikao kimoja mara moja kila wiki mbili.

Kunywa pombe kupita kiasi ni jambo la kawaida na si kwa vijana tu. Kunywa pombe kupita kiasi kunaweza pia kusababisha midundo ya moyo isiyo ya kawaida, ambayo inaweza kusababisha kifo.

Wakati mtu anapokunywa pombe kupita kiwango, inaanza kuathiri ubongo hasa katika eneo ambalo husababisha mwanadamu kufikiri na hivyo kuathiri hisia na uwezo wa kuwaza, msukumo wa misuli hali ya mapenzi na njia za haja ndogo pia uathirika.

Kitengo cha mwisho kuathirika na pombe ni kitengo kinachoongoza mapigo ya moyo mwilini [medulla], hatimaye kipimo cha joto mwilini na kupumua. Inapofika hatua hiyo mtu anahisi usingizi na iwapo ataendelea na unywaji wa pombe, anazimia na vitengo muhimu vya mwili vinaacha kufanya kazi na hilo linaweza kusababisha kifo.

Ugonjwa wa moyo

Japo utafiti umebaini kwamba pombe inaweza kuwa na manufaa kwa moyo, utafiti huu unaonyesha kuwa ni wale wanaotumia pombe kwa wastani, na ni miongoni mwa wanaume wenye umri wa zaidi ya miaka arobaini na wanawake ambao wamepitisha umri wa kujifungua. Manufaa hayo yanaweza kupatikana kupitia kufanya mazoezi, na lishe bora. Zaidi ya kizingiti fulani, unywaji wa pombe huwa sababu ya kuathiri moyo na husababisha magojwa ya moyo.

Unywaji pombe kupindukia kunaathiri moyo. Kunywa pombe kiasi kingi mara kwa mara kunaweza kusababisha kupanuka kwa moyo. Hali hii husababisha ugumu wa kupumua wakati wa mazoezi na jambo hili litahitaji matibabu maalum na haliwezi kutenduliwa.

Ugonjwa wa ini

Bado haijabainika uhusiano kati ya kiwango cha pombe kinachotumiwa kusababisha maradhi ya ini. Utafiti katika taifa la Italia ulionyesha kiwango cha pombe kinapoongezeka mwilini ndivyo athari ya kupata maradhi ya ini huongezeka . Hata hivyo, uchunguzi kutoka taifa la China unaonyesha mtu anapobugia gramu ishirini za pombe kila siku anajiweka maradufu katika hatari ya kupata maradhi ya ini, lakini hatari haiongezeki mtu anapokunywa zaidi ya kipimo hicho. Hata hivyo jambo lililo wazi ni kwamba pombe huongeza hatari ya kupata maradhi ya ini.

Unywaji kwa wastani, ini linaweza kusindika pombe pasipo madhara. Lakini, utumizi wa pombe kupindukia huelemea ini na kusababisha madhara makubwa.

Kunywa kupita kiasi kunaweza kusababisha mafuta kujilimbikiza kwenye ini, na kusababisha seli kuwa duni na kudhoofisha afya ya mtu kiujumla. Ini lenye mafuta huingilia usambazaji wa oksijeni na virutubisho kwa seli za ini, na baada ya muda, husababisha seli za ini kufa. Seli hizi zilizokufa huunda tishu za makovu. Ingawa baadhi ya seli za ini zinaweza kuzaliwa upya kwa lishe bora na kutokunywa pombe, seli zilizozorota sana haziwezi kutenduliwa. Kupuuza hali hiyo kunaweza kusababisha ini kuharibika zaidi na kushindwa kufanya kazi kabisa..

Maumivu ya tumbo/vidonda vya tumbo

Asilimia 20% ya pombe mwanadamu anayokunywa huenda moja kwa moja tumboni; asilimia 80% katika utumbo mdogo. Unywaji wa pombe kupita kiasi hudhuru utando wa viungo hivi na kusababisha maumivu na vidonda vya tumbo.

Madhara ya unywaji wa pombe katika mitazamo na kufanya maamuzi.

  • Jambo ambalo linalohofisha zaidi kuliko hata madhara ya afya ni athari inayosababishwa na pombe kwenye ubongo wa mwanadamu. Tukio ambalo litasababisha madhara mengine. Mwanzo kuathirika ni ubongo, hali hiyo husababisha anayetumia pombe kutowaza vema”. Wakati huo huo mtu anakuwa hana vizuizi vyovyote na kumfanya kuzungumza sana nakujihisi kujiamini. Pombe vilevile inaweza kuathiri uwezo wa kusikia; pombe inapokolea katika damu uwezo wa kusikia sauti, hasa masafa ya chini unadidimia.

Mtu ambaye ameathirika na pombe, akipewa kazi fulani kufanya,

  • Mwanzo anaweza kuwa amesikia vibaya pendekezo hilo, akafikiria kuifanya kazi hiyo kinyume na maagizo.
  • Pili, hawezi kulitafakari pendekezo hilo ipasavyo, kwa hivyo kuna uwezekano mkubwa wa kuliona pendekezo hilo kuwa bora au baya zaidi ya kuliko lilivyo.
  • Kuhisi ujasiri mkubwa wa mafanikio yake kufanya maamuzi yasiyo bora na kutenda kitu

Ambacho kwa kawaida angekikataa, kwa mfano, kuwaomba watu kumi asiowajua kumbusu hapo hapo.

TAIFAUMRI ULIOKUBALIKA
KISHERIA KUNUNUA NA KUNYWA POMBE
Argentina18
Australia18
Cameroon18
Canada18 (MANITOBA, ALBERTA, QUEBEC)
19 (ALL OTHER TERRITORIES)
Colombia18
Costa Rica18
Dominican Republic18
Ecuador18
Misri18
El Salvador18
India18–25 (DEPENDING ON STATE LAWS)
Indonesia21
TAIFAUMRI ULIOKUBALIKA
KISHERIA KUNUNUA NA KUNYWA POMBE
Ujapani20
Malaysia18*
Mexico18
Uholanzi16 (FOR MOST
ALCOHOLIC BEVERAGES)

18 (FOR ALCOHOLIC BEVERAGES
WITH >15% ABV)
Papua New Guinea18
Paraguay20
Peru18
Singapore18
Misri18
Afrika Kusini18
Taiwan18
Thailand18
Marekani21

[Sharia inawakataza waislamu wote kutokunywa vinywaji vya kulevya]

Blank Icons

Kuhusu matumizi mabaya ya dawa za kulevya

Mataifa mengi kote ulimwenguni yana sheria kuhusu matumizi, kumiliki, kuuza na kusafirisha dawa za kulevya na vitu vingine ambavyo sheria hairuhusu. Licha ya kutoelewana kuhusu njia bora ya kukabiliana na matumizi mabaya ya dawa za kulevya, kuna maafikiano juu ya jambo moja: Matumizi mabaya ya vileo ni tatizo na gharama katika jamii na uchumi wa nchi. Kwa mfano mwaka wa 2009, ilikisiwa dawa za kulevya ziliigharimu Uingereza karibia Pauni £16 billion mwaka huo.

Dhihirisho la hilo linatokana na maafikiano yaliyoungwa mkono na Umoja wa Mataifa idara ya kupambana na mihadarati na uvunjaji sheria UNODC kujitolea kukabili swala hili. Wakati mihadarati inatumika, kemikali hiyo inaingia mwilini na inasababisha moja ya mambo mawili: mtu anaweza furahia hilo ama kujihisi vema, au kumfanya mtumiaji kujisikia kutulia ama mwenye uwezo fulani. Bila kujali athari, madawa ya kulewa udhuru ubongo.

Dawa ambazo usisimua ubongo husababisha vipokezi vya kwenye ubongo kuondokewa na hisia. Mtumiaji anahisi kama asiye na matatizo, kwamba amepanda” juu” haraka sana , baada hapo athari za dawa zikiisha, anahisi “ameshuka” kwa kasi sana kama vile alivyokuwa amepanda juu. Hata hivyo, ubongo si eneo la furaha tu, pia ni kitovu cha mantiki, hoja, na ubunifu. Pia hudhibiti hisia zetu na matendo yanayofanyika mwilini petu kama vile kuendesha moyo wetu na kupumua kwetu. Kwa hiyo kemikali yoyote ambayo inaathiiri ubongo wa mwanadamu ina madhara kwa haya yote pia.

Matumizi mabaya ya mihadarati kama tatizo la kiuchumi

Kwa sababu mihadarati inaathiri ubongo, pia inadhuru utendaji wa kazi, kutafakari na kuzalisha mali. Uzembe katika kampuni yoyote ile au kutokuwa makini kunamaanisha uzalishaji duni wa mali na kupungua kwa faida. Ingawaje hasara haionekani kuwa ni muhimu unapoangalia kampuni moja, wakati hasara ya makampuni yote nchini ikijumulishwa, inaweza kufikia mamilioni, ikiwa sio mabilioni ya fedha.

Wengi wanaotumia mihadarati, haswa wale walio na uraibu, huwa na afya mbaya, kwani hutumia muda mwingi kutafuta dawa hizo badala ya kujihusisha na shughuli za kiafya. Hali hii inasababisha mzigo mkubwa kutafuta tiba swala ambalo lingeepukikaa.

Mihadarati haipatikani kwa bei ya chini’. Kufuatia hali hii wengi hujihusisha na visa vya uhalifu minajili ya kupata fedha ya kukidhi hitaji lao. Ikitegemea uhalifu uliofanywa, uharibifu unaweza ukawa mdogo kiasi cha $10 kutelezeshwa kutoka kwenye pochi ya mtu hadi mamilioni ya dola, k.m., wizi katika benki au uchomaji moto nyumba ili kudai pesa za bima.Hii ni pamoja na maswala mengine ya usalama yanayosababishwa na utumizi wa mihadarati .

Ingawa gharama (katika hali ya kifedha) ya matumizi mabaya ya dawa za kulevya inaweza kupimwa kwa kiasi fulani kwa kuhesabu uharibifu wa mwili, uharibifu wa kisaikolojia na kijamii, nambari hizo hazionyeshi kikamilifu gharama halisi ya matumizi mabaya ya dawa za kulevya.

Matumizi ya mihadarati kama tatizo la kijamii

Kutokuwa na faida kazini wanaotumia madawa ya kulewa wanaweza wakajikuta wamefukuzwa kazi ama kuacha shule. Wasipokuwa na kazi au elimu wengi hujihusisha na uhalifu kama njia yao kujikimu maishani.

Mihadarati huwafanya watumiaji kuwa wakorofi sana na wenye kuudhika baada ya “safari” au kwa kukaa muda mrefu pasipo kutumia. Jambo hili linaweza kusababisha mvutano katika jamii, ukiukaji haki za watoto, na inaweza kusababisha kifo. Hali hiyo inaathiri mahusiano ya familia, jamii ambao wanakosa kupata suluu kutokana na hilo wanaweza kuamua kuhama na kusababisha kusambaratika kwa familia.

Hilo ni dhihirisho jinsi uamuzi wa mtu binafsi unavyo athiri uhusiano wake na jamii na mazingira anamoishi. Jinsi John Donne alivyosema, “hakuna mtu anayeweza kujitenga kama kwamba ni kisiwa cha pekee; kila mtu ni kitengo cha bara, liilo sehemu ya dunia, na hilo lizingatiwe.”

Baadhi ya dawa haramu

LSD

MAARUFU KAMA LYSERGIC ACID DIETHYLAMIDE

Majina mbadala: : Acid, blotter, dots
Matumizi : Kwa mdomo
ATHARI ZA MUDA MFUPIATHARI ZA MUDA MREFU
Hali ya kuhisi kuathirika BUlemavu wa kiakili D
Kuongezeka mpigo wa moyo, kupumua, na joto mwiliniUgonjwa wa mtazamo unaoendelea wa maono E
Kufa ganzi
Kizunguzungu
Kupoteza hamu ya kula
Mdomo kukauka
Jasho mwilini
Kichefuchefu
Kutetemeka
Kujizungumzia, maono C
Kukosa uhalisia wa mambo kama vile muda

Bangi

Majina mbadala: Marijuana, weed, grass, pot, ganga
Matumizi : Smoked
ATHARI ZA MUDA MFUPIATHARI ZA MUDA MREFU
Furaha isokikomo FUraibu
Ongezeko la matatizo ya moyoDalili zinazojitokeza unapotaka kuuwacha uraibu huo I
Kushindwa kuwa na mpangilioKutofaulu mambo mengi na tabia H
Matatizo ya kutafakari na kutatua mamboUgonjwa wa Mapafu - bronchitis
Kuathirika hali ya kuhisiMatatizo ya kupumua
Kutokumbuka mamboSaratani ya mapafu
Uoga FUbongo kuathirika N
Kushikwa na mshtuko F

Ecstasy

MAARUFU KAMA MDMA, MDEA OR MDA

Majina mbadala: “E”, happy pills, “X”, XTC
Matumizi : Mdomoni (hutumika sana), kudungwa na sindano au kunuswa au kuwekwa mkunduni
ATHARI ZA MUDA MFUPIATHARI ZA MUDA MREFU
Kuwa na nguvu kupindukiaUraibu
Kujiburudisha na kuhisi mwenye furahaDalili zinazojitokeza unapotaka kuuwacha uraibu huo K
Mwili kuwa na matatizo na vipimo vya joto mwilini JKupoteza uwezo wa kuwaza, kuona na kuyapanga mambo
Matatizo ya kutafakari na kutatua mamboKushindwa kulala
Mapigo ya moyo kuongezaka na shinikizo la damu pia.Hisia kuchemka
Upotoshaji wa wakati na mtazamoUnyogovu
Uwoga kupindukia
Uwoga
Kujizungumzia, maono
Ini na figo kuathirika

Mihemko, ikiwa ni pamoja na rangi, harufu na sauti, huonekana kuimarishwa sana, na katika hali nyingine, mitizamo ya hisi inaweza kuchanganyika katika hali inayojulikana kama sinaesthesia, ambapo mtu huonekana “kusikia” au “kuhisi” rangi na “kuona” sauti.

C. Maono haya hayawezi tabiriwa yanaweza kuwa mema ama mabaya. “Safari” nzuri ni za kufurahisha, za kusisimua kiakili na hutoa hisia ya uelewaji wa juu; kwa upande mwingine, “safari” mbaya zinaweza kusababisha vitu vya kawaida kuonekana vya kutisha na kuanzisha mawazo ya kutisha na hisia za jinamizi za kutia wasiwasi na kukata tamaa ambazo ni pamoja na hofu ya kupoteza fahamu, kifo au kupoteza udhibiti

D. Baadhi ya wanaotumia LSD wanapitia changamoto na kuudhika hali ambayo ilikuwa ya kustarehe inasababisha maumivu ya mda mrefu, na huenda ikasababisha kutoka hali ya kujifurahisha hadi majonzi. Hali hii inaweza kuwa ya mda mrefu.

E. Watumizi wa zamani wa LSD wanapitia changamoto, kuyakumbuka yaliyopita’na inaitwa “HPPD” na wataalamu. Hali hii hujirudia, na ni vigumu kubadilika kwa miaka mingi hata baada ya mwathirika kuacha kutumia mihadarati.

F. Wanasayansi wamebaini utumizi wa mihadarati waweza changia uzuri ama ubaya inategemea mazingara na huathiriwa sana na urithi, hasa wale walio na umri chini ya miaka 18.

G. Dalili unapojaribu kuacha matumizi ya dawa za kulevya ni pamoja na kuhamaki, kuwashwa, wasiwasi mkazo

H. Utafiti wa muda mrefu unabaini wanaotumia bangi miongoni mwa vijana waliopo chini ya umri wa chuo kikuu, watumiaji hawafaulu masomoni ukilinganisha na vijana ambao hawatumii. Wana tabia zisizopendeza, kukaidi mambo, uhusiano mbaya na wazazi, na kujihusisha na marafiki wanaotumia mihadarati.

I. Katika utafiti, kubaini wanaotumia mihadarati kupindukia na wanaotumia kiwango tu,watafiti walibaini wanaotumia kupindukia wanakuwa na ugumu zaidi wa kudumisha umakini, kujisajili, kuchakata na kufuatia maelezo. Hii inatokana na kuathirika kwa ubongo kwa sababu ya matumizi ya marijuana..

J. Madhara ya kimwili yanaweza kudumu kwa wiki kadhaa na kujumuisha mkazo wa misuli, kuuma meno bila hiari, kichefuchefu, kutoona vizuri, macho kusogea haraka, kuzirai, baridi kali na kutokwa na jasho.

K. Dalili za kujiondoa ni pamoja na uchovu, kupoteza hamu ya kula, wasiwasi, huzuni, hofu isiyoweza kudhibitiwa, kukosa usingizi, kupoteza udhibiti wa hisi na ukweli, na matatizo ya kuzingatia.

Ketamine

Majina mbadala: K, special K, vitamin K
Matumizi: Sindano (kama kimiminia), kumezwa (kama tembe) au kunuswa (unga)
ATHARI ZA MUDA MFUPIATHARI ZA MUDA MREFU
Kuhisi kutengwa na duniaUraibu
Kuondokewa na hisiaDalili zinazojitokeza unapotaka kuuwacha uraibu huo L
Mapigo ya moyo kuongezaka na shinikizo la damu pia.Kutoka damu puani
Kufa ganziTatizo la kunusa
Kichefuchefu/kutapikaMaumivu tumboni
KuchanganyikiwaMatatizo ya kupumua
Kupoteza fahamuKitengo ya ya mkojo kuathirika
Matatizo kupumua*While long-term effects seem less severe, immediate effects can lead
to death.
Kupata shida kupumua.
Kuacha kupumua kabisa

Heroini

Majina mbadala: Smack, H
Matumizi : Sindano (kama kimiminia), kunuswa au kuvutwa (unga)
ATHARI ZA MUDA MFUPIATHARI ZA MUDA MREFU
Furaha isokikomoUraibu
Fikra zilizochanganyikiwaDalili zinazojitokeza unapotaka kuuwacha uraibu huo M
Kuwa na hali ya kuamka na kusinzia kila wakatiKushindwa kuwajibika
Kushuka kwa mapigo ya moyo na matatizo ya kupumuaKuhisi uchovu
KuvimbiwaKuathirika kwa ngozi (mahali unapodunga sindano).
Mapafu, figo, na ini kuathirika

L. Dalili hizo ni uchovu, unyogovu, kukasirika, kuwashwa na kukosa usingizi.

M. Dalili zingine ni pamoja na kukosa usingizi, macho kulia, kutokwa na kamasi, kuudhika, kuhisi mwenye mashaka, kutetemeka, maumivu mwilini, kusikia baridi kali, kutokwa na jasho mwilini, kuhara, kutapika na kuwa na tamaa kubwa sana ya kutumia mihadarati.

Methamphetamine

Majina mbadala: Ice, meth, speed, yaba
Matumizi : Sindano (kama kimiminia), kumezwa (kama tembe), kunuswa (unga) au kuvutwa (unga au fuwele)
ATHARI ZA MUDA MFUPIATHARI ZA MUDA MREFU
Matatizo ya mpigo wa moyoUraibu
Kuongezeka kwa mpigo wa damu na joto mwiliniDalili zinazojitokeza unapotaka kuuwacha uraibu huo N
Mwenye fujoKuchanyanyikiwa hisia
KuwashwaWasiwasi na kukasirika
KuchanganyikiwaKuchanganyikiwa
Kukosa usingiziTabia ya kuzua balaa
Ongezeko la kutokuwa na usingiziMeno kuuma
Kutetemeka na degedegeKujizungumzia na maono
Uwoga/wasiwasi na kujutiaMatatizo ya kiakili
HasiraFikra za kujitia kitanzi
KiharusiMaradhi ya ini na figo
Kuathirika kwa moyo na neva
Kifo cha gafla

Kokeni

Majina mbadala: Coke, crack
Matumizi : Sindano (kama kimiminia), kunuswa (unga) au kuvutwa (unga)
ATHARI ZA MUDA MFUPIATHARI ZA MUDA MREFU
Kujihisi mchangamfu na nguvuMatatizo ya mpigo wa moyo
Vipimo vya joto kuongezeka mwilini, shinikizo la damu na mapigo ya moyo kuongezekaMaumivu ya kifua na/au matatizo ya moyo
Mwenye fujoMaatatizo ya kupumua
KuwashwaKiharusi
Kutoona vizuriMshtuko wa moyo na maumivu ya kichwa
Kujizungumzia, maonoMaumivu tumboni na kuhisi kutapika
KichefuchefuUraibu
Kifo cha gafla baada ya matumizi hata mara ya kwanzaDalili zinazojitokeza unapotaka kuuwacha uraibu huo O

N. Dalili zinaojitokeza unapoamua kuacha ni kama vile uchovu na njaa kupindukia, wasiwasi, unyogovu, kuwashwa na kukosa usingizi.

O. Dalili zinazojitokeza unapoamua kuacha ni kama vile wasiwasi, unyogovu, hasira, hisia mchanganyiko, uchovu, kichefuchefu, kutapika na kukosa hamu ya kufanya chochote.

Vinuswa

(KUNUSA GUNDI, ULANGUZI WA VIMIMINIA)

Majina mbadala: Whippets, poppers, snappers
Matumizi : Puani
ATHARI ZA MUDA MFUPIATHARI ZA MUDA MREFU
KulewaUraibu
GanziDalili zinazojitokeza unapotaka kuacha S
Kupoteza hisiaKuvuja damu na vidonda
Kupoteza ufahamuMaumivu na kukohoa
Matatizo ya kupumua hewa safi PKushindwa kujidhibiti
Mshtuko wa moyo QKupata maruwiruwi
Kifo cha gaflaKupoteza fahamu
Kifo kutokana na kunusa RKuathirika kwa macho
Kuathirika kwa mhimili wa hisi
Kuathirika kwa uboho
Kuathirika kwa ubongo, ini na figo
Kuathirika kwa kinga ya mwili
Kifo cha gafla

P. Wakati wakuvuta, mvuke unaosababishwa na kemikali hizo unakusanyika katika mishipa ya damu na kuzuia hewa safi kuingia kwenye damu, hicho ndicho chanzo cha mtu kuzimia ama kushindwa kupumua.

Q. Hili hutokea wakati hewa safi haipenyezi kwenye moyo.

R. Wakati mtumiaji anapokufa kutokana na kushindwa kupumua ama matatizo ya moyo inajulikana kama Kifo cha Ghafla cha Kunusa..

S. Dalili hizo ni kama wasiwasi, unyogovu, kufadhaika, tabia ya ukatili, kizunguzungu , kutetemeka, kichefuchefu, kutokua na usingizi usiku.

PCP

MAARUFU KAMA PHENCYCLIDINE

Majina mbadala: Angel dust
Matumizi : Kumezwa (kama tembe), kunuswa (unga), kuvutwa (unga) au sindano (majimaji))
ATHARI ZA MUDA MFUPIATHARI ZA MUDA MREFU
VIWANGO VYA CHINITT TUraibu
Furaha ya ajabu ajabu/starehe.Dalili zinazojitokeza unapotaka kuuwacha uraibu huo U
Kupoteza fahamu.Kupoteza uzito
Kuhisi kujitengaMatatizo kuongea na kuwaza
Wasiwasi au kuchanganyikiwaKupoteza fahamu
Kusahau mamboUnyogovu
Kuropoka
Kutoona vizuri
VIWANGO VYA KADRI
kufadhaika
Kutokwa na mate kupita kiwango
Kupoteza fahamu ya kutafakari
Kutoafikiana mambo kutokana na uoga
Kubadilisha msimamo mara kwa mara
VIWANGO VYA JUU
Mshtuko wa moyo
Kiharusi
Maatatizo ya kupumua
Kupoteza ufahamu
Kifo cha gafla

T. Mtumiaji hana udhibiti wa matumizi yake. Wengine wanaweza kufurahia wakati wengine wanaweza kuwa katika uchungu.

U. Dalili zinazojitokeza ukitaka kuacha ni pamoja na kuharisha, baridi na kutetemeka.

Extra Content Icons

Maelezo Ziada

Blank Icons

Kuhusu uvutaji sigara

Utafiti unabaini wingi wa madhara ya wanaovuta sigara. Tangia miaka ya 1999, kampuni nyingi tu zinazo tengeza tumbaku wamekubali madhara yanayotokana na uvutaji wa sigara.

Moshi unaotokana na sigara moja una kemikali 7,000. Hizi ni pamoja na:

  • Nikotini, dutu kuu ya kulevya.
  • Carbon monoxide, amayo huzuia mpigo wa damu mwilini.
  • (Tar) Lami, inayojiweka kwenye utando wa mapafu na kuzuia kubadilishana kwa hewa safi O2 na -CO2.
  • Hydrogen cyanide, Inayozuia mapafu kutoa vitu visivyohitajika na hivyo kuathiri mapafu .
  • Zaidi ya kemikali 60 zinazojulikana kusababisha saratani.

Madhara ya uvutaji sigara

Kuambatana na Shirika la Afya Ulimwenguni [WHO] Uvutaji wa sigara ni sababu kubwa ya vifo vingi na ulemavu kuliko maradhi mengine yoyote.

  • Matumizi ya tumbaku yanachangia karibu vifo milioni tano kila mwaka kote ulimwengunir;34 ukilinganishwa, watu milioni mbili waliofariki maradhi ya ukimwi mnamo mwaka 2008.
  • Tumbaku huuwa nusu ya watu wanaoitumia.
  • A smoker aged 11 to 15 years is three times more likely to die a premature death than someone who takes up smoking at the age of 20.
  • Uvutaji wa sigara unasababisha madhara ndani ya mapafu kuongezeka hadi mara 22.
  • Sita kati nane ya vifo kote ulimwenguni vinatokana na utumizi wa tumbaku.
  • Uvutaji wa sigara huongeza hatari ya kupata saratani ya mdomo, uterasi, ini , figo, kibofu, tumbo na mlango wa kizazi na pia ina sababisha saratani ya damu.
  • Uvutaji wa sigara husababisha uharibifu usioweza kurekebishwa wa mapafu, na kusababisha magonjwa sugu ya mapafu, sababu ya nne kubwa ya vifo vya ulimwenguni kote.
  • Mama mja mzito, anayevuta sigara anaongeza hatari ya mimba hiyo kutoka kabla mda wa kujifungua. Na watoto ambao wanazaliwa na wazazi ambao walivuta sigara, wanazaliwa na uzito mdogo na hali hii huwa ni pingamizi kwa ukuaji wa kawaida wa watoto hao.
  • Watoto ambao wazazi wao huvuta sigara wana hatari ya kufa kutokana na ugonjwa wa “kifo cha ghafla cha watoto wachanga (sudden death infant syndrome).
TAIFAUMRI ULIOKUBALIKA
KISHERIA KUNUNUA NA KUNYWA POMBE
Argentina16 / 18 (KUTEGEMEA SHERIA ZA MKOA)
Australia18
Cameroon18
Canada18 (IN MOST STATES)
19 (INAKUBALIKA MAENEO YA MANITOBA, ALBERTANA QUEBEC) (MAENEO MENGINE YOTE)
China18
Colombia15
Costa Rica18
Dominican Republic18
Misri18
India18
TAIFAUMRI ULIOKUBALIKA
KISHERIA KUNUNUA NA KUNYWA POMBE
Ujapani 20
Malaysia18*
Mexico18
Uholanzi16
Papua New Guinea18
Peru18
Singapore18
Afrika Kusini18
Syria18
Taiwan18
Thailand18
Marekani21

Kamari

Kamari, pia inayojulikana kama michezo ya bahati nasibu, inaweza kuchukua aina nyingi. Mifano ya kamari ni pamoja na mbio za farasi, dau la soka, tikiti za bahati nasibu, michezo ya kubahatisha (Roulette, Blackjack, Baccarat) na hata dau ndogo ndogo na marafiki.

Katika tamaduni nyingi, kucheza kamari ni tabia inayokubalika. Kwa mfano, huko Singapore, wengi hununua tikiti za bahati nasibu ya serikali mara kwa mara, na wengine wako tayari kupanga foleni kwa masaa kwenye “vituo vya bahati nasibu” kwa droo kuu. Nchini Australia, katika baadhi ya majimbo, ni kawaida katika baa na vilabu kupanga mashini za kamari. Lebanon ina kasino, ambazo mara kwa mara huwa na matukio ya poka. Kimataifa, mchezo wa kitaalamu wa poka unachukuliwa kuwa mchezo halali.

Hata hivyo nchi nyingi pia zina sheria dhidi ya aina fulani za kamari. Baadhi, kama Saudi Arabia, wana sheria zinazopiga marufuku kabisa kucheza kamari. Nyingine, kama Singapore (kabla ya michezo ya kasino kuhalalishwa mnamo 2005) ilifanya kamari ya kibiashara kuwa haramu, lakini ikaweka masharti ya kamari ya kijamii (mchezo wa poka miongoni mwa marafiki siku ya Ijumaa usiku) na huluki za kamari zinazodhibitiwa na serikali. Hata nchi huria zaidi kama vile Uingereza inaruhusu kamari ya kibiashara mradi tu sheria fulani (kama vile malipo ya ya viwango vya chini, usajili au ushuru maalum wa faida inayotokana na shughuli za michezo ya kubahatisha) kufikiwa. Bila kujali jinsi huria sheria za michezo ya kubahatisha zinavyoweza kuwa, serikali zinatambua hili: kamari huleta matatizo ya kijamii - waziwazi au kwa njia isiyo wazi.

Kamari ina uwezo wa kumfanya mtu kuwa mraibu na ni hatari. Madau madogo kwenye michezo au matokeo mengine inaweza kuonekana kuwa isiyo na madhara yoyote.

Yamkini, kuna mstari mwembamba unaotenganisha uchukuaji hatari uliokokotolewa na kuwa mraibu kwelikweli.

Wengi wa watu wanaocheza kamari ni wacheza kamari walio katika hatari ndogo. Wanafanya hivyo kwa ajili ya kujifurahisha tu au kama shughuli ya kujumuika na marafiki. Kwa kawaida hutumia muda unaodhibitiwa na huwa wameamua mapema kiwango cha hasara. Walakini, uraibu hukua wakati watu hutumia kamari kama njia ya kuyakimbia matatizo au kupata msisimko wa kujihatarisha. Kwao, kushinda imekuwa aina ya kujithibitisha, kuyakimbia matatizo au kusisimka.

Kamari huendelea kutoka kuwa mchezo au shughuli ya kujumuika na jamii na kuwa ni njia yao ya kujithamini au inakuwa ni tumaini la uwongo kama suluhisho la haraka ya shida zao. Lakini familia nyingi za wale waliozoea kucheza kamari watakuambia kwamba wachezaji hao wanashindwa mara nyingi zaidi ya wanavyoshinda, na pesa haziwezi kununua furaha au kufuta maumivu.

Uraibu wa Kamari

Kulingana na Mwongozo wa Uchunguzi na Takwimu za Matatizo ya Akili, Marekebisho ya Maandishi ya Toleo la 4 (DSM IV TR), uraibu wa kamari unaainishwa kama ugonjwa wa kisaikolojia. Kwa utambuzi wa uraibu wa kamari, mteja lazima aonyeshe tabia mbaya ya kamari inayoendelea na inayojirudia ambayo inatimiza angalau vigezo vitano kati ya vifuatavyo:

  1. Anajishughulisha na kucheza kamari.
  2. Anahitaji kucheza kamari akiongeza kiasi cha pesa ili kufikia msisimko anaoutazamia.
  3. Amejitihadi mara kwa mara kudhibiti, kupunguza au kuacha kucheza kamari bila mafanikio.
  4. Huonekana kutotulia au kukasirika wakati wa kujaribu kupunguza au kuacha kucheza kamari.
  5. Anacheza kamari ili kuepuka matatizo au kupunguza hali ya huzuni, kutotulia na kutotosheka.
  6. Hurudi siku nyingine akitegemea mapato hata baada ya kupoteza pesa kwa kucheza kamari.
  7. Huwadanganya wanafamilia, matabibu au wengine ili kuficha kiwango cha kuhusika na kamari.
  8. Amefanya vitendo haramu kama vile kughushi, ulaghai, wizi au ubadhirifu ili kufadhili kamari.
  9. Amehatarisha au kupoteza uhusiano muhimu, kazi, elimu au nafasi ya kazi kwa sababu ya kamari.
  10. Hutegemea wengine watoe pesa ili kukabiliana na hali mbaya ya kifedha inayosababishwa na kucheza kamari.

Madhara ya Uraibu wa Kamari

Uraibu wa kamari unajidhihirisha kwa njia nyingi, pamoja na malalamiko juu ya shida za pesa, unyogovu na mawazo ya kujiua. Waraibu wa kamari wanaweza pia kujikuta hawana kazi na wenye afya mbaya, kwani hawawezi kupata usingizi mzuri na huhisi wasiwasi wakati mwingi.

Pia uraibu wa kamari huingilia uhusiano kati ya watu, na kusababisha kuvunjika kwa familia au mahusiano mabaya ya familia.

Uchunguzi wa kawaida kutoka kwa wanafamilia wa waraibu wa kamari ni pamoja na:

  • Bili za kaya ambazo hazijalipwa
  • Akiba inayotoweka
  • Mikopo isiyoelezeka
  • Vipengee na mali
  • Posho za watoto “zinapotea”
  • Kukwepa mada ya pesa
  • Pesa za mkopo zisizojulikana zilivyotumika
  • Uwekezaji wa hatari kubwa katika biashara zisizo za kweli
  • Kuwa na mtazamo wa kutojali kuhusu kukosa kazi, kupoteza kazi au kutafuta kazi mpya
  • Daima hupungukiwa na pesa licha ya mapato ya kutosha

Tabia hizi zote hudhuru uhusiano wa kifamilia, kwani wanafamilia wote hawawezi kutegemea mcheza kamari kuchangia mahitaji ya familia, au hata kutekeleza mahitaji yake mwenyewe. Kunakuwepo na suala la kuaminiana kwani hawawezi kuwa na uhakika kwamba mcheza kamari anaweza kuchangia fedha zozote kwa ajili ya maslahi ya familia.

Ikiwa mcheza kamari amekata tamaa, anaweza kugeukia njia zisizo halali za kupata pesa, kama vile kukopa kutoka wakopeshaji pesa wasio na leseni au kwa kujihusisha na uhalifu. Vyovyote vile, hii ina athari kwa usalama wa umma. Wakopeshaji hao hunyanyasa wadeni, familia zao na majirani zao wasio na hatia, na shughuli za uhalifu huhatarisha watu na mali.

  • [Kulingana na madokezo ya semina kuhusu “Uraibu wa Kamari: Ufafanuzi na Utambuzi” na “Kuchunguza kwa Uraibu wa Kamari” na Bw Patrick Teo, Mshauri Mkuu, Huduma za Usimamizi wa Uraibu wa Kitaifa, Taasisi ya Afya ya Akili, Singapore, Julai 2006.]
Activities Icons

SHUGHULI MUHIMU
Zoezi 2: Mipaka

Blank Icons

Lengo

Kuhimiza washiriki kuweka mipaka katika tabia hatarishi.

Mahitaji

  • Kitabu cha mazoezi cha mwanafunzi
  • Kalamu ya mate/Kalamu ya wino

Maagizo

1. Waeleze washiriki kwamba sasa wana ukweli wanaohitaji kufanya uamuzi sahihi na wako katika nafasi nzuri sana ya kuamua wapi wanataka kuweka mipaka yao kuhusiana na tabia hatarishi iliyojadiliwa.

2. Katika kitabu cha mazoezi, kila moja ya tabia nne hatarishi inazo kauli sita, kila moja ikielezea hatua zinavyofuatana kadiri tabia hizo zinavyoendelea. Waulize washiriki ni wapi watakapoweka mipaka yao kwa kila moja ya tabia hizi. Wachore mstari mmoja katika hatua hiyo.

Handbook 52 Icons

Mstari wa mpaka uliopendekezwa umechorwa hapa chini, lakini kufuatana na maadili yako na utamaduni wako unaweza kuusogeza popote huo mstari.

POMBE

  • Nitakunywa tu katika mazingira yenye marafiki ama jamii wakati nikifikisha umri unaoruhusiwa kisheria, na itakuwa kinywaji kimoja au viwili tu.
  • Nitakunywa tu katika mazingira yenye marafiki ama jamii lakini nitakunywa kiasi ninachopenda hata kama inamaanisha kwamba nitalewa.
  • Nitakunywa popote, katika maeneo ya burudani nitakayopendezwa nayo, kiasi chochote hata kama ni kulewa sitajali ni nani yupo karibu yangu wakati huo.
  • Zingatia mtazamo wa kidini, kwa mfano, Waislamu wamekatazwa kunywa pombe.

Matumizi ya Dawa za Kulevya

  • Sitagusa mihadarati na nitaepuka hali yoyote ambayo inaweza kunifanya nijaribu kutumia mihadarati.
  • Sitagusa mihadarati kamwe, bali nitadumisha urafiki na wanaotumia dawa za kulevya.
  • Ningependa kujaribu madawa mbalimbali ya kulevya yaliyopo.
  • Sitatafuta mihadarati, lakini iwapo marafiki zangu watatumia nitajaribu kutumia mara moja tu kubaini wanavyoo hisii.
  • Ninaweza tumia madawa ya kulevya’iwapo yanaweza niwezesha nifanye vyema katika masomo ama michezo.
  • Ningependa kufahamu jinsi unavyohisi, kwa hivyo nitamtafuta mtu aliye nazo. Lakini mmoja tu.
  • Ningependa kuchagua moja ya dawa za kulevya; sijali athari za kimwili, kijamii ama kisheria nitakazopata.

Uvutaji Sigara

  • Sitavuta sigara kabisa na sitawakaribia wanaovuta sigara.
  • Sitavuta sigara kabisa, lakini sijali kushirikiana na wanaovuta sigara.
  • Nitavuta sigara wakati ninahisi, na ninapojisikia.
  • Sitaomba sigara, lakini rafiki akinipa moja, nitajaribu kuvuta mkupua mmoja Nihisi jinsi ilivyo.
  • Sitajinunulia sigara, lakini iwapo nina kikundi kinachovuta sigara nitavuta nao, haijalishi ninajiskiaje.
  • Sitanunua pakiti yangu mwenyewe ya sigara/vape, lakini ikiwa niko na kikundi cha marafiki wanaovuta sigara, nitavuta sigara nao bila kujali jinsi ninavyohisi.
  • Nitajinunulia sigara ili nivute wakati nina mkururo au nikiwa na marafiki zangu.

Kamari

  • Nitajiepusha na aina zote za kamari.
  • Nitacheza kamari kama haitumii pesa au hisa.
  • Nitacheza kamari mara mojamoja tukikutana na marafiki zangu wakati ampabo hisa sio kubwa.
  • Nitacheza kamari mara kwa mara wakati hisa ni katika uwezo wangu.
  • Nitacheza kamari kijamii hata bila kujali hisa, maadamu ipo kwenye uwezo wangu.
  • Nitacheza nikiwa na nia ya kumalizia kamari nikiwa na hela nyingi kuliko nilizoanza nazo.

3. Baada ya wote kumaliza zoezi, waombe wachache wao kueleza wameweka wapi mpaka na kwa sababu gani. Na wewe waeleze mipaka yako and sababu zako. (Ili kudumisha mpaka ulio salama na bora, hatupashwi kuvuka mipaka yetu)

Madhara ya Maisha Yasiyo na Mipaka

Slides Icons

Ukosefu wa mipaka iliyo wazi maishani unaweza kusababisha matokeo mabaya.

Majuto

Katika maisha tunapata majuto tunapofanya jambo ambalo baadaye tunatamani tusingelifanya. Majuto yanaweza kuja haraka, kwa mfano kuuguzaa majeraha na maruirui ambayo huambatana na unywaji pombe. Wakati mwingine majuto yanaweza kuchukua miezi au miaka, mfano mtu wa umri wa makamu ameathirika na sigara baaada ya kutumia miaka mingi tangu alipokua kijana anapotambua ana ugonjwa wa saratani ya mapafu. Je, inawezekana kukawa na maisha yasiyo na majuto?

Huenda tusiondoe majuto yote, lakini ikiwepo mipaka iliyo wazi tunaweza kutarajia kufanya maamuzi bora yanayolingana na kile tunachfikiria ni muhimu na si kwa kufuata hisia zetu, homoni, kushawishika na marafiki na kadhalika.

Shida

Pasipo kuwepo na mipaka iliyo wazi, ni rahisi kujiingiza katika tabia za hatari na hata kinyume cha sheria. Kuendesha gari ukiwa mlevi, kutumia mihadarati na kudhulumu wengine ni baadhi ya tabia zinazoghalimu kiasi kikubwa sana kwa wahalifu, familia zao, wahasiriwa wao na jamii.

Baadhi hubisha kwamba wakipata shida ni matatizo yao wenyewe, je hiyo ni kweli?

Dereva mlevi anaweza hatarisha maisha yake na hata ya wengine wanaotumia barabara. Kwa kutokuwa na mipaka muathiriwa na wale walio karibu naye wasio na hatia yoyote wanahasiriwa.

Madhara ya Kimwili na Kihisia

Katika mazingira ambapo hakuna mipaka iliyo wazi na wakati watu wawili wanapendana na mmoja wao au wote wanajiweka katika hali ya hatari, mfano unywaji pombe kupindukia au kutumia mihadarati, ubakaji unaweza kutokea. Hali hiyo ya kubakwa na rafiki inatokea kati ya watu wawili waliozoeana bila ridhaa ya mmoja wao. Hili linaweza kuwa matokeo ya shinikizo kali la kisaikolojia, ingawa kwa kawaida mbakaji anatumia pombe au dawa za kulevya ili kumfanya mwanamke apoteze fahamu. Wanawake wengi ambao wamebakwa kwa njia hii hawakumbuki kilichotokea, ama kutokana na athari za pombe au madawa ya kulevya, au kwa sababu ya kiwewe cha tukio hilo.

Going Deeper Icons

Kwenda Ndani Zaidi

Blank Icons

Maswali ya kujiuliza kabla ya kusema sio jambo la kutilia uzito?

Handbook 54 Icons
  • Je, nitaendelea kufanya jambo hili ikiwa mtu ninayemheshimu sana atakuwa ananiangalia?
  • Je mtu anaweza kuumia? (k.m. marafiki/jamii hata sikukusudia kutenda hilo?)
  • Je, niko tayari kuyakubali matokeo ya matendo yangu?
  • Je, ninaweza kuishi na matokeo haya?

Je, tabia hatarishi huathiri vipi malengo ya baadaye?

Lengo

Kuwafahamisha wanaoshiriki kufahamu wanaweza kunaswa katika hali tata wasipoweka mipaka wazi ya kimwili na kihisia kwenye mahusiano yao.

Usuli

Mahusiano yaliyo bora yanahitaji mipaka ya wazi ya kihisia, kisaikolojia na kimwili. Hilo ni kweli katika uhusiano wowote, lakini haswa uhusiano baina ya mvulana na msichana.

Wakati mvulana na msichana ni marafiki wa karibu sana, mipaka kati yao kama marafiki tu bila kitu kingine cha ziada inahitajika. Kwani mmoja wao anaweza kufikiri kuwa wao ni marafiki wa kawaida tu, huku mwingine anafikiri wao wanachumbiana. Wakajikuta wameingia kwenye eneo lenye matata linalosababisha kuumia, kukata tamaa na kuchanganyikiwa.

Mipaka iliyo wazi zaidi ni mipaka ya kimwili. Wanafafanua ni tabia gani inayofaa, iwe katika urafiki au uhusiano wa uchumba. Wakati mpaka umevukwa bila idhini, humwacha mtu anahisi kukiukwa. Kuweka mipaka ya kimwili ni pamoja na kutumia haki yako ya kusema hapana wakati mtu anajaribu kudharau au kudhalilisha mwili wako.

Watu wengi hawapotezi ubikira wao, siku moja tu. Ni mchakato wa taratibu wa kuvuuka mipaka iliyowekwa, kwenda kinyume na hulka yao na na kuhalalisha matendo yao. Ghafla wanajikuta katikati ya uchu na shauku ya ngono na wanafanya kile wanachohisi kuwa ni sawa kwa wakati huo.

Mipaka ambayo inafaa kuzingatiwa ni ya hisia, na inafaa kulindwa. Mipaka hiyo hukiukwa iwapo mhusika mmoja atakuwa na hitaji zaidi au kumdhibiti mwingine. Katika uhusiano wa mvulana na msichana, wanaochumbiana, wanaoyaweka wazi wakiongea hasa siri za moyoni siku ya kwanza wanapokutana, inawaweka katika hali tata ya uhusiano wa kihisia.

Aina ya hila zaidi ya mipaka ni mipaka ya kihisia, na hii inachukua fomu ya kudanganywa kwa hisia. Mstari huvukwa wakati upande mmoja unapoanza kuwa "uhitaji" au udhibiti wa mwingine. Katika uhusiano wa uchumba, wanandoa ambao walifunua sana na haraka sana, kama vile kushiriki siri zao zote za kina katika tarehe ya kwanza, wanajiweka tayari kwa hali ya juu ya uhusiano wa kihisia.

Activities Icons

SHUGHULI MUHIMU
Zoezi 1: Fafanua uhusiano

Blank Icons

Lengo

Kuweka wazi matarajio yanayotokana na mipaka tofauti iliyopo katika kila aina ya uhusiano baina ya msichana na mvulana.

Mahitaji

  • Kitabu cha mazoezi cha mwanafunzi
  • Kalamu ya mate/Kalamu ya wino

Maagizo

1. Waombe washiriki watie alama ya ndio katika kisanduku ikiwa wanafikiria kuwa ni matarajio ya kuridhisha ya mtu mwingine katika muktadha wa mahusiano yafuatayo baina ya mvulana –na msichana:

Slides Icons
  • Marafiki wa kawaida
  • Marafiki wa karibu
  • Wanaochumbiana kwa uchunguzi (ambapo mmoja au pande zote mbili zimeonyesha upendo)?
  • Kwenye uhusiano uliodhabiti (wote wawili wnapendana)
  • Wameoana, [kuna ahadi kuishi pamoja maishani]
Handbook 55 Icons

Matarajio

Namtarajia:

  1. Kuwasiliana naye tutakapokutana barabarani, ama shuleni
  2. Kuninunulia zawadi wakati wa siku yangu ya kuzaliwa
  3. Kuwa na mazungumzo ya mara kwa mara kwenye simu
  4. Kunipa zawadi au kunifanyia tukio maalumu wakati wa sherehe muhimu kama siku ya kuhitimu
  5. Kusimama nami wakati mambo yanapoenenda kinyume na matarajio mfano kushindwa mtihani ama matatizo nyumbani.
  6. Kusimama nami wakati mgumu na wa majonzi
  7. Kunishangaza na zawadi wakati siitarajii.
  8. Kujumuika pamoja na marafiki zangu ninapomwomba kufanya hivyo
    [Kumbuka: Hangout ina maana ya kujumuika au kushiriki katika shughuli za burudani]
  9. Kuniheshimu na kuwa mwangalifu wa hisia zangu.
  10. Kunieleza matatizo yake na kuhitaji ushauri wangu

2. Waombe wachache wao washiriki majibu yao na chunguza zaidi kama unahisi wako katika eneo tata.

  • Kwa mfano, iwapo mshiri atajieleza angependa kama rafiki yake wa kiume angeacha kila kitu ili awe naye wakati ameshushwa moyo na jambo fulani, muulize atajisikiaje iwapo huyo kijana akighairi miadi naye il aandamane na rafiki yake mwingine msichana.

3. Waeleze washiriki kutumia muda mwingi mkikaa pamoja kunaleta matarajio [hasa kwa wasichana]. Tunahitaji kufahamu mipaka ya hisia inayofaa katika kila hatua ya uhusiano. Iwapo mmoja kati yao anaweza jenga matumaini zaidi ya mwingine jambo hilo linaweza ingiza wasiwasi katika uhusiano.

4 Washirikishe maoni yako kuhusu matarajio yenye afya katika mahusiano mbalimbali ukitoa mifano yako ya kibinafsi.

RAFIKI WA KAWAIDARAFIKI WA KARIBUWANAOCHUMBIANAWAPENZI/ WALIPEANA POSANDOA
A
B
C
D
E
F
I
H
N
J
  • Tanbihi: Mapendekezo yaliyo hapo juu yatategemea mazingira na tamaduni husika.
Slides Icons

Usifurahie eneo ulipo hasa lile lisiloeleweka..

Kuwepo katika eneo lisiloeleweka kwa muda mrefu kunaweza kuleta kuchanganyikiwa, na hali hiyo hudhohofisha uhusiano uliokuwa mwema.

Mfano halisi ni wakati kijana anavyoweza kukiuka mipaka ya kihisia katika urafiki wao:

Kijana mmoja alipata fursa kuelezea aliyoyafahamu kutokana na “urafiki wao”:

  • “Ninamfamu msichana mmoja aliyekuja kwangu akilia kutokana na mvulana ambaye alikuwa rafiki yake kumwomba msichana mwingine waende naye kwenye sherehe ya shule. Ingawa hawakuwa na ukaribu wa mwili, lakini walikaa pamoja kwa muda mwingi na waliongea sana juu ya mambo mengi. Alipojua kwamba alimwomba msichana mwingine kwenda kwenye sherehe ya shule, aliumia kihisia na kumkabili kuhusu uhusiano wao. Mwitikio wa kijana ulikuwa wa mshtuko na kuchanganyikiwa – hakufikiria kama walikuwa na uhusiano mzito. Hilo likamhuzunisha msichana huyo zaidi. Urafiki wao ulivunjika kwa uchungu mwingi.

Mipaka ya Kihisia: Hisia zako ni zako pekee.

Haupaswi kumpa mtu udhibiti mkubwa juu ya hisia zako, miliki hisia zako na kuweka mipaka.

Handbook 56 Icons

1. Chunga matarajio yako

Fahamu lile utakalo, na usilolitaka, miongoni mwa marafiki. Iwapo ulikuwa na siku mbaya na ungelipendelea rafiki kukusikiliza, lakini si mtu ambaye umemfahamu siku mbili au miezi miwili tu. Iwapo una rafiki mwema, asiye wa jinsia yako ni bora kuweka mipaka ya kihisia, pasipo na mipaka mwenzako anaweza kuwaza uhusiano wenu unaendelea kukomaa na wewe unafikiria nyinyi ni “marafiki tu”.

2. Jihadhari na uhusiano wa kihisia

Ni vema kufahamu kwamba unaweza kumweleza matatizo unayokumbana nayo rafiki yako, na unatambua kwamba atakusikiza. Japo ni bora kuchunga na kuweka mipaka katika hisia zako ili usimtegemee mwingine kila wakati jambo linapokusibu. Unahitaji mtu huyo “kukuokoa” kila wakati. Uhusiano wenye utegemezi wa hali hiyo huziacha pande zote mbili kuhisi mmenaswa.

3. Tambua usaliti wa kihisia

Ni vizuri kuwa makini kutokana na matamshi kama vile, “iwapo hutakula nami maakuli ya mchana sitafurahia, sitakula tena .” Kuna tofauti kubwa kati ya kuwa mkweli na mwaminifu kwa marafiki zako kuhusu hisia zako, na kudhibiti hisia zao ili kupata unacho kitaka.

Activities Icons
Blank Icons

Lengo

Kuonyesha hitaji la mipaka katika urafiki wa kimwili na athari zisizoweza kutenduliwa vinginevyo.

Mahitaji

  • Pakiti moja ya biskuti za sandwich za Oreo (au zinazofanana) (vanilla creme) [inayotosha kwa nusu ya darasa]
  • Pakiti moja ya biskuti za sandwich za Oreo (au sawa) (cream ya chokoleti) [inayotosha kwa nusu nyingine ya darasa]

Vinginevyo, unaweza kutumia:

Instructions For The Facilitator Icons
  • kipande kimoja cha mkate na jamu ya sitroberi
  • kipande kimoja cha mkate na siagi ya karanga
  • Wanaojitolea wawili (kwa matokeo bora zaidi, waambie kikundi kuchagua mvulana na msichana mahiri zaidi)

Maagizo

1. Wapatie nusu ya darasa biskuti za sandwich ya Oreo yenye vanilla krimu na biskuti za Oreo zilizo na krimu ya chokoleti kwa nusu nyingine ya darasa.

2. Waombe washiriki waliopata biskuti za sandwich ya vanilla krimu kuoanisha na mtu aliyepata biskuti za sandwich ya krimu ya chokoleti.

3. Waombe washiriki wote waigize hadithi hii unapoisimulia. Unaweza kupata majina ya uwongo ya kuwakilisha biskuti hizo mbili (k.m., Jack na Jill). Hadithi inaweza kusikika kama hi:

  • Jack na Jill wako kwenye mkahawa mtaani, Jack amezama katika kutazama video kwenye YouTube®/katika mchezo wake wa Ulimwengu wa Vita (World of Warcraft®); Jill anazungumza na marafiki zake mtandaoni/anaangalia mpasho wake wa Instagram®.
  • Ghafla kutoka katika chumba hicho, Jill anahisi harufu ya manukato ya kiume aliyojipaka Jack na anavutiwa kukaribia. Anaamua kuhamia meza karibu na Jack.
  • Jack anadondosha simu yake, na anapoinama ili kuiokota, anamwona Jill.
  • Macho yao yanakutana. Cheche zinaruka—ni “upendo - baada ya kuonana mara ya kwanza tu.”
  • Wanaanza kuongea na kuamua kwenda kwenye duka la aiskrimu lililo karibu kwa ajili ya vitandamlo.
  • Wakila vitandamlo, wanagundua kuwa wanayo mengi yanayofanana na kuamua kubadilishana namba za simu na kuongezana kwenye mitandao yao ya kijamii.
  • Wanakutana kwa ajili ya filamu siku iliyofuata, na kisha kuelekea kwenye bustani ambapo mikono yao kwa bahati mbaya inagusana na kujikuta wameshikana mikono.
  • Hivyo ndivyo ulivyoanza uhusiano wao wa ajabu. Wakaendelea kukutana mara kwa mara, na siku moja, wakati Jack alipomrudisha Jill nyumbani, akambusu kwenye shavu.
  • Wakati huo walihisi vizuri sana na kana kwamba hawawezi kuachia hapo. Wakaendelea kubusiana kwa shauku mdomoni na shingoni.
  • Siku moja wakati hakukuwa na mtu nyumbani, Jack akamwalika Jill nyumbani kwake ili wasome. Muda si muda, wakaanza kubusiana, jambo ambalo lilisababisha kutomasana haraka. Bila kufikiria zaidi wakavua nguo zao na kushiriki ngono. (Waambie washiriki wainue biskuti zao za sandiwichi, na kuzitenganisha. Waambie washike ubavu wa biskuti iliyo na krimu zaidi—ili kuwakilisha miili yao, kisha waziunganishe biskuti hizo mbili pamoja—ili kuwakilisha mshikamano unaofanyika wakati wa kujamiiana).
  • Haraka sana, ngono inakuwa lengo la uhusiano wao. Lakini baada ya miezi kadhaa, wanagombana sana na Jill anaamua hampendi Jack hata kidogo. Anaamua kumwacha. (Waambie washiriki wavute biskuti hizo mbili na kuzishikilia ili wazione.)

4. Waulize washiriki wanachokiona wanapotenganisha biskuti ya sandwich. Baadhi ya vanila au cream ya chokoleti imehamishiwa kwenye kipande kingine cha biskuti.

5. Waeleze kwamba maendeleo ya ukaribu wa kimwili yanaweza yasiwe ya haraka/na makali kama jinsi yalivyotokea katika hadithi hii, lakini jambo moja linaweza kusababisha lingine kwa urahisi.

6. Eleza kwamba ngono hujenga uhusiano unaobadilisha wahusika. Kama tu kipande cha biskuti kilicho na vanila na cream ya chokoleti, pande zote mbili huacha sehemu yao kwa mwingine. Hata wanapojaribu kwenda njia mbalimbali, alama walizoweka hubaki.

7. Sisitiza kwamba tendo kali la kimwili na la kihisia kama ngono ni salama ndani ya mipaka ya ndoa tu. Ngono hujenga uhusiano unaothibitisha ahadi ambayo wanandoa waliyoitoa siku ya harusi yao.

Activities Icons

SHUGHULI MUHIMU
Zoezi 3: Hali ya kunata

Blank Icons

Lengo

Kuelezea jinsi suala la ngono linavyo jenga uhusiano.

Mahitaji

  • Seti 1 ya karatasi ya samawi na waridi ziliozounganishwa awali
  • Seti 1 ya karatasi mbalimbali za samawi na waridi (hiari)
  • Gundi

Maagizo

1. Ikiwa unaanza na karatasi mbalimbali za samawi na waridi, zigundishe karatasi hizi pamoja.

2. Onyesha washiriki karatasi iliyobandikwa awali na ueleze kuwa watu wawili wanapofanya ngono, mwili hutoa homoni inayoitwa oxytocin, inayowakilishwa hapa na gundi. Homoni hii hujenga uhusiano mkubwa kati yao (kwa maelezo zaidi kuhusu oxytocin ni nini, tafadhali angalia Maudhui ya Ziada - Oxytocin mwishoni mwa zoezi hili).

3. Wakati gundi imekauka, jaribu kuzitenganisha karatasi. Haijalishi jinsi unavyojaribu kutenganisha karatasi kwa uangalifu, mgawanyiko safi hauwezi kufanyika - karatasi zimeshikamana pamoja.

4. Waeleze kwamba shughuli za ngono zinahusisha na kujumuisha sehemu zote za mwanadamu na kuimarishwa na homoni ya oxytocin inayotolewa na mwili wakati wa ngono. Ukishiriki ngono kabla ya ndoa na mkaachana, matokeo yake ni ni makovu ya kuvunja uhusiano sio kimwili tu bali kihisia, kiroho, na kihomoni pia.

5. Sisitiza kwamba tendo kali kama hilo la ngono ni salama tu ndani ya mipaka ya ndoa. Uhusiano unaotokezwa na urafiki wa kimwili ni gundi inayoimarisha ahadi ambayo wanandoa waliitoa siku ya arusi yao.

Extra Content Icons

Maelezo Ziada

Oxytocin

Ile hatua ya kukuza uhusiano kati, ya wawili wanaopendana kufuatia tendo la kujamiana sio tu ni kutokana na hisia ama maamuzi , mwili wa mwanadamu pia una utaratibu unaosaidia kuunda vifungo vya kihisia vya bio-kemikali kati ya watu. Oxytocin ni homoni ambayo hutolewa wakati mama mja mzito anapojifungua mtoto wake. Homoni inajitokeza na inawezesha mama huyo kuhusiana kwa karibu na mwanawe, ni uhusiano unaomfanya awe mlinzi. Kemikali hiyo hiyo vilevile hutolewa kwa mfano mwanamke anapokumbatiwa kwa sekundi 20 au zaidi.

Wanaume vilevile wanatoa oxytocin pamoja na vasopressin, kemikali yenye nguvu inayosababisha wanaume kushikamana kwa undani sana na wenzi wao kwa maisha yao yote na kuwafanya kuwa kinga yao.

Wakati watu wawili wanaposhiriki ngono, miili yao hutoa homoni hizi ambazo huwawezesha kujenga uhusiano wa kihisia kati yao. Wanaposhiriki ngono na si mara moja, homoni za oxytocin na vasopressin zinatolewa zaidi. Je unaweza kuwazia ni jinsi gani mshikamano hou ulivyo na nguvu ?

Kemikalia ya oxytocin na vasopressin hutolewa pasipo kujali iwapo wawili wameoana ama ni tendo la ndoa la usiku mmoja, hakuna kitu kama “ngono isiyo na masharti” - daima kutakuwa na uhusiano wa kihisia unaoundwa. Kemikali hizi hazina maadili—hazitofautishi kati ya mazuri na mabaya, mema na maovu.

Oxytocin na vasopressin zinapotolewa, huwasha sehemu za ubongo ambazo zinahusiana na tabia ya kijamii kama vile hisia za uhusiano wa kina, na ikiwezekana kuwa “katika mapenzi.” Homoni hizi huimarisha uhusiano kati ya washirika wa ngono. Kwa kweli, shughuli za ngono, zinazoimarishwa na mfumo wa malipo ya kemikali katika ubongo, zinaweza kuleta uraibu. Hivyo ngono ndani ya ndoa ni afya na manufaa, lakini ngono nje ya ndoa ni hatari. Ingawa oxytocin hutolewa kwa wanaume na wanawake, athari zake zinaonekana kuwa na nguvu zaidi kwa wanawake.

Activities Icons

Zoezi 4: Je ________ Inahesabiwa kama kushiriki ngono?

Blank Icons

Lengo

Kuwasaidia washiriki kuelewa nini hutangulia tendo la ngono.

Maagizo

1. Waombe washiriki wote wasimame. Kwa kila kauli, washiriki watakaojibu ndiyo watapaswa kukaa chini wale watakaojibu hapana watabakia wamesimama.

2. Kauli: “Je, unaweza kusema “ulishiriki ngono” na mtu ikiwa shughuli ya karibu zaidi uliyoshiriki ilikuwa ________?”

  • Kubusu kwa muda mrefu: Kubusu mdomo kwa mdomo kunakohusisha ulimi (pia hujulikana kama busu la Kifaransa)
  • Kubusu hadi shingoni: Kubusu kwa shauku, kwa muda mrefu popote kutoka kwenye mabega kwenda juu; wakati mwingine inaweza kusababisha michubuko inayojulikana kama “hickies” au kuumwa kwa upendo
  • Kutomasana: Kubembeleza mwili wa mtu mwingine alivevaa nguo huku ukibusu, k.m., tumbo, lakini bila kujumuisha sehemu za siri.
  • Kutomasana sana: Kubembeleza mwili wa mtu mwingine aliye uchi huku ukimbusu, pamoja na sehemu za siri.
  • Uchezaji wa ngono: Tendo lolote linaloiga kujamiiana kwa kuchochea nyege sana lakini bila kupenya halisi; ni pamoja na ngono ya mdomo, kupiga punyeto, kuvua nguo, ngono bila kuvua nguo, nk.
  • Kujamiiana: Kushiriki ngono ikiwamo na kuupenya uke.

3. Iwapo wengi wa washiriki wanafikiri kuwa inachukuliwa kuwa ni “ngono” tu wakati wa kujamiiana na si kila kitu kingine kabla ya hapo (kubembeleza bila kuvaa nguo zao au kubembeleza sana), kuna uwezekano kwamba watachora mstari/mpaka kwenye hatua za mwisho za ukaribu wa kimwili.

4. Vijana wengi huamini kwamba wanaweza kufanya “chochote isipokuwa . . .” na bado wawe “bikira” Kwa nini hiyo sio busara? Je, ni uwezekano gani ambao vijana wengi wataacha kabla tu ya kujamiiana?

  • Ukaribu wa kimapenzi sio wa kimwili tu-kuna kihisia (hisia zako), kimaadili (maadili na matokeo), kijamii (jinsi unavyohusiana na wengine) na vipengele vya kiakili (tathmini na kufanya uchaguzi) pia. Oxytocin hutolewa wakati wa msisimko, kwa hiyo pia kuna kuambatanishwa na kuunganishwa wakati wa msisimko. Hii ina maana kwamba hata kama hukukusudia kujiunganisha kihisia, kibaolojia (jinsi tulivyoumbwa) umeunganishwa na kuambatanishwa bila idhini yako.
Activities Icons

Zoezi 5: Hatua za kuimarisha uhusiano

Blank Icons

Lengo

Kuwasaidia washiriki kuzijua hatua mbalimbali za ukaribu zinazosababisha kuimarika kwa uhusiano.

Mahitaji

  • Seti 2 za lebo za “Hatua za Kuunganisha”.
  • Watu 20 wa kujitolea (wavulana 10 na wasichana 10) + 2 wavulana na wasichana wa ziada wataojiunga karibu na mwisho wa zoezi hili

Maagizo

1. Waliojitolea wasimame katika vikundi viwili, kimoja cha wavulana na kingine cha wasichana wakiacha nafasi kati yao inayotosha kuunda mstari kati ya hivi vikundi viwili.

2. Sambaza seti moja ya kadi kwa wasichana na seti moja kwa wavulana. Kila mtu aliyejitolea anapaswa kuvaa lebo moja, ambayo iko wazi inaweza kusomwa na wengine wote.

3. Ndani ya vikundi vyao, waombe waliojitolea wajipange kulingana na wanavyofikiria mlolongo wa uhusiano unavyoendelea.

4. Watakapomaliza, linganisha mipangilio ya kati ya kikundi cha wavulana na cha wasichana.

5. Mwombe mvulana wa ziada aliyejitolea asimame kwenye mstari pale ambapo anafikiria urafiki unatafsiriwa kuwa uhusiano. Vivyo hivyo msichana wa ziada wa kujitolea naye afanye.

6. Wavulana wanaweza kuchora mstari baada ya kugusana kwa kiasi kikubwa kimwili kama vile “mkono hadi kiuno,” ambapo kwa wasichana, “mkono kwa mkono” kwa kawaida ikiwakilisha kushikana mikono katika uhusiano.

7. Jadili yanayofanana na yanayotofautiana katika mitizamo na matarajio ya ukaribu wa kimwili kati ya jinsia hizi mbili.

Dkt. Desmond Morris, mwandishi wa kitabu kuhusu tabia [Intimate Behavior], anaeleza kwamba wanaochumbiana wanahitaji kupitia hatua mbalimbali za urafiki wao ikiwa wanapenda uhusiano wao uwe wa kudumu, yaani kuelekea kuoana, waanze na hali ya kawaida.

Slides Icons
  • 1. Jicho kwa mwili
  • 2. Jicho kwa jicho
  • 3. Sauti kwa sauti
  • 4. Mkono kwa mkono
  • 5. Mkono kwenye bega
  • 6. Mkono hadi kiuno
  • 7. Uso kwa uso
  • 8. Mkono hadi mwili
  • 9. Kugusa chini ya kiuno
  • 10. Kujamiiana
  • *Kwa makusudi ya zoezi hili hatua mbili (mkono kwenye kichwa na mdomo kwenye matiti) vimeondolewa. Zoezi hili limenukuliwa toka The 12 Stages of Bonding, Life on the Edge, Sura ya 6, uk. 88-93, © 1995, na Dkt. James Dobson]

Kwa nini tunahitaji kwenda kwa utaratibu na polepole kupitia hatua za kuimarisha uhusiano?

  • Mfano rahisi utakuwa unapojaribu kuchezea ndege ulaya au nyumba uliyojitengenezea kwa kutumia karatasi ulizoziunganisha na gundi. Ikiwa ni kabla ya kukauka, karatasi zitaachana. Lakini ikiwa unaipatia muda wa kutosha kukauka, nguvu ya gundi ngumu itaidumisha.
  • Hatua za baadaye zinapofikiwa kabla ya wakati, kama vile marafiki wanapobusiana siku ya kwanza wanapokutana au kufanya ngono kabla ya ndoa, kuna kitu cha thamani kinapotea kutoka katika uhusiano huo. Itadhoofisha ndoa yako ya baadaye na familia haitakuwa imara.
Activities Icons

SHUGHULI MUHIMU
Zoezi 6: Mbali ni mbali kiasi gani?

Blank Icons

Lengo

Kuwasaidia washiriki kufanya uamuzi sahihi na kujua wapi pa kuweka mipaka ya ukaribu wa kimwili katika uhusiano.

Mahitaji

  • Mshumaa mfupi
  • Kitoa baruti
  • Viberiti

Maagizo

1. Elezea umuhimu wa kujua jinsi mwanadamu alivyoumbwa katika maswala ya unyumba.

MSWADAKITENDO
Joe anaelezea jinsi sisi sote ndani yetu tunao mshumaa uliyowashwa wa kuwapenda wale wa hisia tofauti.

Wakati uhusiano unapoanza,unaridhika mkiwa pamoja lakini baada ya muda unakuwa na hitaji la kushikana mikono.
Washa mshumaa.

Washa kiberiti kwa kutumia mshumaa.
Baada ya muda, unataka kuendeleza uhusiano huo na hisia ya mapenzi inaanza kuchipuka. Usipokuwa makini utaanza kutomasana na swala moja litazua jingine mpaka mnajikuta mmeshiriki ngono. Kama tendo hilo ni nje ya ndoa, mara nyingi uhusiano unaishia hapo na kuvunjika

Kilichokuwa kizuri na kilicho leta furaha tele kimegeuka kuwa kichungu kama ndimu.Vijana wengi ambao walijiusisha katika vitendo vya ngono kabla ndoa wanajihisi hatia, aibu, na kujuta kwa kuwa tendo hilo halitafutika mioyoni mwao. Maji yaliyomwagika hayawezi kuzoleka. Shikilia baruti iliyochomeka waeleze wanaoshiriki wanaona nini (kilichoungua, kimechomeka, na cheusi).
Washa kiberiti cha pili kutumia kiberiti cha kwanza, washa kiberiti cha tatu kutumia cha pili.

Washa baruti ukitumia kiberiti cha tatu. Baruti itaisha wakati ambapo unapofika eneo la uhusiano kuvunjika.

2. Onyesha slaidi ya “umbali upi ni mbali zaidi?”:

  • Hamu ya kufanya mapenzi huongezeka kuambatana na ukaribu wa miili yenu ulivyo.
  • Uliza: Kwa vile umetambua jinsi tulivyoumbwa, je ni wapi utaweka mipaka katika maswala ya kujamiana?

Ni wapi mipaka itaafiki msimamo wako?

  • Unapovuka mpaka ni wakati akili haitafakari tena (maana imezidiwa papo hapo ikilinganishwa na mtu anayetumia mihadarati au pombe) na badala yake homoni ndizo zinazokuendesha. Hilo huanzishwa na busu la muda mrefu ambalo linaendeleza mchakato haraka sana hadi kufikia tendo la ngono.

3. Chagua swali moja au mawili kati ya yafuatayo ya kuuliza:

  • Kila mwanaadamu anao uwezo wa kujizuia.Iwapo wanaochumbiana watachagua kujizuia hadi waoane, unadhani ni hatua gani wanapashwa kuweka mipaka kwenye ukaribu wao.
  • Kushikana mikono? Kubusiana mpaka hata shingoni, kukumbatiana na kutomasana? Kufanya hivyo bila nguo? Kwa nini, toa sababu?
  • Hamu ya tendo la ngono huendelea hatua kwa hatua. Hasa wanaposhikana mikono, hatua ya pili ni kukumbatiana na kupiga busu mpaka shingoni, na kadhalika. Iwapo wanaochumbiana hawajaweka mipaka wazi mwanzoni mwa uhusiano wao ni nini kinaweza kufanyika?

4. Wakumbushe washiriki uhusiano unapovunjika, aliyejihusisha na tendo la ngono ndiye atakayeathirika mawazo. Walioshiriki ngono hawawezi kuachana kihisia bila mabaki (kama katika shughuli za “Hali ya Kunata” na “Mchanganyiko wa Vidakuzi”). Wameitoa sehemu yao wenyewe na kumpatia aliyeachwa. Pitia vipengele vitano vya ukuaji vilivyotajwa katika Sura ya 1 “mwili wa mwanadamu ” : Akili, mazingira, hisia, mwili na maadili mema, – katika kutoa ukumbusho swala la ngono, si tendo la mwili peke yake.

Waombe washiriki, kuchora mstari wima kwenye sehemu ya grafu katika kitabu cha mazoezi mahali ambapo wataweka mipaka ya binafsi kuhusu kukaribiana kimwili.

Unavuka mipaka pale?

  • Mikono yako inaanza kugusa gusa
  • Unaanza kuondoa nguo
  • Unafanya jambo ambalo huwezi kumfanyia mtu unamheshimu
  • Unaibua hisia ambazo zinashinda uwezo wako wa kufanya uamuzi
  • Kupapasa kumetengewa kuhamsha hisia za mapenzi.
    Ngono imelengewa ndoa.
    Ndoa imepangiwa kuwa ya maisha.
  • [Nukuu kutoka kitabu cha Sex, Love, and Dating cha George Eager]
Youre Going Too Far When Graphic

Lengo

Kuwasaidia washiriki kufahamu matokeo yanayohusu hisia, jamii, na mwili wanaposhiriki ngono kabla ya ndoa.

Usuli

Dkt. Henry Cloud na Dkt John Townsend katika kitabu chao kinachoitwa Mipaka (Boundaries) wameandika kwamba “Uamuzi wowote una matokeo yake; mema ama mabaya, hiyo ni sheria ya maisha . Ikiwa unavuta sigara, kuna uwezekano mkubwa kwamba utaendeleza utapeli wa mvutaji sigara, na unaweza hata kupata saratani ya mapafu. Ukitumia fedha kupita kiasi, kuna uwezekano mkubwa utapata simu kutoka kwa wadai, na unaweza hata ukawa na njaa kwa sababu huna pesa za kununua chakula. Kwa upande mwingine, ikiwa unakula vizuri na kufanya mazoezi mara kwa mara, utapata matatizo machache ya afya. Ukiweka bajeti kwa busara, utakuwa na pesa tele za kulipa mahitaji yako ya chakula.”

Kila tendo lina matokeo yake; mema ama mabaya. Suala la ngono nje ya ndoa lina matokeo mengi yaliyo tofauti na magumu. Wanaoathirika sio tu wale wanaohusika katika tendo la ngono, lakini wale walio karibu nao pia, yaani, familia, marafiki na hata jamii.

Activities Icons

Zoezi 1: Mito Ingeweza Kuongea

Blank Icons

Lengo

Kuwaonyesha washiriki mtandao wa matokeo ya kujamiiana kabla ya ndoa unavyoonekana katika maisha halisi.

Mahitaji

  • Mashuka ya kitanda
  • Lebo zilizo na majina (ya wasichana na wavulana). Nyuma au mbele ya vitambulisho vya majina, andika herufi (kama inavyoonyeshwa hapa chini) kwenye kona ya kulia.
If Pillows Could Talk 1

Mifano:

  • Rob – CH/HI,
  • Mary – CH
  • Carol – HI
  • Patti – HE
  • Todd – HE
  • Cindy – HE
  • Steve – ?
  • Joe – CH
  • Eileen – HP/TR
  • Jeannie – ?
  • Gary – HP/TR
  • Ronnie – HI
  • Julie – HI
  • Ann – ?
  • Jeff – ?
  • Peter – HP
  • Sue – HP
  • John – HI
  • Washiriki 18, ikiwezekana wasichana 9 na wavulana 9
  • Vipande 18 vya uzi (karibu mita 1 kila moja)
  • Slaidi ya “Iwapo mito ingeweza kuongea”

Maagizo

1. Mpatie lebo ya jina kila aliyejitolea, kadri iwezavyo wapatie wasichana majina ya kike na vile vile wavulana majina ya kiume.

2. Tandaza shuka sakafuni mbele ya chumba. Hakikisha kuna nafasi ya kutosha kwa waliojitolea kusimama hapo.

3. Waambie kwamba watakaposikia “jina” lao linaitwa, waje mbele na kusimama kwenye shuka.

4. Anza kuwasomea kwa sauti :

  • “Hii ni hadithi ya mapenzi kati ya Sue na John.
  • (Sue na John wasimame mbele kwenye shuka)
  • Sue na John wamekuwa marafiki kwa miezi minne. Wanahisi uhusiano wao umeendelea hadi kufikia hatua ya kufanya ngono kabla ya ndoa, lakini hawajazungumzia historia yao ya ngono.
  • Lakini UKWELI ni kwamba hadithi inaanza na Mary na Rob.
  • (Waambie Sue na John waende kando, mmoja kushoto na mwingine upande wa kulia wa shuka. Mary na Rob wasimame kwenye shuka)
  • Mary na Rob walishiriki ngono kabla ya ndoa kwa miezi mitano ya uhusiano wao.
  • (Mary na Rob kila mmoja ashikilie ncha moja ya uzi ili kuwakilisha uhusiano wa kingono)
  • Wakati huo, Rob alijihusisha na matumizi ya dawa za kulevya na hakuwa mwaminifu kwa Mary akalala na Patti na Carol.
  • (Bila kuachia kamba Rob aliyoshikilia na Mary, mwambie Rob ashike nyuzi nyingine 2 kwa mkono wake mwingine ili kuungana na Patti na Carol)
  • Kitu ambacho Rob hakujua ni kwamba Mary alishawahi kushiriki ngono na Joe.
  • (Bila kuachia uzi ambao Mary ameshikana na Rob, mwambie Mary ashike kamba nyingine kwa mkono wake mwingine ili kuungana na Joe.)
  • Rob hakuwahi kuuliza kuhusu historia ya ngono ya Patti na Carol. Ikiwa angefanya hivyo, angegundua kwamba Carol alikuwa amelala na Jeff na Ronnie, na Patti alikuwa amelala na Todd.
  • (Bila kuachilia kamba Carol aliyoishika na Rob, mwambie Carol azishike nyuzi nyingine 2 kwa mkono wake mwingine ili kuungana na Jeff na Ronnie; Bila kuachia uzi ambao Patti ameshikilia na Rob, mwambie Patti ashike uzi mwingine ili kuungana na Todd.)
  • Historia ya ngono ya Todd ni pamoja na kulala na Cindy. Historia ya Ronnie ni pamoja na kulala na Julie na Jeannie.
  • (Bila kuachia uzi ambao Todd ameshika na Patti, mwambie Todd ashike uzi mwingine kwa mkono wake mwingine ili kuungana na Cindy; Bila kuachia uzi alioshika Ronnie na Carol, mwambie Ronnie ashike nyuzi nyingine 2 kwa mkono wake mwingine ili kuungana na Julie na Jeannie)
  • Mary alipogundua kuwa Joshua hakuwa mwaminifu alikasirika, akaachana naye na kulala na Steve muda mfupi baada ya kuachana.
  • (Bila kuachilia uzi Mary alioshikilia na Rob na Joe, Mary ashike uzi mwingine ili kuungana na Steve.)
  • Mary hakujua kuhusu historia ya ngono ya Steve. Steve alikuwa amelala na Ann na Eileen.
  • (Bila kuachia uzi Steve alioushika na Mary, mwambie Steve ashike nyuzi nyingine 2 kwa mkono wake mwingine ili kuungana na Ann na Eileen.)
  • Eileen alilala na Gary muda fulani baada ya kulala na Steve. Pia Eileen na Peter waligusana kwenye sehemu za siri wakiwa uchi, (ngozi kwa ngozi), ingawa hawakukamilisha tendo la kujamiiana.
  • (Bila kuachilia uzi Eileen alioushikilia na Steve, Eileen ashike nyuzi nyingine 2 kwa mkono wake mwingine ili kuungana na Gary na Peter—ingawa Eileen hakufanya ngono na Peter, kugusana kwao ngozi hadi ngozi kunachukuliwa kuwa uhusiano uliowaunganisha kingono.)
  • Kumbuka kwamba hii ilipaswa kuwa hadithi ya mapenzi kati ya Sue na John.
  • (Waambie Sue na John warudi kusimama kwenye shuka popote pale watakapoweza kupata nafasi.)
  • Je, wameunganishwaje na watu hawa waliosimama kwenye shuka?
  • Julie (Mwambie Julie ainue mkono wake kuonyesha mahali alipo kwenye shuka) alikuwa amelala na John.
  • (Bila kuachia uzi ambao Julie ameushikilia na Ronnie, mwambie Julie ashike uzi mwingine kwa mkono wake mwingine ili kuungana na John.)
  • Sue hakuwahi kujamiiana, lakini alikuwa na uhusiano wa karibu sana na Gary, wakiwa wamegusana sehemu za siri wakiwa uchi.
  • (Bila kuachia uzi Gary alioushika na Eileen, mwambie Gary ashike uzi mwingine kwa mkono wake mwingine ili kuungana na Sue—ingawa Sue hakufanya ngono na Gary, mgusano wao wa sehemu za siri wakiwa uchi unachukuliwa kuwa uhusiano uliowaunganisha kingono.)

5. Katika hatua hii, waambie washiriki walio na HI kwenye kona ya chini, upande wa kulia wa lebo ya majina yao kuinua mikono yao. Waambie kwamba HI inawakilisha VVU na wale walioinua mikono yao wanawakilisha wale ambao sasa wameambukizwa VVU. Unaweza kuendelea kusoma baadhi ya ukweli kuhusu VVU. Kama bado kuna muda wa kutosha, unaweza kueleza maana ya herufi zao nyingine (CH, HP, TR) na kusoma ukweli kuhusu magonjwa hayo ya zinaa.

  • Rob – CH/HI [Klamidia na VVU]
  • Mary – CH [Klamidia]
  • Carol – HI [HIV]
  • Patti – HE [Herpes]
  • Todd – HE [Herpes]
  • Cindy – HE [Herpes]
  • Steve – ? [bila uhakika]
  • Joe – CH [Klamidia]
  • Eileen – HP/TR [HPV na Trichomoniasis]
  • Jeannie -? [bila uhakika]
  • Gary – HP/TR [HPV na Trichomoniasis]
  • Ronnie - HI [VVU]
  • Julie – HI [VVU]
  • Ann -? [bila uhakika]
  • Jeff -? [bila uhakika]
  • Peter – HP [HPV]
  • Sue – HP [HPV]
  • John - HI [VVU]

Unaweza kuangazia uchunguzi ufuatao:

  • Sue hakuhitaji kujamiiana ili kupata magonjwa ya zinaa.
  • John aliambukizwa VVU kwa kulala na Julie, ambaye alikuwa amelala na Ronnie, aliyekuwa na virusi hivyo.
  • Kwa wale ambao hawana magonjwa ya zinaa, wanaweza kuona ahueni sasa, lakini kumbuka kwamba baadhi ya magonjwa ya zinaa hayana dalili na yanaweza kugunduliwa baadaye sana. Hata kama magonjwa ya zinaa hayajaonekana, bado yanaweza kuambukizwa. Ikiwa umekuwa na shughuli za ngono, njia pekee yake ya kujua kama huna magonjwa hayo, ni kupimwa.
Slides Icons

6. Onyesha slaidi inayoonyesha utando mgumu wa mahusiano na jinsi magonjwa mbalimbali ya zinaa yalivyoambukizwa.

  • Tendo la ngono halikunuiwa kukuangamiza.

Ni tendo moja tu mwanadamu hutenda kabla hajajipata katika hatua tata ya kupata maradhi yanayo sababishwa na ngono asipo kuwa mwangalifu. Mwanadamu anastahili kuwa na mchumba mmoja na kuzingatia uwaminifu. Wakati wa harusi yako, ni wewe tu na mke/ mme wako je unataka ujihusishe na watu 17? Kabla ya kuoa/kuolewa.

Unaweza kujumuisha taswira ya slaidi ya makala ya jarida la Time, “Picha ya Ngono za Vijana,” ya Februari 14, 2003, ili kuonyesha kuwa haya hutokea katika maisha halisi. Katika utafiti huu mahususi wa shule moja ya sekondari ya Marekani, wanafunzi wengi walikuwa na mpenzi mmoja au wawili tu lakini hata hivyo waliounganishwa na mtandao wa wanafunzi 288, na kuwaweka katika hatari ya kuambukizwa magonjwa ya zinaa kwa sababu walioshiriki nao ngono walikuwa nao wameshiriki ngono na wengine.

If Pillows Could Talk 2

Ukweli wa Haraka juu ya magonjwa ya zinaa

Kisonono

Maambukizi ngono (ya uke, ya mdomoni au ya mkunduni), kutoka mama hadi mtoto
Inafanya nini? Huvamia mfupo wa uzazi na ikiwa haitachunguzwa kwa mapema husambaa hadi kwenye ngozi na maungo.
DALILIATHARI ZA MUDA MREFU
WANAWAKEMatatizo ya ukuaji
Uchungu wakati wa kujamiianaMatatizo ya uzazi
Uchungu wakati wa kukojoa
Kutapika
Kitengo nyeti kuwa yenye rangi ya manjano ama kijani kibichi
WANAUME
Usaha kwenye uume
Maumivu/kusikia kuungua wakati wa kukojoa
WOTE
Kuwashwa kwa mkundu
Usaha toka mkunduni
Maumivu kwenda choo
Kuwashwa na maumivu ya koo
Shida kumeza
DAWA AU TIBA? KISONONO KINAWEZA KUTIBIWA KUPITIA KUMEZA DAWA ZA KUUA BAKTERIA.

Herpes

Maambukizi kupitia tendo la ngono (ya uke, ya mdomoni au ya mkunduni), kugusana ngozi na aliyeathirika, na mama kwa mwanawe.
Inafanya nini?
DALILIATHARI ZA MUDA MREFU
 DALILI ZA MWANZOMaumivu yanayotokea mara kwa mara kutokana na mkururo wa mawazo ugonjwa,uchovu , kukaa juani au hedhi
makundi ya vidonda venye uchungu
Maumivu wakati wa kukojoa
Dalili kama za mafua
MEDICATION OR CURE? There is no cure for herpes. However, medication can help to speed up healing and
lessen the pain of the sores, as well as control recurrences.

HPV

HUMAN PAPILLOMAVIRUS

Maambukizi kupitia tendo la ngono (ya uke, ya mdomoni au ya mkunduni), kugusana ngozi na aliyeathirika, na mama kwa mwanawe.
Inafanya nini?
DALILIATHARI ZA MUDA MREFU
Dutu za uzaziniSaratani ya kizazi
Mara nyingi hakuna dalili zinaonekanaSaratani ya uume
Maumivu wakati wa kukojoaSaratani ya mkunduni
Dalili kama za mafuaSaratani ya mdomo
DAWA AU TIBA? Haina tiba. Hata hivyo, zipo chanjo na matibabu.V

V. Wakati HPV ikitokea, madakatari wanashauri kwenda kupimwa mara kwa mara hospitalini kwa ajili ya swala la saratani; kwa wanawake wengi ,virusi hivyo hutoweka pasipo kuathiri afya iwapo vitashughulikiwa . Chanjo ya HPV inalenga aina mbili zinazosababisha asilimia 70% za saratani ya uzazi; hata wale ambao waliopata chanjo wanaweza kupata maradhi hayo

Ugonjwa wa ini - Hepatitis B

Maambukizi Kupitia tendo la kujamiana (ya uke, ya mdomoni au ya mkunduni),mama kwa mwanawe, kutumia sindano moja na kupatiwa damu ya aliyeathirika
Inafanya nini? Ugonjwa wa ini
DALILIATHARI ZA MUDA MREFU
UchovuUgonjwa wa ini
Maumivu upande wa chini tumboniSaratani ya ini
Kupoteza hamu ya kula
Kichefuchefu/kutapika
Maumivu ya viungo
Kuumwa na kichwa
Homa
Vipele
Hakuna dalili W
DAWA AU TIBA? Tiba zake ni nadra sana. Hata hivyo, inaweza ikaondoka yenyewex.X

W. Asilimia 50% ya walioathirika hawaonyeshi dalili yoyote. Dalili huonekana kati ya wiki sita na miezi sita baada ya mtu kuambukizwa.

X. Watu wengi walioathirika virusi vinatoweka kati ya wiki nne mpaka nane. Watu wachache wanabaki na virusi kuwaambukiza wengine maisha yao yote.

PID

UVIMBE WA NYONGA

Maambukizi Mara nyingi, PID ni matokeo ya magonjwa ya zinaa ambayo hayajatibiwa,
kama vile klamidia au kisonono.
Inafanya nini? Hushambulia mfumo wa uzazi wa mwanamke.
DALILIATHARI ZA MUDA MREFU
Mwanzoni hakuna dalili YKuwa tasa Z
Kutoka damu kusiko kawaidaMimba za ectopic
Kutokwa uchafu ukeniMaumivu ya muda mrefu
Maumivu ya tumbo na mgongo
Homa/kusikia baridi
Kichefuchefu/kutapika
Maumivu ya uke wakati wa ngono
DAWA AU TIBA? Madaktari wanaweza kuagiza antibiotics na kushauri kupumzika kitandani na kujiepusha na ngono. Kesi mbaya zaidi zinaweza kuhitaji upasuaji ili kurekebisha au kuondoa kizazi.

Y. Mwanzoni, PID haionyeshi dalili zozote. Hata hivyo, wakati maambukizi yanavyoendelea, dalili zinaweza kuanza kuonekana.

Z. Kadiri idadi ya maambukizo ya PID ambayo mwanamke amekuwa nayo, ndivyo hatari ya kuwa mgumba inavyoongezeka.

Trichomoniasis

Maambukizi Ni vimelea vinavyotoka kwa mtu aliyeambukizwa hadi kwa mtu ambaye hajambukizwa wakati wa ngono.
Inafanya nini? Husababisha kuvimba sehemu za siri ambayo hurahisisha kuambukizwa VVU.
DALILIATHARI ZA MUDA MREFU
Usumbufu wakati wa kukojoaVVUTrichomoniasis isipotibiwa huongeza hatari ya kuambukizwa na
Kuwashwa kidogo hadi kuvimba sana
Kuwashwa au maumivu ndani ya uume
Kutokwa na uchafu kwenye uume
Kuwashwa, kuwaka, uwekundu au maumivu ya uke
DAWA AU TIBA? Trichomoniasis inaweza kutibiwa na dawa zilizoagizwa na daktari.

Kaswende

Maambukizi kushiriki ngono (ya uke, ya mdomoni au ya mkunduni), kuguasana ngozi na aliyeathirika, mama kwa mwanawe wakati wakulea mimba.
Inafanya nini? Inapoingia inakwenda moja kwa moja kwenye viungo vya mwili muhimu na kuvidhuru
DALILIATHARI ZA MUDA MREFU
HATUA YA MWANZO (SIKU 21 - 90 BAADA YA MAAMBUKIZI):HATUA YA MWISHO:
Maumivu mahala ambapo virusi vilipata kupenyezaMshtuko wa moyo
Kupoteza hamu ya kulaMaumivu makali
Kufura kwa teziDementia
DALILI ZA KATI (WIKI 3 - 6 BAADA YA VIDONDA):Kifo cha gafla
2-to-6-week-long body rashes, often on the palms or
soles of the feet
Dalili kama za mafua
Kufura kwa tezi
DAWA AU TIBA? Inapotambulika mapema inaweza kutibika kwa antibiotics. Ikiwa imekaa sana inaweza pia kutibika na antibiotics lakini matibabu yake ni mazito zaidi na inaweza kusababisha madhara ya daima.

HIV

VIRUSI VYA UKIMWI VYA BINADAMU

Maambukizi Kubadilishana maji ya mwili (damu au manii), mama kwa mtoto, kutumia sindano pamoja, kuongezewa damu ya mtu aliyeathirika.
Inafanya nini? Inavunja mfumo wa kinga ya mwili.
DALILIATHARI ZA MUDA MREFU
Dalili kama za mafuaUnyonge/kutokuwa na kinga ya mwili
Kufura kwa teziKupata UKIMWI
HomaKifo cha gafla
Kuumwa na kichwa
Uchovu
Maumivu ya misuli
Kunaweza kusiwepo na dalili zozote mpaka UKIMWI unapoanza
DAWA AU TIBA? Hakuna tiba ya VVU au UKIMWI. Dawa zinaweza kuboresha Maisha au kuyarefusha tu..
Activities Icons

SHUGHULI MUHIMU
Zoezi 2: Koroga na Changanya

Blank Icons

Lengo

Kusaidia washiriki kuelewa kwamba kushiriki ngono kabla ya ndoa kunaleta hatari ya kupata magonjwa ya washirika wote wa zamani wa wale unaofanya nao ngono.

Mahitaji

  • Vikombe vidogo vya plastiki kwa kila mshiriki
  • Maji
  • Siki nyeupe
  • Soda ya kuoka katika vitingisha pilipili

Maagizo

1. Tayarisha kikombe kimoja kwa kila mshiriki:

  • Jaza robo tatu ya idadi ya vikombe kwa maji (nusu kikombe) na robo ya vikombe na siki nyeupe (nusu kikombe).
  • Weka alama ya doti ndogo nyeusi kwenye vikombe vya siki.

2. Nasibu mpe kila mshiriki kikombe na umwombe azunguke chumbani kumwaga na kuchanganya “maji” yaliyo kwenye kikombe chake na kile cha washiriki wengine. Usiwaambie washiriki kwamba baadhi ya vikombe vina siki.

3. Waache waendelee kwa dakika 2-3 kabla ya kuwaomba washiriki warudi kwenye viti vyao na vikombe vyao.

4. Washirikishaji wazunguke chumbani na kuweka soda ya kuoka kwenye kila kikombe.

5. Mapovu yatatokea kwenye vikombe vyenye siki. (Hii itakuwa ni karibu ya wote waliomimina na kuchanganya.)

  • Waombe washiriki walioona mapovu kwenye vikombe vyao kuinua mikono yao—wanawakilisha wale ambao sasa wameambukizwa magonjwa ya zinaa.

6. Waombe washiriki ambao wameshika vikombe vilivyowekwa alama ya nukta nyeusi kusimama. Lielezee darasa kwamba washiriki waliosimama wanawakilisha wale ambao tayari walikuwa na magonjwa ya zinaa na walikuwa wanawaambukiza wengine walipokuwa wakizunguka kuchanganya vikombe vyao vya “maji.” (Wale walio na mapovu kwenye vikombe vyao wanapaswa kuwa wengi kuliko wale ambao vikombe vyao vina nukta nyeusi.)

7. Onyesha kwamba washiriki wanaweza “kufanya ngono” (kuchanganya “maji” yao) na mtu mmoja tu, lakini mtu huyo anaweza “kufanya ngono” na watu wengine wawili ambao wamekuwa na wapenzi wengi.

  • Kwa busara waulize washiriki wachache wasishiriki katika shughuli hii, (yaani, wasiruhusu “maji” kutoka kwenye vikombe vingine kuchanganywa na vya kwao). Watawakilisha wale ambao wamechagua kutoshiriki ngono kabla ya ndoa na hawako katika hatari ya kuambukizwa na magonjwa ya zinaa.
Slides Icons

Kumbuka: Unalala na kila mtu ambaye mpenzi wako amelala naye. Ngono kabla ya ndoa inajumuisha hatari ya kupata magonjwa ya washirika wote wa zamani wa yule unayeshiriki naye ngono.

Activities Icons

SHUGHULI MUHIMU
Zoezi 3: Mtandao wa madhara

Blank Icons

Lengo

Kuwasaidia washiriki watafakari madhara ya kujihusisha na ngono kabla ya ndoa.

Blank Icons

CHAGUO LA 1

Mahitaji

  • Ubao mweupe/chati mgeuzo
  • Chaki

Maagizo

1. Kwenye ubao, andika maneno haya: “Madhara ya Ngono Kabla ya Ndoa.”

Slides Icons

2. Waombe washiriki wapendekeze madhara yanayoweza kutokea iwapo watashiriki ngono kabla ya ndoa. Wanapotaja majibu yao, yaandike ubaoni kama hivi inavyoonyeshwa hapa chini..

Handbook 59 Icons

3. Iwapo kuna jambo linakosekana katika huu mchoro wafahamishe washiriki na uliongeze ubaoni.

4. Baada ya kuorodhesha madhara ya ngono kabla ya ndoa wafahamishe washiriki kuwa mtayaangalia haya madhara moja moja ili waelewe kwa nini na wapi pa kuweka mipaka inapokuja kwenye swala la ngono.

Instructions For The Facilitator Icons

Tanbihi:

  • Ili kuwe na mtiririko bora wa maudhui, anza na madhara ya kihisia, yakifuatiwa na mimba na kisha magonjwa ya zinaa.
  • Wape fursa wanaoshiriki kutoa maoni yao kwa yale ambayo tayari wanayajua .
  • Wezesha zoezi kwa kuuliza maswali ya kuongoza, kutoa taarifa zinazokosekana na kurekebisha dhana potofu.

Mafanikio ya zoezi hii yanategemea uwezo wa mwezeshaji kuwashirikisha washiriki bila kuwadharau au kunaswa katika kuwapatia taarifa nyingi kupita kiasi.

Blank Icons

Chagua mbadala hapa chini ikiwa kikundi hakikuweza kupendekeza madhara ya ngono kabla ya ndoa.

Blank Icons

CHAGUO LA 2

Mahitaji

  • 22 wa kujitolea
  • Kadi 3: kadi ya bluu ya “Madhara ya Kihisia”, kadi nyekundu ya “Mimba” na kadi ya zambarau “Maambukizi ya Magonjwa ya Zinaa”
  • Kadi 19 zenye: 5 “Matokeo ya Kihisia,” 3 “Mimba,” 8 “ Maambukizi ya Magonjwa ya Zinaa “ na kadi 3 “zinazohusiana na magonjwa ya zinaa”

Maagizo

1. Onyesha slaidi ya “Mtandao wa Matokeo: Madhara ya Ngono Kabla ya Ndoa”.

2. Watu 3 waliojitolea kushikilia kadi za “Madhara ya Kihisia,” “Mimba” na “magonjwa ya zinaa”, wasimame sehemu tofauti za chumba pakiwapo na nafasi kati yao.

3. Sambaza kadi 19 zilizobaki kwa watu watakaojitolea.

4. Wakisikia neno “Nenda,” watu 19 waliojitolea wakimbie na kusimama pamoja na mmoja wa wale watu 3 wenye kadi za matokeo.

5. Hakiki makundi, kuanzia na Madhara ya Kihisia, kisha Ujauzito, na mwisho magonjwa ya zinaa. Kadi 3 za madhara ya magonjwa ya zinaa ziwe za mwisho kabisa, na usisitize kwamba haiishii tu kwa magonjwa ya zinaa. Kuna hatari nyingi zaidi za kiafya zinazokuja pamoja na magonjwa haya ya zinaa.

6. Waelezee kundi kwamba huu mtandao wa madhara haya utarejelewa mara kwa mara kwenye hili somo.

Going Deeper Icons

Kwenda Ndani Zaidi

Blank Icons

Ngono – Hakuna uwajibikaji?

Athari za kihisia

Consequences Of Premarital Sex Graphic

Athari za kihisia za ngono kabla ya ndoa

Blank Icons
  • Imenukuliwa kutoka: Lickona, T. (2007) 10 emotional dangers of premature sexual involvement. The Fourth and Fifth Rs: Respect and Responsibility, 13(2): 1 – 6.] https://www.jstor.org/stable/42001755
Handbook Slides 60 Icons

1. Kubadili misimamo
Ngono kabla ya ndoa haisababishi tu kujihisi duni bali pia hutufanya kupoteza msimamo wa sisi ni akina nani. Tendo hilo linatuondolea kushtakiwa na dhamira zetu. Kama vile vidole vyetu vinakuwa sugu baada ya kucheza na gitaa kwa muda mrefu na kutosikia maumivu. Tendo la ngono linakuwa ni jambo la kujitosheleza tu na bila kuhesabu gharama yake au kufikiria jinsi linavyoathiri watu wengine.

2. Majuto
Licha ya uhuru wa kijinsia ambao umeenea katika jumuiya ya leo, wasichana wengi huishia kutumaini mvulana waliyelala naye atapiga simu, hata kama walikubaliana kwamba ni ushirika wa usiku mmoja tu. Wavulana pia, wanakuwa na majuto, haswa wakati uhusiano mzuri unaharibiwa kwa sababu ya kushiriki ngono.

Hatia inaweza kutokea kwa kushtakiwa na dhamiri baada ya tendo la ngono; kwa wengine, inatokana na imani za dini yao. Hatia inakuja wakati mtu anatoa mimba ya haramu. Ingawaje anaweza kujiona kama kwamba ameepukana na majukumu mengi lakini, athari za muda mrefu za uavyaji mimba hujumuisha majuto na hatia ya muda mrefu. Hili litashughulikiwa kwa mapana zaidi baadaye.

3. Hofu
Jinsi tutakavyoona hakuna kinga yoyoye inayotoa kinga asilimia 100% . Daima kuna changamoto ya kupata mimba ama magonjwa ya zinaa. Hivyo kushiriki ngono kabla ya ndoa kunasababisha wasiwasi unaotokana na kutokuwa na hakika ya matokeo.

4. Hofu ya kuwajibika
Vijana ambao walisalitiwa baada ya kushiriki ngono katika uhusiano wa mwanzo si rahisi kuwaamini wengine katika uhusiano utakaofuata, wanaogopa kusalitiwa tena.

5. Kujihisi duni na kutojiheshimu
Aibu inaweza kutokea kutokana na hisia za kutumiwa, kuambukizwa magonjwa ya zinaa, kutenda kwa msukumo au kukubali shinikizo au majaribu.

Hata ngono ya mdomo inaweza kusababisha wasichana kupoteza heshima yao. Wasichana wengine hufikiri kwamba kuanzisha au kufanya ngono ya mdomo ni kumpa mvulana kile anachotaka huku akiepuka kupata mimba. Walakini ukweli kuhusu ngono ya mdomo unabaki:

  • Mvulana anayemheshimu sana msichana au anayemjali hataomba ngono ya mdomo
  • Magonjwa mengi ya zinaa yanaweza kuambukizwa kupitia ngono ya mdomo
  • Kushiriki ngono ya mdomo kunaweza kusababisha hisia sawa za kutumiwa
  • Mvulana anayefanya wasichana wafanye ngono ya mdomo hana heshima.

Vijana wengi wanasema wanaota ndoto ya kuwa na ndoa yenye furaha siku moja. Jinsi gani ngono kabla ya ndoa huathiri ndoa vibaya?

Kwanza kunaweza kuwa na tabia ya kumlinganisha mwenzi wako na washirika wako wa zamani ambao mlitengana miaka mingi tu iliyopita. Wakati mwingine ni ile taswira tu na swala hilo linaweza athiri uhusiano wenu wa ngono katika ndoa.

Pili, kuna hatari ya kutokuwa mwaminifu katika uhusiano huo. Ikiwa hatukujifunza kukataa majaribu kabla ya ndoa, ni jinsi gani tunatarajia kuweza kukataa baada ya hapo?

Kushiriki ngono nje ya ndoa ni jambo linaweza sababisha uhusiano uliokuwa bora kuvunjika. Wakati lengo lililokuwa jema la kufahamiana linabadilika ghafla na kuwa ngono, vipengele vingine vya uhusiano vinaacha kuendelezwa na kukua. Hilo husababisha hisia hasi kutokea na uhusiano kuharibika.

Mimi silewi na hisia; Haiwezi ni athiri? Je ni kweli?

Hisia hasi sio tu huathiri watu « wanaotambua hisia zao » bali hata wale wasiotambua. Watu wanaweza kuzikandamiza hisia kwa akili zao, lakini zinapata njia ya kujitokeza hatimaye kwa njia nyingine. Ukweli ni kwamba mwili wa mwanadamu una uwezo wa kuunda vifungo vya kihisia baina ya watu. Hilo hutokana na kemikali ya oxytocin, homoni hiyo inaongeza uhusiano wa kihisia baina ya watu wawili.

Kwa sababu oxytocin hutolewa bila kujali ikiwa ni ngono katika ndoa au tendo la usiku mmoja tu, hakuna kitu kama “ngono isiyo na masharti” - daima kutakuwa na uhusiano wa kihisia.

Mimi ni mjamzito. Nifanyeje?

Kuna chaguo tatu::

  • Kuavya Mimba
  • Uzazi
  • Kuasili

Kuavya Mimba

Kuna Kuavya mimba kwa asili wakati mwanamke “anapoteza” mtoto. Kwa upande mwingine, utoaji mimba wa kuchagua, ni wakati mwanamke anachagua kutumia utaratibu ulio na madhumuni ya kuiondoa mimba.

Katika baadhi ya nchi, utoaji mimba unakuzwa kama njia halali ya kudhibiti uzazi.

Walakini, utoaji mimba hauwezi kuchukuliwa kama vile kuondoa uvimbe au saratani. Sio “tu” kuondolewa kwa “lundikizo la seli.” Ni kuyaondoa maisha ya mwanadamu, ambayo huja na athari kubwa kwa mama. Kutoa mimba sio tendo lisilo na hatari zake. Uavyaji mimba husababisha madhara ya kimwili na ya kihisia pia.

Athari za kimwili za kuavya mimba

  • Asimilia 17% ya wanawake hupata matatizo ya kimwili kama vile kutokwa na damu kusiko kwa kawaida au maambukizi ya fupanyonga baada ya kutoa mimba.
  • Wanawake ambao wametoa mimba moja makusudi wana hatari kubwa zaidi ya 36% ya kuzaa kabla ya muda wao wa ujauzito wakilinganishwa na wanawake ambao hawajawahi kutoa mimba.
  • Wanawake waliotoa mimba hapo awali wana asilimia 93% ya hatari inayoongezeka ya kuzaa kabla ya muda wa kujifungua mimba zitakazofuata

Hisia huathirika baada ya kuavya mimba

  • Asilimia 60% ya wanawake walioavya mimba hupata kiwango fulani cha mfadhaiko wa kihisia baadaye; nusu yao wameainisha kuwa ni mafadhaiko makali sana.

Jambo hili haliwatatizi wavulana. Kweli ama uongo?

  • Uongo; Japo wavulana hawapitii hali ya uchungu wa kimwili,wanapitia uchungu katika hisia na mawazo yao wakati wake zao ama wachumba wao wanapitia hilo. Na hasa kama walichangia kuafikia uamuzi wa kuavya mimba.

Uzazi

Mwanamke anapokuwa mja mzito ana uamuzi wa kuibeba mimba ile hadi atakapojifungua na kuchukua jukumu la kumlea mtoto wake peke yake, na baba wa mtoto, au kupata msaada kutoka kwa wazazi wake. Hata hivyo kuna mambo mengi ya kuzingatia wakati wa kufanya uamuzi huu, kwa mfano.

  • Ndoa: Je niko tayari kuolewa? Huyu ni mtu ambaye ningelipenda kuolewa naye, tuzeeke pamoja?
  • Mtu ambaye ni mfano bora: Je tutakuwa kielelezo kizuri kwa watoto wetu?
  • Pesa: Ni nani atakayelipia mahitaji ya mtoto? Je baba wa mtoto atatoa mchango wake? Ni nani atakaye fanya kazi? Kuna sheria katika nchi nyingi zinazomwajibisha baba wa mtoto kuchangia katika mahitaji ya mtoto.
  • Elimu/maisha: Je tutaendelea na masomo yetu na kuyamudu maisha kama tulivyo sasa?
  • Majukumu: Je sote wawili tunajitolea kubeba majukumu ya kumlea mtoto wetu?
  • Kujitoa: Je tuko tayari kuweka kando mipango yetu ili kumlea mtoto wetu.
  • Msaada wa familia; Mtandao wa kijamii: Je tunayo familia na marafiki ambao wanaweza kusaidia kumlea mtoto?
  • Muda mrefu baadaye: Je baada ya muda mrefu, watu ambao wamejitolea kutusaidia sasa watakuwa bado wapo?

Vijana wanaweza kuwa wazazi wazuri ikiwa wako tayari kuvumilia kunakohitajika ili kumlea mtoto. Wanahitaji msaada mwema na wao kuwa wamekomaa kuchukua jukumu la kuwa wazazi. Kutenga vizuri muda wa masomo, kazi, na uzazi si jambo la kuchukuliwa kuwa la mzaha! Baadhi ya vijana hawako tayari kuacha uhuru wa ujana wakati wanapopata mtoto, wanaweza kusahau majukumu yao ya kila siku. Hivyo wanaweza kushindwa kuwa wazazi wazuri wanao fahamu majukumu yao.

Kuasili

Ikiwa hauko tayari kuwa mzazi katika hatua hii ya maisha yako, unaweza kufikiria chaguo la tatu kufanya mpango wa kuasili mtoto wako.

Kumtoa mtoto wako kwa wazazi wengine kumlea haimaanishi kwamba humpendi mtoto wako au kwamba unaepuka wajibu wako. Ukweli, inamaanisha kinyume kabisa—kwamba unataka mtoto wako aende kwenye familia iliyo bora zaidi iwezekanavyo, na kwamba unataka kuwajibika kwa maisha yako wewe mwenyewe pia.

Katika baadhi ya nchi, wazazi wa kibaolojia wanaweza kuchagua familia ya kuasili kwa ajili ya mtoto wao. Katika nchi nyingine, mashirika ya kuasili watoto huwachunguza wazazi wanaoweza kuwalea kulingana na vigezo vilivyofikiriwa kwa uangalifu ambavyo ni lazima wavitimize kabla ya mtoto kuwekwa katika familia hiyo.

Hapa kuna baadhi ya maswali muhimu unayoweza kuzingatia wakati unachagua kuasili:

  • Je ni kitu gani ninachotaka kwa ajili ya maisha ya mtoto wangu?
  • Ni ni kitu gani ninachotaka kwa ajili ya maisha yangu, sasa na katika siku zijazo?
  • Je, kuna kitu chochote ambacho familia ya kumuasili inaweza kumpatia mtoto wangu ambacho mimi siwezi kumpatia sasa?

Ukizungumza na shirika la kuasili haimaanishi kuwa unafanya uamuzi usioweza kutenduliwa. Inamaanisha tu kwamba unapata taarifa inayohitajika ili ufanye uamuzi bora. Baadhi ya maswali ya kuuliza wakala wa kuasili ni:

  • Ni nani atakayechagua familia ya kuasili?
  • Ikiwa nitataka kuwasiliana na mtoto wangu baada ya kuzaliwa na baada ya kuasili, je, hilo linawezekana?
  • Ikiwa sitaki kuwasiliana baada ya kuasili, je, hilo linawezekana?
  • Je, ninaweza kupata usaidizi wa gharama za matibabu na maisha wakati ninapofanya mpango wa kumuasili mtoto?
  • Nani atalipa ada za wakili wa kuasili?
  • Je, ushauri nasaha baada ya kuasiliwa unapatikana na nani atalipia?

Iwapo huwezi kumpa mtoto wako nyumba ya wazazi wawili, hapa kuna baadhi ya mambo ambayo unapaswa kuzingatia wakati wa mchakato huu muhimu wa kufanya maamuzi:

  • Mahusiano ya mtoto, kujistahi, na mafanikio yake huathiriwa vyema anapokua katika nyumba yenye upendo ambapo wazazi wote wawili huchangia ukuaji wa mtoto.
  • Watoto katika familia zisizo na baba wana uwezekano wa kukua katika umaskini mara tano zaidi ya wale walio na baba.
  • Hali halisi ya kuwa mama asiye na mwenzi inamaanisha kwamba fursa za uchumba, ndoa, elimu ya juu na kazi nzuri na maisha ya starehe zinaweza kuwa chache zaidi.

Hivi ndivyo msichana mmoja alivyosema juu ya chaguo lake la kufanya mpango wa kuasili mtoto wake:

  • “Sikuwa tayari kuwa mzazi, kwa hiyo nilimchagulia mtoto wangu wazazi wazuri. Sikuwa tayari kumpa mtoto wangu nyumba, lakini nilifanya jambo ambalo hakuna mtu mwingine angeweza kufanya— nilimpatia uhai mtoto wangu.”

Hakuna majibu rahisi unapopata ujauzito ambao hukupangwa. Jipatie muda wa kutafakari ukweli wote na uchaguzi wote ili kufanya uamuzi bora kwa ajili yako na mtoto wako.

Activities Icons

Zoezi 4: Mtoto ambaye hajazaliwa

Blank Icons

Lengo

Kusaidia washiriki kuelewa kwamba kushughulikia mimba ya ujana kunahusisha kufanya uamuzi mzito kuhusu maisha ya mwanadamu mwingine.

Mahitaji

  • Mtoto wa plastiki na kadi inayoambatana naye
Slides Icons

Maagizo

1. Weka slaidi ya “Mtoto ambaye hajazaliwa”.

Handbook 62 Icons

2. Anza kwa kumshika mtoto kwenye ngumi iliyofungwa au kumtoa mfukoni ili kueleza jinsi fetasi ilivyo ndogo karibu wiki 14. Walakini, katika kamwili haka kadogo:

Wiki ya 3

  • Moyo unadunda

WIKI 11

  • Anapepesa macho na kumeza
  • Anaweza kukunja ngumi.
  • Anazo alama za vidole
  • Uwezo kuhisi joto, mguso, mwanga na kelele.
  • Ananyonya kidole gumba
  • Viungo vyote vwa mwili vinafanya kazi
  • Anao uzito takribani gramu 28 Anaurefu wa sentimita 6.3 - 7.6cm

3. Weka slaidi ya “Wiki ya 18” mshale kitengo ya wiki kumi na nane toa maelezo kwamba jinsia ya mtoto inaweza kutambulikana waziwazi.

4. Weka Slaidi ya “Wiki ya 22” onyesha mshale ule. Nywele zipo kichwani na mwilini na mtoto anaweza hisi maumivu. Kuanzia hatua hii hadi wiki ya 32, mtoto anahisi uchungu zaidi kuliko wakati mwingine wowote wa ukuaji wake.

5. Weka slaidi ya “Wiki ya 28”. Waambie washiriki kuwa ikiwa mtoto huyu atazaliwa basi
anaweza kuishi akitunzwa kwa uangalifu mkubwa katika kitengo cha wagonjwa mahututi.

6. Wafamishe washiriki iwapo watachagua kushiriki vitendo vya ngono mapema wanajiweka katika hatari ya kupata mimba na ni bora wafanye maamuzi yaliyo bora kutokana na hilo. ULIZA: Je mimba ni swala la msichana tu? Inaathirije wavulana? Sio swala la msichana tu! Na wavulana wanashiriki pia jukumu linaloambatana na kumleta mtoto duniani na changamoto za kihisia zinazoambatana na uamuzi mkubwa namna hiyo.

Magonjwa ya zinaa (STIs)

Hata kama hutapata mimba, wakati wowote unaposhiriki tendo la ngono unakuwa hatarini kuambukizwa magonjwa ya zinaa. Ingawa baadhi ya maradhi haya ya zinaa yanaweza yakatibiwa iwapo yatagundulika mapema ,mengine hayana tiba na yanaweza kudhibitiwa tu.

Ukweli: kuhusu magonjwa ya zinaa

  • Kuna zaidi ya visa milioni 374 vinavyoripotiwa kila mwaka duniani vinavyotokana na magonjwa ya zinaa (kisonono, kaswende, Klamedia na Trikonomi) wanaoathirika kiwango kikubwa ni watu kati ya umri wa miaka 15 na 49.
  • Kila mwaka idara inayoshughulikia HPV (human papillomavirus) huripoti visa nusu milioni 570,000 wanaoathirika na saratani ya shingo ya kizazi kote ulimwenguni
  • Duniani, madhara yanayotokana na ngono yana visa vingi na vinaathiri uchumi na afya; hasa, magonjwa ya zinaa husababisha 17% ya hasara za kiuchumi kutokana na afya mbaya.

Wanachosema vijana:

“Hilo halitanipata.”

  • Hili hutokana na mawazo yenye nguvu waliyonayo vijana wengi hivi kwamba katika matukio ambapo kuna zaidi ya asilimia 50% ya kuathirika, wanaamua kuamini tu kwamba wao na wale walio karibu nao watakuwa katika wale wachache wenye kupata bahati.

“Ninamwamini mpenzi wangu.”

Unaweza kweli? Je mmefahamiana kwa muda gani hata umwamini na maisha yako? Na unajuaje kwamba anasema kile anachojua unataka kusikia ili kusudi mshiriki ngono? Na iwapo anadai kwamba yeye angali bikira, kwamba anapendekeza kujamiiana nawe inapaswa kukufanya ujiulize kama hajawahi kumpatia mwingine ombi hilo.

Activities Icons

Zoezi 5: Mwili Wangu

Blank Icons

Lengo

Kuonyesha washiriki jinsi ukimwi unavyoathiri mwili wa mwanadamu.

Mahitaji

  • Vibandiko vyenye majina
  • Watakaojitolea sita (Ili kupata matokeo bora uliza kikundi kuchagua waigizaji wazuri)

Maagizo

1. Watu watakaojitolea sita kuigiza mchezo huo. Wape majukumu yafuatayo:

  • Mwili wangu (mrefu, mtu mwenye afya)
  • WBC -Damu iliyo na kinga dhabiti mwilini (mlinzi mwenye nguvu)
  • Virusi vya ukimwi (mbaya, mhalifu)
  • Kikohozi
  • Homa
  • Kuhara

2. Wapange waigizaji ifaavyo:

  • Tukio linaanza kwa Mwili wangu akiwa amesimama kati ya jukwaa akionekana mwenye furaha sana. Kando ya Mwili wangu, WBC anajitokeza akichupia kama mwanandondi akipigana na hewa akijaribu kuukinga Mwili wangu dhidi ya maadui wote nje ya jukwaa. Upande mwingine waaigizaji waliobakia wanasubiri ishara zao.

3. Anza kukisimulia kikundi kwa mtiririko: “Huu ni Mwili wangu. (Onyesha Mwili wangu.)

Huu ni Mwili wangu.

Mwili wangu ni imara na una afya. (Mwili wangu unaruka juu na chini ukitutumia misuli yake kuonyesha nguvu na afya yake)

Mwili wangu unalindwa na mlinzi aitwaye WBC. (Elekeza kwa WBC, ambaye anarusha ngumi chache hewani.)

Sasa, WBC haimaanishi bondia wa kimataifa bali Chembe Nyeupe za Damu. Hizi ndizo hukinga Mwili wangu ili maradhi yoyote yasiupate. Wacha tuone kinachotokea wakati kikohozi kinaposhambulia Mwili wangu. (Kikohozi kinaukaribia Mwili wangu, kikikohoa kwa nguvu na Mwili wangu unaanza kukohoa pia. Lakini kikohozi kinapokaribia Mwili wangu, WBC anakuja kati yao na kuwatenganisha.)

WBC yu tayari kupigana na kikohozi. (WBC na Kikohozi wanaanza kupigana. Mwili wangu unaendelea kukohoa.) Mara WBC anamshinda Kikohozi ambaye anarudi nyuma. (Kikohozi kinatoka kwenye jukwaa . Mwili wangu unarukaruka na kujitanua tena.) Tumpigie WBC makofi. (pigeni makofi pamoja na watazamaji. WBC anapokea shangwe zile kwa heshima na kuinama.)

Sasa Homa inamvamia Mwili wangu. (Homa, inaukaribia Mwili wangu huku ikitetemeka.) Pengine ni homa ya malaria au homa ya matumbo. (Mwili wangu unaanza kutetemeka.) Lakini WBC yuko tayari kupigana na Homa. (Kwa mara nyingine, WBC anasimama baina ya Homa na Mwili wangu na kuwatenganisha.) Kunazuka vita … (WBC na Homa wanapigana. Mwili wangu unaendelea kutetemeka. WBC anaishinda Homa. (Homa inatoka kwenye jukwaa. Mwili wangu unaacha kutetemeka.) Ni shukrani kwa WBC, kwani Homa ilibidi iondoke kwenye Mwili wangu. Mwili wangu una nguvu na afya tena. (Mwili wangu unarukaruka ukitabasamu na kujitanua.) Tumpigie WBC makofi. (pigeni makofi pamoja na watazamaji. WBC anapokea shangwe zile kwa heshima na kuinama.)

Sasa Kuhara kunakuja kushambulia Mwili wangu. (Kuhara kunaukaribia Mwili wangu huku kuhara kunjishikilia tumbo lake kukilia kwa maumivu. Mwili wangu pia unaanza kulia kwa maumivu na kuinama ukijishikilia tumbo.) Lakini kwa mara nyingine WBC yu tayari kuulinda Mwili wangu. (Kwa mara nyingine, WBC anasimama baina ya Kuhara na Mwili wangu na kuwatenganisha.) Kuna zuka vita. (WBC na Kuhara wanapigana. Mwili wangu unaendelea kujishika tumbo na kulia kwa maumivu. (WBC anamshinda Kuhara. (Kuhara kunatoweka kwenye jukwaa. Mwili wangu unaacha kujishikilia tumbo na kulia kwa maumivu.) Kwa mara nyingine WBC ameulinda Mwili wangu. Shukrani kwa WBC, kwani Mwili wangu una nguvu na afya tena. (Mwili wangu unarukaruka ukijitanua kuonyesha afya yake nzuri.) Sasa tunaona jinsi WBC alivyo muhimu kwa Mwili wangu. Tumpigie WBC makofi. (pigeni makofi pamoja na watazamaji. WBC anapokea shangwe zile kwa heshima na kuinama.)

Lakini sasa Mwili wangu umepatwa na VVU, virusi visababishavyo UKIMWI. (VVU anaanza kuunyemelea Mwili wangu.) Pengine hii ilitokea kupitia ngono na mtu mwenye virusi au kutoka kwa damu ya mwenye virusi. (VVU anatoa tabasamu kubwa. WBC anaingia kati yake na Mwili wangu. Mwili wangu unaendelea kusimama hapo kana kwamba hakuna tatizo lolote.)

Wacha tuone kitakachotokea. (WBC na VVU wanaanza kupigana. Wakati huu, VVU anaonekana ndiye mpinzani mwenye nguvu zaidi ya WBC.) VVU anapigana na WBC kwa muda mrefu na kwa nguvu zaidi kuliko magonjwa mengine yalivyofanya. (WBC na VVU wanapigana kwa muda mrefu, lakini VVU anamshinda WBC. WBC anasalimu amri.)

Haiwezekani! VVU amemwangamiza WBC? (VVU anasimama kwa ushindi na kujitanua misuli. WBC anatingisha kichwa kwa huzuni na kusimama nyuma ya Mwili wangu huku akionyesha hadhira mgongo. Mwili wangu unaendelea kuonyesha kana kwamba hakuna kasoro yoyote.)

Mwili wangu hauonyeshi dalili zozote kwa wakati huu. Mwili wangu bado unaonekana kuwa mwenye nguvu na afya. (Mwili wangu unatabasamu na kujipongeza. VVU anasimama kando yake huku naye pia akitabasamu na kujipongeza.)

Baada ya muda mfupi tutaona kitakachotokea wakati Kikohozi kinapokuja kuushambulia Mwili wangu tena. (Kikohozi kinaukaribia Mwili wangu kikikohoa kwa nguvu. Mwili wangu unaanza kukohoa kwa nguvu pia. WBC anageuka, kuwaonyesha hadhira kuwa hana uwezo na kuupa Mwili wangu mgongo wake. VVU anasimama kwa maringo kando ya Mwili wangu. Kikohozi anashikana mikono na VVU kando ya Mwili wangu na VVU. Mwili wangu unazidi kukohoa kwa nguvu.)

Sasa Homa inarudi kuushambulia Mwili wangu. (Homa inamkaribia Mwili wangu ikitetemeka. Huku Mwili wangu, ukiendelea kukohoa, unaanza kutetemeka pia. WBC anageuka kwa sikitiko kuwaonyesha hadhira kuwa hana uwezo na kisha anageuka nyuma ya Mwili wangu. Homa inashikana mikono na VVU na inasimama kando ya Kikohozi. Mwili wangu unaendelea kukohoa na kutetemeka.)

Kuhara sasa kunashambulia Mwili wangu. (Kuhara kunaukaribia Mwili wangu, kukiinama kwa maumivu. Mwili wangu ukiendelea kukohoa nakutetemeka, unaanza kulalamika na kujishikilia tumbo. WBC anageuka, anatikisa kichwa na kurudi nyuma ya Mwili wangu. Kuhara kunashikana mikono na VVU na kusimama kando ya Homa. Mwili wangu unaendelea kukohoa, kutetemeka, kulia kwa maumivu na kujishika tumbo. VVU anaikunja mikono na kutabasamu.)

Mwili wangu, sasa ni mgonjwa sana una Kikohozi, Homa na Kuhara.

WBC hawezi kuusaidia na hivyo Mwili wangu unadhoofika zaidi. Sasa umepatwa na UKIMWI. (Mwili wangu, unaendelea kukohoa na kutetemeka pamoja na kulia kwa maumivu kisha unaanguka chini.)

Hatimaye, Mwili wangu unaaga dunia. (Mwili wangu unaanguka chini kwa njia ya kutatanisha. VVU anawashika mikono ya ushindi Homa, Kikohozi na Kuhara.)”

Blank Icons

4. Waeleze dasara kuwa VVU husababisha UKIMWI na hivyo kusababisha chembe nyeupe za damu kudhoofika na kushindwa kupambana na magonjwa. Hatimaye magonjwa hayo humuua mtu asiye na kinga ya mwili.

Activities Icons

MBADALA
Zoezi 5: Mwili Wangu

Blank Icons

Lengo

Kuonyesha washiriki jinsi ukimwi unavyoathiri mwili wa mwanadamu.

Mahitaji

  • Sanduku dogo/tungi ya uwazi (inayowakilisha Mwili Wangu)
  • Mawe madogo (yanayowakilisha mafua, kikohozi, homa, kuhara)
  • Kitambaa (vipande vichache vilivyofungwa kwa mkanda wa mpira kwenye mdomo wa mtungi (inaonyesha WBC)
  • Maji (yanayowakilisha VVU)

Maagizo

1. Waeleze washiriki kwamba mtungi unawakilisha mwili wako, na tishu, kama seli zako nyeupe za damu (WBC).

2. Wakati Mafua, Kikohozi, Homa au Kuhara vinapojaribu kuingia kwenye mwili wetu (weka mawe madogo kwenye tishu),
WBC italinda mwili wetu. Ingawa sisi ni wagonjwa, tutapona na tutapona haraka.

3. Lakini VVU inapojaribu kuingia katika mwili wetu (kumwaga maji kwenye tishu), haishambuli mwili wetu mara moja, lakini inashambulia na kudhoofisha WBC yetu. Ndiyo maana mtu aliye na VVU anaweza kuonekana kuwa wa kawaida bila dalili.

4. Baada ya hayo, tunapoambukizwa na Mafua, Kikohozi, Homa au Kuhara, (weka mawe juu ya uso wa tishu zenye unyevu), zinaweza kuingia kwa urahisi katika mwili wetu kwa sababu WBC yetu imedhoofika. Wakati huu, hatuponi vizuri au haraka na hatimaye tunaweza kushindwa na magonjwa na maambukizo mabaya.

VVU hukua na kuwa UKIMWI, mfumo wa kinga ya mwili (chembe nyeupe za damu) hupoteza uwezo wake wa kupigana na magonjwa mengine na, hatimaye, magonjwa hayo mengine huua mwili usio na kinga.

Blank Icons

VIRUSI VYA UKIMWI (VVU)/UKIMWI

Pengine ugonjwa wa zinaa unaoangamiza zaidi ni VVU/UKIMWI.

Handbook Slides 63 Icons

UKIMWI ni VVU?

  • HIV VVU inamaanisha Virusi Vya Ukimwi. Mtu ambaye ameambukizwa virusi vya ukimwi hatajua hilo hadi atakapo chukua uamuzi kupimwa, kwa sababu virusi vya ukimwi hutaviona tu kwa macho. Wakati mtu anapo athirika anaweza kufikiri ni tatizo tu la kawaida. Virusi vinapoingia katika mwili wa mwanadamu vinasambaa polepole mwilini hadi anapoathirika, vikiua kinga yake mwilini na hilo husababisha anapougua kinga yake kuwa hafifu. Hakuna tiba ya ukimwi bali maisha ya mwandamu yanaweza refushwa na dawa zinazopunguza makali ya ukimwi.

UKIMWI ni nini?

  • Ukimwi Ukosefu wa Kinga Mwilini. Ukimwi si tofauti na Virusi vya Ukimwi bali ni hatua ya mwisho ya maambukizi ya ukimwi. Hatua hiyo ya mwisho ni hatari iwapo mtu atakumbwa na mafua yanaweza kugeuka haraka na kuwa pneumonia na kusababisha kifo.

VIRUSI vya UKIMWI VINASAMBAZWA VIPI? Virusi vya ukimwi vina sambazwa vinapoingia kwenye damu. Hii inaweza kutokea kupitia:

1. Majimaji ya uke ama shahawa

  • Kufanya mapenzi na mtu aliyeathirika

2. Damu

  • Kuongezewa damu kutoka kwa mtu aliyeathirika.
  • Kushiriki sindano na mtu aliyeathirika.
  • Kutoboa mwili/masikio, kujichora tattoo, tohara, taratibu za kuchanganya damu.
  • Iwapo una kidonda cha wazi na damu iingie humo ya mtu aliye na virusi vya ukimwi

3. Mama hadi mwanawe

  • Mama aliyeambukizwa anampatia mtoto mchanga wakati wa ujauzito, kujifungua na kunyonyesha

Nani yuko hatarini?

  • Mtu yeyote atakaye fanya ngono na mtu ambaye nimwathiriwa wa virusi
    Inaweza kuwa kupitia ngono ya kawaida, ya mkundu au ya mdomoni kati ya jinsia tofauti (hasa mume-na-mume). Mtu aliye athirika anasambaza virusi kupitia damu, maji ya uke ya mwanamke, shahawa ya mwanamume. Virusi huingia kwenye mfumo wa damu kwa njia ya mahali wazi ulipojikata, vidonda, utando wa mucous kama vile tishu za uke, uume, mkundu, na mdomo.
    Kumbuka kwamba inawezekana mtu aliye athirika kuwa na mwili unaonekana na afya.
  • Mtu yeyote ambaye amegusana na damu iliyoambukizwa (Kupitia vidonda wazi na kudungwa na sindano iliyotumika na mtu aliye athirika na haiajaoshwa ipasavyo
    awezajipata katika hali ya hatari).

    Mtu aliyeambukizwa akitumia sindano, damu yake inabaki ndani ya sindano. Bila kuiosha ipasavyo, ikitumiwa kwa kujichora au kutoboa masikio inaweza kuambukiza virusi.
  • Ukiongezwa damu ambayo ina virusi vya ukimwi.
    Nchi nyingi bado hazina miundombinu ya kuhakikisha damu yote inapimwa kabla ya kutumika kumwekea mgonjwa.

JE UKIMWI UNA TIBA? HAPANA!

  • Hadi kufikia sasa ukimwi hauna tiba, aliyeathirika hana budi kuishi na virusi hivyo maisha yake yote.

VVU/UKIMWI kwa Hesabu

  • Watu milioni 1.5 waliambukizwa VVU mnamo 2020
  • Watu milioni 37.7 walikuwa wanaishi na VVU mnamo 2020
  • Watu 680,000 walikufa kwa magonjwa yanayohusiana na UKIMWI mnamo 2020 Hicho ni kifo 1 kila sekunde 46. Ingawa idadi ya vifo imepungua sana kwa miaka mingi, UKIMWI bado ni janga la kimataifa. UKIMWI unaweza kuonekana kama tatizo la kitakwimu kwa baadhi yetu, lakini kama mtu anayeugua UKIMWI alikuwa mtu tunayemjua au hata kumpenda, mtazamo wetu unabadilika.
  • UKIMWI ni tatizo la kila mtu, na tunaweza kufanya kitu kuhusu hilo kama kizazi.
Activities Icons

Zoezi 6: Salama au hatari?

Blank Icons

Lengo

Kuwasaidia washiriki kuelewa jinsi virusi vya ukimwi vinavyoenezwa.

Mahitaji

  • Kitabu cha mazoezi cha mshiriki
  • slaidi iliyoandikwa “Salama au hatari?”
Slides Icons

Maagizo

1. Weka slaidi ya “Salama au hatari?” na uwaambie washiriki kufungua vitabu vyao vya mazoezi.

Handbook 64 Icons

2. Waombe washiriki kutathmini kama ni ‘hatari” au “salama’ kwenye zoezi lifuatalo (ikiwa muda hautoshi, chagua maswali machache tu)

3. Wanaweza kuonyesha chaguo lao kwa kunyoosha mikono yao ikiwa ni “Salama” na kutengeneza alama ya mkato kwa mikono yao ikiwa ni “Hatari” (kwa kipindi cha mtandaoni, wanaweza kutumia majibu ya “dole gumba” kama ni “Salama” na majibu ya “X” kama ni Hatari).

4. Kukumbatia mtu aliye na virusi

  • Salama, maana hakuna maji ya ngono au damu yanayohusika.

5. Kufanya ngono na mtu aliyeathirika.

  • Hatari, kuna mguso na unyevunyevu wakati wa kujamiiana.

6. Kula kwenye meza moja na mtu aliyeathirika.

  • Salama, maana hakuna maji ya ngono au damu yanayohusika.

7. Kulala nyumba moja na mtu aliyeathirika pasipo kujamiiana

  • Salama, maana hakuna maji ya ngono au damu yanayohusika.

7. Kushikana mikono na mtu aliyeathirika

  • Salama, maana hakuna maji ya ngono au damu yanayohusika.

8. Kulala nyumba moja na mtu aliyeathirika pasipo kujamiiana

  • Salama, maana hakuna maji ya ngono au damu yanayohusika.

9. Kumsaidia aliyeathirika kuingia ndani ya gari

  • Salama, maana hakuna maji ya ngono au damu yanayohusika.

10. Kula chakula kimoja.

  • Salama, maana hakuna maji ya ngono au damu yanayohusika.

11. Kutumia mswaki wake mtu aliayeathirika

  • Hatari, maana nyote wawili mnaweza kuwa mna tatizo na fizi zenu zinaweza kuwa zinatoka damu na damu iliyoambukizwa inaweza kupitia mswaki ikaruhusu virusi kuingia mwilini mwako. Hii ni hatari ndogo

12. Kusafisha matapishi ya mwenye virusi.

  • Hatari, iwapo kuna damu katika matapishi hayo na anaye piga deki ana sehemu ndogo mkononi iliyokatika, virusi vinaweza kuingia kwa njia hiyo. Tumia glavu wakati wote.

13. Kupigana busu na mtu aliye athirika

  • Hatari, kwa kuwa ni kawaida kuwepo kwa vidonda vidogo nje au ndani ya mdomo, na damu inaweza kuchanganya wakati wa kumbusu kwa shauku. Hatari ni ndogo, lakini magonjwa mengine ya zinaa yanaweza kuenea kwa busu la mdomoni, na kuongeza hatari ya kuambukizwa na VVU.

14. Mtu aliyeathirika anapokohoa ama kupiga chafya karibu nawe.

  • Salama, sababu hakuna damu au maji ya ngono yaliyohusika. VVU haipiti hewani.

15. Kuogelea na mtu aliye athirika salama.

  • Salama, kwa sababu hakuna maji ya ngono au damu inayohusika na hata kama muogeleaji aliyeambukizwa ana jeraha wazi, virusi havipitishwi kwenye maji au hewani.
  • Kama ni bwawa la kuogelea, beseni ya maji moto, ziwa, mto au bahari, virusi huishi kwa muda mfupi tu nje ya mwili na haviwezi kupitishwa kwenye ngozi ambayo haijakatika.

16. Kutumia wembe pamoja.

  • Hatari, damu inaweza kuwa katika wembe ule, ambayo inaweza kuchanganyika na damu yako ikiwa utajikata wakati wa kunyoa.

Hitimisha matendo salama au hatari:

Matendo ya hatari kubwa

  • Vitendo vilivyo na hatari, ni pamoja na kufanya ngono, kupiga busu la muda la mapenzi na mtu aliyeambukizwa (na mtu ambaye ana VVU, au ambaye hali yake haijulikani, kwa ngono ya mdomo au busu la mapenzi wakati kuna vidonda mdomoni)
  • Kuchubua mwili,kujichora,kutumia sindano moja na kutumia vifaa vya sindano ambavyo havijaoshwa vizuri Kuwekewa damu ambayo haijapimwa

Matendo salama

  • Tendo la ndoa baina ya mke na mume ambao walijitunza kabla ya kuoana na watasalia waaminifu katika uhusiano wao.
  • Kupeana mikono au kugusana kawaida (k.m., kukumbatiana au kumbusu kwenye shavu) na mtu aliyeambukizwa.
  • Kulisha au kutunza mtu aliayeathirika na virusi vya ukimwi (kama hakuna mguso wa damu))

VVU haisambazwi kwa njia ya:

  • Kutumia bafu moja
  • Kutumia choo kimoja
  • Kutumia simu moja/kibodi
  • Kutumia chombo cha maakuli ama kitabu kwa pamoja
  • Vifaa vya ofisini
  • Kutumia chemichemi za maji
  • Chemchemi za maji
  • Kuumwa na mdudu aliye muuma mtu aliyeathirika
  • Sisitiza kuwa hakuna jinsi unavyoweza kujua ikiwa mtu ameathirika au la isipokuwa tu kwa mtu huyo kupimwa Virusi Vya Ukimwi (VVU)..

Salama au hatari

Kamilisha “Mtihani wa Urafiki” mtandaoni kwa kiungo hiki kiungo hiki cha tathmini.

Activities Icons

Zoezi 7: Hadithi au Ukweli?

Blank Icons

Lengo

Kusaidia washiriki kuelewa ukweli kuhusu Virusi Vya Ukimwi (VVU)/Ukimwi.

Mahitaji

  • Kitabu cha mazoezi cha mshiriki
  • Kalamu ya mate/Kalamu ya wino

Maagizo

Waambie washiriki wajibu maswali yafuatayo kama ni ukweli au ni hadithi.

Handbook Slides 65 Icons

1. Kufanya ngono na bikira utapona virusi vya Ukimwi.

  • Dhana. Hakuna tiba ya ukimwi. Ukiwa na virusi vya ukimwi na kujamiiana na mtu (bikira au asiye bikira) unahatarisha maisha yake kwa kumwambukiza na virusi vya ukimwi.

2. Watu walio na virusi vya HIV wanaweza kuishi miaka mingi vila kufahamu hali zao.

  • Ukweli. Njia pekee ya kutambua hilo ni kupimwa. Watu wengi walio athirika hawafahamu hali yao. Kabla ya dalili mtu anaweza ishi miaka kumi.

3. Unaweza kuishi maisha mazuri ukiwa na HIV.

  • Ukweli. Ndio unaweza! Pasipo kupokea matibabu ipasavyo aliye na virusi hatimaye atafikia kiwango cha ukimwi. Kabla ya hapo unaweza jitolea kuwafahamisha wengine kujiepusha na ngono za mapema kabla ya ndoa na kuwa waaminifu katika jamii zao. Anayetumia dawa anaweza ishi miaka mingi na virusi vya ukimwi na kuchelewesha VVU kuwa UKIMWI kamili.

4. Virusi vya ukimwi/UKIMWI husambazwa kupitia mguso wa damu na kidonda cha mtu aliye na virusi.

  • Ukweli. Ukimwi husambazwa kupitia majimaji ya mwili, shahawa, maji ya uke, na damu wakati yanakutana na mtu asiye athirika kutoka mtu aliye athirika, kupitia ngono, mama hadi mwanawe, kupitia njia ya kunyonya, kuongezewa damu ya mtu aliye athirika na kutumia sindano ya mtu aliyeathirika).

5. Unaweza kupata virusi vya Ukimwi hata ukitumia kondomu.

  • Ukweli. Mpira wa kondomu unapunguza tu viwango vya kuambukizwa.

6. Yeyote aliye na VVU/UKIMWI alipata kuutokana na kutokuwa mwaminifu katika ndoa.

  • Dhana. Watu wengine hupata ukimwi kupitia damu ambayo haikuwa salama, kutumia sindano na wembe uliotumika na mtu aliye na virusi, mtoto kuzaliwa na mama mwenye virusi vya ukimwi, na hata kutoka kwa wenzi wao walioambukizwa.

7. Watu walio na VVU/ukimwi wanaweza ishi miaka mingi iwapo watakula vyema na kupokea matibabu.

  • Ukweli. Matibabu na kula vizuri ni njia iliyo bora kusaidia seli nyeupe za mtu aliye athirika zinazopambana na maambukizi. Hata hivyo, hakuna chanjo au tiba ya VVU/UKIMWI.

8. VVU/Ukimwi hudhofisha mwili na maradhi kama malaria, kifua kikuu na pneumonia kumkumba mtu aliye athirika.

  • Ukweli. Wakati mfumo wa kinga unapodhoofika inakuwa vigumu mwili kupigana na maradhi hata yale ya kawaida kama mafua

9. Mtu anayeonekana kama ana afya njema (hakuna dalili kudhibitisha huyu ana VVU) bado anaweza kuwaambukiza watu wengine.

  • Ukweli. Mtu aliye na virusi vya ukimwi anaweza kuwaambukiza wengine. Huwezi kujua kama mtu ana VVU kwa anavyoonekana tu.

Hadithi au Ukweli

Kamilisha “Mtihani wa Urafiki” mtandaoni kwa kiungo hiki kiungo hiki cha tathmini.

Going Deeper Icons

KWENDA NDANI
Kujadili VVU/UKIMWI

Blank Icons

Lengo

Kuwasaidia washiriki kutafakari jinsi VVU huathiri zaidi ya mtu mmoja.

Mahitaji

  • Karatasi
  • Chaki
  • Chati/Ubao
  • Kitabu cha mazoezi cha mshiriki

Maagizo

1. Kwa kutumia nchi yako au kuchagua nchi yenye kiwango cha juu cha maambukizi ya VVU, jadili: Je, itakuwa na maana gani katika nchi wakati watu wengi wataambukizwa VVU na kufa kutokana na UKIMWI?

Andika athari hizi kwenye chati /ubao mweupe. Baadhi ya athari ni kama zifuatazo:

  • Familia hutumia pesa nyingi kununua madawa, badala ya chakula jambo ambalo lina sababisha familia nzima kuteseka. (kijamii, kiuchumi)
  • Idadi ya watoto yatima huongezeka wakati wazazi wao wanapofariki kutokana na ukimwi (kijamii, kiuchumi)
  • Vijana walioathirika hawawezi kufanya kazi ama kutoa mchango wa fedha katika familia wanapoathirika (kijamii, kiuchumi).
  • Vijana wanapokufa katika umri mdogo ndoto ya taifa kuwa na viongozi wa kesho hudidimia. (kijamii, kisiasa)
  • Walioathirika watalazimika kutunza watoto wao wenyewe, ambao wanaweza kuambukizwa, pamoja na wazazi wao ambao ni wazee. (kijamii)
  • Babu na bibi wanalazimika kuwalea yatima ambao wazazi wao wamekufa kwa maradhi ya ukimwi. Mara nyingi bibi ndiye pekee aliye mtu mzima wa ukoo anayewatunza wajukuu. Katika baadhi ya nchi zilizoathirika sana, ni kawaida kumkuta bibi akiwalea zaidi ya wajukuu 20. (kijamii)
  • Serikari inabidi kuongeza fedha kwa ajili ya huduma ya afya, fedha ambazo zingeweza kutumika kuboresha jamii kwa mfano elimu na miundombinu na kadhalika (kijamii, kiuchumi, kisiasa)

2. Wape muda kama kundi au kama mtu binafsi kuandika insha fupi, shahiri, au mabango kwa mada zifuatazo:

Jadili na uwasilishe

  • Eleza ukimwi ni nini
  • Ningependa kutendewa namna gani?
  • Kwa nini vijana wako kwenye hatari kubwa ya kuambukizwa na VVU?

3. Wapatie muda wa dakika tano ili wawasilishe mawazo yao.

Slides Icons

Maelezo Ziada

Kuwahudumia walio na virusi vya ukimwi/UKIMWI.

Kwa sababu mtu ana VVU haimaanishi kwamba tumtendee tofauti na vile tungemtendea mtu ambaye hana VVU. Kwa kweli, kuwa na uangalifu zaidi kunaweza kuonekana kama kumdhihaki au kumshusha. Kwa hivyo tunawezaje kuonyesha kuwajali watu walio na VVU?

  1. Usijibadili
    Watu wanaokuzunguka wanaweza kujua unapobadilika, watu walio na virusi vya ukimwi sio tofauti, pia watu watatambua ukibadilika. Unapokuwa mwangalifu sana na unapojitahadharisha kupita kiasi hasa kana kwamba umebeba yai unaweza kuwaumiza, kwani utajenga ukuta wa kuzungumza nao. Waonyeshe kujali kama ambavyo ungewafanyia marafiki zako wengine.
  2. Usiogope kuwakaribia
    HUWEZI kupata ukimwi kupitia kuwa karibu na watu walioathirika ama kusalimiana ama kukumbatia mtu wa aina hiyo.
  3. Usiwe tatizo/sababisha hatari ya afya yao
    Iwapo hujisikii vizuri, usihatarishe afya yao kwa kusambaza magonjwa kwao. Ikitokea kwamba unakohoa ama kupiga chafya, hakikisha unafunika mdomo wako na kugeukia mbali na alipo mtu aliyeathiriwa na VVU/UKIMWI. Japo ni mambo madogo, lakini kama kinga yao imeisha dhoofika, mafua ya kawaida yanaweza kusababisha hatari ya maisha yao.

Urafiki wako na watu walioathirika sio lazima ubadilike. Mtazamo wao haubadiliki, tabia na hekima yao bado ni ile ile, ni mtu yuleyule kabla ya wao kuwa na virusi vya ukimwi. Hakuna haja ya kumwepuka au kumbagua.

Take Home Activity Icons

Zoezi la kupeleka nyumbani:
Kampeni dhidi ya ukimwi

Blank Icons

Washiriki waunde mpango wa kushughulikia janga la VVU/UKIMWI katika nchi mahususi duniani Wanaolengwa ni watu kati ya umri miaka 15 hadi 24 . Mpango ni pamoja na lengo la jinsi watakavyo endeleza kampeni hiyo na rasilimali watakayotumia kufanya hilo. Washauri kuwaza na kubuni mbinu bora.

Lengo

Kuwasaidia washiriki kufahamu ni njia gani zilizopo ambazo hupunguza hatari ya kupata mimba na maradhi yanayotokana na ngono na kuwasaidia kutambua kwamba njia pekee ya uhakika ya kuepuka matokeo haya mi mpaka bora wa kutoshiriki ngono kabla ya ndoa.

Usuli

Jinsi ilivyodhihirika katika vitengo vwa mwanzo, kujamiiana kabla ya ndoa kuna madhara mengi mengine yanaweza kuzuiliwa na mengine hayawezi. Madhara ya kihisia hayaepukiki, ya mwili baada ya tendo hilo yanaweza kuepukika, mbinu tofauti za ulinzi, hutoa viwango tofauti vya kupunguza hatari. Ni njia gani iliyo na dhamana bora zaidi? Kati ya mbinu hizo zote kutojiusisha na ngono kabla ya ndoa kunatoa ulinzi wa asilimia mia ya kinga.

Mwanafunzi bora mwenye umri wa miaka 23 alikataliwa na chuo kikuu cha hadhi kwa sababu alikuwa ameambukizwa VVU.

Baadaye alikubaliwa katika chuo kikuu kingine lakini kuna vikwazo kwa madarasa ambayo anaweza kuhudhuria. Alifanya ngono tangu akiwa na umri wa miaka 16, Timmy (si jina lake halisi) alijipatia ujuzi kuhusu “ngono salama”.

Alipogundua alikuwa ameambukizwa VVU, alimwambia daktari wake wa magonjwa ya akili, “Nilikuwa na wapenzi wachache tu wa ngono, na nilichukua tahadhari muhimu. Kwa nini mimi?”

Uliza:

  • Timmy alifanya uamuzi sahihi. . . kitu gani kilimharibikia?
  • Kuiweka imani yake katika “ulinzi” usio sahihi.
Activities Icons

Zoezi 1: Moja kati ya madhara

Blank Icons

Lengo

Kuwasaidia washiriki kuelewa tofauti kati ya kupunguza hatari na uondoaji hatari kabisa.

Mahitaji

  • Ubao mweupe/ chaki
  • Chaki

Maagizo

1. Katika eneo lingine la ubao andika kishazi.

  • “Tutawezaje kupunguza hatari ya kufanya ngono kabla ya ndoa?”
Handbook 67 Icons

2. Waombe washiriki kupendekeza njia za kupunguza hatari. Wanapopaza sauti kutoa majibu yao, yaandike ubaoni. Majibu hayo yanaweza kuonekana kama hii picha ifuatayo:

3. Ikiwa kuna vitu vyovyote vilivyokosekana kwenye orodha, vipendekeze kwa kikundi na uviongeze kwenye ubao pia.

4. Baada ya kuorodhesha njia zote zinazowezekana, eleza kwamba utakuwa ukiangalia kila moja, ili waweze kufanya uamuzi sahihi kuhusu wapi wataweka mipaka yao linapokuja suala la ngono

Instructions For The Facilitator Icons

Tanbihi: Hakikisha kuwa kutoshiriki ngono ni jambo la mwisho kujadiliwa kwenye wavuti ili uweze kusisitiza ujumbe wa kuondoa hatari ukilinganisha na kupunguza hatari kunakotolewa na njia nyingine zote za ulinzi.

Wape fursa wanaoshiriki kutoa maoni yao kwa yale ambayo tayari wanayajua .

Wezesha zoezi kwa kuuliza maswali ya kuongoza, kutoa taarifa zinazokosekana na kurekebisha dhana potofu.

Mafanikio ya zoezi hii yanategemea uwezo wa mwezeshaji kuwashirikisha washiriki bila kuwadharau au kunaswa katika kuwapatia taarifa nyingi kupita kiasi.

Handbook 67 Icons

Vipimo vya Kupunguza Hatari

MBINU YA KUJIKINGAKIWANGO CHA KUTOFAULU KUPANGA UZAZIKUJIKINGA NA MAGONJWA YA ZINAA
Vikinga Zinaa vya MdomoniHakuna kinga dhidi ya kushika mimbaHakuna kinga dhidi ya kushika mimba
Vififisha chembe-ume (manii)29%Hakuna
Kutomwaga Manii kwenye Uke27%Hakuna
Mipira ya kondomu ya wanawake21%Haijulikani
Kiwambo-uke16%Kuna idhibati ya kukinga ugonjwa
Mipira ya kondomu15%HIV ≈ 80% (ikitumiwa wakati
wote)
HPV = 70%
Kisonono ≈ 50%
Herpes ≈ 50%
Upangaji Uzazi wa Kawaida12-25%Hakuna
Tembe za baada ya ngono/ Tembe za dharura11-25%Hakuna
Tembe za kupanga uzazi8%Hakuna
Vifaa vya kizazi (IUD)<1%Hakuna
Uhasiwaji<1%Hakuna
Kutoshiriki Ngono Kabla ya Ndoa0%100%
  • Kiwango cha “kawaida” cha kutofaulu kwa watumiaji kinarejelea asilimia 85 ya wanawake wanaopata mimba bila kutarajia katika mwaka wa kwanza wa matumizi ya kawaida.
Slides Icons

Maelezo Ziada

Vikinga zinaa vya mdomoni

  • Vikinga Zinaa vya Mdomoni
    Aina hii ya kinga huwa ni mpira mgumu wenye umbo la kimstatili. Hutumiwa tu katika ngono za kutumia mdomo ambapo mpira huu hukinga ngozi za wanaofanya ngono kugusana, inawezekana kukinga magonjwa ya zinaa. Mbinu hii haikingi upataji mimba.
  • Vififisha chembe-ume (manii)
    Hizi ni kemikali zinazoua au kufifisha chembe-ume na hivyo kuzuia uwezekano wa chembe-ume hizo kufikia chembe-uke na kutunga mimba. Kufaulu kwake huwa asilimia 41%. Hata hivyo, huongeza ufaulu wa zile kinga mimba nyingine zinapotumika pamoja (k.m kondomu na kiwambo-uke). Kando na kuwa kufaulu kwake ni kwa chini mno, vifisha chembe-ume huweka wanawake katika hatari ya magonjwa ya mishipa ya mkojo. Baadhi ya wanawake pia huhisi kujikuna baada ya kutumia mbinu hii. Vijenzi vya kemikali hii ni, nonoxynol-9 (N9) ambayo imetambulikana kuumiza ngozi ya uume na kusababisha vidonda na pia inaweza kung’oa kiwambo cha uke au mkundu. Hii huongeza uwezekano wa watumiaji wake kupata magonjwa ya zinaa.
  • Kutomwaga manii kwenye uke (pia hujulikana kama kutoa uume)
    Huu ni wakati ambapo mwanamume hutoa uume wake kutoka uke na kumwaga manii nje ya uke. Hata hivyo, manii yanaweza kubakia kwenye uume Vilevile, mbinu hii inahitaji tajriba na kwamba mwanamume anafaa kuweza kukisia wakati atakapomwaga. Hali hizi huifanya mbinu hii kutotegemewa kabisa na watakao kukinga upataji wa mimba. Mbinu hii haikingi majonjwa ya zinaa.
  • Mipira ya kondomu ya wanawake
    Kondomu ya wanawake inakaribiana na kondomu ya wanaume , tofauti inavaliwa na wanawake kwa kawaida hutengenezwa kwa muundo wa plastiki, ingawa matoleo ya mpira yapo sokoni. Ina bei ghali ukilinganisha na ya wanaume na pia hazipatikani kwa urahisi. Kondomu ya wanawake inazuia mimba kwa kiwango kile kile kama za kiume ingawa chini kidogo. Kuna ushahidi mdogo kwamba inapunguza hatari ya kuambukizwa na maradhi yanayotokana na ngono.
  • Kiwambo-uke
    Kiwambo-uke ambacho huvaliwa na wanawake, hutumika kama kikinga upataji mimba. Kiwambo hicho huwekwa kwenye mlango wa uzazi ambapo kinashikiliwa na misuli ya kitengo hiyo. Ili iweze kutumika ifaavyo ni lazima mbinu hii kutumika pamoja na vififisha chembe-ume. Watumiaji wa mbinu hii wako kwenye hatari ya kupata magonjwa ya mishipa ya mkojo hasa pale kiwambo-uke hakijakaa vizuri, au dalili za mshutuko wa sumu ikiwa kitaachwa kwa zaidi ya saa 24. Imependekezwa kuwa kwa kufunika mlango wa uzazi, kiwambo-uke hutoa ulinzi fulani dhidi ya magonjwa ya zinaa.
    Hata hivyo utafiti wa kutosha na kufaa unafaa kufanywa ili kufafanua nadharia hii.
  • Mipira ya kondomu
    Mipira ya kondomu imekubalika kama njia bora ya kujikinga wakati wa kujamiiana. Zinachukuliwa kwamba ni bora katika kuzuia maradhi yanayotokana na tendo la ndoa na mimba zisizohitajika. Ni kutokana na hilo mashirika mbalimbali ambayo yanajiusisha na kampeni kuelemisha wanadamu swala la kuenea kwa magonjwa ya zinaa na masuala ya ngono ya vijana yanaendeleza matumizi ya kondomu kama njia kuu ya uzazi wa mpango na ulinzi. Serikali tofauti zimesadikishwa sana kwamba kondomu ni jibu la matatizo yanayozunguka ngono ya vijana hivi kwamba zimeruhusu utengenezaji na uuzaji wa kondomu ndogo zilizokusudiwa wavulana wa umri wa miaka.
  • Upangaji uzazi wa asili
    Upangaji uzazi wa asili (pia inajulikana kama mbinu za ufahamu wa uwezo wa kushika mimba, mbinu ya midundo).mbinu hii inatumika sana na familia tofauti katika kuwa makini wakati ambapo kipindi cha yai ya mwanamke linapokaribia siku zao za hedhi na hapo kuepuka kujamiiana. Jinsi tatu kufanya hilo: kuhesabu siku kwa kuchunguza kamasi ya kizazi, kuhesabu siku kabla na baada ya hedhi, na kupima joto la mwili wa mwanamke. Ingawa muda wa mizunguko unaweza kubadilika kidogo kutokana na sababu za kimazingira, kamasi ya seviksi na joto la mwili bado vinahusiana sana na wakati wa uzazi. Kwa matumizi kamili, mbinu za asili za kupanga uzazi zinaunganishwa nana wanaume kutumia mipira ya kondomu kuepuka mimba zisizotarajiwa.
  • Kuzuia Mimba kwa Dharura (pia inajulikana kama kidonge cha asubuhi-yabaadaye, kidonge cha baada ya ngono)
    Mbinu hii inazuia msichana kupata mimba ambaye hakutumia kinga yoyote wakati wa kujamiiana. Inaweza kutumika hadi masaa sabini na mbili baada ya kujamiiana, japo ni bora ikitumika mapema ili iweze kufanya kazi iliyokusudia chini ya masaa kumi na mbili. Vidonge hufanya kazi kwa kubadilisha homoni za mwili ili kwamba ovulation itacheleweshwa au safu ya ndani ya uterasi ibadilishwe, na hivyo kuzuia yai lolote lililorutubishwa kujipachika kwenye bitana, ambapo maisha ya mwanadamu hupotea. Vidonge haviwezi kuzuia magonjwa ya zinaa.
  • Vifaa vya Kizazi
    Vifaa vya kizazi (IUDs) ni mbinu ya kupanga uzazi itumikayo kwa muda mrefu na ambayo inaweza kurekebishwa. Matumizi yake huhusisha kuingiza kifaa chenye umbo la T kwenye kizazi hasa na mhudumu wa afya. Kifaa hiki huathiri jinsi manii yanayotembea na hivyo huyakinga dhidi ya kukutana na yai. IUD pia yaweza kutumika kwa kukifanya kizazi kutoweza kuhimili kijusi pale utungaji unapotokea, ambapo maisha ya mwanadamu hupotea.
    Baadhi ya IUDs pia hutoa homoni ambazo huongeza uwezekano wa kutopata mimba. Hata hivyo IUDs hazitumiki kukinga magonjwa ya zinaa
  • Uhasiwaji (kukata mishipa-ume au mishipa-uke)
    Uhasiwaji hutumika kukinga mimba kabisa. Katika mbinu hii mishipa-uke au mishipa-ume hukatwa au kuzibwa ili kukinga chembe-uzazi kutoka. Hata hivyo uhasiwaji hauathiri mzunguko wa mwanamke kupata hedhi. Vilevile hauzuii wanaume kumwaga wakati wa kujamiiana. Wakati mwingine, mbinu hii inaweza kusitishwa lakini kwa bei ghali mno na viwango vya chini vya kufaulu. Vilevile mbinu hii haizuii magonjwa ya zinaa
Activities Icons

Zoezi 2: Mashindano ya Kupuliza Puto

Blank Icons

Lengo

Kusaidia washiriki kuelewa kondomu hupunguza hatari lakini haiondoi hatari kabisa.

Mahitaji

  • Puto 5 (Kumbuka: moja iwe na matundu yaliyotobolewa mapema)
  • Watu 5 wa kujitolea (ikiwezekana wote wanaume)

Maagizo

1. Mpe kila mtu aliyejitolea puto, waeleze kwamba utakapo hesabu mpaka tatu, wanapaswa kupuliza puto yao haraka iwezekanavyo mpaka ifikie ukubwa wa vichwa vyao. Unaweza kutoa zawadi kwa yule atakayeijaza puto wa kwanza.

2. Puto iliyo na matundu inapaswa kushindwa kupanuka au kupasuka

3. Onyesha slaidi ya “Kondomu hutoa upunguzaji wa hatari kwa VVU kwa asilimia 80% pekee”..

4. Eleza kwamba kondomu 1 kati ya 5 haifanikiwi kwa sababu ya dosari za utengenezaji; ama inapasuka au inavuja.

5. Ongezea kwamba hata kwa matumizi kamili na sahihi kwa kila tendo la ngono, kondomu haiwezi kumlinda mtu kikamilifu dhidi ya VVU. Takwimu zinaonyesha kuwa hupunguza hatari kwa asilimia 80% tu.

Matumizi ya kondomu hayawezi kuhakikisha ulinzi wa asilimia 100% dhidi ya magonjwa yoyote ya zinaa.[97] Hata kwa “matumizi kamili,” bado kuna nafasi kwamba msichana anaweza kuwa mjamzito. Matumizi kamili yanafafanuliwa kuwa kutumiwa kila wakati (100% ya wakati) na yakiwa matumizi sahih.

Kulingana na shirika la Afya Ulimwenguni (WHO), ufanisi wa kondomu kuzuia mimba unafikia asilimi 97%, kwa matumizi thabiti na sahihi.[98] Kwa matumizi ya kawaida, hata hivyo, ufanisi wa kondomu hushuka hadi kati ya 86 hadi 90%. [99] Ili kuhitimu kama matumizi thabiti na sahihi, watumiaji wa kondomu lazima wazitumie kwa kila tendo la ngono, na kufuata maagizo yaliyotolewa kwenye kisanduku (ambacho kwa kawaida huwa na takriban hatua saba). Kwa bahati mbaya, katika kusisimka kabla ya ngono, wachache wanachukua muda ili kuhakikisha kuwa wanaitumia kondomu kwa usahihi, au kila mara.

Uliza:

  • Ikiwa vijana tayari wanashiriki ngono kwa sababu hawawezi kujizuia, itawezekanaje waweze kutumia kondomu kikamilifu na ipasavyo katika hali ya msisimko wa ngono?
  • Watu wazima wamejulikana kutotumia kondomu kwa usahihi au kila mara kama njia ya kuzuia mimba.

Je, unafikiri ni jambo la kweli au haki kutarajia vijana kutumia kondomu kikamilifu?

  • Hata kwa wale wanaotumia kondomu ipasavyo kila mara wanaposhiriki tendo la ndoa, kondomu sio hakikisho dhabiti kuepuka madhara.

Mfano mwema ni mwanamke aliyepata mimba licha ya kutumia mpira wa kondomu:

  • Mwanamke aliyehudhuria mafunzo alitoa ushuhuda jinsi mme wake alivyotumia mpira wa kondomu wakati wa kujamiana mara zote tatu na bado akapata mimba mara tatu. Walikuwa wameoana, hivyo angalau yalikuwa mazingira salama kwa watoto kuletwa katika ulimwengu huu. Lakini fikiria ingekuwa ni msichana ambaye hajaolewa.
Slides Icons

Maamuzi bora

Kuambatana na upungufu wa aina nyingine zote za kujikinga, je ni maamuzi yapi ambayo yatalinda hisia, mawazo na afya njema?

Handbook 69 Icons

Chagua moja kati ya manne:

  • 1. Utakaa tu bila kufanya lolote?
  • 2. Utajumuika na umati?
  • 3. Utaendelea/kuzidi kufanya ngono?
  • 4. Hutashiriki kabisa vitendo vya ngono?

Watu ambao hawajachagua kutoshirikii ngono hadi ndoa inabidi kuelewa kuwa uamuzi wao unawawekwa katika kitengo kimoja kati ya viwili vifuatavyo:

  • Kutofanya lolote ama kuenenda na umati na hivyo kuruhusu chochote kuwatokea bila mpango katika maisha na kwenye mahusiano yao.
  • Kuamua kuendelea kushiriki vitendo vya ngono.

Watu katika vikundi hivi viwili wapo katika hatari ya kuathirika kimwili na kisaikolojia, kwa kushiriki ngono nje ya ndoa. Madhara yanaweza kuwa kupata maradhi yanayotokana na ngono kama vile herpes, klamadia au VVU, kupata mimba ya haramu, kuavya mimba ama kuzaa, kuvunjika kwa uhusiano, na unyogovu.

Vijana wanahitaji kufahamu madhara ya tendo la ngono kabla ya ndoa yenyewe na hilo linaweza kuhatarisha maisha yao. Kwa asili ya ujana wao, vijana wengi wanaamini kwamba mimba au magonjwa ya zinaa hayawezi kuwapata wao. Wanahitaji kukumbushwa kuwa linaweza kuwakumba na kuathiri malengo na ndoto zao walizojiwekea kwa ajili ya maisha yae baadaye.

Uamuzi wako ni upi?

KUTOSHIRIKI NGONO

Kuwasaidia washiriki kufikiria kila hatua katika mchakato wa maamuzi kuhusu ngono na kuwatayarisha kupima matokeo ya kila chaguo wanalolifanya badala ya “kufurahia papo hapo” na kujutia matokeo yake ya baadaye.

Mshirikishi ahitimize somo hili kwa kusisitiza uwekaji mipaka kabla ya kushiriki ngono ili kujiepusha na majuto ya matokeo yasiyofaa

Activities Icons

SHUGHULI MUHIMU
Zoezi 3: Kufanya Maamuzi Yanayohusu Ngono

Blank Icons

Lengo

Kuwasaidia washiriki kuorodhesha faida na hasara za kushiriki ngono kabla ya ndoa.

Mahitaji

  • Ubao mweupe/chati mgeuzo
  • Chaki

Maagizo

1. Chora mchoro ufuatao kwenye ubao mweupe/chati mgeuzo

KUSHIRIKI NGONO KABLA YA NDOANDIYOHAPANA
FAIDA
HASARA

2. Wahimize washiriki kupendekeza faida na hasara za kusema NDIYO kwa kushiriki ngono kabla ya ndoa, na pia kusema HAPANA kwa kushiriki ngono kabla ya ndoa.

3. Tathmini matokeo na kikundi, ili waelewe kanuni na pia kulimiliki suala hilo..

Majibu yanayowezekana:

KUSHIRIKI NGONO KABLA YA NDOA NDIYOHAPANA
FAIDAKujisikia vizuri

Kutopoteza urafiki

Kila mtu anafanya
Kujistahi

Kutopata magonjwa ya zinaa, mimba,
wasiwasi, na majukumu yasiyo ya lazima
HASARAUwezekano wa kupata mimba

Kuambuizwa/Magonjwa ya zinaa

Kupoteza ubikira

Majuto
Kupoteza urafiki

Uwezekano wa kudhihakiwa

4. Sehemu ya tabia njema ni kufanya maamuzi mazuri, kwa hivyo wasaidie washiriki kufanya uchaguzi mzuri kwa kutathmini matokeo ya uchaguzi wao na matokeo ya muda mfupi/mrefu wa maamuzi yao.

Kutojiridhisha papo hapo na kusubiri mpaka baadaye huleta thawabu kubwa zaidi kuliko kuyafurahia maisha wakati huu huu ambako kunaweza kuwa na majuto ya kudumu maishani mwako kote.

Eleza kwamba faida za kushiriki ngono kabla ya ndoa ni za muda mfupi lakini hasara zake ni za muda mrefu; na hasara za kutoshiriki ngono mpaka wakati wa ndoa ni za muda mfupi lakini faida zake ni za muda mrefu.

Kutoshiriki ngono sio tu kusema hapana. Kwa kweli, ni kusema ndiyo kwa mambo mengine mengi. Sio kizuizi lakini ukweli ni kwamba kunaruhusu vijana kuwa na uhuru mwingi wanaoutamani. Unavuna thawabu za kujidhibiti kingono

KUSHIRIKI NGONO KABLA YA NDOANDIYOHAPANA
FAIDA

MUDA MFUPI

MUDA MREFU

HASARA

MUDA MREFU

MUDA MFUPI

Blank Icons

Hitimisho

Slides Icons

Mipaka na uchaguzi wa uhuru wa kweli na usio na majuto
Badala ya kutuwekea vizuizi, mipaka hutupatia usalama wa kuwa watu halisi na kufurahia mahusiano mazuri—na kuishi maisha ya “kutokuwa na majuto.”

Going Home Icons

Kwenda Nyumbani

Maswali ya Majadiliano ya Mzazi/Kijana kwa Kitengo cha 3

Mzazi mpendwa,

Handbook 69 Icons

Katika Sehemu ya 3 ya Hakuna Majuto, wanafunzi walijifunza kuhusu umuhimu wa kuweka mipaka inayofaa na matokeo ya kuvuka mipaka ya ngono.

Maswali:

  1. Ni nini baadhi ya mipaka muhimu tuliyo nayo kama familia ambayo inategemea maadili yetu ya familia?
  2. Je, ni tabia zipi zisizokubalika ambazo umeziona katika urafiki/ mahusiano?
  3. [Mzazi] Je, utakuwa na mipaka gani linapokuja suala la uhusiano wa kimapenzi na uchumba?
  4. Jadili sababu kwa nini magonjwa ya zinaa yameongezeka katika kipindi cha miaka 20 iliyopita.

Mada hii inawasaidia vijana kuelewa kwamba kuna changamoto katika kujenga mahusiano mema, lakini inawezekana kwa mtazamo na kanuni zenye afya, na kujifunza umuhimu na thamani ya kusubiri kushiriki ngono mpaka wakati wa ndoa.

KITENGO 4.1 Nini hiki ninachohisi?

KITENGO 4.2 Uhusiano wa mvulana-Msichana

KITENGO 4.3 Utamu wa ngono na ahadi ya ndoa

KITENGO4.4 Maelezo mapya ya Kutoshiriki kabla ya ndoa!

MODULE 4.5 Kujitolea kuwa msafi

Lengo

Kuwasaidia washiriki kubainisha kati ya hisia za watu wa jinsia tofauti na kujifunza tofauti kati ya upendo, tamaa na kuvutiwa.

Usuli

Neno upendo hutumika sana kwa ulegevu kwenye lugha ya Kiingereza, kwamba njia bora ya kufafanua upendo ni kueleza kile ambacho sio upendo. Hali ya kuwa kwenye “upendo”, ama kule kuvutiwa na mtu huenda ikawa ndio mwanzo wa uhusiano. Kuwa na hisia za mapenzi kwa mtu au kuvutiwa naye sio vibaya, ila hiyo peke yake haitatosha kuupitisha uhusiano kwenye wakati mgumu. Uaminifu na upendo wa kudumu unahitaji tabia nzuri – subira, heshima, uzingativu, ulinzi, ustawi, matumaini na uaminifu.

Wakati hisia ya kuvutiwa na mtu inapozidi kiasi, inaweza kuwa tamaa. Tamaa ni ubinafsi. Unapomtamani mtu unamchukulia mtu huyo kama chombo cha kutimizia haja zako kingono. Katika mchakato huu mzima hakuna hali ya kuzingatia maslahi ya mtu mwingine.

Activities Icons

SHUGHULI MUHIMU
Zoezi 1: Upendo ni nini?

Blank Icons

Lengo

Wasaidie washiriki kutambua dhana sahihi ya upendo.

Mahitaji

  • Ubao mweupe. Maka za rangi tofauti

Maagizo

Wahimize washiriki kuorodhesha maneno au vishazi ambavyo vimetumika kufafanua au kuelezea upendo. Wawezeshaji waandike majibu ya washiriki kwenye ubao mweupe.

  • (Zoom na washiriki waongeze majibu yao kwa kuyaandika)

Baada ya zoezi, wawezeshaji watajadili na kuamua ni majibu gani ni maelezo ya upendo, tamaa au kuvutiwa tu kulingana na ufafanuzi wao.

Handbook 71 Icons

Wawezeshaji wanaweza kuchora:

  • mraba juu ya maneno yanayoonyesha UPENDO
  • mduara juu ya maneno yanayoonyesha KUVUTIWA
  • piga msitari katikati ya maneno yanayoonyesha TAMAA

Watu ni wagumu na mahusiano yanaweza kuwa magumu. Tunapoanza kutambua na kuelewa tofauti kati ya upendo, tamaa na kuvutiwa, tunaweza kuanza kujenga msingi imara katikati ya utamaduni wa “kuunganisha” na kuendeleza mahusiano yenye maana na ya kudumu.

Activities Icons

Zoezi 2: Kitu Kidogo Kinacholeta Kichaa Kinaitwa Upendo

Blank Icons

Lengo

Wasaidie washiriki kutambua dhana sahihi ya upendo kupitia maoni ya watu wengi.

Mahitaji

  • Sehemu za video, begi la bop (roly poly)
Video Clips Icons

Maagizo

1. Cheza baadhi ya maonyesho kwenye filamu ama vipindi vya televisheni vinavyoonyesha sifa za upendo halisi.

2. Uliza:

  • Je, huu ni upendo? Kwa nini?
  • Acha washiriki waeleze dhana zao kuhusu upendo. Usijihusishe kukosoa dhana mbovu wakati huu. Huenda ukapata maneno mengi yenye “hisia”. Tambua hisia hizo..

Upendo kwa mara ya kwanza

Mnaonana kwenye chumba kilichojaa watu. Macho yenu yanakutana. Mioyo yenu inanyong’onyea. Mara moja “unafahamu”: Umempata yule uliyekuwa ukimtafuta.

Ni upendo wa “kuona kwa mara ya kwanza”… lakini kile tunachokiita “upendo wa kumwona mara ya kwanza” mara nyingi hugeuka kuwa “tamaa mara yakwanza.”

  • Ni nini tunachosema hasa?
  • Napenda sura yako/sauti yako hii mara ya kwanza.
  • Inahusu jinsi nilivyohisi wakati nilipokuona.
  • Nitafurahi ikiwa nitakufahamu zaidi..

Mimi ndiye mlengwa, jinsi ninavyohisi na kile ninachotaka.

Kwa kweli, hizi sio hisia za upendo, bali ni msingi wa KUVUTIWA. MVUTO.

Upendo ni nini?

Upendo ni…
Upendo huvumilia na hufadhili.
Upendo hauhusudu, hautakabari, haujivuni au haukosi kuwa na adabu.
Upendo unajali wengine zaidi yako hautafuti mambo yake,
Upendo hautaki kile usichokuwa nacho,
Haujilazimishi kwa watu wengine, sio kila mara “mimi kwanza”.
Upendo hauoni uchungu,
na Hauhesabu mabaya.
Haufurahii udhalimu bali
Hufurahia ukweli unaposhinda.
Upendo haufi moyo, huvumilia yote, huamini yote,
hutumaini yote, hustahimili yote, hutafuta kilicho bora,
Upendo hauangalii yaliyo nyuma, haupungui neno wakati wowote.
Upendo haushindwi kamwe.

  • Paul of Tarsus 1 Corinthians 13:4-8

Upendo ni ...

  • Kujitoa na kutokuwa na ubinafsi kwa wengine; ni kumkubali mwenzako kwa uaminifu na kumtakia mwenzako mema.

K 5 za Upendo

  1. Kujali – kuzingatia maslahi ya mtu mwingine zaidi yako .
  2. Kuwasiliana - juhudi za kimakusudi za kuunganika na kushiriki pamoja changamoto, na ndoto zenu.
  3. Kupongeza – sio kutafuta ukamilifu lakini kumkubali, kumhimiza na kumuunga mkono na kumtia moyo ukimsaidia mwingine awe mtu bora.
  4. Kujitoa – Kushikilia uhusiano wenu licha ya changamoto na hata nyakati zikiwa ngumu.
  5. Kutambua Ubingwa – Kila mara unamhimiza mtu mwingine na kuafiki uwezo/nguvu zake badala ya kumkosoa

K ya 6 – Kuamua/Kuchagua

Kinyume na imani ya mwanadamu kuwa hitaji letu la msingi ni “kuingia” kwenye mapenzi, lakini kuchagua kumpenda mwengine na kupendwa kwa dhati-licha ya kutokamilika kwa mtu. Msingi wa aina hii wa upendo sio hisia tu, bali unahitaji juhudi na nidhamu.

Blank Icons

Kielelezo: Mfuko wa Bop / Roly Poly

Mapenzi ni kama mfuko imara ambao unaweza kuendelea kusimama hata usukumwe chini kwa nguvu kiasi gani kwa sababu ya msingi wake imara, unaolinganishwa na utunzaji, kujitolea, mawasiliano n.k. [sukuma begi la bop huku na huko].

Mapenzi ni kama mfuko imara ambao unaweza kuendelea kusimama hata usukumwe chini kwa nguvu kiasi gani kwa sababu ya msingi wake imara, unaolinganishwa na utunzaji, kujitolea, mawasiliano n.k. [sukuma begi la bop huku na huko.

Going Deeper Icons

Kwenda Ndani Zaidi

Blank Icons

Wasaidie vijana kutafakari kwa undani zaidi upendo wa kweli ni nini kwa kutafakari maswali haya. Unaweza kuwezesha na kujadili maswali haya. 

  • Unafikiri inamaanisha nini kumpenda mtu kikweli?
  • Je, unamheshimu vipi mtu na jinsi gani unapokea upendo wake vizuri?
  • Je, unamjali vipi mtu mwingine bila ubinafsi?
  • Fafanua kujitoa katika uhusiano?
Activities Icons

Zoezi 3: Je, hii ni KUVUTIWA TU (MVUTO)?

Blank Icons

Lengo

Wasaidie washiriki kuelewa kuvutiwa tu au kupendezwa ni nini. [Mwezeshaji anaweza kutumia neno kuvutiwa tu au kupendezwa, kulingana na umuhimu wa kitamaduni]

Mahitaji

  • Sehemu za video, Maneno ya kwenye muziki, Mapovu
Video Clips Icons

Maagizo

1. Cheza klipu kutoka kwenye filamu za hivi majuzi au programu za televisheni zinazoonyesha vipengele vya mtu kuvutiwa au cheza video ya hivi majuzi ya muziki inayoonyesha vipengele vya kuvutiwa jumuisha maneno ya wimbo kwenye kitini au slaidi tofauti.

2. Uliza washiriki kuangalia muziki na kuchagua semi zenye maneno ya mapenzi. Watofautishe kuvutiwa (hisia) na upendo (chaguo).

Kuvutiwa ni nini?

Pia inajulikana kama kupendezwa, mara nyingi ni hisia zisizo halisi, za kupita kiasi au za msukumo wa kuvutiwa na mtu mwingine k.m, jinsi mtu anavyofanana, tabia zake pamoja na taswira yake. Kuvutiwa kunawezekana kukawa ni ishara za mwanzoni ambazo zinaweza kukua na kukomaa na hatimaye ukawa upendo uliokomaa na usio na masharti.

Blank Icons

Kielelezo: Mapovu

[Piga viputo kuelekea juu]

Angalia mapovu haya, je, si yanapendeza? Lakini je, yanadumu kwa muda mrefu? Ni nini kinachotokea ninapoyagusa? [gusa moja ya mapovu nalo litapasuka] Waeleze washiriki kwamba kuvutiwa na mtu ni kama kiputo hiki. Kunaweza kutokea haraka sana lakini hakukai muda mrefu kuvutiwa kunabadilika au kuisha kwa urahisi.

Nini kinatokea tukivutiwa na mtu?

Tunahisi hisia za ghafla mwilini

  • Hisia hizo mara nyingi ni nzito na za kupita mipaka lakini hazina msingi yaani, tunafikiri kuwa tutakuwa na furaha milele na mtu huyu, lakini hatuwezi kusema ni kwa nini.

Tunaanza kubadili tabia

  • Unajikuta ukitenda matendo mazuri [ kujifanya] mbele ya mtu uliyevutiwa naye. Hujihisi kuwa na uhalisi wako mwenyewe wakati mtu huyo akiwa karibu nawe. Ni bora kuwasiliana naye katika mazingira ya makundi, ili muweze kufahamiana vizuri kwenye hali mbalimbali.

Unaanza kuwa na picha potovu/isiyo halisi kwa mtu huyo. Unapovutiwa na mtu wa jinsia tofauti, unaanza kujenga picha na mawazo ya kuwa mtu huyo ni mkamilifu-huoni upungufu wake!

Hisia hizo zinapanda zikishuka– zinapotea haraka kama zilivyokuja

  • Kwa sababu hatuna taarifa ya kutosha kuhusu mtu huyo na tumejenga mawazoni kwamba yeye ni mkamilifu tunapogundua kuwa mtu wetu “mkamilifu” ana mapungufu, uhalisi unatufumbua macho na hisia zetu kwao zinafifia haraka.

Kufuatilia aliyekuvutia kwenye mitandao ya kijamii—kutakuumiza zaidi

  • Ingawa ni jambo la kawaida kutaka kujua na kutaka maelezo zaidi na taarifa kuhusu maisha ya aliyekuvutia, kutumia muda mwingi mtandaoni kumfuatilia huumiza amani yako na kukufanya usiwe na tija. Muda unaoutumia kumchunguza huathiri hali yako pia, haswa wakati huyo mpendwa wako akichapisha picha na mtu mwingine.
Activities Icons

Zoezi 4: Upendo ama Kuvutiwa?

Blank Icons

Lengo

Wasaidie washiriki kutofautisha kati ya upendo na kuvutiwa tu.

Mahitaji

  • Watu 12 wa kujitolea
  • Kadi 6 zenye rangi tofauti kila moja ikiwa na swali “Upendo ama Kuvutiwa”
  • Kadi 6 za majibu “Upendo” na “Kuvutiwa” zenye rangi zinazolingana na Kadi za maswali.
  • Ubao mweupe
  • Tepu nyeusi

Maagizo

1. Kwenye bodi nyeupe, chora jedwali lenye laini mbili– moja lenye neno “Upendo” na nyingine “Kuvutiwa”.

2. Wajumuishe waliojitolea 12 (wawili wawili) na uwagawie kadi sita za majibu.

3. Wambie kuwa kila swali unaloweka ubaoni, litaelezea iwapo jibu ni upendo ama kuvutiwa.

4. Waambie wabandike kadi zenye majibu kwenye safuwima inayostahili na waeleze kwanini majibu yanaangukia upendo ama kuvutiwa.

Baada ya maswali yote sita kujibiwa, hivi ndivyo jedwali lenye rangi nyeupe linafaa kufanana:

MVUTOUPENDO
Nini ambacho hunivutia kwake zaidi?Umbo la kuvutia, Kipaji/ujuziHulka/ tabia
Wengine wana maoni gani kutuhusu?Familia yangu na marafiki wa karibu hawataki uhusiano huuFamilia yangu marafki wa karibu wanaelewana naye
Mahaba yalianzaje?Haraka (siku ama wiki); yalikuwa ni “mahaba Mara tu nilipomwona”Baada ya kumfahamu kwa miezi/ miaka michache
Ninahisi vipi kumhusu?Kuvutiwa kwangu kunabadilika kulingana na mudi YanguKuvutiwa kwangu ni thabiti na kunaweza kubashiriwa
Mahaba yana athari gani kwangu?Sijihisi, wakati mwingine natenda jambo ambalo si kawaida yanguMimi nafurahia hali yangu. Mimi ni mtu bora zaidi sasa.
Mtazamo wangu kwa jumla ni upi kuhusu uhusiano?Namtarajia atoe; Ninahisi wivu harakaSote tunagawa na kutoa; nataka awe bora zaidi

Mshirikishi anaweza kubadilisha maswali yaangazie umuhimu ama mambo ambayo hutokea kwenye kijiji/jumuiya yako kila mara.

Nini ambacho hunivutia kwake zaidi?

  • Je, ni umbo lake ama mambo yanayovutia hisia zangu tano?

Wengine wana maoni gani kutuhusu?

  • Je, wengi wanakubali ama kukataa uhusiano wetu? Je, wanatulia tunapoketi nao ama wanakosa amani? Je, uhusiano unahusisha watu wengi ama wachache?

Mahaba yalianzaje?

  • Je, yalikuwa ni mapenzi kwa mara ya kwanza ama yalianza baada ya miaka mingi ya uhusiano/urafiki? Punje la mahaba linaweza likaanza kwa urahisi iwapo watu wawili watakaa pamoja na kila mara?

Ninahisi vipi kumhusu?

  • Kiwango changu cha kumtaka ni kipi. Je kinabadilikabadilika kulingana na hisia zangu (kwa sababu upendo ni zaidi ya hisia)?

Mahaba yana athari gani kwangu?

  • Je, nachanganyikiwa nikiwa pamoja naye? Je namwogopa, na je naogopa asigundue jambo linalonihusu? Ukweli na uaminifu ni muhimu kwa upendo kukua.

Mtazamo wangu kwa jumla ni upi kuhusu uhusiano?

  • Je, unahusu tu jinsi ninavyohisi ama ninavyotaka? Ama unahusu tu kugawana na kutoa? Kimsingi kuvutiwa ni ubinafsi lakini upendo ni kupeana bila masharti bila kutarajia chochote

Kimsingi, mvuto hukua haraka na mara nyingi huzingatia vitu visivyo vya kudumu kama vile sura, uwezo na hata sauti ya mtu. Hukufanya ukatenda tofauti na jinsi wewe ulivyo kwa kawaida. Lakini jinsi mvuto unavyotokea kwa haraka ndivyo unavyopotea hivyo hivyo. Athari za kuvunjika kwa mahusiano hayo ya kuvutiwa hukaa kwa muda lakini baadaye hutoweka pia.

Upendo, kwa upande mwingine huchukua muda wa kuukuza na hukuzwa ninyi wawili mkichukua muda wa kufahamiana kwa kina. Unajifurahia nakujipenda unapokuwa na mwenzako na hata kumkubali mwenzako jinsi alivyo. Iwapo mwenza ataondoka kwa sababu yoyote, uchungu utakaotokea utakuwa mchungu na utachukua muda mrefu kupona kuliko inayotokea kwenye uhusiano wa kuvutiwa tu.

Mfano halisi wa tofauti kati ya upendo na kuvutiwakulingana na swali, “Mahaba yalianzaje”:

  • Nilikuwa ninaamini kuwa “mapenzi ya siku ya kwanza” yalikuwa ni mahaba makuu. Hivyo ndivyo ningeelezea uhusiano wangu wa kwanza na mpenzi wangu wa kiume. Miezi 2 baada ya kumfahamu kupitia vipindi vya wanafunzi wapya chuoni, nilishawishika kuhusu “upendo” huu na haikunisumbua kuwa nilikuwa nawatupilia mbali marafiki zangu. Upepo wa mahaba, ungeita hivyo ukipenda – yaliisha haraka jinsi yalivyoanza, lakini kwa uchungu na hasira. Nilipotafakari niligundua kuwa ningemfahamu zaidi iwapo ningechukua muda wa kushinda naye kwa kipindi kirefu kama marafiki tu.
Activities Icons

Zoezi 5: Kufafanua TAMAA

Blank Icons

Lengo

Wasaidie washiriki kuelewa ubaya wa tamaa.

Mahitaji

  • Kitoa baruti

Kielelezo: Cheche za kumelemeta

Washa cheche za kumelemeta na uwaulize washiriki, “Nani anayetaka hizi?”

Tamaa ni kama mng’aro huu, (sisitiza kila neno) kali, inaleta shauku, ya kusisimua, ya kufurahisha, ya kuvutia, ya kustaajabisha, nzuri na ya kutamanika (isubiri iteketee). Lakini kama mng’aro huu, tamaa haidumu. Na mara inapoungua, inapoteza mvuto wake na kutupiliwa mbali.

Tamaa ya ngono inaweza ikaelezwa kuwa ni hamu kubwa sana ya msukumo wa mwili,na uchu wa kutaka kushiriki ngono. Kiasili ina ubinafsi na haizingatii hisia na maslahi ya mtu mwingine

Hatupaswi kuchanganya kuvutiwa kwa kawaida na tamaa.

Kuvutiwa kwa kawaida ni kitu cha asili. Wakati mtu mzuri anapopita na tunazingatia uzuri wake (jambo ambalo hutokea mara kwa mara), sio sawasawa na kumtamani mtu huyo.

Tamaa inahusisha uchaguzi na tendo la utashi. Kwa kiasi fulani ni uamuzi wa kukifuatilia kitu unachokitaka badala ya kukiachia kipite. Ni kujitoa kwa msukumo wa asili bila kujizuia.

Tunapoamua kujizuia na kutofuatilia huu msukumo wa ngono inaweza kuleta kukata tamaa.

Kujidhibiti

Lakini habari njema ni kwamba kujidhibiti binafsi kunawezekana. Tunaweza kujifunza kuruhusu msisimko wetu wa hisia utupite bila kukita mizizi akilini na moyoni. Ni kama methali hii iliyoshirikiswa kwa muda mrefu: Huwezi kuwazuia ndege kuruka juu ya kichwa chako, lakini unaweza kuwazuia wasijenge kiota kwenye nywele zako. Hiyo ndiyo maana ya kuishinda tamaa. Itachukua kujitolea na mapambano, nidhamu, na kukua—haya yote ni hatua za kukomaa na kuwa mtu mzima.

Kuheshimu na Kuthamini

Njia nyingine ya kushinda tamaa ni kumuona mtu huyo kuwa ni mtu wa thamani na wa kuheshimiwa. Badala ya kushawishiwa na tamaa, mtazame mtu huyo ukitabasamu kama rafiki, ugeuke na kuondoka. Jifunze kushiriki katika urafiki wenye maana na mazungumzo bora na watu wa jinsia tofauti.

Tunaweza kushinda tamaa kwa kutomtazama mtu kama kitu cha kutumika bali kumpenda kwa usahihi - wa thamani na wa kuthaminiwa.

Je, unatumika kukidhi haja za ngono za mwenzako au umenaswa katika uhusiano wa unyanyasaji?

Ikiwa ni hivyo, tafadhali wasiliana na mshauri wa shule ama mtu mzima mwaminifu akusaidie ili uondoke kwenye uhusiano huo

Ni muhimu kukiri wakati mtu amevuka mipaka yako. Uhusiano mzuri ni ule ambao msingi wake ni wa urafiki, heshima na thamani. Zungumza na sauti yako isikike.

Tazama maudhui juu ya Alama za Uhusiano Usiofaa hapa chini.

Instructions For The Facilitator Icons

Kwa Wawezeshaji:
Ukipata swali linalohusiana na unyanyasaji au ubakaji:

  • Waelekeze washiriki kwenye nambari ya simu isiyolipisha ambapo wanaweza kuzungumza bila kujulikana.
  • Wahimize washiriki kuandika masuala au matatizo yao, na kuyaweka kwenye kisanduku, ikiwa wanaogopa kuzungumza na mwalimu/mwezeshaji ana kwa ana.

Kushughulikia Ufichuzi:

Kukabiliana na madai ya unyanyasaji na ubakaji kwa kijana ina ugumu lakini ni lazima lichukuliwe kwa uzito na kushughulikiwa kwa uangalifu na haki.

MAMBO AMBAYO USIFANYE:

  • Usijaribu kukabiliana na hali hiyo wewe mwenyewe. Badala yake, rejelea suala hilo kwa msimamizi wako na mfanyakazi wa kijamii anayeshughulikia unyanyasaji.
  • Usimhoji mtoto au kijana. Badala yake, ondoa maelezo ya mtoto na nambari yake ya mawasiliano kwa rufaa.
  • Usiulize maswali ya kuongoza. Usishinikize kupata habari au mawaidha.
  • Usitoe mawaidha au kutoa maelezo mbadala.
  • Usichukue hatua yoyote ambayo inaweza kudhoofisha uchunguzi wa baadaye kama vile kumhoji mhutumiwa au wazazi/mlezi.

Ripoti madai ya unyanyasaji shuleni au kwa mfanyakazi wa kijamii aliyeteuliwa.

Wakati wa Ufichuzi:

  • Wapatie mazingira ya usalama
  • Mhakiki mtoto
  • Sikiliza na usifanye dhana
  • Uwe mwenye kuunga mkono na asiyehukumu
  • Usitoe ahadi kwa mtoto/kijana
  • Epuka kukataa
  • Usihoji.
Instructions For The Facilitator Icons

RIPOTI TUHUMA YOYOTE YA UDHALILISHAJI NA KUTELEKEZWA WATOTO.

Slides Icons

NGONO ≠ UPENDO 

Hakuna mkataba – huwezi kushiriki ngono kupata upendo, na kushiriki ngono hakumaanishi kuwa unampenda mtu huyo.

Kimsingi, kuna dhana kuwa wasichana hushiriki ngono na wanaume iliwa wapendwe. Wavulana kwa upande mwingine hukidhi hisia/upendo wa msichana ili washiriki ngono naye.

Nini hiki ninachohisi?

Huenda ikawa ni kati ya tatu tulizozitaja – upendo, kuvutiwa, ama tamaa. Kama kijana, ni asili kuwa na mvuto kwa mwenzako – sio makosa. Lakini hizo hisia hazipashwi kukuthibiti na kuamua matendo yako.

Handbook 72 Icons

Hivyo basi kua ukomae ili uweze kutenda yale ambayo yana manufaa kwako na kwa wengine.

Je Unatambua tofauti?

UPENDOINFATUATIONTAMAA
Ni...kujitoahisiahamu
Hujengeka...Baada ya mudaharaka na kutowekaharaka
Huthamini...Utu, tabiaAnavyopendeza, talantabinafsi
Msingi wake...ukweliudanganyifumsukumo
Huzingatia...“WEWE”“MIMI’“MIMI’

Lengo

Kuwawezesha washiriki kujifunza njia za kuwasiliana kiafya na watu wa jinsia tofauti bila kuingia katika hali za kutatanisha.

Usuli

Shukrani kwa mitandao ya kijamii, kutuma ujumbe mfupi na kukutana kwa kirafiki mtandaoni, teknolojia mpya imefafanua kwa upya jinsi tunavyowasiliana, ambayo ni sehemu kubwa ya uhusiano, kulingana na Kevin Carr, mwandishi mahiri, mzungumzaji na mtangazaji wa Television. https://www.youtube.com/watch?v=70HdOIiWfe4

Hamu ya matokeo ya papo hapo na kujiridhisha papo hapo haitusaidii kuungana vyema katika uhusiano wa maana. Hata kwa maendeleo ya teknolojia ya kisasa yenye chaguo na fursa zisizo na kikomo, hatuwezi kuepuka hamu yetu ya uhusiano wa kina na wa maana na ushirika.

Shinikizo Zinazowakabili Vijana

Kuwa na uhusiano na kubarizi kwa mvulana/msichana kumekuwa na umaarufu na kunakubalika miongoni mwa vijana. Kwa sababu ya hili, shinikizo ni kwa vijana kujitosa kwenye uhusiano huu wa mvulana-msichana.

Ingawa uhusiano huu unaweza kuonekana kuwa mzuri, shinikizo ambalo vijana hukabiliana nalo ikiwa ni mtu kutoka shuleni kwao, ikiwa wataachana, kulingana na marafiki waliowazunguka, inatia aibu wao kukutana na mpenzi wao wa zamani kila siku - na hii inaweza kuwa mateso kiakili na kuchosha. Hii inaweza kuwa sababu kwa nini vijana zaidi wanageukia uhusiano wa mtandaoni.

Shinikizo lingine ni kwamba ni rahisi kuingia katika hali zenye kuleta maelewano au kuwa katika “hali”.

  • Situationship ni uhusiano wa kimapenzi ambao haujafafanuliwa au haujawekwa. Inaweza kutegemea urahisi au hali ya muda mfupi.

Hali hii (wakati mwingine pia inajulikana kama “urafiki-husiano”), ambapo watu wawili ni zaidi ya marafiki. Wanaweza kuwa wanakaa muda mwingi pamoja na wanaweza hata kuwa na upendo wa kimwili lakini wanahisi kuwa hawajajitoa kama marafiki hasa. Wanaweza kuwekezwa katika uhusiano fulani wa kihisia lakini bila kujitoa. Mpangilio huu unaweza kuwa mchungu na wa utata kwa angalau mmoja wa wahusika.

Shinikizo la vijana kuunganishwa vizuri katika jambo hili la mvulana-msichana sio lazima liwe gumu. Kunaweza kuwa na mwingiliano mzuri na wa maana kati ya wavulana na wasichana bila kuingia katika hali za utata.

Going Deeper Icons

Kwenda Ndani Zaidi

Blank Icons

Kuwa katika uhusiano kumebadilika sana; itafaa kuwauliza washiriki jinsi wanavyoifafanua ili kuelewa mtazamo na mawazo yao.

Activities Icons

SHUGHULI MUHIMU
Zoezi 1: Hatua za Uhusiano

Blank Icons

Lengo

Wasaidie washiriki kuelewa hatua za uhusiano na faida za kuendelea polepole. Sio mbio, ni marathoni..

Maagizo

1. Onyesha washiriki slaidi ya “Hatua za Uhusiano”.

2. Wakusanye washiriki katika vikundi vidogo kwa ajili ya majadiliano au wahimize kutoa majibu yao kwa sauti.

3. Uliza: Ni vipengele gani muhimu unavyohitaji kwa kila hatua ya uhusiano?

4. Baada ya washiriki kujibu, wawezeshaji wanaweza kutoa mawazo yao kwa kila kategoria yenye maudhui yafuatayo..

Slides Icons

Kuanzia Urafiki Hadi Ndoa

Rejelea mahusiano yote kati ya mvulana na msichana kwenye soma la 3 – urafiki wa juu juu, urafiki wa karibu, kuvutiwa, uhusiano thabiti na kisha ndoa.

Hatua ya 1: Urafiki

  • Ili kuepuka ama kutokabiliwa na maumivu yasiyo ya lazima, tunahitaji kufahamu jinsi uhusiano unavyostawi. Mahusiano mengi huanzia urafiki – kipengele cha msingi na muhimu. Inahitaji muda na juhudi lakini manufaa yake ni kwamba unapata kujifahamu na kumjua mwenzako vizuri zaidi kwenye mchakato kutathmini.
  • Furahia urafiki badala ya kutathami iwapo mtu wa jinsia tofauti anaweza kuwa mpenzi mzuri.
Handbook 73 Icons
  • Kidokezo#1: Usione kila rafiki yeyote mwema (wa jinsia tofauti) kama unayemtarajia kuwa mpenzi.
  • Kidokezo#2: Usianze kuota kuhusu “na je ikiwa” – na je ikiwa ni mpenzi wangu? Na je ikiwa ananipenda?Vipi kama tukienda kula chakula pamoja?
  • Kidokezo #3: Mnapowasiliana mtandaoni na shughuli za ana kwa ana muwe kwenye makundi na marafiki wengine
  • Kidokezo #4: Usijifanye, unapomwandikia na mnapokuwa pamoja uhalisi wako ubakie ule ule.

Hatua ya 2: Burudani na jinsia tofauti

  • Hatua inayofuata ni wakati unapoanza burudani na mtu, pande zote mbili zinakuwa na nia ya kufahamiana zaidi. Ingawa inaweza isiwe ya kipekee, hatua hii ni ya uchunguzi inaweza kuelekea kwenye kutenga urafiki wenu ukawa wa kipekee. Mbali na mtu ambaye wanaburudika naye, watu hao huenda wakawa na marafiki wengine wa jinsia tofauti. Lakini wanapoanza kwenda nje wakiwa wawili tu, wakati unaotumiwa pamoja na marafiki wengine unaweza kupunguzwa sana.
  • Kidokezo #1: Amua kuwa hamtakuwa muda mwingi peke yenu.
  • Kidokezo #2: Endelea kubarizi kwenye makundi – Hapa ndipo mtakapoona kila mmoja wenu anavyoingiliana na kushirikiana na wengine kwenye mazingira na mipangilio tofauti. Mitazamo yenu itakuwa halisi na ya kweli.
  • Kidokezo #3: Msigusane! – Muwe wazi kuhusu mipaka yenu - Wakati mwingine urafiki hauko tayari kwenda kwenye hatua ifuatayo, lakini kwa sababu marafiki tayari wameanza kushikana mikono, na wanaweza kuwa wameendelea kubusiana, wanawajibika “kurasimisha” uhusiano.

Hatua ya 3: uhusiano thabiti/uchumba

  • Uhusiano unapokua, inajenga uthabiti mnapofahamiana, mnaanza pia kuwa na matarajio – matarajio ambayo mtakingana na kulinda uhusiano wenu. Hapa ndipo pia mnapojitolea kuchunguza uwezekano wa kuishi maisha ya baadaye pamoja – kwenye ndoa.
  • Kidokezo #1: muwe na mtu mzima/ wanandoa ambao mnaweza kushiriki nao changamoto za uhusiano huu.
  • Kidokezo #2: endelea kubarizi makundini licha ya kuwa muda wa peke yenu utaongezeka – dumisha mahusiano ya mara kwa mara na marafiki wa karibu na muwahusishe kwenye “ulimwengu wenu”.
  • Kidokezo#3: dumisha mipaka halisi ya kimwili– kwa kweli, tendo la ngono huwa bora kwenye mazingira ya ndoa. Usijaribu kufahamu kina cha mto kwa kuingiza mguu wako na udhanie kuwa utasalia kuwa bikira. Hivyo basi jambo la busara na heshima kufanya ni kuendelea kujenga uhusiano, kuwasiliana na kuwa waaminifu. (Rejelea K 5 za upendo)

Hatua ya 4: Ndoa

  • Kilele cha matarajio ya mchakato huu mzima ni ndoa na ndoa ni ya maisha. Kuwa kwenye ndoa ni uamuzi wala sio hisia; sio tu kemia.
  • Kumbuka: Ni hatua ya kupitiwa polepole, na sio mbio!!

Mfano halisi wa kuendelea kutoka urafiki kufikia ndoa:

  • Nilimfahamu mke wangu kwa miaka 10, tangu tulipokuwa shuleni, kabla hatujafunga ndoa. Tulijua kwamba itakuwa vigumu kwetu kusubiri hadi tuwe watu wazima waliokomaa na wanaojitegemea, kwa hiyo tuliwaomba wazazi wetu watuwajibishe baada ya kuhudhuria warsha wa uhusiano. Kututia moyo kwao kulitusaidia sana kuwa na subira na kutoruhusu homoni zetu na tamaa zetu za ujana zitushinde.
Extra Content Icons

Maelezo Ziada

Blank Icons

Hatari ya Kuendelea na Mahusiano Bila Kufanya Uamuzi Wowote Badala ya Kuamua Kuoana

Kulingana na Scott Stanley, Ph.D. na Galena Rhoades, Ph.D. katika ripoti iliyoitwa “Kabla Sijaamua Kuoana” iliyofadhiliwa na Mradi wa Kitaifa wa Ndoa katika Chuo Kikuu cha Virginia, kizazi kimoja au viwili vilivyopita, watu waliunda uhusiano na kufanya ahadi tofauti na wanavyofanya leo. Wakati huo, wapenzi walikusudia na kuamua kufunga ndoa, kuishi pamoja, na kuzaa watoto.

Leo, kulingana na Stanley na Rhoades, ndoa inafikiriwa mwishoni. Takriban asilimia 90 ya wapenzi hushiriki ngono kabla ya ndoa, kulingana na utafiti mmoja, na takriban watoto wanne kati ya kumi huzaliwa na wazazi ambao hawajafunga ndoa. Wapenzi wengi huishi pamoja kabla ya kufunga ndoa.

Baada ya kuchunguza zaidi ya wapenzi elfu moja Waamerika, Stanley na Rhoades walifikia mkataa muhimu:

Wapenzi wengine huendelea na mahusiano bila kufanya maamuzi maalum yoyote, wakati wapenzi wengine hufanya maamuzi kwa makusudi kupitia hatua mbalimbali za mahusiano. Wanandoa katika kategoria ya mwisho wanafanikiwa zaidi katika mahusiano yao.

Wasiofanya maamuzi maalumu yoyote, mmoja au wote wawili wanajikuta wanakubali kuoana kwa sababu inaonekana kama hatua inayofuata “ya kimantiki”.

Kujitoa ni muhimu

Kujitoa ni muhimu. Kulingana na Dk. John Gottman: Ni kuhusu kuonyesha kupitia maneno na matendo yako kwamba uko katika uhusiano kwa hali zote kwa mema na mabaya, na kwamba mnaweza kutegemeana.

Kama Mtaalamu aliyeidhinishwa Gottman Zach Brittle anavyosema, “Kujitoa ni juu ya chaguo. Na sio tu kuchagua mwenzi wako, bali pia ni kuchagua uhusiano siku baada ya siku.

Bila kujitoa, wapenzi huanza kukuza chuki kwa kile wanachofikiri kinakosekana katika uhusiano wao badala ya kuwa na shukrani kwa kile walicho nacho.

Ikiwa una wasiwasi kuwa unaweza kuingia kwenye ndoa bila kuamua, hapa kuna maswali matano ya kujadili na mwenzako kuhusu nia ya uhusiano wenu.

  1. Kwa nini tunataka kufunga ndoa?
  2. Tutafanya nini ikiwa ndoa yetu itayumba?
  3. Tunaweza kufanya nini ili kupata uwazi zaidi kuhusu wakati wetu ujao pamoja?
  4. Tuna maoni gani kuhusu ndoa kulingana na familia zetu za asili?
  5. Je, ni maadili gani ya msingi tunayoshiriki kuhusu kuwa na watoto, dini, fedha, maadili ya kazi na falsafa za jumla kuhusu maisha?
    https://www.gottman.com/blog/the-dangers-of-sliding-instead-of-deciding-to-get-married/

Kuishi pamoja ni wazo baya kwa sababu huondoa msingi inayojenga uhusiano imara, ndoa na familia.

KUJITOA !

[Angalia maudhui zaidi juu ya Kuishi Pamoja hapa chini]

Kuburudika na mtu wa jinsia tofauti au Hapana

Kuburudika na mtu wa jinsia tofauti ni nini?

Ufafanuzi mpana, ni wakati watu wawili wa jinsia tofauti wanafurahia shughuli za jumuiya, kwa mfano, kutazama filamu, kwenda ufukweni, n.k. Kwa ufafanuzi wake haimaanishi uhusiano “mzito”. Vijana wengi wanatafuta mtu ambaye anawapenda jinsi walivyo, mtu ambaye wanaweza kushiriki naye mawazo na hisia zao.

Sio burudani na mtu wa jinsia tofauti zote ni za mahaba, lakini zinaweza kusababisha mapenzi. Kwa kweli, burudani nyingi huanza bila mahaba, lakini uhusiano unapoendelea, zinakuwa za kimapenzi. Sio lazima tayari kuwa katika uhusiano thabiti ili kuwa na burudani.

Burudani thabiti huleta matarajio. Ikiwa mnakutana mara kwa mara, k.m., kila Alhamisi jioni baada ya darasa ili mpate chakula cha jioni na kuzungumza kuhusu maisha, inajenga matarajio ya kukutana kila Alhamisi. Ukiamua kwa ghafla kufanya mipango mingine siku ya Alhamisi, utamwacha mwenzako akijiuliza, Je! nilifanya jambo baya?

Burudani pamoja inaweza kuwa na afya ikiwa tutajifunza jinsi ya kuweka mipaka iliyo wazi (ya kimwili na ya kihisia). Tatizo huanza wakati vijana wanaingia katika eneo lisilo na mwelekeo (kimwili na kihisia) na hali ya uhusiano inaanza kuwachanganyikia. Mara nyingi hutokea wakati vitendo na tabia zinatangulia kabla ya kujitoa kwa kila mmoja.

Kwa mfano, marafiki wa karibu wanaoanza kushikana mikono au kukaribiana kimwili, mmoja anaweza kutoka burudani akifikiri kuna mengi zaidi kwenye urafiki huu huku mwingine akiwa amependa tu hisia za “ukaribu.” Matokeo yake mara nyingi ni mmoja au pande zote mbili kuumia.

Burudani na jinsia tofauti haitakuletea ukamilifu. Ni vyema kutoshiriki burudani na mtu wa jinsia tofauti ukiwa shule ya secondari au chuo kikuu na kufurahia kuwa na marafiki na wewe kuwa rafiki mzuri. Hakuna njia ya uchawi ya kuchumbiana. Kutokengeushwa wakati wa ujana wako kunaweza kukusaidia kuepuka maumivu ya moyo ya uhusiano wa kimapenzi, ambayo kwa umri huo mara nyingi hayaendi popote na hayafiki mbali.

Dhibiti teknolojia yako. Mitandao ya kijamii, kutuma SMS na simu yako mahiri hurahisisha maisha na mawasiliano ya papo hapo kupatikana kwa urahisi lakini haiwezi kuchukua nafasi ya muunganisho na uhusiano wa maisha halisi. Ni jukumu letu kutumia zana hizi za ajabu za kiteknolojia kwa busara ili kuimarisha na kujenga uhusiano wetu kupitia njia tofauti za mawasiliano.

Ni jambo la kawaida kudhania kuwa mazungumzo ya mtandaoni yanavutia zaidi kuliko maingiliano ya ana kwa ana, lakini hakuna kibadala cha kutumia muda halisi pamoja. Pata usawa mzuri wa wakati kati ya maisha ya mtandao na halisi.

Lengo la kuburudika na mtu wa jinsia tofauti

Waombe washiriki kuangazia madhumuni ya burudani baina ya jinsia tofauti kabla ya kufichua majibu hapa chini:

  • kujifahamu na kumfahamu mwenzako na wengine vizuri
  • kujenga mbinu za mawasiliano na kuwa na marafiki
  • kujenga mbinu za kijamii– jinsi ya kumshughulikia mtu wa jinsia tofauti
  • kumtafuta mwenzi wa ndoa

Mambo 10 ambayo ungependa kujua kuhusu burudani na mtu wa jinsia tofauti

  1. Jinsi unavyoburudika kutaelekeza maisha ya ndoa yako.
  2. Unaweza kuwa na burudani na watu kadhaa kabla ya kufunga ndoa.
  3. Maadili na imani yako vina athari kubwa kwa mahusiano yako ya burudani na jinsia tofauti.
  4. Usiigize ndoa hadi uoe/kuolewa.
  5. Jinsi unavyobeba mizigo mingi kwenye uhusiano, ndivyo utakavyobeba mizigo hiyo baada ya uhusiano kuvunjika.
  6. Familia yako na rafiki wa karibu wanaweza kujua ikiwa wewe na huyo mwenzako mnafaana.
  7. Usiende burudani na mtu ambaye huwezi kumuoa.
  8. Mtu mwema akiwa mahala pabaya, matokeo yake yatakuwa mabaya.
  9. Sio vyema kuwa na uhusiano na mtu wa jinsia tofauti hadi ukomae na u tayari kuoa ama kuolewa (weka umri unaoonekana unafaa katika utamaduni wako).
  10. Burudani na jinsia tofauti haipaswi kamwe kumaanisha kwamba mtu “anadaiwa” ngono na mtu mwingine kwa sababu walibarizi pamoja, walitumia pesa na kuwa na wakati mzuri.

    Kwa njia sawa na kwamba magari hayaui watu, madereva walevi hufanya hivyo, uchumba hauumizi watu, lakini uchumba kwa njia zisizo za udhibiti hufanya hivyo. . . . Kujifunza jinsi ya kupenda, kuwa mwaminifu na kuwajibika, kuwatendea wengine jinsi ungetaka kutendewa, kusitawisha kujidhibiti, na kujenga maisha yenye kuridhisha kutahakikisha burudani na jinsia tofauti iliyo bora.
    – Dakt. Henry Cloud na John Townsend, Mipaka katika burudani na jinsia tofauti:

Kuchagua kwa hekima “wakati gani” na “ni nani” kwenda burudani naye kunaweza kumaanisha kwamba utalazimika kukataa baadhi ya mialiko. Kukataliwa kunaweza kuwa kuchungu sana ikiwa hakukufanyika vizuri. Wakati mvulana anapomuomba msichana kwenda burudani naye (au msichana kumuomba mvulana), yeye sio tu kumwomba atoke naye; pia anamjulisha kuwa anampenda. Anauweka wazi moyo wake. Ikiwa msichana atakataa tu na kuondoka bila kusema chochote, anabaki na swali la “kwa nini?” Bila kupewa sababu inayofaa, anaweza kufikiria, bila shaka mimi si mzuri wa uso ya kutosha, sina haiba ya kutosha, au sikumuomba kwa usahihi. Kwa maneno mengine, anafikiria amekataliwa kwa sababu ya jinsi alivyo, wakati inaweza kuwa ni kwa sababu msichana hayuko tayari kuwa kwenye uhusiano. Je tunawezaje kusema hapana tunapoombwa kwenda burudani bila kumuumiza mtu?

Kumkatalia mtu kwenda burudani bila kumvunja moyo

Waombe washiriki watoe mapendekezo ya kukataa mwaliko wa kwenda burudani bila kumuumiza mtu moyo.

  • Uwe na adabu
  • Toa sababu ya kweli - Kwa mfano, “Kwa kawaida siendi burudani na jinsia tofauti” au “Sioni uhuru kwenda na wewe kwa sababu sijakufahamu kwa muda mrefu.”
  • Pendekeza njia mbadala - Inaweza kumaanisha kuwaomba marafiki wengine mwende pamoja.
  • Usijisifu - Usianze kuwaambia wengine jinsi ulivyomkatalia mtu mwingine au kumfanyia mzaha.

Jinsi ya Kukabili kukataliwa – kuuguza moyo uliovunjika

Mahusiano ya zamani – Namna ya kukabili matengano?

  • Onyesha hisia zako – Tambua uchungu unaosababishwa na kuvunjika kwa uhusiano bila kujali ni nani aliyeanzisha. Zungumza na marafiki ama jamaa zako ambao wanaweza kukusikia na hata kukufariji.
  • Usijihurumie– Usigeukie nyimbo na filamu za majonzi na masikitiko. Unaweza ukapata nafuu kwa muda lakini zinaathiri uwezo wa kujenga mahusiano ya baadaye. Kuwa na matumaini.
  • Kubali sababu ulizopewa - Hakuna maelezo ya kuridhisha kueleza kwa nini umekataliwa. Hakuna mantiki inayoweza kuondoa maumivu unayohisi. Kwa hivyo usitafute moja.
  • Usimgeuze mpenzi wako wa zamani kuwa adui yako – wakati mwingine tunaposhindwa kuthibiti maumivu tunakuwa na uchungu kwa waliokuwa wapenzi wetu. Hatua hii inaongeza tu muda wa maumivu na hutapenda jinsi ulivyobadilika na kuwa mtu mwenye kinyongo.
  • Amua kusamehe –Kadiri unavyotamani kwamba mpenzi wako wa zamani ahisi uchungu kama wewe unavyohisi, fahamu kuwa kutosamehe kunakuumiza zaidi kuliko yule mwengine. Kuamua kusonga mbele na maisha kwa neema kunajenga tabia nzuri na ukomavu.
  • Tafuta shughuli mbadala – chagua zoezi jipya kujaza nafasi ya muda uliokuwa ukishinda na mpenzi wako wa zamani kama vile kubarizi na marafiki, kucheza mpira wa timu n.k
  • Epuka kuvizia - Usimvizie mpenzi wako wa zamani kwenye mitandao ya kijamii. Itaongeza maumivu.
  • Hili litapita – Ingawaje kutengana kunaumiza sana, jikumbushe kuwa sio mwisho wa ulimwengu - yatapita. Kubali kwamba unaumia na ingawa ni vigumu kuamini lakini utapona tu

Ikiwa unamjua mtu aliyevunjika moyo, uwe na huruma, kwa sababu msaada wa kijamii umeonekana kuwa muhimu katika kupona. Na uwe na subira, kwa sababu itachukua muda mrefu zaidi kwa rafiki yako kupona na kuendelea na maisha kuliko vile unavyofikiria.

Bendera Nyekundu katika Uhusiano

Slides Icons

Katika uhusiano wowote, kuna baadhi ya tabia mbaya, ambazo zinaweza kutatuliwa, lakini ikiwa zinaanza kuunda muundo usio bora, hupaswi kuishi na hasi.

Handbook 76 Icons

Binafsi: Tabia hizi za uharibifu huleta tu madhara kwako kwa muda mrefu, kwa mfano.:

  • 🚩 Anakataa kukubali makosa (au kuomba msamaha mara kwa mara kwa kosa hilohilo lakini habadiliki)
  • Mwenye jeuri au kiburi
  • Si mwaminifu (kusema uongo chini ya “hali maalum”)
  • Tabia ya uraibu (k.m., kuvuta sigara, kucheza kamari, kunywa pombe, kucheza michezo kupita kiasi, n.k.)

Mtu binafsi: Wakati mwingine sifa za uharibifu hujitokeza wakati mtu anapohusiana na wengine, kama vile:

  • 🚩 Ubinafsi au kudhibiti (kujijali tu, na kutoheshimu mipaka, ghiliba)
  • Kulaani (kukosoa kupita kiasi)
  • Kusengenya sana
  • 🚩 Huelekea kukasirika kupita kiasi au wivu (kukasirika kwa urahisi au kutilia mashaka sana)

Hizi zote ni bendera nyekundu ambazo unapaswa kuzitilia maanani.

Slides Icons

Kimsingi, chagua mtu anayekuheshimu na kukupenda! Chagua mtu asiyepuuza maoni yako, asiyekugandamiza mbele ya wegine, asiyepuuza hisia zako, au kukushinikiza kufanya kitu ambacho hutaki kufanya (pamoja na kushiriki ngono).

Lengo

Kusaidia washiriki kuelewa utamu wa ngono na wakati mwema wa kushiriki ngono ni kwenye ndoa.

Usuli

Vyombo vya habari vinaweza kutuambia kuwa ngono ya mapema ni sehemu ya asili ya kujitosa kwenye mapenzi; thamani ya ubikira na usafi vinaonekana kama utamaduni wa zamani na umepitwa na wakati. Lakini tunaona ngono ya mapema inawaacha wakiwa wapweke wakikata tamaa ya kupata upendo wa kweli. Ukweli ni kuwa burudani ya jinsia tofauti huridhisha wakati ambapo hakuna ushirikiano wa ngono maana kunakuwa hakuna matatizo ya kihisia yanayotokana na kushiriki ngono kabla ya ndoa.

Je Ngono ni nzuri?

Waeleze washiriki kuwa ujinsia wetu ni kama gundi (shughuli ya awali katika Sura ya 3: Karatasi ya Rangi).

Handbook Slides 77 Icons
  • Ngono ni nzuri
  • Ngono ni tamu
  • Ngono inaibua ukaribu
  • Ngono ina nguvu
  • Ngono huunganisha watu wawili pamoja.

...katika ndoa.

Ngono inakusudiwa kuwaunganisha watu pamoja. Hatuwezi kuchagua ikiwa kila tendo la ngono litawaunganisha washirika. Tendo la ngono haliwezi kuondolewa kutoka kwenye madhumuni yake ya kuunganisha. Kutumia kipande cha mkanda wa gundi ambacho kilishatumika, kunasababisha kupoteza kunata kwake. Kwa njia hiyo hiyo, ngono kabla ya ndoa hutufanya tupoteze uwezo wetu wa kuunganishwa siku zijazo.

Wapenzi wanaosubiri kushiriki ngono hadi ndoa wanafurahia:

  • Uhusiano thabiti zaidi na wa kuridhisha
  • Ubora wa tendo la ngono
  • Mawasiliano bora na wenzi wao.

Tamaa ya ngono

Slides Icons

Waulize washiriki kama moto ni mzuri au mbaya [wengi watajibu kuwa ni mzuri na pia ni mbaya]

Moto unaweza kuwa jambo zuri sana kwa sababu unaweza kututia moto au kupika chakula kitamu kwa ajili yetu. Lakini pia unaweza kuwa jambo baya sana. Unaweza kuchoma na kuharibu nyumba na misitu ikiwa hauko ndani ya mipaka iliyo salama.

Moto katika shimo la kuchoma nyama/mekoni (mipaka) ni mwema—lakini unapoutoa nje ya mahali pake, unaweza kutudhuru.

Tamaa ya ngono ni kama moto. . . ambayo inaweza kuwaka vizuri mekoni pake ambako ni kwenye ndoa.

Thawabu za kujithibiti kingono

Handbook Slides 78 Icons
  • Huru kutokuwa na madhara ya kihisia ya ngono nje ya ndoa.
  • Huru kutokuwa na magonjwa ya zinaa.
  • Huru kutokuwa na mimba na matatizo ya kimwili na kihisia yanayotokana na uvyaaji mimba .
  • Huru kuendeleza mipango yangu.
  • Huru kuhusiana kwa jinsi nilivyo na wala si kwa sababu ya ngono.
  • Huru kushiriki uhusiano wa halisi na ukaribu na atakayekuwa mwenzi wangu wa maisha.
  • Huru ku jiheshimu na kuwaheshimu wengine.
  • Huru kuwa kijana bila bughudha.
  • Huru kuwa wewe halisi.

Neno la maana hapa ni nini ? UHURU!

Ni kuhusu kusema “NDIO!” Kwa uhuru! [wakumbushe washiriki Kitengo cha 3 Faneli ya Maisha]

Sote tunapenda wazo la kuwa huru, haswa vijana. Kutoshiriki ngono kunaruhusu vijana uhuru wa kukua na kufarahia mahusiano, bila kuwa na wasiwasi wa kukabiliwa na athari za ngono kabla ya ndoa.

Kwa nini Usubiri?

"Unapompenda mtu, utamfanyia yaliyo mema pekee,”

– Tim Stafford

Iwapo ni upendo wa kweli, utasubiri mtu sahii na wakati ufaao.

Nitajuaje iwapo yeye ndiye sahihi?

Unajua ikiwa wewe na yule unayempenda mmesimama mbele ya marafiki na familia na kuahidi kuoana na kuishi kwenye ndoa siku zote za maisha yenu.

Anayefaa kwa ngono ni yule utakayemuoa.

Nitajuaje kuwa wakati unafaa?

Kuna wakati mwema unaokwenda sambamba na moyo, akili na mwili wakati unaposema “Nakubali”siku yako ya ndoa Wakati ufaao wa ngono na mahaba ni siku ya ndoa.

Ngono imelengewa ndoa.

Inaweza tu kutendwa na mtu mmoja ambaye ameahidi kujitoa kwako maisha yako yote.

Kusubiri ni ishara ya upendo wa kweli na uvumilivu. Mtu yeyote anaweza kusema. Ninakupenda,” lakini sio kila mtu anaweza kusubiri na kuthibitisha kuwa ni kweli.

Activities Icons

SHUGHULI MUHIMU
Zoezi 1: Mtihani wa Ndoa

Blank Icons

Lengo

Kutambulisha kwa washiriki dhana sawa ya ndoa.

Mahitaji

  • Slaidi ya “Maswali ya ndoa”
  • Kadi za ukubwa wa A6 za rangi ya kijani na manjano (kila mshiriki awe na kadi moja ya kijani na moja ya njano) au unaweza kuwaomba washiriki wanyooshe mikono juu kama ni “Kweli” na watengeneze alama ya msalaba kwa mikono yao kama “Sio kweli”. Kwa vipindi vya mtandaoni, tumia emoji za majibu

Maagizo

1. Wambie washiriki kuwa unaposoma taarifa kuhusu ndoa, fikiri kuhusu zile ambazo ni za kweli ama za uongo?

Handbook Slides 79 Icons

2. Kwa kila taarifa, washiriki wainue kadi za kijani iwapo wanafikiri kuwa taarifa ni ya kweli na kadi ya njano ikiwa ni uongo.

  • 1. Kumpata mwenzi wa maisha kutanikamilisha.
    Uongo. Wewe umekamilika bila mwenzi. Una uwezo wa kutambua wewe ni nani na kuendeleza maisha yako. Ama kwa kweli unapojitambua una uwezo wa kujenga mahusiano thabiti. Kadiri ya jinsi mtu anavyoendeleza maisha yake binafsi ndivyo anavyoleta heshima, uhuru na furaha katika uhusiano.
  • 2. Watu wanaopendana sana hawatakuwa na ugomvi/migogoro/kutokubaliana.
    Uongo. Kila mtu ni wa kipekee na kila mara kutakuwa na tofauti zitakazosababisha migogoro. Lakini watu wawili wanaopendana na wamejitoa kwa mwenzao, watasuluhisha tofauti zao badala ya kuziepuka.
  • 3. Ni muhimu kuoana na mtu ambaye ana imani kama ya kwako.
    Kweli. Imani yako itachangia kufanya uamuzi utakaochukua. Kuoana na mtu mwenye imani sawa kutakufanya wewe na mwenzako kuwa katika kiwango kimoja cha msingi, na kuruhusu uhusiano wenu kupiga hatua.
  • 4. Kama hatuelewani ni vyema tupeane talaka badala ya kuishi maisha ya usumbufu kila siku..
    Uongo. Ni jambo la kunufaisha kutatua mizozo yenu badala ya kuvunja uhusiano wenu kwa ajili ya tofauti zenu. Watu wanaoshikilia uhusiano wao huona matokeo ya uhusiano kuimarika. Talaka ina athari hasi za muda mrefu hasa kwa watoto.
Blank Icons

Kiapo cha Ndoa kina maana gani?

Ndoa ni kitu cha kudumu, ngono hufanyika kati ya mume na mke ambao wamejitoa na kila mmoja wao anamjali mwenzake.

Katika ndoa tunachagua :

kupenda bila kujali…

  • Kitakachotokea
  • Ninavyohisi
  • Yeyote nitakayekutana naye
  • Ninapokuwa na matatizo
  • Hisia nilizonazo haijalishi kama ninahisi kupenda ama hapana

Upendo ni uamuzi. Ndoa ni ahadi.

  • Uamuzi wa kila siku wa kujitoa kwa wenzi wetu ndio hufanya tofauti na mahusiano mengine.
  • Tunaishi kwenye jamii potovu ambayo inashikilia dhana ya “kununua na kutupa”. Lakini dhana hiyo imeanza kuingia na kuathiri jinsi tunavyowaona watu – kama vile tunavyotumia vifaa vyetu– “kuvitupa” wakati havifikii matarajio yetu au “kuboresha” muundo tofauti ukionekana kuwa bora zaidi.
  • Kwenye sherehe ya ndoa, bwana na bibi harusi huahidi kusalia pamoja kwa vyovyote vile viwavyo, hadi “kifo kiwatenganishe”. Kujitoa huku kunatoa hakikisho la hisia na uhuru wa mume na mke kugunduana ama kutambuana kila siku, mwaka baada ya mwingine. Ni katika mazingira kama hayo ambao mahitaji ya kingono yanaweza kutimizwa katika utimilifu wa kweli, bila uwoga ama hatia kwa sababu wanajua kuwa mwenzangu yuko hapa wakati wote.
  • Watu wengine husema, “Kwa kuishi pamoja, tunaweza kuona jinsi tutakavyoelewana tutakapofunga ndoa,” au “Tutafunga ndoa hatimaye, kuna tofauti gani?”
  • Hali zinazosababisha vijana kuishi pamoja zinaweza kujumuisha kugawana kodi ya malazi wanapokuwa chuo kikuu ili kuokoa pesa za kodi. Kimsingi, kuishi pamoja ni jaribio la ndoa kama vile gari la majaribio. Gari halina hisia za kuumizwa ikiwa dereva atalirudisha kwa muuzaji na kuamua kutolinunua baada yakuliendesha kwa majaribio. Hili hapa ni tatizo la “kujaribia kumwendesha “ mtu mwingine: Ni vizuri ikiwa wewe ni dereva, inaumiza sana wakati wewe ndiye gari.

Pia kuna wapenzi ambao huona kwamba wazo la ndoa halina maana, halihitajiki, ni kandamizi na la zamani. Badala yake, wanachagua kuishi pamoja na kupata uzoefu wa kuwa na ukaribu na mtu, lakini bila kujitoa kwake. Wao huwa na hisia kwamba upendo ni kuhusu kuwa “katika wakati huu,” na kwamba ili kufurahia mahusiano ni kuishi dakika kwa dakika. Hata hivyo, mara tu wakati unapoisha na hawahisi tena kwamba mtu huyo ni “sahihi”, wanaondoka kwenye mpango huo na kwenda kwa mtu mwingine. Hakuna msingi wa kujitoa kwa mwenzao katika uhusiano wa namna hiyo, ni dhaifu kabisa.

Makubaliano ya Kuishi Pamoja

Kuishi pamoja kunahusisha mpangilio unaozingatia kile ninachotaka, na kile ambacho ni bora au kinachofaa mimi. Makubaliano hayo ni kama haya: “Unaweza kunitumia mradi tu uniruhusu na mimi nikutumie.” “Niko tayari kukuruhusu unitumie kama bidhaa, mradi tu unaniruhusu nikuchukulie kama bidhaa pia.” Lakini haya ni makubaliano ya uongo. Tunaweza kusema mwanzoni kwamba tunakubali kuwa “tuko wagumu kama chuma,” lakini hakuna mtu anayeweza kuahidi kwa hakika kwamba hakutakuwa na hisia za majuto ikiwa uhusiano huo utaharibika.

Tofauti na ndoa, wapenzi wanaoishi pamoja hujizoeza kutojitoa kikamilifu katika maisha yao ya “pamoja”. Wanaweza kuhisi hofu mara nyingi, wakishangaa kama wenzi wao kwa namna fulani watachukua fursa ya kuathirika kwao. Kwa hivyo, kuna uwezekano wa kuwa na mguu mmoja nje ya mlango, katika muda wote wa mpangilio huu.

Handbook Slides 80 Icons

Kuishi Pamoja. . . Kunaweza Kuwatenganisha

Ukweli ni kwamba kuishi pamoja kunaweza kuwatenganisha. [Hii haimaanishi kwamba kila wapenzi wanaoishi pamoja kabla ya ndoa watapata mambo yafuatayo; wala hatusemi kwamba kutoishi pamoja kunahakikisha uthabiti. Hata hivyo tunachunguza mitindo na data kwa ujumla, na inaonyesha matokeo haya.]

Utafiti unaonyesha wapenzi wanaoishi pamoja:

Unaweza ukawa unajua kinyume cha hayo hapo juu, lakini utafiti huu unaonyesha matokeo yanayowezekana mkiishi pamoja. Je, uko tayari kucheza kamari kwa matumaini kwamba unaweza kuwa mmoja wa walio tofauti?

  • “Fungate hutokea mara moja maishani, hivyo jiletee kile ambacho hujawahi kuwa nacho.” – Joe White

Lengo

Kuwasaidia washiriki kuelewa maana ya kutoshiriki ngono na thamani ya kuwa safi zaidi ya usafi wa mwili tu.

Usuli

Wengi wamebisha kuwa kutoshiriki ngono hakuwezekani kwa vijana. Lakini je, ni kitu ambacho hakiwezekani? Cha muhimu kwenye suala hili ni kutambua thamani ya mtu, kujenga tabia nzuri ya kufanya maamuzi mema, na thamani ya ngono katika uhusiano wa maisha wa ndoa.

Kutoka kwa hatua ya utafiti, kusubiri kushiriki ngono hadi wakati wa ndoa kuna faida. Hata hivyo, tunapaswa kukumbuka kwamba ujinsia unahusisha mambo mapana zaidi (na ya kina) zaidi ya kubaki tu safi au kushiriki ngono au la; inahusisha utambulisho wako, kujistahi, hisia yako ya kuwa na mtu anayekuthamini kipekee na hamu ya ukaribu na mtu huyo. Tunapaswa kwenda ndani zaidi ya kuwafundisha vijana wetu sio tu “kusema hapana,” ila kuwasaidia kufuatia ukamilifu, mahusiano yenye afya, na yenye ukaribu.

Mwandishi na mzungumzaji mashuhuri Dk. Juli Slattery anatukumbusha kwamba ukaribu ni zaidi ya ngono ya kimwili—ni hisia ya kujulikana, kuthaminiwa, na kupendwa.

Tunaishi katika ulimwengu unaohujumu uhusiano wa karibu katika kila hatua huku wakikuza ngono kama mbadala wa kutosha. Hakuna kiasi cha ngono (halisi au ya kichwani) kinaweza kufidia ukosefu wa ukaribu.

Vijana wetu wanaweza kuolewa au kutoolewa mbeleni, lakini bado wanaweza kuwa na mahusiano ya ukaribu na ya maana yaliyo ya kina kirefu. Tunahitaji kuwasaidia vijana wetu kuelekeza hamu yao ya urafiki wa karibu kwa njia zinazofaa.

Zaidi ya hayo, mapambano ya kukaa safi hayaishi siku ya sherehe ya harusi. Usafi wa kijinsia ni vita katika maisha yote ya watu wazima. Inachukua sura tofauti tu katika ndoa.

Activities Icons

SHUGHULI MUHIMU
Zoezi 1: Ni Kitu Gani Kilicho cha Thamani Kwako?

Blank Icons

Lengo

Wasaidie washiriki kukiri thamani ya usafi.

Maagizo

1. Waombe washiriki waonyeshe au waeleze kitu ambacho ni cha thamani sana kwao.

2. Mara tu wanapofichua kipengee chao, waulize washiriki wachache kwa nini wanafikiri kitu hiki ni cha thamani kwao.

3. Waulize wanafanya nini ili kukitunza, kukilinda na kukihifadhi. (Wana mipaka gani ili kukilinda?)

4. Baada ya hayo, wawezeshaji wanaweza kutoa mfano wa kibinafsi wa kile ambacho ni cha thamani kwao na kile wanachofanya ili kukilinda na kukihifadhi. Kwa mfano, unaweka vitu vyako vya thamani kwenye sefu (mipaka) ambayo inakusudiwa kulinda kile unachokithamini.

USAFI pia ni kitu chenye thamani na thamani kubwa. Je, tutaweka mipaka gani ili kuutunza, kuulinda na kuuhifadhi?

Usafi ni muhimu kwa sababu. . . ya thamani yake ya ajabu

Kufuatia usafi ni kutafuta utimilifu kama mtu

  • Kichwa - Moyo - Mkono (wakumbushe washiriki kuhusu mfano wa tabia nzuri katika Sura ya 1)
Handbook Slides 81 Icons

Fuata usafi na KICHWA chako

  • katika MAWAZO yetu kuhusu jinsia tofauti (Kiakili)
  • katika MANENO tunayosema na kuwaambia jinsia tofauti (Kijamii)

Fuata usafi kwa MOYO wako

  • Linda HISIA zetu na usiziruhusu ziathiri mwingiliano na watu wa jinsia tofauti. (Kihisia).

Fuata usafi na MKONO wako

  • Chora mipaka ya KIMWILI (Mwili) —Kataa kushiriki ngono kabla ya ndoa
  • Usafi ni zaidi ya kile unachokifanya [Kufanya], NDIVYO ULIVYO [Ulivyo].
  • Ni mtindo wa maisha; unakufafanua na utakufaidi.

NDIYO MAANA NI WA THAMANI SANA

  • "Kutafuta usafi sio kuhusu kusitiri tamaa, lakini ni kuhusu kuelekeza maisha ya mtu kwenye lengo kubwa zaidi.” — Dietrich Bonhoeffer
Activities Icons

Zoezi 2: Barua kwa mwanangu wa Kiume/Kike ajaye

Blank Icons

Lengo

Kusaidia washiriki kuimarisha sababu za kutoshiriki ngono na kuwa wasafi kwa kuwa na mtazamo wa “muda mrefu ujao” na “picha kubwa”.

Mahitaji

  • Kitabu cha mazoezi cha mwanafunzi

Maagizo

1. Waombe washiriki kuandika barua kwa wana wao watarajiwa wa kiume/kike wakijumuisha hoja zifuatazo:

  • Toa sababu kwa nini wanpaswa kusubiri kushiriki ngono hadi ndoa.
  • Waeleze sababu ambazo zitawafanya wasubiri hadi ndoa ndipo washiriki ngono na uwaelezee athari za ngono ya mapema, k.m, matukio ambayo wamewaona marafiki wakifanya makosa.
  • Elezea ni kwa nini kusubiri hadi wakati wa ndoa ni uamuzi muhimu na wa busara na kwanini kutoshiriki kunawapa uhuru wa kufanikisha ndoto na malengo yao maishani.

2. Kisha washiriki watie saini mwisho wa barua “Mama” ama “Baba” – sio majina yao.

Shiriki mfano halisi wa kile ambacho wewe (mwezeshaji) ungemtakia mwanao. Yaweza kuwa kwa njia ya kusoma barua ulioandika kwa mwanao unayemtarajia.

Activities Icons

Zoezi 3: Uunganishaji

Blank Icons

Lengo

Kuwasaidia washiriki kujua kwamba ngono ya mapema kwenye mahusiano hututawanya na huchukua muda kuponywa ama kurejelea hali ya kawaida, LAKINI tunaweza kuanza upya tena.

Mahitaji

  • Nakala za picha “sura” za kila kundi dogo
  • Mkasi
  • Gundi
    [wawezeshaji wanaweza kutumia picha ya kijana kutoka katika jumuiya yao].
Small Group Icons

Maagizo

1. Gawanya washiriki kwa makundi madogo ya washiriki 6-7.

2. Pitisha picha kwa kila kikundi. Inamisha picha hiyo (uso chini).

3. Agiza kila mtu kwenye kikundi akate sehemu ya picha hiyo na kuipitisha kwa mwenzake, picha hiyo ikiinamishwa wakati wote.

4. Changanyaa vipande vya picha hiyo ikiwa bado imeinamishwa.

5. Onyesha slaidi ya “iliyochanika” na uelezee kuwa kila mara tunaposhiriki ngono, tunawapatia sehemu yetu – kiakili, kijamiii, kimwili na hata kitabaka– kwa kila uhusiano mpya. Kila uhusiano unapokwisha, mshikamano unavunjika. Hisia zinazozunguka “kuvunjika” mara nyingi ni mseto –wakati mwingine kuna maumivu makali kuona umeachwa, wakati mwingine tunaona nafuu na hata mara nyingine kukasirika. Hii inaitwa “mizigo mizee” ambayo tunaileta kwenye ndoa, na kusababisha kutoaminiana, kuogopa tutaachwa, hofu ya hisia za uchungu, magonjwa ya zinaa – mambo mengi ambayo huleta msongo kwenye ndoa. Hata hivyo mtu ambaye amekuwa akishiriki ngono kwa muda anaweza kuamua kuacha na kuanza tena. Anaweza kujithibiti na kutoshiriki ngono hadi wakati wa ndoa.

6. Washiriki waweke sehemu zilizokatwa (zikiinamishwa) pamoja kwa kutumia gundi. Wakishakamilisha wazigeuze. Washiriki watagundua kuwa kuna mapengo kwenye picha hiyo.

7. Onyesha picha “iliyogundishwa pamoja” na uelezee mapengo yanawakilisha majeraha ama alama ambayo zinasalia – athari za kihisia, kisaikolojia ama kiroho (na wakati mwingine kimwili) . Vipande hivyo vipo, lakini vinahitaji uangalifu na umakinifu kuviweka pamoja. Inawezekana kujifunza tena kujiamini na tabia zenye afya njema katika mahusiano.

Unaweza Ukaanza Tena!

Handbook Slides 82 Icons

Washiriki ambao wamekuwa wakishiriki ngono wanahitaji kufahamu kuwa inawezekana kuacha na kupata uthabiti wa kujitoa kutoshiriki ngono hadi siku ya ndoa. Kurejelea uthabiti baada ya kushiriki ngono ya mapema sio rahisi haswa wakati vijana wako bado kwenye uhusiano ambao ndipo waliposhiriki ngono. Uamuzi wa kudunisha kutoshiriki unahitaji kuvunjilia mbali uhusiano huo ili kupata uthabiti na kupata muda wa kufanikisha malengo yako.

Hatua za Kuanza Upya

Iwapo ungependa kupata uthabiti na usishiriki ngono hadi siku ya ndoa, unafaa kufuata hatua hizi. Hatua:

  1. Simamisha uhusiano kwa muda kadhaa
    Iwapo uko kwenye uhusiano ambao mnashiriki ngono, unahitaji kuuvunja kwa muda, ili kuepuka mazingira hayo. Wewe na mwenzako itabidi mkubaliane kuhusu kurejesha udhibiti na kujitoa kutoshiriki ngono. Hii ina maana ya muda wa kutokutana ili kujitolea kiakili, kihisia na “kujipanga upya” na kuweka ahadi thabiti ya kusubiri hadi siku ya ndoa..
  2. Kumbuka kuwa wewe ni wa thamani na unastahili kutunzwa kwa uangalifu na heshima
    Unaweza kuwa umefanya uamuzi mbaya kwa kujihusisha kwenye ngono, lakini hilo haliondoi thamani yako. Ni kama shilingi 100 ambazo zimekanyagwa lakini thamani yake ingali ni shillingi 100..
  3. Tumia muda na nguvu zako vizuri
    Tumia muda wako pamoja na nguvu kujenga mahusiano na kukuza ujuzi wako – kama vile kukuza talanta ama michezo mipya.
  4. Jichunguze na ujiangalie tena
    Elekeza mtazamo wako kwenye malengo na ndoto zako ili hata uwe bora zaidi. Chunguza tena jinsi ulivyojiingiza kwenye uhusiano wa kingono. Je ni suala la mipaka? Ama unaweza kuwa ulijaribu kutafuta thamani yako kwa watu wa jinsia tofauti?
  5. Jizungushe na marafiki ambao wataunga mkono uamuzi wako.
    Kaa karibu na marafiki ambao wataunga mkono hatua yako ya kutoshiriki ngono na tabia nyingine hatarishi. Iwapo marafiki zako wote wanashiriki ngono ama wanalewa, basi huenda usifaulu kuacha licha ya juhudi zako. Zaidi ya yote tafuta mtu mzima unayemwamini wa kukuwajibisha.
  6. Andika ahadi ya kujitoa kusubiri
    Hifadhi nakala ulioandika mahali ambapo unaweza kukumbushwa. Shiriki uamuzi wako na mtu mzima unayemuamini na anaweza akakusaidia kuwajibikia katika miaka yako ya ujana.

Vipi ikiwa umefuata usafi na kungoja?

Baadhi yenu mnaweza kujiona kuwa ni wa ajabu au wa kuchosha na mmekosa furaha zote. Lakini hiyo ni hadithi.

Ukweli ni kwamba muda uliosubiri SIO wakati ulioupoteza.

Handbook Slides 83 Icons

Ni wakati ambapo:

  • Urafiki hujengwa
  • Ujuzi mpya unakuzwa
  • Unapata maana kupitia kazi ya kujitolea na huduma
  • Unafuatilia malengo na kazi yako

Kupitia kusubiri unajitayarisha, unajiweka katika nafasi nzuri, na unaishi kadiri ya kusudi lako la kipekee!

Unaposubiri weka nia na kuishi ukifuata kusudi lako la kipekee.

Nini maana ya Kutoshiriki Ngono?

Handbook Slides 84 Icons

Kutoshiriki ngono kuna maana ya kujitenga; kuepuka. Sio kama vile njia nyingine za kujikinga, kutoshiriki sio jambo analoweza kukushauri daktari ama unaweza kununua. Njia hii ya uzazi wa mpango, ikiwa itaitwa hivyo, inaleta kinga asilimia 100.

Na ni hakikisho la kuepuka mimba zisizohitajika, maradhi ya zinaa na miseto ya hisia. Hata hivyo ili kudumisha uamuzi huo, washiriki wanafaa kutafuta makundi ambayo yana mawazo sawa na hayo yatakayowaunga mkono na pia kuwahimiza.

Kutoshiriki ngono hadi siku ya ndoa, ni uamuzi ambao mtu huchukua na kuepuka vitendo vyote vya ngono hadi siku ya ndoa. Inajumuisha kufanya uamuzi wa kuepuka hali zote za ngono, ya mdomoni, ya mkunduni, kutomasana, na kupiga punyeto kwani huamsha hisia zetu za ngono na kuharibu usafi wetu.

Kwa kuamua kutoshiriki ngono, unajitolea kuepukana na:

  • Mawazo ya tamaa kwa mtu wa jinsia tofauti.
  • Maneno ambayo yanadhalilisha ama yanamfanya wa jinsia tofauti kuwa kama chombo.
  • Hisia zitawale mipaka yako.
  • Kudhibiti hisia za mtu mwingine ili ushiriki naye ngono.

Ngono ni zaidi ya kitendo chenyewe. Inahusisha pia shughuli nyingine ambazo zinatangulia kabla ya tendo lenyewe. Tunafaa kuchora mipaka kabla ya kujikuta tumesisimka na uchu.

Sio tu kuhusu “La” – hakuna picha za ngono, hakuna busu, hakuna ngono, nk. Kwa kweli unasema “Ndio” unapojithibiti na kuamua kuweka mipaka. Kutoshiriki ngono ni kujithibiti na kufanya maamuzi ya afya na ya busara.

Ni wito wako. Unathibiti vipi maisha yako ya ngono kwenye ujana wako na miongo inayokuja? Kufahamu athari za kushiriki ngono kabla ya ndoa hakutakusaidia iwapo hutafanya uamuzi kuzihusu.

Kataa kuamua na tayari umeshaamua.

Uamuzi kuhusu ngono na mahusiano sio wa kubahatisha. Uamuzi wako leo utaathiri maisha yako ya baadaye.

Lengo

Kutoa changamoto kwa washiriki kuchagua uamuzi wa kutoshiri ngono/kuwa safi hadi ndoa.

Awamu hii ni ya muhimu sana kwa warsha hii. Yote uliyoyasema na kuyafanya kabla ya kiwango hiki, yanalenga kujenga mazingira mazuri ambapo washiriki wanapewa fursa ya kufanya uamuzi.

Washiriki sasa wanapashwa kuelewa ya kutosha ama kufahamu kuhusu athari za ngono ya mapema ili wafanye uamuzi wa busara, jinsi wanavyotaka kuishi maisha yao na kufanya mahusiano yao

Ni muhimu uwaelekeze washiriki kutumia ufahamu wao kufanya maamuzi wakizangatia kile walichojifunza. Kumbuka kushirikisha mioyo na akili zao ili uamuzi wa kutoshiriki ngono ufanywe kwa moyo wote wala sio kwa sababu ya hisia, shinikizo au kwa huzuni.

Activities Icons

SHUGHULI MUHIMU
Zoezi 1: Kujitolea kuwa safi

Blank Icons

Lengo

Kuwahimiza washiriki kuahidi kuwa wasafi na kutoshiriki ngono kabla ya ndoa

Mahitaji

  • Kadi za kujitolea
  • Muziki wa mandharinyuma unaotuliza

Usuli

1. Elezea kuwa kufahamu athari za ngono ya mapema hakutakuwa na maana iwapo mshiriki hatafanya uamuzi. Wahimize wajitolee kufanya ahadi hiyo LEO.

2. Elezea kuwa kadi hizo zitawahimiza kuthamini malengo na ndoto zao kwa kutoshiriki ngono hadi siku ya ndoa. Wakati mwingine ni rahisi kuwajibika tukinakili ahadi zetu kwenye daftari na kuahidi uaminifu wetu kwa kuandika majina na kutia sahihi. Kutia saini kadi hizo kunamaanisha kuwa haijalishi maisha uliokuwa ukiishi, kuanzia leo unaahidi kutoshiriki vitendo vya ngono ama tabia hatarishi zitakazo athiri usafi wako.

Handbook Slides 85 Icons

3. Anza kushiriki hadithi yako (muziki wa chini kwa chini utasaidia) Ukielezea safari yako na kujitolea kwa usafi. Lengo ni kuwachochea wanafunzi kuwa na mtazamo wa kuona usafi kuwa zawadi kuu ambayo ni ya thamani.

4. Washiriki wasome kwa sauti kwenye kadi zao: hii inaashirikia kujitolea kwangu, familia yangu, mwenza wangu na wana wangu wa siku za usoni kutoshiriki ngono kuanzia leo hadi siku nitakayofungua ndoa.

5. Watie changamoto washiriki kujitolea kutoshiriki hadi siku ya ndoa. Wambie wachukue zile kadi na kuzitia saini. Kisha watafute shahidi atakayetia saini pia. Shahidi huyo anafaa kuwa mtu mzima wa kuaminika, mzazi ama mwelekezi [sio rafiki ambaye anakabiliwa na changamoto hizohizo za maisha] ambaye atawawajibisha na kuwaunga mkono katika uamuzi wao.

6. Wakumbushe washiriki kwamba kufuata usafi si tu kuhusu kutoshiriki ngono kabla ya ndoa—ni kuhusu kufuata utimilifu kama mtu. Thamani ya kweli ya chaguo lao haipo katika malipo ya ndoa bora na ngono katika siku zijazo, lakini malezi ya sifa chanya za tabia, kujithamini na utambulisho ambao utawapa uwezo wa kusema hapana kwa ushawishi mbaya, tabia hatari na ndio, hata. ngono kabla ya ndoa. Usafi wa kijinsia unatokana na ufahamu wa kina ya kwamba wewe ni nani—Mtu wa kipekee—kama mwanamume au mwanamke—mkamilifu, wa thamani, na sifa za kipekee, aliyeumbwa kwa ajili ya mahusiano yenye afya.

7. Malizia warsha kwa kuwathibitisha washiriki juu ya thamani na ujasiri wao katika kuweka msimamo. Ikiwa muda unaruhusu, washiriki waulize maswali.

Going Deeper Icons

Kwenda Ndani Zaidi
KWA WAWEZESHAJI

Blank Icons

Je, lengo kuu la usafi wa kijinsia ni lipi?

Kuacha kufanya ngono ni hatua muhimu ya kwanza ya kuwafundisha vijana wetu kuhusu kujamiiana kwa afya. Sio tu kusema hapana kwa ngono kabla ya ndoa. Inatokana na kuelewa kwamba muundo asilia wa ngono ni katika muktadha wa ndoa na kujaribia nje ya mipaka ya ndoa huleta matokeo mabaya.

Utamaduni wa sasa umedhamiria kupotoka kutoka kwa muundo huu wa asili kwa kufanya kile kinachohisi vizuri na sawa.

Zaidi ya elimu

Shinikizo la ndani na nje ambalo vijana wetu wanakabiliwa nalo linahitaji zaidi ya elimu ya kujiepusha tu shuleni na ndani ya jamii. Vile vile, ahadi yenye nguvu ya usafi inaweza kuwa ishara ya nje ya kujitolea kuacha ngono, lakini vijana wetu lazima wapatiwe picha kamili ya ujinsia.

Tunahitaji kufanya kazi pamoja kama wazazi, washauri, shule, jumuiya, mashirika ya kidini, n.k., ili tusafiri pamoja na vijana wetu.

Tunahitaji kwenda zaidi ya usafi wa kijinsia hadi utimilifu wa kijinsia, tukiwasaidia vijana KUISHI MAISHA WAKIWA WAZIMA, BILA MAJUTO.

Going Home Icons

Kwenda Nyumbani

Maswali ya Majadiliano ya Mzazi/Kijana kwa Kitengo cha 4

Mzazi mpendwa,

Katika Kitengo cha Hakuna Majuto® 4, wanafunzi walijifunza kuhusu umuhimu wa mahusiano mazuri na thamani ya kungoja hadi ndoa ili kufanya ngono.

Kwa madhumuni ya maswali ya majadiliano, fasili za upendo usio na masharti, tamaa na mvuto vilivyotumika katika Sura ya 4 ni kama vifuatavyo:

Handbook 85 Icons
  • Ufafanuzi wa Upendo Usio na Masharti: Kujitoa kunakotegemea kumjali mwenzako bila ubinafsi. Unamkubali kwa uhuru katika uaminifu na kumtafutia mema. Katika mahusiano ya ngono, uhusiano huu unaunganisha watu hawa na kuongezea zaidi kujitoa kwao.
  • Ufafanuzi wa Tamaa: Tamaa kali ya ngono au uchu mkubwa sana, kama katika tamaa ya mamlaka. Hamu ya ngono au msukumo wa mwili.
  • Ufafanuzi wa Kuvutiwa: Upendo usio wa kweli au wa kupita kiasi au msisimko unaovutia hisia na misukumo, nyakati nyingine huitwa tamaa. Kuvutia kunaweza kuwa kivutio cha awali ambacho, kwa wakati na kujitoa, kitakua na kuwa upendo uliokomaa na usio na masharti.

Maswali:

  1. Wanafunzi waliulizwa ni ufafanuzi upi utasaidia uhusiano wa kudumu.
    Je, unaweza (Mzazi) kusimulia hali ulipokuwa katika shule ya sekondari ambapo uliona marafiki wakifuata baada ya kuwa na mvuto, tamaa, na/au upendo usio na masharti? Matokeo yalikuwa nini? Je, unaweza (Kijana) kutaja ni marafiki wangapi unaowajua ambao wana uhusiano unaotokana na mvuto, tamaa au upendo usio na masharti? Matokeo yalikuwa ni nini?
  2. (Mzazi) ni jambo gani muhimu zaidi unalotaka kijana wako atambue kuhusu ndoa?
  3. (Kijana) Mweleze mzazi wako ahadi yako ya kutoshiriki tendo la ndoa hadi ndoa.
    Jadili sababu ulizozichagua za kuifanya ahadi hii. Jadili mawazo yatakayokusaidia kuitimiza ahadi yako.
No Apologies White Logo

Copyright 1997, 2026 Focus on the Family | Email: help@noapologies.com

Privacy Policy